Wakristo tushukuru sana ndoa zinaweza kuvunjwa mahakamani, Makanisa hayana msaada, Sheria zetu za ndoa zipo mdomini tu ila si kwa uhalisia

Wakristo tushukuru sana ndoa zinaweza kuvunjwa mahakamani, Makanisa hayana msaada, Sheria zetu za ndoa zipo mdomini tu ila si kwa uhalisia

R-K-O

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2023
Posts
482
Reaction score
2,178

Kuvunja ndoa ya kikristo ni mpaka kifo ama kuchepuka, Kwanini wakristo hawatii sheria zao wanakimbilia mahakamani kuvunja ndoa kwa sababu zingine?​


-Mke au mume wako ni mwema kabisa tabia njema wala hana tatizo, mara paap! Kapata kazi huko Marekani, likizo yake ya kurudi ni wiki 2 tu mwaka mzima,

- Mke au mume wako ni mwema kabisa tabia njema, mmeoana mkiwa vijana wadogo, baada ya siku kadhaa mwenzako kakamatwa kwa kesi ya mchongo anahukumiwa jela kifungo cha maisha,

- Mke anakunyima unyumba mwaka mzma, ulikula kiapo muishi wote no mara waaaa! Hakuna kiapo kilisema muachane kisa tamaa yako ya kufanya mapenzi imekuzidi, kwanini msivumiliane mpaka kifo

- Maningia kwenye ndoa unakuja kupata habari mke wako alishatoa mimba tano, mmekaa miaka sita hakuna mtoto, kwanini msivumiliane mpaka kifo

- Mke anachukia ndugu na mama wa mme wake, anamtukana mama yako, uliapa kwamba mtaachana hadi kifo, kwanini msivumiliane mpaka kifo

Na kama kuna kanisa linavunja ndoa nje ya hizo sababu basi ni wazi hawaheshimu dini yao.

Huko mahakamani kumekuwa kimbilio la kwaristo wengi kuvunja ndoa kwa sababu zingine kabisa nje ya hizo mbili.
 
Sheria zipo kinadharia tu sio kwa vitendo.
 
Kanisa halitoi cheti cha ndoa. Cheti cha ndoa ni cha serikali
Kuachana kwenye ndoa ni mpaka kifo kiwatenganishe ama moja wenu achepukue,

Nje ya hapo ni dhambi.

Kwanini wakristo hawataki kufuata sheria zao ?
 
Kuachana kwenye ndoa ni mpaka kifo kiwatenganishe ama moja wenu achepukue, Nje ya hapo ni dhambi. Kwanini wakristo hawataki kufuata sheria zao wanakumbilia kuzivunja mahamani?

Lakini ajabu wanandoa wengi hukimbilia mahakamani kuvunja ndoa zao kwa vitu nje ya hivyo viwili.

-Mke hapendi ndugu zako, Utaweza kuishi nae mpaka kifo kiwatenganishe ?

-Mke ni tasa ama mume hatungi mimba, muendelee kuishi mpaka kifo kiwatenganishe bila watoto ?

- Mke anamnyima mme unyumba na mwanaume viungo vyako vya uzazi vipo active, asiende mahakamani kwanini ?

- Mume anatoa kipigo kila siku, Huyu atakuua, Kifo hakitakutenganisha bali atakuaa ndio mtengane ?

- Mke ni mshirikina aliekubuhu, tia kiburi hapo ujidai kuendelea kuishi nae kama hujawa ndondocha .

- Mke / Mume kaenda jela maisha, na hapo huna hata mtoto, kuna ndoa hapo ?
Kwa sisi Wakristo wafia dini, utasa siyo sababu ya kumuacha mkeo. Ukiisoma Biblia vizuri utagundua kwamba mke wa Ibrahim (Sarah) alikuwa tasa lakini Ibrahim aliendelea kumpenda akiamini kwamba siku moja Mungu atamjalia mwana, na kweli wakaja kumzaa Isaka.

Mke wa Isaka (Rebeca) naye alikuwa tasa baadaye akajaliwa na Mungu akamzaa Esau na Yakobo.

Halikadhalika na mama yake Samson (mke wa Manoa) naye alikuwa tasa lakini Manoa hakumuacha, baadaye wakamzaa Samson.

Hata mke wa Elkana aitwaye Hana alikuwa tasa baadaye akamzaa Samweli.

Kuna mahali kwenye Biblia Elkana anaonekana kumfariji mkewe kwa kumwambia asinung'unike kwa kutopata mtoto. Unaweza kuanza kusoma kuanzia 1 Samweli 1:2, huo hapo chini ni mstari wa 8.

1 Samweli 1:8
[8]Elkana mumewe akamwambia, Hana, unalilia nini? Kwani huli chakula? Kwa nini moyo wako una huzuni? Je! Mimi si bora kwako kuliko watoto kumi?

Then said Elkanah her husband to her, Hannah, why weepest thou? and why eatest thou not? and why is thy heart grieved? am not I better to thee than ten sons?
 
Makanisani wanawambia nyie mvumiliane tu

Ova
 
Kuachana kwenye ndoa ni mpaka kifo kiwatenganishe ama moja wenu achepukue,

Nje ya hapo ni dhambi.

Kwanini wakristo hawataki kufuata sheria zao ?

Hawafuati Kwa sababu ni sheria za Uongo na hazina uhalisia.
Ndio maana Ukristo unaonekana kama Ukafiri Kwa sababu ya sheria za Uongouongo.

Hakuna kwenye amri za Mungu sheria isemayo ndoa ni mpaka kifo ilhali kuna mlango wa Talaka ikiwa kuna kuhitilafiana
 
Kwa sisi Wakristo wafia dini, utasa siyo sababu ya kumuacha mkeo. Ukiisoma Biblia vizuri utagundua kwamba mke wa Ibrahim (Sarah) alikuwa tasa lakini Ibrahim aliendelea kumpenda akiamini kwamba siku moja Mungu atamjalia mwana, na kweli wakaja kumzaa Isaka.

Mke wa Isaka (Rebeca) naye alikuwa tasa baadaye akajaliwa na Mungu akamzaa Esau na Yakobo.

Halikadhalika na mama yake Samson (mke wa Manoa) naye alikuwa tasa lakini Manoa hakumuacha, baadaye wakamzaa Samson.

Hata mke wa Elkana aitwaye Hana alikuwa tasa baadaye akamzaa Samweli.

Kuna mahali kwenye Biblia Elkana anaonekana kumfariji mkewe kwa kumwambia asinung'unike kwa kutopata mtoto. Unaweza kuanza kusoma kuanzia 1 Samweli 1:2, huo hapo chini ni mstari wa 8.

1 Samweli 1:8
[8]Elkana mumewe akamwambia, Hana, unalilia nini? Kwani huli chakula? Kwa nini moyo wako una huzuni? Je! Mimi si bora kwako kuliko watoto kumi?

Then said Elkanah her husband to her, Hannah, why weepest thou? and why eatest thou not? and why is thy heart grieved? am not I better to thee than ten sons?
Vipi kuhusu mke wako kuanza kukunyima tendo mwaka mzima na viungo vyako vya uzazi kila siku vinajaa

usijibu kama huna nguvu za kiume ama ni shoga
 
Kuna jambo moja wale wakristu majina na wapenda short cut ndio wanashabikia yasiyo ya msingi kama uvunjaji ndoa.

Kwanza lazima ujue tangu kabla ya kufunga ndoa ya kanisa haivunjiki (labda kama kuna mashart yaliyowekwa yalikiuka na kuifanya batili).
Tunasikia kelele nyingi kuhusu DP world kwamba tusiingie huo mkataba maana hakuna namna ya kujitoa.

Sasa kabla ya kufunga ndoa na yule unayetaka kufunga nae ndoa umejiandaa. Kukosa kwako kujiandaa hakulifanyi kanisa kuwa mtuhumiwa wa shida zako. Jiandae vema mtafute wa kufa na kuzikana sio wa kuishia njiani.

Misimamo hii na mingine mingi ya kanisa ndio imefanya ukristo kuwepo duniani hadi leo.

Kanisa pia linakiruhusu jkiona huwezindoa ishi peke yako
 
Hayo sio mambo ya kushabikia dunia ya sasa ina matatizo sana...Suala la kuvunjika ndo ni emergency sana na hatari kwa watoto zaidi ...

Achana kufikria baadhi ya mapungufu ya kinadamu na ya asili kama utasa hizi ni emergency.

unaweza kusema mke hapendi ndugu zako kwani wao ndo wanemuoa? kama wewe ana kuheshimu basi ,utakuja fukuza mkeo kisa ndugu ila tambua hao ndugu wanapita na ndo ina lengo ya nyie wenza kuishi milele..Ipo siku utabaki pekeako mke umemtimua na ndugu kila mtu karudi kwake.
 
Vipi kuhusu mke wako kuanza kukunyima tendo mwaka mzima na viungo vyako vya uzazi kila siku vinajaa

usijibu kama huna nguvu za kiume ama ni shoga
[emoji23][emoji23]

Eti usijibu kama huna nguvu za kiume ama ni shoga, dah! [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna jambo moja wale wakristu majina na wapenda short cut ndio wanashabikia yasiyo ya msingi kama uvunjaji ndoa.

Kwanza lazima ujue tangu kabla ya kufunga ndoa ya kanisa haivunjiki (labda kama kuna mashart yaliyowekwa yalikiuka na kuifanya batili).
Tunasikia kelele nyingi kuhusu DP world kwamba tusiingie huo mkataba maana hakuna namna ya kujitoa.

Sasa kabla ya kufunga ndoa na yule unayetaka kufunga nae ndoa umejiandaa. Kukosa kwako kujiandaa hakulifanyi kanisa kuwa mtuhumiwa wa shida zako. Jiandae vema mtafute wa kufa na kuzikana sio wa kuishia njiani.

Misimamo hii na mingine mingi ya kanisa ndio imefanya ukristo kuwepo duniani hadi leo.

Kanisa pia linakiruhusu jkiona huwezindoa ishi peke yako
Inatokea huyo mke wako kafungwa jela kifungi cha maisha

Hapo vp

Usilete sheria za baadhi ya makanisa kwamba wanaweza kupindisha hizo sheria 2,
 
Sheria ya ndoa ya kikristo ni mpaka kifo kiwatenganishe. Kuna nyingine tena?
 
Hayo sio mambo ya kushabikia dunia ya sasa ina matatizo sana...Suala la kuvunjika ndo ni emergency sana na hatari kwa watoto zaidi ...

Achana kufikria baadhi ya mapungufu ya kinadamu na ya asili kama utasa hizi ni emergency.

unaweza kusema mke hapendi ndugu zako kwani wao ndo wanemuoa? kama wewe ana kuheshimu basi ,utakuja fukuza mkeo kisa ndugu ila tambua hao ndugu wanapita na ndo ina lengo ya nyie wenza kuishi milele..Ipo siku utabaki pekeako mke umemtimua na ndugu kila mtu karudi kwake.
Ndoa nyingi za kikristo mabinti huwa watiifu kwenye uchumba lakini huyatoa makucha baada ya ndoa maana wanajua wapo sawa na wanaume, mwanaume hawezi kuongeza mke na akithubutu tu anafungwa jela kwa kuvunja sheria na / au mali kupigwa panga pasu kwa pasu.

Mwanamke unakuta alikuwa na nidhamu kabla ila mkiingia kwenye ndoa anaanza kiburi cha wazi wazi na anakunyima tendo la ndoa mwaka mzima, utaweza ?
 
[emoji2089][emoji2089][emoji2089][emoji2089][emoji2089][emoji2089]
 
Inatokea huyo mke wako kafungwa jela kifungi cha maisha

Hapo vp

Usilete sheria za baadhi ya makanisa kwamba wanaweza kupindisha hizo sheria 2,
Kama sheria ipi wanaweza kupindisha. Huko kwenye NGO mnazoziita makanisa wanweza kupindisha kila kitu hata wanazo biblia zao fuatilia. Inapokuja suala la ukristu kwanza Kanisa mama Katoliki kisha Lutheran, Anglican, Orthodox na mengine ambayo ni taasisi kimuundo na utendaji.

Hayo mengine mtu anajiamulia yeye na mkewe nini cha kufanya au kusema wanaweza kufanya lolote ila sio hayo makanisa nguli.

Kifungo cha mkeo akifanyi ndoa ife, mpaka kifo cha mmoja wenu.
Wala ugumba au utasa hauwatenganishi.

Kuna sharti moja la msingi sana hata serikalini hutumika. Consumation of marriage. Yaani ile siku ya kufunga ndoa au siku yeyote baada ya kufunga ndoa mlifanya tendo la ndoa.

Kama lilifanyika basi ndoa hiyo ilikamilika na ni halali.

Kama ilivyo kwenye mikataba mingine yeyote inayo vipengele vinavyopelekea uvunjaji wa ndoa vijue kabla ya kufunga ndoa husika.

Pia sio lazima ufunge ndoa kanisani (maana naona unakereka) unaweza kufunga ya kiserikali au hata ya kimila. Huko uvunjaji wake ni rahisi sana kama unataka urahisi kwenye kuvunja ndoa.

By the way, ukifunga ndoa hiku ukiwa na nia ya kuvunja hiyo ndoa itavunjika tu. Ila kama huna motive ya kuivunja utailinda milele na mtakuwa na raha daima.

Pia kuwa na raha daima haina maana hakuna changamoto zitakuwepo zitapita zitawaacha salama, magonjwa yatakuja yatapita, wanyatiaji watakuja watapita na mwisho mtafurahia uzee wenu na mtakuwa na cha kusema kwa wajukuu wenu.

Hivi mkeo anakuaje na kesi ya kufungwa maisha na wewe usihusishwe na kesi hiyo? It gets two to tangle.
 
Back
Top Bottom