Wakuu Msaada: Biashara haiendi ghafla, nifanyeje?

Wakuu Msaada: Biashara haiendi ghafla, nifanyeje?

Ushapigwa mazingaombwe....

Watu wakija wanaona kama DUKA LA MKAA VILE.... AU DUKA LA MAJANI YA KULISHIA NG'OMBE VILE 😏😏😏
 
Wewe jamaa ni mjinga usiyejielewa. Mara umesema duka analiendesha single mother uliyezaa naye na wewe huhusiki! Hapohapo unasema kijana amekupa taarifa mara mzigo umeingiza mpya?! Nchi hii ina wajinga wengi sana alisikika Masai mmoja aitwaye Godwin Mollel mnamo mwezi wa Februari Mwaka 2023
Mkuu Hata kiswahili Cha kidato Cha tatu ulifeli?.

Mwandishi ana mbinu mbalimbali za uandishi.


Nakurahishia wee kilaza kuelewa.


Nilikua na Mwanamke ,nilimkuta ni mtalaka.


Nikawa naye, baadae akabeba ujauzito.


Bahati mbaya wakati wa kujifungua Kuna shida mtoto alipata.


Sasa kuepusha usumbufu wa kuombwa Hela Kila Mara.

Nikajipanga ,Nikafungua Duka hili la nguo., Nikamwambia. usimamie ,kwaajili ya mtoto wetu .


Nikamuwekea kijana awe muuzaji,, ila muda mwingi autumie Kwa mtoto wetu .Yeye pia Huwa anaenda Kila siku Jion na wikiendi anashinda muda wote.


Sasa Mzigo wa Duka Huwa ni lazima Mimi ndio niagize, Mimi ndio nifate, au kama kutumwa, utumwe niupokee Kisha niwapelekee Dukani... Umenielewa bwana Kilaza !!.


Kwa Ivo, mambo yote yanapotokea lazima nijuzwe.


Kwa akili yako hii, Wacha tu CCM ya MsogaGang, iendelee kutunyoosha.
 
Chuma ulete hiyo......

Nenda kwa Mwamposa nunua maji ya upako au mafuta ya upako uje umwagie hapo...........utakuja kutoa ushuhuda mwenyewe humu.
Mkuu Mwamposa alikuja Mkoan , Bidada alinunua Katoni Moja la maji, na mafuta vichupa vitano.

Ila hamna kitu Mkuu, sio kwamba namsemea vibaya Mwamposa.
 
Shusha bei
Mkuu inawezekana Moja ya Sababu nayopatia watejani bei ndogo.


Huwa nawaambia wauze bei ya kawaida, inafikia wakati, wauzaji wengine wanakuja Kumzodoa kijana ,kwamba kwann anauza bei ndogoo!!.



Kwa mfano..Msimu Huu wa Mfungo wa Kiislam, Niliwambia washushe bei ya mavazi yote ya Kiislam , kuanzia wakubwa mpaka watoto.
 
Pole sana ila uliwahi kuwakumbuka wazazi hivi karibuni? Sadaka unatoa? Ulishajihusisha na hawa wachungaji wa mchongo?
Bidada hapo Kwa wachungaji wa mchongo anawafagilia sana.

Kuna kipindi mpaka akaagiza mafuta upako kutoka Kenya.
 
Ni Duka langu la Nguo , Sasa Wiki ilopita Niliingiza Mzigo Mpya , katika hali isiokawaida Mara nyingi Nikishaleta Mzigo Mpya , nikiwapigia wateja wangu, Huwa Ndani ya Siku Mauzo nikaribuu 150K


Kijana ananiambia Alikuja Jiran ( Jiran naye ana frame pemben ya Huduma yake) akamuomba elfu Kumi, na alipompa tu Toka hapo Hajauza .

Mara ananiambia, Kuna Mwanamke Alikuja kama mteja, akaishia kushika shika Nguo weee akasepa, tokea hapo Biashara imesimama.


Wakuuu ,hamna Mauzo toka Ijumaa mpaka Leo Jumanne, hamna hata Mia, Mzigo Mpya, Kila mtu akija anausifiaaa Sanaa, lkn anaishia kusema nitarudi ila harudiii.

Wakuuu hata Mia, hata Miaaa!!


Au niamin tu ni hali,,,, ndio Kuna Siku Mauzo yanakua kiduchu ila huwez kosa Hata 30K.


Naondoaje Hili Jinamizi ?? ... Ni Duka ambalo niliamua kulifungua Kwa ajili ya Mwanamke ( Singo mama, nilizaa naye ) hivo nikalifungua ila Kila kitu anakisimamia yeye maana mtoto wetu alipata shida fulan ivi ivo sikutaka zile simu za mara Kwa mara za Hela .


( Huyo jamaa alomuomba Kijana elfu Kumi, ni rafiki wa aliyekua Mume wa Singo mama huyu nlozaa naye, na huyu alokua Mume amekua akimtangaza na kumuombea mabaya sana huku akisema Biashara yenyewe itafungwa tuu, Jamaa ana cheo Kwa tawi Moja la vya Dola, amekua anamchomea sana utambi Hadi mpaka TRA inafikia wakati wanataka kutuongezea Kodi bila sababu za msingi. ).
Mkuu umesha tengenezwa hapo biashara ukifanya mchezo utalifunga hilo duka lako la nguo.Nitafute kwa wakati wako ili niweze kupatengeneza upate wateja wengi tu.
 
Back
Top Bottom