Wakristo wasio Wasabato wanaruhusiwa kula paka, panya, kobe, kinyonga, kenge, kunguru, nyani, n.k?

Wakristo wasio Wasabato wanaruhusiwa kula paka, panya, kobe, kinyonga, kenge, kunguru, nyani, n.k?

Huyo jamaa anaeweka magazeti marefu ashaharibu uzi, anadhani yupo kwenye magroup yake ya whatsapp.

Huku jamiiforums inapendeza unavyotoa hoja iwe direct, mambo ya magazeti huku ni tofauti
Nimesema mimi umeanzisha ligi hii ni battle patachimbika wanakuja 10 km huyo huu uzi hautaisha leo, nautabiria utafika mbali saaaana huu uzi
 
Hakuna Leta hapa hiyo Biblia ,Mimi na version Zote, hayo maneno yapo hivo hivo kwa Lugha ya asili ,

Ni tafsiri zenu tu zinawapiga chenga mnajikuta mnakula kila UCHAFU
Suala la yesu kusafisha vyakula vyote limeweka kwenye mabano kuashiria hayo maneno hayakuwemo bali ni uchambuzi wa waliondika biblia hizi mpya zilizotafsiriwa

Nashangaa kuona biblia za kiswahili zimeunganisha kabisa moja kwa moja bila mabano ili ionekane kwamba maneno haya yalikuwemo kwenye biblia

Hivyo basi, Biblia za kiswahili zimechachachuliwa kudanganya waumini, ukiwemo wewe unaebisha mpaka mishipa kukutoka shingoni ukidhani kwamba maandiko hayo yalikuwemo kwenye biblia kumbe kuna mhuni kayatoa mabano ionekane ni maandiko yaliyokuwemo, poleni sana kwa kuchezewa akili mda wote huu mkiaminishwa uongo.

Hebu cheki matoleo haya tofauto ya biblia za kiingereza wameweka mabano, hata google wameweka mabano,


Screenshot_20221111_033030.jpg



alieandika biblia ya kiswahili kahujumu wakristo wengi wa Tanzania wanaoendelea kula vichafu wakidhani Yesu alivitakasa
 
KULA NGURUWE NI DHAMBI NA ADHABU YAKE NI KALI ,NI IMEAHIDIWA SIKU YA KIAMA ,

Isaya 65

1 Watu wasionitaka wanauliza habari zangu; nimeonekana na hao wasionitafuta; naliliambia taifa lisiloitwa kwa jina langu,

2 Nitazameni, nitazameni. Mchana kutwa nimewanyoshea mikono yangu watu walioasi, watu waendao katika njia isiyo njema, wakifuata mawazo yao wenyewe;

3 watu wanikasirishao mbele za uso wangu daima, wakitoa dhabihu katika bustani zao, na kufukiza uvumba juu ya matofali;

4 waketio kati ya makaburi, na kulala katika mahali pao pa siri; walao nyama ya nguruwe, na mchuzi wa vitu vinichukizavyo u katika vyombo vyao;

5 watu wasemao, Simama peke yako, usinikaribie mimi, kwa maana mimi ni mtakatifu kuliko wewe; watu hao ni moshi puani mwangu, moto uwakao mchana kutwa.

6 Tazama, neno hili limeandikwa mbele zangu. Sitanyamaza, lakini nitalipa, naam, mimi nitawalipa ujira wao vifuani mwao;

SASA KINA MWAMPOSA ,GWAJIMA ,MWAKASEGE,MFALME ZUMARIDI,N.K WANASEMA KULENI NGURUWE ,MUNGU AMERUHUSU

Mungu Sio kigeugeu ,kaahidi kabisa hapo SIKU YA KIAMA ATATOA KICHAPO HATARI KWA WALA NGURUWE NA MACHUKIZO MENGINE
Nimesoma na kuupenda ujengaji wako wa hoja katika mada hii japo kuna mistari kwenye wakolosai hujaigusa.

Pia ninaona ni dhahiri kuna kitu bado haujakifahamu kuhusu ujio wa Yesu Kristo duniani na mtu anayemuamini Yesu anakuwaje ndani ya Kristo.

Ni jambo la kustaabisha kwamba mtu anaamini kuwa ukila nyama fulani utahukumiwa. Ni kukosa kulijua tumaini la wito wetu katika Kristo Yesu.

Pia kuna kitu kimoja cha hatari sana unakifanya ambacho kinanifanya nipate mashaka makubwa unasimama kweli ndani ya Kristo? Unawezaje kuwataja kwa majina na kuwakejeli watumishi wa Mungu?

Paulo mtume alifuta kauli na tamko alilofanya kinyume na kuhani mkuu ingawa ilikuwa dhahiri kwamba kuhani alikuwa amekosea. Unafanya makosa makubwa sana kumsema mtumishi yeyote hata kama yupo wrong.

Kazi yetu ni kuwaombea tu, warumi 14:4 unasema, " u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha"
 
Biblia feki hii!! Unasoma Biblia feki!! Hayo maneno yanakuwaga kwenye mabano naona kwa sasa wameamia kuyafanya yaonekane yalikuwemo...

Badili biblia, hio biblia siwezi shangaa kuna amri ya 11
Tuletee original manuscripts ili tuangalie kama yalikuwepo au yaliwekwa na waliotafsiri.
 
Tuletee original manuscripts ili tuangalie kama yalikuwepo au yaliwekwa na waliotafsiri.
Wala hakuna haja ya kwenda mbali, ingia google tu utaona biblia karibia zote zimewekea mabano,,, Biblia hizi za kiswahili zilizounganisha bila mabano ni uhuni mtupu wa kuwalaghai waumini wadhani yalikuwa ni maandiko halisi...

Poleni sana kwa kudanganywa kwa muda mrefu, mabano haya hapa 👇👇

Screenshot_20221111_033030.jpg
 
Picha linaamza nipo darasani

Tunaambiwa tukusanye alama za marks za masomo yote tuliyofanya, kila mmoja anaandika nami bila hiyana naandika marks zangu zoote, kuna binti baada ya kuangalia karatasi ya majina na marks na kuona marks zangu anagundua nimefanya vizuri saaana na sio kawaida ila sijionyeshi km walivyofanya wengine

Nabaki kua mshangao kwa wengine lakini sina furaha wanashangaa huyu mboni ndio amefanya vizuri ila hana furaha ana tatizo gani?

Mda wa kuondoka unafikà naelekea nyumbani, nikiwa njiani nakutana na yule binti anaanza kunitania kwamba najifanyà sina akili kumbe ni bonge moja la genius, naanza kumkimbiza tunapandisha vilima tunashuka chaka kwa chaka mpaka juu kilimani, tunafika kwenye nyumba moja nzuru ya vioo ipo kilimani

Binti anapita mlangoni ila mimi nafika nakutana na kioo kinanizuia nisiingie ndani, kuangalia ndani binti ananicheka mara anatokea kijana mmoja anaanza kunisaidia kuingia kwa kuvivuta vioo kutoka chini kwenda juu ili mimi niingie ndani, vinamshinda anatokea kijana mwingine anamsaidia maana vioo vilikua viwili wanajitahidi hadi wanavinyanyua mpaka juu sasa unabaki wakati wa mimi tu kupita na kuingia ndani,

Nikaanza kupita kwa kujihami maana wakiviachia vinanifyeka vibaya vibaya nikawaka km najihami kwa kuvishika ili niingie kumbe nilivyovishika wao wakaamua kuniachia nimeingia mpaka ndani nikajisahau nikaviachia nikidhani bado wamenisaidia kuvishika vikavunjika vipande vipande pale pale,

Kuangalia nyuma nakuta kuna Mzee yupo mlango akaawa amebaki mdomo wazi anashangaa kwanini nimevunja vioo huku kanitolea macho anashindwa aanze kuniambia kipi na kipi aache, nikaona yupo stand by kuanza kuingia ndani na kutoa kichapo, nikasema isiwe tabu kuangalia huku yule binti simuoni kuangalia huku wale vijana siwaoni, nikasema sasa hapa nabaki nasubiri nini? Nikajikongoja nikatafuta mlango wa nyuma nikaupata uko wazi nikapita nikatoka nje

Nikaanza kutimua mbio huku nyuma namuona Mzee kaja na kundi kubwa la watu wakawa wananikimbiza nikaruka sana majaruba, nikakatisha kwenye mito midogo midogo wao wako nyuma wananifukuza tu tena bila kuchoka na cha ajabu wananofukuza kimya kimya

Ndoto hii acha niamke sasa...
 
Nimesoma na kuupenda ujengaji wako wa hoja katika mada hii japo kuna mistari kwenye wakolosai hujaigusa.

Pia ninaona ni dhahiri kuna kitu bado haujakifahamu kuhusu ujio wa Yesu Kristo duniani na mtu anayemuamini Yesu anakuwaje ndani ya Kristo.

Ni jambo la kustaabisha kwamba mtu anaamini kuwa ukila nyama fulani utahukumiwa. Ni kukosa kulijua tumaini la wito wetu katika Kristo Yesu.

Pia kuna kitu kimoja cha hatari sana unakifanya ambacho kinanifanya nipate mashaka makubwa unasimama kweli ndani ya Kristo? Unawezaje kuwataja kwa majina na kuwakejeli watumishi wa Mungu?

Paulo mtume alifuta kauli na tamko alilofanya kinyume na kuhani mkuu ingawa ilikuwa dhahiri kwamba kuhani alikuwa amekosea. Unafanya makosa makubwa sana kumsema mtumishi yeyote hata kama yupo wrong.

Kazi yetu ni kuwaombea tu, warumi 14:4 unasema, " u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha"
Petro mwanafunzi wa Yesu aliposoma maandiko ya Paulo alichanganyikiwa ,itakuwa Mwamposa ,au Gwajima wenye Njaa ?

JUZI nilikuwa safarini , njiani nilimsikia muislamu akiponda Sana Agano jipya akidai limeruhusu kula nguruwe , wakati agano la Kale limekataza, nikajisemea Moyoni , NI KUTOKUELEWA TU.......

Mtume Petro alitoa angalizo juu ya usomaji wa nyaraka za Paulo na akatoa onyo lifuatalo:

#2 Petro 3:15-17
Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa;
vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.

Sio Petro tu ndio anadai kwamba nyaraka za Paul ni ngumu, bali hata watu wengine pia wanasema nyaraka za Paul ni ngumu, Na Paul yeye mwenyewe anashuhudia kwamba watu wanasema nyaraka zake ni nzito/ ngumu:

2 Wakorintho 10:9-10
nisije nikaonekana kana kwamba nataka kuwaogofya kwa nyaraka zangu.
Maana wasema, Nyaraka zake ni nzito, hodari; bali akiwapo mwenyewe mwilini ni dhaifu, na maneno yake si kitu.

.
Hivyo inabidi umakini mkubwa sana unapokutana na aya tata katika Nyaraka za Paul, pia ieleweke kwamba Nyaraka zote za Paul alikuwa anashugulika na kutatua migogo ya kiimani iliyokuwa inatokea ndani ya Kanisa baina ya washiriki, na pia alikuwa anashugulika na walimu wa uwongo waliokuwa wakiingiza mafundisho potofu ndani ya kanisa. Ikumbukwe kwamba makanisa yote ambayo Paul anayaandikia nyaraka ni makanisa ya watu waliokuwa na mchanganyiko baina ya Wayahudi na watu wa Mataifa, mengine yalikuwa ni machanga katika imani.
 
Nimesoma na kuupenda ujengaji wako wa hoja katika mada hii japo kuna mistari kwenye wakolosai hujaigusa.

Pia ninaona ni dhahiri kuna kitu bado haujakifahamu kuhusu ujio wa Yesu Kristo duniani na mtu anayemuamini Yesu anakuwaje ndani ya Kristo.

Ni jambo la kustaabisha kwamba mtu anaamini kuwa ukila nyama fulani utahukumiwa. Ni kukosa kulijua tumaini la wito wetu katika Kristo Yesu.

Pia kuna kitu kimoja cha hatari sana unakifanya ambacho kinanifanya nipate mashaka makubwa unasimama kweli ndani ya Kristo? Unawezaje kuwataja kwa majina na kuwakejeli watumishi wa Mungu?

Paulo mtume alifuta kauli na tamko alilofanya kinyume na kuhani mkuu ingawa ilikuwa dhahiri kwamba kuhani alikuwa amekosea. Unafanya makosa makubwa sana kumsema mtumishi yeyote hata kama yupo wrong.

Kazi yetu ni kuwaombea tu, warumi 14:4 unasema, " u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha"
WARUMI SURA YA 14.

Warumi 14:5-7
Mtu mmoja afanya tofauti kati ya siku na siku, mwingine aona siku zote kuwa sawasawa. Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe.
Yeye aadhimishaye siku, huiadhimisha kwa Bwana; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; tena asiyekula, hali kwa Bwana, naye pia amshukuru Mungu.
Kwa sababu hakuna mtu miongoni mwetu aishiye kwa nafsi yake, wala hakuna afaye kwa nafsi yake.

Nawasalimu katika jina la BWANA WETU YESU KRISTO:

Ikiwa kuna aya zinazowachanganya Wakristo wengi, pamoja na Waislamu, ni mafungu yanayotoka katika Nyaraka za mtume Paul, na ndio maana hata mtume Petro alitoa angalizo juu ya usomaji wa nyaraka za Paulo na akatoa onyo lifuatalo:
#2 Petro 3:15-17
Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa;
vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.
Sio Petro tu ndio anadai kwamba nyaraka za Paul ni ngumu, bali hata watu wengine pia wanasema nyaraka za Paul ni ngumu, Na Paul yeye mwenyewe anashuhudia kwamba watu wanasema nyaraka zake ni nzito/ ngumu:
2 Wakorintho 10:9-10
nisije nikaonekana kana kwamba nataka kuwaogofya kwa nyaraka zangu.
Maana wasema, Nyaraka zake ni nzito, hodari; bali akiwapo mwenyewe mwilini ni dhaifu, na maneno yake si kitu.
.
Hivyo inabidi umakini mkubwa sana unapokutana na aya tata katika Nyaraka za Paul, pia ieleweke kwamba Nyaraka zote za Paul alikuwa anashugulika na kutatua migogo ya kiimani iliyokuwa inatokea ndani ya Kanisa baina ya washiriki, na pia alikuwa anashugulika na walimu wa uwongo waliokuwa wakiingiza mafundisho potofu ndani ya kanisa. Ikumbukwe kwamba makanisa yote ambayo Paul anayaandikia nyaraka ni makanisa ya watu waliokuwa na mchanganyiko baina ya Wayahudi na watu wa Mataifa, mengine yalikuwa ni machanga katika imani.

#Sasa kabla ya yote inabidi tuzingatie mambo yafuatayo ili tuweze kuelewa nyaraka za Paulo na vitabu vingine:
1. Waraka huo aliwaandikia watu gani?
2. Kulikuwa na changamoto gani ?
3. Alishughulika vipi na hiyo changamoto.

Kwa hiyo kwa utangulizi huo, naomba tuchungze baadhi ya hoja zinazo patikana katika Warumi 14. Miongoni mwa hoja ambazo hujengwa na baadhi ya wakristo katika kitabu hiki ni
1. Siku zote ni sawa, hivyo unaweza kuabudu siku yoyote ile.
2. Ikiwa mwenzako anakula nguruwe wewe kumnyoshea kidole.
3. Hakuna kitu kilicho najisi kwa asili yake.

Kama ambavyo nimetangulia kusema Kanisa la Rumi lilikuwa na mchanganyiko wa Wayahudi na Watu wa mataifa, Rumi ilifikiwa na injili na mitume baada ya Yesu kupaa mbinguni, watu wengi wa mataifa waliokuwa wakisali katika kanisa la Rumi na Korintho, mwanzo walikuwa ni wapagani, wakijihusisha na ibada za sanamu, na hivyo baada ya kuipokea injili waliachana na upagani. Hata hivyo changamoto zilizokuwa zinalikabili Kanisa la Rumi, ndizo changamoto zilizokuwa zinalikabili Kanisa la Korintho.

#CHANZO CHA MIGOGORO JUU YA CHAKULA:

Kwa sababu kanisa lilikuwa linajumuisha Wayahudi na Wamataifa, hivyo mgogoro ulikuwa kati ya waumini wa Kiyahudi na waumini wa kimataifa.
Sasa hawa waumini wasio wayahudi zamani kabla ya kumpokea Yesu walikuwa Wanatoa sadaka kwa masanamu, kisha ile nyama ilikuwa inapelekwa Masokoni kwa ajili ya kuwauzia watu, lakini baada ya kumpokea Yesu wakaachana na ibada za sanamu, na hata nyama zilizokuwa zinauzwa masokoni wakawa hawanunui, kwa kuhofu zitakuwa zimeolewa sadaka kwa sanamu na hivyo watajitia unajisi ,matokeo yake wakawa wanakula mbogamboga tu.
Na Baada ya Paul kupata habari hizo juu ya huo mgogoro na ndipo anaandika waraka huu kwa Warumi. Na anaanza kwa kusema:

#Warumi 14:1-2
Yeye aliye dhaifu wa imani, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake.
Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.

Kwa hiyo Paul anawaambia mtu akiwa mdhaifu wa imani wamkaribishe, haijarishi anakula nyama au hali asihukumiwe kwa imani yake aliyonayo. Kwa sababu imani yake ameijenga kwa Mungu.
Ndipo sasa mgogoro ukainuka kanisani Wakristo wa kimataifa wakaanza kuwaona Wakristo wa Kiyahudi wamepotoka maana wanakula nyama zilizotolewa sadaka kwa sanamu, na Wayahudi nao wakawa wanawaona Wakristo wa kimataifa wamepotoka kwa kutokula nyama.

Lakini waumini wa Kiyahudi kwa sababu wao walikuwa hawajui historia ya zile nyama zinazouzwa masokoni, wao wakawa wananunua na kula, mbaya zaidi wakawa wanakula mbele za waumini wapya tena ndani ya mahekalu ya sanamu, na Paul anatoa onyo kwa kwa wale wanaokula nyama kwa kusema kwa dhamili zao:

# Warumi 14:22
Ile imani uliyo nayo uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiyejihukumu nafsi yake katika neno lile analolikubali.

# 1 Wakorintho 8:10
Kwa maana, mtu akikuona wewe uliye na ujuzi, umeketi chakulani ndani ya hekalu la sanamu, je! Dhamiri yake mtu huyo, kwa kuwa yu dhaifu, haitathibitika hata yeye naye ale vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu?

#1 Wakorintho 8:7-8
Bali ujuzi huu haumo ndani ya watu wote; ila wengine kwa kuizoelea ile sanamu hata sasa hula kana kwamba ni kitu kilichotolewa sadaka kwa sanamu; na dhamiri zao, kwa kuwa dhaifu, hunajisika.
Paul anawaonya wale waliokuwa wanajiona wapo imara katika imani kwamba si vizuri kufanya mambo hayo hadharani, itawafanya wale waumini wapya kudhoofika kiroho.

Hivyo ikawa waumini wakienda sokoni kununua nyama walikuwa wanaanza kuuliza kwa wauzaji je, hii nyama imetolewa sadaka kwa sanamu au la, Na ndio maana Paul anawaambia Kanisa la Korintho wakienda sokoni wasianze kuulizauliza kwamba nyama hii imetolewa sadaka kwa sanamu au la, bali anawaambia kwa sababu ya dhamili wanunue maana hawawezi ukapata majibu sahihi:
#1 Wakorintho 10:25
Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri;

Lakini kama mtu dhamiri yake haimruhusu basi asile maana atakuwa anatenda dhambi:
#Warumi 14:23
Lakini aliye na shaka, kama akila, amehukumiwa kuwa ana hatia, kwa maana hakula kwa imani. Na kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi.

Fikiria hata wewe mwenyewe hivi umeenda sokoni ukaanza kuuliza nyama hii ni kibudu? unamuuliza muuzaji Au nyama hii ni ya leo au ya jana? Unadhani atakupa majibu sahihi? Ni wachache sana watakao kwambia ukweli. Hata sisi wenyewe tunanunua nyama kwenye mabucha kwa sababu dhamiri zetu zinatutuma kwamba ni nyama sahihi, lakini kiuhalisia kuna nyama nyingi haramu zinauzwa katika mabucha na wengi tumezila, hata nyingine ni za matambiko. Isitoshe vipo vyakula vingi tunavyokula sasa na tuna vipenda, ambavyo laiti tungejua mazingira na jinsi vinavyo tegenezwa hatungependa kula vile vyakula.
Au ni mara ngapi umekula nyama ambayo hujui ni aina gani ya nyama au ni aina gani ya ndege?

Sasa hawa ndugu zetu wa Rumi na Korintho wakienda sokoni au wakialikwa mahali kwa mtu au katika sherehe, swali la kwanza walikuwa wanawauliza wahusika je, nyama hii imetolewa sadaka kwa sanamu? Wakiambiwa ndio basi hawali ile nyama..

Hivyo chanzo cha mgogoro ni juu ya ulaji wa nyama zilizo tolewa kafara kwa sanamu, ni makosa makubwa kutumia sura hii kuharalisha ulaji wa nguruwe, maana sio kiini cha mgogoro. Na haimaye Paul anatoa ushauri katika nyaraka zote mbili kwamba ni bora kuachana na ulaji wa nyama, ambao unasababisha migogoro ndani ya kanisa;

#Warumi 14:21
Ni vyema kutokula nyama wala kunywa divai wala kutenda neno lo lote ambalo kwa hilo ndugu yako hukwazwa.

#1 Wakorintho 8:13 Kwa hiyo, chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu.
 
Dhambi ya USHOGA Ni Sawa na DHAMBI ya kula Nguruwe ,panya,kenge ,na najisi nyingine

USHOGA NI NAJISI, NGURUWE NI NAJISI ,PANYA NI NAJISI, KENGE NI NAJISI, N.K

Nakupa Ushahidi wa kiamaandiko

Makosa ya kawaida Mungu anayaita Dhambi , ila Yale najisi anayaita MACHUKIZO ,

Ulaji Nguruwe unaitwa MACHUKIZO

Wakawi 11

7 Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu.

20 Tena vyote vitambaavyo vyenye mabawa viendavyo kwa miguu minne, hivi ni machukizo kwenu

KWA NABII ISAYA ANA GRUOP PIA ULAJI NAJISI KAMA MACHUKIZO

Isa 66:17 Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma ...

... wakila nyama ya nguruwe, na MACHUKIZO, na panya; watakoma pamoja, asema BWANA


USHOGA NI MACHUKIZO

Law 18:22

. Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni MACHUKIZO.


UMEONA KUNA DHAMBI NA MACHUKIZO

MUNGU anapozungumzia NAJISI ANAZIITA MACHUKIZO ,

USHOGA NA ULAJI NAJISI(NGURUWE,KENGE,N.K) NI SAWA

Kwa Mungu wote adhabu Ni moja
Umewahi kumsoma Cornelio? Yesu kafafanua vizuri kwamba kimuingiacho mtu hakiwezi kumtia unajisi maana chatoka kwenda chooni (Chakula), Bali kimtokacho mtu (mawazo) ndicho chaweza kumtia mtu unajisi.

Lakini pia imeshauriwa kuacha kula Kama kufanya hivyo kutamchukiza ndugu yako.
 
Umewahi kumsoma Cornelio? Yesu kafafanua vizuri kwamba kimuingiacho mtu hakiwezi kumtia unajisi maana chatoka kwenda chooni (Chakula), Bali kimtokacho mtu (mawazo) ndicho chaweza kumtia mtu unajisi.

Lakini pia imeshauriwa kuacha kula Kama kufanya hivyo kutamchukiza ndugu yako.
Yale Yale mnasoma Biblia Kama Gazeti , pia mnategemea kina Mwamposa,Gwajima ndio wawatafsirie Biblia ,mtapotea


Ishu ya Kornelio ,Ni Ndoto Kuhusu wayahudi(wasafi) na wamataifa(Najisi)

Nyie kwa Uroho wenu mmegeuza kichaka Cha kula mbwa,kenge,Mende,konokono,Nguruwe

NAOMBA NITOE ILO ANDIKO NA KUFAFANUA ,JAPO INAWEZA KUWA NDEFU ,NIWIE RADHI

#ALIVYOVITAKASA_ MUNGU_ USIVIITE_ WEWE_ NAJISI. #Matendo 10:15

Nawasalimu kwa jina la BWANA WETU YESU KRISTO.

Maono aliyooteshwa Petro mara nyingi yametumiwa na baadhi ya watu kuthibitisha kwamba ni halali kula chochote, kwa sababu kimeumbwa na Mungu.

#Matendo ya Mitume 10:15-16

Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, Vilivyotakaswa na Mungu, usiviite wewe najisi.

Jambo hili likatendeka mara tatu; kisha kile chombo kikapokewa tena mbinguni.

Sina dhana ya kupinga ulaji wa vitu najisi maana kama MTU alishaamua kupinda shingo ni vigumu kuinyoosha kwa kumkataza asile, bali nataka nipinge utumiaji vibaya wa Neno la Mungu.

Sasa wale wanaotumia fungu hili kwa kutetea ulaji wa nguruwe, kambare nk. Ni seme kwamba ni wapotoshaji wa maandiko. Maana hoja katika sura hiyo haihusiani na ulaji wa vyakula hata kidogo.

Ukisoma #matendo sura ya 10:1.... Inazungumzia habari za mtu mmoja anayeitwa #Kornelio, ambaye alikuwa Mrumi, Huyu ni mtu wa Mataifa hakuwa Myahudi.. Mtu huyu alikuwa mcha Mungu lakini alihitaji mtu wa kumfundisha vizuri na kumbatiza.

Mtu ambaye alikuwa karibu na Rumi ni Petro, ambaye alikuwa katika mji wa Yafa. Lakini sasa Petro alikuwa #Myahudi, na Wayahudi walikuwa hawachangamani na watu wa Mataifa waliwaona ni #NAJISI.

#Yohana 4:9 Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)

Kwa vyovyote Petro hangeweza kwenda kwa Kornelio, mtu wa mataifa, maana mtu ambaye alibainika akiwa anachangamana na watu wa Mataifa alikuwa anaonekana ni najisi na pia ilibidi atengwe, Kwa hiyo Petro alikuwa mwoga sana katika suala la kuchangamana na watu wa Mataifa kwa kuwaogopa Wayahudi wenzake: Na Paul anabainisha kwamba Petro alikuwa muoga kuchangamana na watu wa Mataifa.



#Wagalatia 2:11-12

Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu.

Kwa maana kabla hawajaja watu kadha wa kadha waliotoka kwa Yakobo, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa; lakini walipokuja wao, akarudi nyuma akajitenga, huku akiwaogopa waliotahiriwa.

hivyo lengo la Mungu ni kwamba kupitia yale maono AVUNJE utengano kati ya Wayahudi na watu wa Mataifa, maana Petro hangeweza kwenda bila KUVUNJA kwanza ule utengano. Na lengo la Mungu ni kumuokoa Kornelio ambaye ni mtu wa mataifa.

#HIVYO BASI: wale

#wanyama, ndege na wadudu ambao ni Safi waliashiria Taifa la Israeli, ambao walikuwa WAMETAHIRIWA

#Wanyama, ndege na wadudu najisi waliashiria watu wa Mataifa, ambao hawakuwa WAMETAHIRIWA.

#MAMBO YA #KUJIHOJI:

1. Kumbuka haya ni maono, si kitu halisi, kilichotumika hapa ni lugha ya picha, Mfano Nabii Daniel katika Danieli sura ya saba aliona maono na ndoto : Na katika maono haya aliona wanyama wanne wanatoka baharini wanyama hao ni Simba, Dubu, Chui, na mnyama wa kutisha. Sasa tukisema tuchukulie Maono/ ndoto kwamba ni kitu halisi; sasa jiulize ni lini Simba, Dubu na Chui wakaishi baharini?

2. Petro ni mwanafunzi aliyeishi na Yesu miaka mitatu na nusu, na ikiwa Yesu aliruhusu kula vitu najisi, Peto hangekataa kwa kusema:

#Matendo ya Mitume 10:14 …, Hasha, Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu au najisi.

3. Kauli ya Petro ya kusema: Hasha, Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu au najisi. Ni uthibitisho tosha kwamba Petro ambaye ni mtume wa Yesu alifahamu vitu najisi na visivyo najisi, na ndio maana alikataa kula.

4. Kauli ya Petro ya kusema: Hasha, Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu au najisi. Ni uthibitisho tosha kwamba Yesu hajawahi kuruhusu kula vitu najisi hadi anakufa. Na laiti kama Yesu aliruhusu, Petro hangekataa.

Na ndio maana Petro mwanyewe ijapokuwa aliona wanyama, ndege na wadudu, Lakini alijua yale ni maono tu, na hivyo alitaka kujua maana halisi ya yale maono: na wakati Petro anafikiria maana halisi ya yale maono, ndipo na mlango unagongwa, na wale watu waliotumwa na Kornelio wakaingia:

#Matendo ya Mitume 10:17 Hata Petro alipokuwa akiona shaka ndani ya nafsi yake, maana yake ni nini maono hayo aliyoyaona, wale watu waliotumwa na Kornelio, wakiisha kuiulizia nyumba ya Simoni, wakasimama mbele ya mlango,

Kwa hiyo Petro akawa ameshafahamu maana halisi ya yale maono kwamba yalimhusu Yeye kama Myahudi inabidi aende akachangamane na Familia ya Kornelio ambaye alikuwa ni mtu wa Mataifa.

Na ndio maana Petro baada ya kufika kwa Kornelio anathibitisha kwa kusema.

#Matendo ya #Mitume:10.28

Akawaambia, Ninyi mnajua ya kuwa si halali mtu aliye Myahudi ashikamane na mtu aliye wa taifa lingine wala kumwendea, lakini Mungu amenionya, nisimwite mtu awaye yote mchafu wala najisi.

#NOTE: Kwa hiyo kauli ile ya kusema:….., Vilivyotakaswa na Mungu, usiviite wewe najisi. #Matendo ya Mitume 10:15

Ilimaanisha kwamba kifo cha Yesu kilishaondoa utengano kati ya Waisrael na watu wa Mataifa, Hivyo Petro hapaswi kuwatenga watu wa Mataifa kwa kuwaona ni Najisi/ Hawafai, Maana Biblia inasema:

#Wagalatia 3:28 Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu.

Hivyo Mungu alitumia maono ya wanyama, na ndege na wadudu, kwa sababu Petro alifahamu kwamba Si kila kitu kinafaa kuliwa.

#NOTE: Sasa ili ujue kweli kwamba hoja kubwa ilikuwa ni utata wa kuchangamana na watu wa Mataifa, hebu tusome matendo sura ya 11, baada ya Petro kurudi Yerusalemu akitokea kwa Kornelio nini kilitoke:

#Matendo ya #Mitume 11:2-8

Na Petro alipopanda kwenda Yerusalemu, wale walio wa tohara wakashindana naye,

wakisema, Uliingia kwa watu wasiotahiriwa ukala nao.

Petro akaanza kuwaeleza kwa taratibu, akasema,

Nalikuwa katika mji wa Yafa, nikiomba, roho yangu ikazimia, nikaona maono; chombo kinashuka, kama nguo kubwa inatelemshwa kutoka mbinguni kwa pembe zake nne, kikanifikilia.

Nikakitazama sana, nikifikiri, nikaona wanyama wa nchi wenye miguu minne, na wanyama wa mwituni, nao watambaao, na ndege wa angani.

Nikasikia na sauti ikiniambia, Ondoka, Petro, ukachinje ule.

Nikasema, Hasha, Bwana, kwa maana kitu kilicho kichafu au kilicho najisi hakijaingia kabisa kinywani mwangu.

#Waweza #Endelea…….

Hivyo ndugu zangu mnaotumia aya hiyo ya matendo 10:15, kuwafundisha watu wale chochote kilicho mbele yao mnakosea sana na ikiwa kuna mtu amefundishwa hivyo basi jua ulidanganywa na hao walimu wa uwongo.

Na ikiwa kuna mtu amekuwa akiwafundisha watu kula vitu najisi kupitia aya hiyo, Nakusihi kwa mamlaka ya jina la Yesu uache maana unapotosha watu.

Yesu mwenyewe alitambua kuna chakula na visivyo liwa:

#Luka 11:11-12

Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka?

Au akimwomba yai, atampa nge?

Yesu amebainisha kabisa kwamba vipo vitu vingine sio vyakula na haipaswi watu wapewe, ina maana #Jiwe sio chakula, #Nyoka sio chakula, #Nge sio chakula:

Hivyo ukimuona mtu anakula nyoka , Panya, Nguruwe, Kambare, Nge NK. Jua ni tamaa zake, na uchu wa chakula, na sio agizo la Mungu.

Kwa hiyo wale mnaosema Kimwingiacho mtu hakimtii unajisi, bali kimtokacho, basi fikirieni pia kauli hiyo ya BWANA YESU. Lakini pia fikirieni juu ya mlevi anayekunywa pombe, maana naye inamwingia kinywani na inaenda kutoka chooni.

Mtume Paul naye anasema si kila kitu kinafaa kuliwa:

1 #Wakorintho 10:23 Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo.

Ni kweli vitu vyote ni halali kwa sababu vimeumbwa na Mungu, lakini sio kila kitu kimeumbwa kwa lengo la kuliwa, maana vingine havijengi mwili bali vinabomoa mwili.

Pia Paulo anasema: 1 #Wakorintho 10:31 Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.

Sasa ikiwa unataka kujua ni Chakula gani ukila ni kwa utukufu wa Mungu? Basi Nenda:

#Kumbukumbu la Torati 14:4-8

Wanyama mtakaokula ni hawa ng'ombe, na kondoo, na mbuzi,

kulungu, na paa, na kongoni, na mbuzi wa mwitu, na paa mweupe, na pofu, na mbuzi wa mlima;

na kila mnyama aliyepasuliwa ukwato, ukapasuka ukwato wake zikawa mbili, naye ni mnyama mwenye kucheua akatafuna tena, katika wanyama wote, ndiye mnyama mtakayemla.

Lakini, hawa msile katika wale wenye kucheua, na hao waliopasuliwa ukwato; ngamia, na sungura, na kwang'a, kwa kuwa hucheua, lakini hawakupasuliwa kwato, ni najisi kwenu;

na nguruwe, kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui, huyu ni najisi kwenu msile nyama zao, wala mizoga yao msiiguse.

Hivyo maana halisi ya maono haya MUNGU alikuwa anataka kuondoa dhana potofu kwa Petro ya kuwaona watu wa Mataifa ni NAJISI, hawafai kuokolewa.

Jambo la msingi pia: IKIWA Yesu aliruhusu ulaji wa nguruwe, bila shaka Petro hangekataa kula maana ameishi na Yesu miaka mitatu na Nusu. Hivyo kwa jibu la Petro la kusema Kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu au najisi inaonesha Petro hajawahi kula nguruwe, wala Yesu hajawahi kuruhusu kula nguruwe?

Ikiwa Petro ambaye ndiye mtume mkubwa anasema hajawahi kula vitu vichafu, je wewe unamfuata mtume gani anayeruhusu kula vitu najisi?
 
Kwa kuwa sisi ni wakristo ni kwamba sisi tunafata nyayo za Yesu Kristo, Ni vipi kitu ambacho hakusema Yesu Kristo kinawekewa mabano ya kuweka uchambuzi wa maono ya waliotafsiri biblia ? mbaya zaidi kuna biblia hata hayo mabano hayamo, uchambuzi umeunganishwa kuonekana ni maandiko matakatifu yaliyokuwemo kwenye biblia.

Kimuingiacho mtu hakimtii unajisi ni jibu alilotoa Yesu baada ya kuulizwa kwanini wanafunzi wake waliokuwa na njaa walikula mahindi wakiwa njiani bila kuosha mikono, kwa sheria walizojiwekea viongozi wa mda huo waliona kwamba kula bila kuosha mikono kunamtia mtu unajisi, Yesu ndipo akawasahisha kwamba sheria zao hazipo sawa na kwamba kula bila kuosha mikono hakumtii mtu unajisi... sasa Je hapa kulikuwa na haja ipi ya watafsiri kuongeza maneno yao kwamba maana yake ilikuwa ni karuhusu kula vyakula ambavyo havikutakaswa kama mijusi, kenge na nguruwe wakati kilichokuwa kinazungumziwa ni kula bila kuosha mikono ??

Wasabato walipuuzia hayo mabano maana hayakuwa maneno ya Yesu na kazi ya watafsiri sio uchambuzi, wakristo wengine wakadhani ni Yesu kawapa kibali wakaona ni ruksa ya kula chochote.

Sasa najiuliza kwamba mbwa, konokono, vinyonga, kunguru, paka, chunusi, kobe, n.k wanaweza kuliwa ?

Mfano kuna samaki na wanyama wana sumu ama huleta madhara wakiliwa na wakawekwa kwenye kundi la vyakula visivyofaa, Mungu alikosea kusema hawatakiwi kuliwa ?

Halafu pia nashangaa Biblia za sikuhizi za kiswahili zimeunganisha hayo maneno bila kuweka mabano, ni wazi kabisa wakristo wengi wanaamini haya maneno yalikuwemo bila kujua kuna uhuni umefanyika kuyaunganisha, maskini mweee!! Mtu anabisha mpaka mishipa inamtoka shingoni kwasababu ya mistari iliyopachikwa ambayo haikuwahi kuwepo, ni ujanja ujanja tu ukafanyika kupachika
Kula hakumpeleki mtu motoni. Kuna dhambi za msingi kabisa za kuzikimbia. Sio kula kitimoto au chochote.
 
Nyinyi wasabato na ndugu zenu katika imaan, pigeni kelele weee! Mpaka mchoke.

Linapokuja suala la huyu mdudu 🐖 aisee siwezi kuwaelewa kamwe.
 
Kula hakumpeleki mtu motoni. Kuna dhambi za msingi kabisa za kuzikimbia. Sio kula kitimoto au chochote.
UKISOMA SURA HII ,UTAONA KUNA MOTO KWA WALA NGURUWE NA DHAMBI/MACHUKIZO MENGINE ,WOTE JEHANUM


Dhambi ya USHOGA PIA Ni Sawa na DHAMBI ya kula Nguruwe ,panya,kenge ,na najisi nyingine

USHOGA NI NAJISI, NGURUWE NI NAJISI ,PANYA NI NAJISI, KENGE NI NAJISI, N.K

Nakupa Ushahidi wa kiamaandiko

Makosa ya kawaida Mungu anayaita Dhambi , ila Yale najisi anayaita MACHUKIZO ,

Ulaji Nguruwe unaitwa MACHUKIZO

Wakawi 11

7 Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu.

20 Tena vyote vitambaavyo vyenye mabawa viendavyo kwa miguu minne, hivi ni machukizo kwenu

KWA NABII ISAYA ANA GRUOP PIA ULAJI NAJISI KAMA MACHUKIZO

Isa 66:17 Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma ...

... wakila nyama ya nguruwe, na MACHUKIZO, na panya; watakoma pamoja, asema BWANA

USHOGA NI MACHUKIZO

Law 18:22

. Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni MACHUKIZO.

UMEONA KUNA DHAMBI NA MACHUKIZO

MUNGU anapozungumzia NAJISI ANAZIITA MACHUKIZO ,

USHOGA NA ULAJI NAJISI(NGURUWE,KENGE,N.K) NI SAWA

Kwa Mungu wote adhabu Ni moja
 
Nyinyi wasabato na ndugu zenu katika imaan, pigeni kelele weee! Mpaka mchoke.

Linapokuja suala la huyu mdudu [emoji241] aisee siwezi kuwaelewa kamwe.
SIO WASABATO NI MUNGU KUPITIA NABII ISAYA



Isa 66:17 Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma ...

... wakila nyama ya nguruwe, na MACHUKIZO, na panya; watakoma pamoja, asema BWANA
 
Kula hakumpeleki mtu motoni. Kuna dhambi za msingi kabisa za kuzikimbia. Sio kula kitimoto au chochote.
UNABISHANA NA MAANDIKO?

TENA UKIANZA AYA YA KWANZA ANASEMA ANAONGEA NA WATU WASIOITWA KWA JINA LAKE(WAMATAIFA)


Isaya 66:17 Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma ...

... wakila nyama ya nguruwe, na MACHUKIZO, na panya; watakoma pamoja, asema BWANA


SHIDA MNATAKA MWAMPOSA,GWAJIMA, MWAKASEGE, ZUMARIDI,MTUME BILIONEA, MZEE WA UPAKO ,NA MATAPELI WENGINE NDIO WAWASOMEE MAANDIKO NA KUWATAFSIRIA
 
Back
Top Bottom