Wakristo kitu gani kimewakuta mpaka mmeanza kuwaiga waislamu?

Kaka kwa mujibu wa imani yako? Je kuna kitu chochote ambacho Mwenyezi Mungu hana uwezo wa kukifanya?
"Naye juu ya kila kitu ni muweza.."

Lakini hasifiki kwa sifa za viumbe vyake ambazo ni sifa za upungufu, yeye amekamilika na ametukuka kutokana na mapungufu yeyote.
 
"Naye juu ya kila kitu ni muweza.."

Lakini hasifiki kwa sifa za viumbe vyake ambazo ni sifa za upungufu, yeye amekamilika na ametukuka kutokana na mapungufu yeyote.

Jibu swali " Mungu anaweza kufanya kitu chochote "?
 
Hapo kwenye Sayansi kuprove Quran kuwa true umepigwa na TikTok video za kiislamu...hamna kitu kama hicho
 
MUNGU hayuko peke yake huko MBINGUNI, kuna viumbe wengine, nae YESU alikuwa katikati ya hao viumbe
Brother naheshimu mawazo yako, but I have to respectfully disagree with you, yesu si mmoja kati ya viumbe wengi waliopo mbinguni, hapana, ana title na position kubwa sana mbinguni, unapomzungumzia yesu, mzungumzie kwa ukubwa wake na uungu wake.
 
Neno dini limetajwa mara chache sana ktk biblia. Yesu alionesha kuwa dini bado haiwezi mtu kushinda dhambi. Ndiyo maana wayahudi washika dini walimsulubisha.
 
Hivi ni Kristo au Kristu? Au ni Kiswahili tu au kuna upotofu?
 
Umeandika maneno ya pumba kuhusu imani ya dini ya kiislam iweje Waislam wawe na dini pasipokuwa na imani? Ukiwa Muislam kitu cha kwanza unatakiwa uwe na imani ya dini yako ndipo hapo Uslam wako utakuwa umekamilika pasipo na imani haujawa Muislam wa ukweli. Wale wanao jichukulia Sheria mikononi mwao kuwahukumu watu waliofanya makosa katika dini hao tunaweza kuwaita magaidi sio Waislam. Huwezi kumhukumu mtu pasipo na kumpeleka katika vyombo vya sheria. Katika Dini ya kiislam kuna sheria zake endapo mtu atakapo kiuka sheria za Dini ya kiislam anafaa kupelekwa kwa sheikh wa Mkoa au kadhi ili akapate kuhukumiwa sio wewe Muislam mwenzake ukaamuwa kuchukuwa sheria mikononi mwako umuhukumu utakuwa umevunja sheria za Dini ya kiislama na pia sheria ya Seikali iliyopo katika nchi yako. Ninakuacha hapo nalog off.
 
Mbona umejichanganya mkuu mpaka aibu kusoma, we sema tu ni ustaadh sio dhambi. Kwa sababu kwa maelezo yako umesifia Islam ni dini sio Imani afu ukakandia Ukristo ni imani sio dini, kibaya umejisahau ukasema wewe ni mfuasi wa dini za jadi za kiafrika.

Yaani umechanganya madafu mpaka aibu.

Acha nikutoe tongotongo Afrika haina dini bali ina imani 'way of life' hapa nazungumzia imani za jadi kila kabila lina utaratibu wake haufanani hata kidogo na kabila lingine, rastafari kila mtu anaweza kuwa rasta kwa kutunza tu misingi ya imani bila kujali taratibu za ibada wala sheria za kibinadamu, pia tuna Khemetician(old Egypt) au Ausarian hawa wapo kiroho zaidi ila hawana ibada za kila week bali ni misingi ya kiroho tu, unajifunza ukifuzu ndo umefuzu unaenda kufundisha wengine wenye wito kama wako. Ambapo karibia imani zote za jadi za kiafrika zinamfanano na Ausarian kwa kuwa huko ndo chimbuko la imani zote za kiafrika.

Kiufupi dini kuu zinazojulikana ni Ukristo na Uislam.

Kwa sababu kwenye imani za kiroho dini ni kitu dhaifu sana na ni kwaajili ya kuwafunga watu dhaifu wale ambao hawana uwezo wa kutafsri mambo ya kiroho yaani vipofu wa imani wapo kimwili zaidi. Hivyo kusema ukristo ni imani unaupaisha ukristo katika viwango ambavyo haijavifikia, ukristo ni dini tu iliyowafunga vipofu wa kiroho dhaifu kama vipofu wenzao wengine.

Sasa wewe unaposema una dini ya jadi ya kiafrika nitajie Afrika kuna dini gani, ipi hiyo, we sema ni Ustaadh mganga wa jadi wa kutumia kitabu usijifiche kwenye uafrika waafrika hatuna upuuzi unaoitwa dini, dini zililetwa na vipofu dhaifu wa imani kuwaongoza vipofu wenzao.

Dini = Religion (English) limetokana na neno la kilatini Re-Ligare
Re
= again,
Ligare = bind or tie together yaani wafunge tena na tena wasijechomoka zizini au nje ya box wakaujua ukweli.
Mbaya zaidi dini za sasa ni political religion/ dini za kisiasa

Walau dini za zamani bado zinatunza misingi ya imani kiroho kama kwa wakristo kuna Orthodox(ambapo hata marasta wanafuata misingi yake) na waislamu kuna Sufism. Mambo ya maarifa usiongelee mihemko.
Halafu usiishie kusema imani sema imani ya kiroho, unaweza kuwa na dini ila huna imani ya kiroho, ila ukiwa na imani ya kiroho dini kwako ni trakatraka moja ambayo hata hauihitaji, kwa sababu ushalipata kusudi la Mungu.
 
Maneno mengi, lakini hakuna kitu! 'Incarnation' (Mungu kuwa mtu) ina maana ya jinsi wewe unavyoweza kuongea na mtoto mdogo. Je, utafanyaje? Itabidi ujishushe kama mtoto na utumie lugha ambayo mtoto ataelewa. Mungu hufanya vivyo hivyo anapotaka kuongea nasi. Hujifanya/huwa kama sisi. Full stop! Mtoto ukimwongelesha lugha ya wakubwa, unapoteza muda wako. Ni methodolojia ya kufikisha ujumbe fulani kwa addressees wanaokusudiwa.
 
Miungu bandia kwa mujibu wa nani? Kumbuka hata huyo Mungu wako kwa wanaoabudu miti kwao huyo wanamuona muongo vile vile.

Msipende kujipa haki wakati hamna uhalali wa kumiliki hizo dini mlizoletewa kwa aibu na vifo vya babu zenu.
 
LIKUD liquid
 
Wamehoji kutofanana kwake na ukristo, maana ukristo ni doing like Jesus, Imani inayodhihilishwa Katika mwili, siyo kwamba ukristo hauna Sheria,tena Sheria zake ni Kali Sana,ila ziko rohoni siyo physically. Mfano amwangaliye mwanamke na kumtamani= zinaa , ukimchukia mtu= umeua etc,
Kwamba wanaowapiga mawe wazinzi Ni wanawake tu?
Ila kupitia hoja yako nimegundua wewe ni mfuasi wa Rastafarian Roy [emoji120] graphology zinaonyesha hivyo [emoji120]
 
Credit [emoji120][emoji120] uko sahihi Sana yuko stagini anaimba dangote baba lao,malisa baba lao... Yaani wanajitukuza Sana wao kuliko MUNGU [emoji24]
 
Umesema Ukristo hauna sheria?
Una maanisha Yesu Kristo hana sheria?
Mimi ni mkristo na ninakwambia sheria ya Kristo ipo, na ni Kali kuliko sheria za Musa na Tourati.

Embu nukuu sheria yoyote ya Yesu, kisha nipe na adhabu yake.
Kisha niambie nani anayetoa hiyo adhabu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…