Wakristo wenye wadada wa kazi wa Kiisilamu acheni kuwanyanyasa kwasababu ya kufunga Ramadhani

Wakristo wenye wadada wa kazi wa Kiisilamu acheni kuwanyanyasa kwasababu ya kufunga Ramadhani

BAKIIF Islamic

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2021
Posts
600
Reaction score
1,843
Fikiria kutokula au kunywa wakati wa mchana kwa siku 30 mfululizo moja kwa moja sio jambo jepesi. "Mtazamo wa mwezi huu kimsingi sio kujizuia au kufunga, bali ni mkusanyiko wa nguvu na akili ya Muislamu juu ya utambuzi wa Mwenyezi Mungu na maisha ya ibada ya uchamungu."

Haipendezi bint wako wa kazi unamkataza kufunga kwakuwa familia yako hapo ni ya kikristo, unamkataza kujistiri na kuvaa ushungi kwasababu hupendezwi na mavazi hayo, hata sehemu ya kuswalia unamkataza asifanye ibada katika nyumba yako.

Vyema kumruhusu binti wa kazi kurudi nyumbani kwao kila mwezi wa Ramadhani ikiwa unakerekwa na yeye kufunga akiwa hapo nyumbani kwako, wengine mnawalazimisha waende kanisani na kudiriki kwenye maombezi ya kukemewa, na ibada mbalimbali za Kikristo hapo nyumbani mkijua kabisa huyu ni binti wa Kiisilamu.

Imani hailazimishwi bali inatengenezwa kwa namna wewe utavyomtendea na kumpa uhuru na kuamini kile anacho kiamini, na kumfanyia wema katika mahitaji yake ya ibada ikiwemo kumnunulia nguo ya sikukuu kama unavyofanya kwa watoto wako wakati wa pasaka, kisha kazi kwako itakuwa kumshawishi kwa hoja za ki-maandiko ili aikubali imani yako nasio vinginevyo.


WhatsApp Image 2022-04-08 at 11.59.49 PM.jpeg
 
Maisha magumu haya binti wa kazi anataka apewe bajeti ya 30K kwa ajili ya futari na daku kwa siku,wakati wa kufuturu anataka mazagazaga kama yupo Muscat,mara tende,harua na vyakula laini laini.

Waajiri wachache wa kikristu ndio wanaweza kuwapa futari ya uhakika kwa mabinti wao wa kazi.

Wengi wetu bora liende sio kwa ubaya ila mifuko iko mitupu.
 
Ni ngumu sana kuishi nyumba ya mtu ambaye hamko Imani sawa hata Kama ni ndugu tu, maana dini zote zinafundisha kwamba hakikisha walionyumbani kwako wanaamini kama wewe.

Ni vyema kwenda kufanya kazi kwa mtu ambaye unajua kabisa Imani ziko sawa ili kuepusha migongano.

Au kama ni Imani tofauti basi hakikisheni mnawekeana utaratibu kabla ya kuingia mkataba na Kila mtu anauridhia
 
Dah....., Uko Sawa. Ni Kama Vile Waislamu Wengine Kipindi Cha Mfungo Kuwalazimisha Wengine Wote Wafunge sio Sawa.

Mifano ipo nimeiweka akiba wapi Wanalazimisha!
Hairuhusiwi muislamu kumlazimisha mkristo kufunga wakati wa mfungo, utampa chakula chake kama kawaida na hata wakati wa kufuturu vyema na yeye aje afuturu hata kama ni mkristo, nasio wakati wa kufuturu ajifungie ndani au mumtenge, ispokuwa katika nchi za kiisilamu inatarajiwa kwamba hata wasio Waislamu wafuate sheria za kufunga hadharani. Unaruhusiwa kula, kunywa na kuvuta kwa faragha nasio hadharani.
 
Japokuwa ni stori ya kubumba ikisindikizwa na picha ya kugoogle, nyani haoni kundule. Waislam wanapowazuia wakristo kula popote hususani migahawani kule Zanzibar yenyewe ni haki na hii ya kumlisha mtoto mdogo ni haramu?

Pamoja na brainwashing tuliyopitia waafrika yatupasa kutumia maarifa ya kuzaliwa nayo--- hiyo ni ajira ya mtu na iko wazi watoto kama huyo kwenye picha yako feki hawafungi, je ulitaka nani amlishe kama si huyo aliyejitoa kuifanya hiyo kazi kwa ujira anaolipwa?

Na hii akili ya kuzuia hadi mama nitilie kupika au kule hadharani kule Zanzibar imeshirikisha ubongo kweli au ndio tatizo la brainwashing in the name of religion?
 
Hairuhusiwi muislamu kumlazimisha mkristo kufunga wakati wa mfungo, utampa chakula chake kama kawaida na hata wakati wa kufuturu vyema na yeye aje afuturu hata kama ni mkristo, nasio wakati wa kufuturu ajifungie ndani au mumtenge, ispokuwa katika nchi za kiisilamu inatarajiwa kwamba hata wasio Waislamu wafuate sheria za kufunga hadharani. Unaruhusiwa kula, kunywa na kuvuta kwa faragha nasio hadharani.
Ndiyo kinachofanyika kwenye majumba ya waislamu?
Nenda Zanzibar tu hapo, mtu ni mkristo na ananyumba yake lakini haruhusiwi kula mchana kwa kuwa amezungukwa na waisilamu.

Hakuna muisilamu anayeweza kumruhusu hausegirl wake alete kitimoto nyumbani na apikie vyombo vya bosi wake.
 
Ukishaenda kwenye nyumba ya mtu na Imani yako lazima mgongano wa kidini utokee tu
 
Kuna ukweli hapo kweli? Ama ni njia ya kutafta huruma?
 
Si
Maisha magumu haya binti wa kazi anataka apewe bajeti ya 30K kwa ajili ya futari na daku kwa siku,wakati wa kufuturu anataka mazagazaga kama yupo Muscat,mara tende,harua na vyakula laini laini.

Waajiri wachache wa kikristu ndio wanaweza kuwapa futari ya uhakika kwa mabinti wao wa kazi.

Wengi wetu bora liende sio kwa ubaya ila mifuko iko mitupu.
Sio kweli ndugu yangu,tunafuturu vyakula vya kawaida sana na kulingana na uwezo wa mtu,uji wa kawaida sababu ya tumbo kukaa mda mrefu bila kula kitu,hapo unaweza kula ugali wali na n.k,

Vingine vinavyofata ni uwezo wa muhusika
 
Maisha magumu haya binti wa kazi anataka apewe bajeti ya 30K kwa ajili ya futari na daku kwa siku,wakati wa kufuturu anataka mazagazaga kama yupo Muscat,mara tende,harua na vyakula laini laini.

Waajiri wachache wa kikristu ndio wanaweza kuwapa futari ya uhakika kwa mabinti wao wa kazi.

Wengi wetu bora liende sio kwa ubaya ila mifuko iko mitupu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ndiyo kinachofanyika kwenye majumba ya waislamu?
Nenda Zanzibar tu hapo, mtu ni mkristo na ananyumba yake lakini haruhusiwi kula mchana kwa kuwa amezungukwa na waisilamu.

Hakuna muisilamu anayeweza kumruhusu hausegirl wake alete kitimoto nyumbani na apikie vyombo vya bosi wake.
Zanibar huko mbali mbna? Hapa hapa Dar.
 
Back
Top Bottom