Wakristo: Vita ya Israel inayoendelea ni ishara tosha kuwa wakati wa kuja kwake mwana wa Adamu (YESU) umekaribia. Tuamke

Wakristo: Vita ya Israel inayoendelea ni ishara tosha kuwa wakati wa kuja kwake mwana wa Adamu (YESU) umekaribia. Tuamke

Ufunuo 22:11-12

Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu;na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu;na mwenye haki na azidi kufanya haki;na mtakatifu na azidi kutakaswa.Tazama naja upesi,na ujira wangu u pamoja nami,kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
Amina Mkuu be Blessed
 
Break time.

 
Ndo Africa tunasumbuliwa na huu Ujinga Sijasoma alafu hapo hapo unatoa Judgement Huku ukiwa hujasoma kilicho andikwa kwa hakika una shida mkuu.
soma kwanza ndo utoe Judgement
Bado unaendelea kuandika pumba......
 
Kutoka mitandaoni...

TAIFA LA ISRAEL NA UNABII WA SIKU ZA MWISHO.

Na Joshua Ntagala
Taifa la israel ni taifa takatifu la Mungu,
utakatifu wake sio katika matendo ya kiuungu lakini ni takatifu kwa maana ya kwamba limetengwa kwa ajili ya matumizi ya Mungu(ardhi yake,watu wake, wametengwa kwa ajili ya kutimiza mipamgo ya Mungu).

Wakati wa mfalme Sulemani Mungu alimwelekeza mfalme huyo ajenge hekalu na alimpa maelekezo ya kila hatua na namna ya kulijenga hekalu hilo.

Moja kati ya maelekezo hayo ni kuchinja NG"OMBE MKE MWEKUNDU,asiyekua na kipaku(doa) na kumchoma na majivu yake kuyatunza ili kutengeneza maji yanayoitwa maji ya FARAKANO ambayo yatatumika kulitakasa eneo ambapo hekalu hilo litajengwa(Hesb19:2,5-9).

Katika biblia kwa nyakati tofauti kuna mahekalu matatu ya sulemani





kitabu cha Nehemia kinazungumzia jinsi jitihada za kulijenga hekalu hilo zilivyokua.

Hekalu hilo la pili ndilo lililokuwepo mpaka wakati wa Yesu na katika vitabu vya injili tunaposoma habari za hekalu basi ni hili hekalu la pili linalozungumzwa hapo(Luka 2:46).

UNABII
Sikumoja Yesu alifika karibu na mji wa Yerusalemu akauona mji akaulilia na kutoa unabii huu "Halitasalia jiwe juu ya jiwe".

Akiwa na maana kwamba maadui wa israel watawapiga na kuusambaratisha mji wote kiasi cha kubomoa majengo yote yaliyomo humo ikiwa ni pamoja na hekalu hilo la pili (Luka19: 41-44).

Miaka 70 baadaye Yesu akiwa ameshapaa yapata miaka 30 hivi, hekalu hilo lilibomolewa tena na mwaka wa 125 taifa la israel lilisambaratishwa na kutawanywa kwa kipindi kirefu sana. Na eneo hilo lilikuja kukaliwa na waarabu na taifa la israel likawa halipo kabisa kwenye ramani ya dunia.

Lakini kama ilivyo,, taifa la israel ni taifa takatifu la Mungu haliwezi kupotea au ardhi yake kuchukuliwa na mtu mwingine yeyote maana ni ardhi ya Mungu.

(Walawi 25:23) Neno kabisa kabisa kama lilivyotumika hapa linamaana : Hata wakija watu wengine katika ardhi hio haitakua yao kabisa.

Sasa hekalu la tatu linakuja kutajwa kua litakuwepo tena; na kwa maana hio litakuja kujengwa tena.
Hekalu la tatu sasa linakuja kutajwa katika (2thesoln 2 :1-4) ambapo mpinga kristo ataketi akijifanya kua kama Mungu

*(Ufunuo 11:1-2)
Eneo yalipokuwapo hayo mahekalu ( la 1 na la 2) ni katika mlima unaoitwa "moria" katika mlima huu ndipo Ibrahimu alipo mpeleka isaka kumchinja na badala yake Mungu akamwonesha mwanakondoo wa kumchinja

(Mwanzo 22:1-2)
Eneo hili linajulikana kwa jina "TAMPLE MOUNT" na kwa sasa upo msikiti mkubwa sana unaoitwa "al aqsa". Pia upo msikiti mwingine unaoitwa " The dom of the rock".

Msikiti wa al aqsa ni mahala pa 3 kwa utakatifu kwa wa islamu pakwanza pakiwa ni
1. Maka
2. Madina
3. al aqsa+ dom of the rock( inaoneaha ni jinsi gani eneo hilo kurudi mikononi mwa israel itakavyokua sio kazi rahisi,itapasa vita)

MKAKATI WA ISRAEL KURUDI KATIKA ARDHI YAO
Ilitabiriwa baadae israeli watarudi katika ardhi yao na baada ya kurudi itakapo timia miaka 70 watapewa milki ya ardhi yao
(Daniel 9:1-2)
(Yer29:10-11)

Maneno hayo yalitimia kama yalivyo
Mwaka 1948 waisrael walijikusanya kutoka pande zote za dunia na kurudi katika ardhi yao na ilipiganwa vita ya masaa machache sana takribani 6 tu nawaisrael kuchukua sehemu ya ardhi yao na mwaka huo 1948 ndipo lilitangazwa kuwapo taifa la israeli.

Miaka 70 baadae 1948+ 70= 2018
6/12/2017-- Rais Donald Trump alitangaza rasmi kuutambua mji wa yerusalemu kua makao makuu ya israel na mwaka 2018 alizindua ubalozi wa marekani mjini yerusalemu na unabii ukatimia kama ulivyo.

Dunia nzima tarehe 21/12/2017 ilikaa kikao cha umoja wa mataifa kumpinga Donald trump kwa uamzi huo ili litimie lile neno " THOUGH ALL NATIONS OF THE EARTH ARE GATHERED AGAINST JERUSALEM(Well translated in English)"(Zekaria12:1,3).

Siku hio ilipigwa kura na mataifa 128 wakailaani marekani na rais wake kwa uamzi huo na kuilaani israel pamoja na azimio hilo.

Katika Africa: Togo pekee ndio waliwasapoti israel.

Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi walikwepa kupiga kura

Inasikitisha Tanzania tulipiga kura kinyume cha israel na marekani).

Katika ulimwengu wa Roho nyakati hizi marekani atapingwa sana, Donald trump atapingwa sana na wewe unaweza kua miongoni mwa wanaompinga lakini leo umepata ufunuo huu usiwe miongoni mwa wanaompinga Trump kwa sababu Trump anaisupport Israel, ukimpinga/ kumlaani Trump una ilaani isarael na atakae ilaani israel atalaaniwa.

Sasa maandalizi ya kulijenga hekalu la 3 katika eneo hilo la al aqsa yanaendelea ,na vifaa vyote vinavyo hitajika katika ujenzi vimeshanunuliwa kwa msaada wa kanisa kote duniani na 10/9/2018 (jumatatu), lilitokea tukio la kushangaza tena kwani alizaliwa ng'ombe mke mwekundu asie na doa lolote kwa uchunguzi wa kina yaani DNA test .Hii inamaanisha ng"ombe huyo ni maalum kabisa kwa ajili ya kutengeneza maji ya farakano yatakayo tumika kulitakasa eneo ulipo msikiti huo wa al aqsa, kabla ya ujenzi wa hekalu la 3 kama tulivyoona katika maelekezo alopewa suleman wakati anajenga hekalu la Kwanza hesabu 19:1-9) 29/9/2019 msikiti wa al aqsa ulizuiliwa na jeshi la Israel na kuwazuia waislam wote kuingia kufanya ibada

Manaake nini? Itafikia Muda waislam watakosa uvumilivu wa kisiasa na kuamua kuingia vitani na kwa sababu ya vitendo hivyo vya israel,,na katika vita hio ndipo msikiti huo utavunjwa ili lijengwe hekalu la 3 ambalo kanisa likiwa tayari limekwisha kunyakuliwa mpinga kristo atafunuliwa na kuketi katika hekalu hilo akijifanya yeye kua ni Mungu.

2Thesoln 2: 1-12
Mstari wa 4: mpinga kristo hana budi kuinuka na kuketi katika hekalu

Mstari wa 6: linalo mzuia mpinga kristo kujulikana na kuinuka waziwazi ni kanisa (yaani watakao nyakuliwa) mpaka watakapo ondolewa,yaani watakapo nyakuliwa

mstari wa 7: lakini ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi, uasi umekithiri kuliko unavyoweza kufikiri,, ni kwa sababu tu upo Tanzania unaweza usijue uasi unaoendelea huko duniani kwa sasa, lakini kanisa linajitahidi kuuzuia huo uasi mpaka litakapo ondolewa (yaan litakapo nyakuliwa).

Mstari wa 8: baada ya kanisa kunyakuliwa ndipo atafunuliwa yule asi yaani mpinga kristo ili aketi katika hekalu la 3 litakalokua tayari limeshajengwa.

Kwahyo muda mfupi sana kabla ya kubomolewa msikiti huo tukio la unyakuo wa kanisa lapasa kua limeshafanyika ili kumpisha mpinga kristo afanye mambo yake kama ilivyo andikwa.

Kama tunavyofahamu,
SIKU WALA SAA ya kuja kwa mwana wa adamu hakuna aijuaye na Yesu ametuachia dalili tu zitakazoonesha kua hio siku i karibu.

Kumbuka hakuna ajuae kua vita itatokea lini na ni muda gani msikiti huo utabomolewa na nini kitakua chanzo kikuu cha vita hio baina ya palestina na israel.Sasa tunapoyaona hayo yakiendelea tunajua tupo mwishoni kwa kiasi gani, na kwa hivyo tujiweke tayari.

Tusizidiwe na ndege wa angani ambao wanajua majira ya kujiliwa kwao ( yeremia 8 :7).

Tunajua kutambua ishara za uso wa mbingu kwamba kutakua na dhoruba lakini ishara za siku za mwisho hatuwezi kuzitambua (mathayo 16:3).

Tuwe kama wana wa isakari watu wenye akili za kujua nyakati ili wajue ni lipi liwapasalo kutenda katika nyakati hizo (1 nyakati 12:32).

MWENYE MASIKIO NA ASIKIE NENO HILI AMBALO ROHO AYAAMBIA MAKANISA


(Ufunuo 22:11--12~~Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu;na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu;na mwenye haki na azidi kufanya haki;na mtakatifu na azidi kutakaswa.Tazama naja upesi,na ujira wangu u pamoja nami,kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.) we

NB: SIYO WAKIRSTO TU HATA WALE AMBAO BADO HAWAJAMKULI YESU KUWA MWOKOZI WA MAISHA YAO BASI MDA BADO UPO, KUBALI KUMPOKEA YESU LEO AWE BWANA NA MWOKOZI WAKO.
Kumbuka Bado kitambo kidogo Mwana wa Adamu atakuja.

Ubarikiwe wewe uliesoma huu ujumbe. Natumaini umepata kitu.

UBARIKIWE SANA!

Moja ya somo huwa kulielewa ni shughuli ni unabii.
Umefafanua vizuri sana.

Jambo moja wengi hawalijui ni kuwa, kuna mkataba umoja wa mataifa wa Marekani kuilinda Israel hadi mwisho wa dunia! Sijui kama msomaji unanielewa?
 
ukristo unaoujua umetokea kwa warumi,

israeli watu wengi ni waislamu, wayahudi,

acheni kukurupuka....

waisraeli hata hawana hayo mawazo ya 'taifa teule'

Sawa hawana hayo mawazo ya taifa teule ila we umeelimishwa elewa hivyo kuwa wana u-special flani hivi duniani tofauti na mataifa mengine!

Na kwa taarifa yako ni wengi mno duniani, wametapakaa nchi nyingi sana na wanajuan!

Ukiwafanyia ubaya iwe kwa kukusudia au bahati mbaya, kisasi italipwa tu hata ipite miaka 100 iko siku watalipiza ubaya uliowafanyia!
 
Mungu alishindwa vipi kuiumba dunia isiyo na migogoro? Alishindwa vipi kumzuia shetani asilete uasi wake humu duniani? Alishindwa vipi kuzuia mateso wanayopitia watoto walioko Gaza ambao hawana dhambi yoyote?

Siku ya hukumu ikifika (kama kweli ipo), nitamwambia face to face, hakwepi lawama kwa haya yanayotokea duniani.

Kama ambavyo mpishi anabeba lawama chakula kikipikwa vibaya, ndivyo ambavyo Mungu anatakiwa kuwajibika kwa kuumba ulimwengu pamoja na walimwengu wenye madhaifu!


With all your mighty powers, you could have easily fix all this shit dear God. Why leave it all to me?

We ndo utakuwa wa kwanza kukiri na kusema hivi ni za kweli na za hukumu zako!
 
UBARIKIWE SANA!

Moja ya somo huwa kulielewa ni shughuli ni unabii.
Umefafanua vizuri sana.

Jambo moja wengi hawalijui ni kuwa, kuna mkataba umoja wa mataifa wa Marekani kuilinda Israel hadi mwisho wa dunia! Sijui kama msomaji unanielewa?
Nakupata Mkuu
 
Israel na Ukristo wapi na wapi? Kila siku mnaambiwa hapa kuwa ISRAEL hawautambui huo Ukristo. Israel ni ya Wayahudi na Waislam. Hiyo vita sio ya kidini ni vita ya kinchi au vita inayofanania na ya kikabila, Jeshi la Israel lina waislam wengi sana, na bado wanaishambulia Palestina.
 
Bado unaendelea kuandika pumba......
Una Shida zako binafsi.

Ushauri sogelea Kituko Cha Afya kilichopo jirani yako kwa ajili ya matibabu zaidi ya Afya ya akili.

Zaidi ya hapo Nenda kanisani utubu dhambi zako
 
Israel na Ukristo wapi na wapi? Kila siku mnaambiwa hapa kuwa ISRAEL hawautambui huo Ukristo. Israel ni ya Wayahudi na Waislam. Hiyo vita sio ya kidini ni vita ya kinchi au vita inayofanania na ya kikabila, Jeshi la Israel lina waislam wengi sana, na bado wanaishambulia Palestina.
Umesoma thread Vizuri au umesoma juu juu na kukimbilia Kutoa maoni.

Hakuna sehemu nimesema Kuwa Israel ni wakristo.
Ushauri zaidi Rudi kwenye thread usome tena Uelewe
 
mkuu maswali yako yanaonesha ni dhahiri hujasoma na hujafanya utafiti wa kutosha kuhusu haya mambo.

Fahamu ya kuwa ugomvi wa Israel na Palestine ni imani

S
asa tafiti kuanzia hapa ...iweje imani izue ugomvi wote huu usioisha Karne na Karne? Ukijibu hili swali itakufaa.
Ule ugomvi hauhusiani na IMANI.
 
Yule harudi tena ni kama wewe ukifa au unaowafahamu ndugu zako waliokufa hawawezi Rudi!!
 
Kutoka mitandaoni...

TAIFA LA ISRAEL NA UNABII WA SIKU ZA MWISHO.

Na Joshua Ntagala
Taifa la israel ni taifa takatifu la Mungu,
utakatifu wake sio katika matendo ya kiuungu lakini ni takatifu kwa maana ya kwamba limetengwa kwa ajili ya matumizi ya Mungu(ardhi yake,watu wake, wametengwa kwa ajili ya kutimiza mipamgo ya Mungu).

Wakati wa mfalme Sulemani Mungu alimwelekeza mfalme huyo ajenge hekalu na alimpa maelekezo ya kila hatua na namna ya kulijenga hekalu hilo.

Moja kati ya maelekezo hayo ni kuchinja NG"OMBE MKE MWEKUNDU,asiyekua na kipaku(doa) na kumchoma na majivu yake kuyatunza ili kutengeneza maji yanayoitwa maji ya FARAKANO ambayo yatatumika kulitakasa eneo ambapo hekalu hilo litajengwa(Hesb19:2,5-9).

Katika biblia kwa nyakati tofauti kuna mahekalu matatu ya sulemani





kitabu cha Nehemia kinazungumzia jinsi jitihada za kulijenga hekalu hilo zilivyokua.

Hekalu hilo la pili ndilo lililokuwepo mpaka wakati wa Yesu na katika vitabu vya injili tunaposoma habari za hekalu basi ni hili hekalu la pili linalozungumzwa hapo(Luka 2:46).

UNABII
Sikumoja Yesu alifika karibu na mji wa Yerusalemu akauona mji akaulilia na kutoa unabii huu "Halitasalia jiwe juu ya jiwe".

Akiwa na maana kwamba maadui wa israel watawapiga na kuusambaratisha mji wote kiasi cha kubomoa majengo yote yaliyomo humo ikiwa ni pamoja na hekalu hilo la pili (Luka19: 41-44).

Miaka 70 baadaye Yesu akiwa ameshapaa yapata miaka 30 hivi, hekalu hilo lilibomolewa tena na mwaka wa 125 taifa la israel lilisambaratishwa na kutawanywa kwa kipindi kirefu sana. Na eneo hilo lilikuja kukaliwa na waarabu na taifa la israel likawa halipo kabisa kwenye ramani ya dunia.

Lakini kama ilivyo,, taifa la israel ni taifa takatifu la Mungu haliwezi kupotea au ardhi yake kuchukuliwa na mtu mwingine yeyote maana ni ardhi ya Mungu.

(Walawi 25:23) Neno kabisa kabisa kama lilivyotumika hapa linamaana : Hata wakija watu wengine katika ardhi hio haitakua yao kabisa.

Sasa hekalu la tatu linakuja kutajwa kua litakuwepo tena; na kwa maana hio litakuja kujengwa tena.
Hekalu la tatu sasa linakuja kutajwa katika (2thesoln 2 :1-4) ambapo mpinga kristo ataketi akijifanya kua kama Mungu

*(Ufunuo 11:1-2)
Eneo yalipokuwapo hayo mahekalu ( la 1 na la 2) ni katika mlima unaoitwa "moria" katika mlima huu ndipo Ibrahimu alipo mpeleka isaka kumchinja na badala yake Mungu akamwonesha mwanakondoo wa kumchinja

(Mwanzo 22:1-2)
Eneo hili linajulikana kwa jina "TAMPLE MOUNT" na kwa sasa upo msikiti mkubwa sana unaoitwa "al aqsa". Pia upo msikiti mwingine unaoitwa " The dom of the rock".

Msikiti wa al aqsa ni mahala pa 3 kwa utakatifu kwa wa islamu pakwanza pakiwa ni
1. Maka
2. Madina
3. al aqsa+ dom of the rock( inaoneaha ni jinsi gani eneo hilo kurudi mikononi mwa israel itakavyokua sio kazi rahisi,itapasa vita)

MKAKATI WA ISRAEL KURUDI KATIKA ARDHI YAO
Ilitabiriwa baadae israeli watarudi katika ardhi yao na baada ya kurudi itakapo timia miaka 70 watapewa milki ya ardhi yao
(Daniel 9:1-2)
(Yer29:10-11)

Maneno hayo yalitimia kama yalivyo
Mwaka 1948 waisrael walijikusanya kutoka pande zote za dunia na kurudi katika ardhi yao na ilipiganwa vita ya masaa machache sana takribani 6 tu nawaisrael kuchukua sehemu ya ardhi yao na mwaka huo 1948 ndipo lilitangazwa kuwapo taifa la israeli.

Miaka 70 baadae 1948+ 70= 2018
6/12/2017-- Rais Donald Trump alitangaza rasmi kuutambua mji wa yerusalemu kua makao makuu ya israel na mwaka 2018 alizindua ubalozi wa marekani mjini yerusalemu na unabii ukatimia kama ulivyo.

Dunia nzima tarehe 21/12/2017 ilikaa kikao cha umoja wa mataifa kumpinga Donald trump kwa uamzi huo ili litimie lile neno " THOUGH ALL NATIONS OF THE EARTH ARE GATHERED AGAINST JERUSALEM(Well translated in English)"(Zekaria12:1,3).

Siku hio ilipigwa kura na mataifa 128 wakailaani marekani na rais wake kwa uamzi huo na kuilaani israel pamoja na azimio hilo.

Katika Africa: Togo pekee ndio waliwasapoti israel.

Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi walikwepa kupiga kura

Inasikitisha Tanzania tulipiga kura kinyume cha israel na marekani).

Katika ulimwengu wa Roho nyakati hizi marekani atapingwa sana, Donald trump atapingwa sana na wewe unaweza kua miongoni mwa wanaompinga lakini leo umepata ufunuo huu usiwe miongoni mwa wanaompinga Trump kwa sababu Trump anaisupport Israel, ukimpinga/ kumlaani Trump una ilaani isarael na atakae ilaani israel atalaaniwa.

Sasa maandalizi ya kulijenga hekalu la 3 katika eneo hilo la al aqsa yanaendelea ,na vifaa vyote vinavyo hitajika katika ujenzi vimeshanunuliwa kwa msaada wa kanisa kote duniani na 10/9/2018 (jumatatu), lilitokea tukio la kushangaza tena kwani alizaliwa ng'ombe mke mwekundu asie na doa lolote kwa uchunguzi wa kina yaani DNA test .Hii inamaanisha ng"ombe huyo ni maalum kabisa kwa ajili ya kutengeneza maji ya farakano yatakayo tumika kulitakasa eneo ulipo msikiti huo wa al aqsa, kabla ya ujenzi wa hekalu la 3 kama tulivyoona katika maelekezo alopewa suleman wakati anajenga hekalu la Kwanza hesabu 19:1-9) 29/9/2019 msikiti wa al aqsa ulizuiliwa na jeshi la Israel na kuwazuia waislam wote kuingia kufanya ibada

Manaake nini? Itafikia Muda waislam watakosa uvumilivu wa kisiasa na kuamua kuingia vitani na kwa sababu ya vitendo hivyo vya israel,,na katika vita hio ndipo msikiti huo utavunjwa ili lijengwe hekalu la 3 ambalo kanisa likiwa tayari limekwisha kunyakuliwa mpinga kristo atafunuliwa na kuketi katika hekalu hilo akijifanya yeye kua ni Mungu.

2Thesoln 2: 1-12
Mstari wa 4: mpinga kristo hana budi kuinuka na kuketi katika hekalu

Mstari wa 6: linalo mzuia mpinga kristo kujulikana na kuinuka waziwazi ni kanisa (yaani watakao nyakuliwa) mpaka watakapo ondolewa,yaani watakapo nyakuliwa

mstari wa 7: lakini ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi, uasi umekithiri kuliko unavyoweza kufikiri,, ni kwa sababu tu upo Tanzania unaweza usijue uasi unaoendelea huko duniani kwa sasa, lakini kanisa linajitahidi kuuzuia huo uasi mpaka litakapo ondolewa (yaan litakapo nyakuliwa).

Mstari wa 8: baada ya kanisa kunyakuliwa ndipo atafunuliwa yule asi yaani mpinga kristo ili aketi katika hekalu la 3 litakalokua tayari limeshajengwa.

Kwahyo muda mfupi sana kabla ya kubomolewa msikiti huo tukio la unyakuo wa kanisa lapasa kua limeshafanyika ili kumpisha mpinga kristo afanye mambo yake kama ilivyo andikwa.

Kama tunavyofahamu,
SIKU WALA SAA ya kuja kwa mwana wa adamu hakuna aijuaye na Yesu ametuachia dalili tu zitakazoonesha kua hio siku i karibu.

Kumbuka hakuna ajuae kua vita itatokea lini na ni muda gani msikiti huo utabomolewa na nini kitakua chanzo kikuu cha vita hio baina ya palestina na israel.Sasa tunapoyaona hayo yakiendelea tunajua tupo mwishoni kwa kiasi gani, na kwa hivyo tujiweke tayari.

Tusizidiwe na ndege wa angani ambao wanajua majira ya kujiliwa kwao ( yeremia 8 :7).

Tunajua kutambua ishara za uso wa mbingu kwamba kutakua na dhoruba lakini ishara za siku za mwisho hatuwezi kuzitambua (mathayo 16:3).

Tuwe kama wana wa isakari watu wenye akili za kujua nyakati ili wajue ni lipi liwapasalo kutenda katika nyakati hizo (1 nyakati 12:32).

MWENYE MASIKIO NA ASIKIE NENO HILI AMBALO ROHO AYAAMBIA MAKANISA

(Ufunuo 22:11--12~~Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu;na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu;na mwenye haki na azidi kufanya haki;na mtakatifu na azidi kutakaswa.Tazama naja upesi,na ujira wangu u pamoja nami,kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.) we

NB: SIYO WAKIRSTO TU HATA WALE AMBAO BADO HAWAJAMKULI YESU KUWA MWOKOZI WA MAISHA YAO BASI MDA BADO UPO, KUBALI KUMPOKEA YESU LEO AWE BWANA NA MWOKOZI WAKO.
Kumbuka Bado kitambo kidogo Mwana wa Adamu atakuja.

Ubarikiwe wewe uliesoma huu ujumbe. Natumaini umepata kitu.
Amina 😍
 
Sikupingi hata kidogo mkuu ila mbona huku nilipo kuna watu bado hata hawajasikia jina la huyu Yesu, nikiwa na maana ya kwamba iliandikwa kuwa kila kiumbe lazima kiwe na taarifa hii

Sio kila mwanadam duniani atahubiriwa au kulipokea neno la Mungu!

Mathayo 5:5

Heri walio maskini wa roho maana hao watauridhi ufalme wa mbinguni.
 
Maswali yako tayari Yana majibu kwenye Biblia.
Na Mungu anasema hivi mambo yote yatapita lakin Neno lake litasimama ambayo ni Biblia.
Kwaiy Mkuu maswali ukimulza Mungu yeye atakuambia Kuwa Biblia hii hapa soma na ndo atatumia kuhukumu.

Kukatisha Story majibu ya maswali yako yapo Mwanzo kuanzia Sura ya kwanza tangu uumbaji mpaka Uasi wa Mwanadamu na Kusababisha mateso haya yote.
Nafikiri soma kitabu Cha mwanzo Chote utapata majibu ya maswali yako.

Please [emoji120]
Jaribu kujibu wachangiaji kwa kuambatanisha vifungu vya biblia kwa ufupi kuliko akafungue bible!

Kumbukumbu la Torati 29:29

Mambo ya siri ni ya BWANA, Mungu wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu milele, ili tuyafanye maneno yote ya sheria hii.
 
Back
Top Bottom