Wakuu hebu tumalize utata hapa, INDUCTION COOKER vs MULTICOOKER nani ni mkombozi wa mapishi kwa umeme

Ukiwa na microwave, pressure cook, Blackstone, jiko la gesi lile la umeme na oven kwa pamoja .na gunia moja la mkaa miasha utayaona rahisi sanaa. Umeme sahizi wa kumwaga tuachana na mikaa watanzania.
 
Kwa haya maelezo, aisee watu wanapigwa sana. Kuna jamaangu anajikuta mtoto wa town sana, anayo kama hiyo ameweka mtoa mada, siku zote anaita ni induction cooker, kiufupi tu mwanangu alipigwa, 😁 asante sana mkuu Mamaya
 
Ila ninaamini asilimia kubwa humu tuko kwenye matumizi ya kuni, mkaa na kidogo gas ingawa wengi wanaigiza ili waonekane sio wanyonge kama sisi tulivyo.
Hapana! Watumiaji wa kuni hata huko vijijini ni wachache wengi wanatumia gesi au mkaa, nyumba za kisasa si rafiki tena kwa matumizi ya kuni na mkaa.
 
Asee nili nunua hiki kini saidie na kujaza jaza gas ila naona sufuria yake ni kama alitakiwa kubaki na kitu baada ya kupikia inabidi niamishe nioshe na kuifuta vizuri maana ina wai kupata kama kutu ivi . Au nme pigwa apa
 

Attachments

  • 1.jpg
    17.5 KB · Views: 8
  • Screenshot_20241011_174223_Google.jpg
    151.5 KB · Views: 9
Asee nili nunua hiki kini saidie na kujaza jaza gas ila naona sufuria yake ni kama alitakiwa kubaki na kitu baada ya kupikia inabidi niamishe nioshe na kuifuta vizuri maana ina wai kupata kama kutu ivi . Au nme pigwa apa
Hii itakua Kenwood feki
 
Mult cooker ni nzuri kwa ajili ya kupikia vyakula vya muda mrefu ie maharagwe, makongoro, utumbo.

Induction cooker nzuri sana maana haipotezi umeme
Siyapendi makongoro. Kuna mtu anapika kwake ayo makwato?
 
Kuongezea hapa pressure cooker inasaidia kwenye vitu vinavyochukua muda kama Maharage, ukiweka Maharage kwenye Gesi ama jiko la umeme ni gharama sana.
Unaweza ukatumia pressure cooker kwenye umeme, gesi au hata mkaa, kuna pressure cooker ambazo ni sufuria sio directly electrical kwahio unaweka kwenye moto sababu sufuria lipo sealed trapped steam inaharakisha mapishi...
 
Wanasema mashine zinaharibu nguo ni kweli?
 
Wanasema mashine zinaharibu nguo ni kweli?
5% ndiyo.
Kwa mfano mapambo yaliyobandikwa kwa gundi, visikizo vya chuma na lebel dhaifu hung'oka.

Kama nguo umezitumbukiza kwa mchanganyiko wa aina za nguo bila kuzichambua mf: shuka, net, mashati na suruali kwa pamoja husokotana na baadhi katika msuguano huo mashine inapofanya kazi huchanika ama kukatuka.

Inashauriwa kufua nguo zenye mtindo mmoja, kama ni suruali, ziwe suruali tu usichanganye na mashati, pia shuka zifuliwe peke yake.

Nguo za ndani ndiyo unaweza changanya na soxy pamoja na Tshirt.

Ukishazoea kufua kwa kutumia mashine hauwezi kuacha, ni nzuri sana inarahisisha maisha.

Halafu mashine za kisasa ni energy sever hazitumii umeme mwingi, mimi nguo zenye uzito wa kg 20-30 hufua kwa nusu unit tu.
 
Asante kwa maelezo,kumbe suala la umeme katika hizi mashine sio la kuhofia kabisa
 
Asante kwa maelezo,kumbe suala la umeme katika hizi mashine sio la kuhofia kabisa
Usihofie mkuu, hasa kama una familia ya watu 4 ama 6, waweza kufua pamoja na kukausha kwa unit2 tu kwa mwezi.

Maana tunavaa na kurundika kwenye ma dust bin tukisubiri mpaka yajae, hapo tayari unakuwa umeshafika mwezi.

Siku ya kufua inakuwa ni moja tu mzigo mkubwa wa kg 20-30 kutoa.
 
Safi sana nimepata wazo la kuwa nayo,bei zake zikoje kwa unavyojua?
 
Natumia inductio. na Pressure coocer familia ya watu 6 na natumia unit4 kwa siku,


Unit 4 ? Mmhh ndogo sana mbona, in a day mimi natumia unit 14 hadi 16 na situmii umeme kupikia ni AC LG dual inverters za 12,000 BTUs 3 na 18,000 BTUs ya sebuleni plus 1 freezer kubwa double door and 1 fridge kubwa double door, + 1 LG washing and drying machine 20kg/12kg front load, of course na taa zote za usiku..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…