Wakuu, nimekuta mil 300 kwenye Bank account yangu - sizijui!

Wakuu, nimekuta mil 300 kwenye Bank account yangu - sizijui!

Naomba ushauri tu, leo nimekuta Mil 300 zimo kwenye account yangu ya Benki - Sijui zilikotoka sasa naomba ushauri kwenu:

1. Niripoti bank yangu kwamba kuna mzigo sijui ulikotoka
2. Nikae kimya kwanza kusikilizia
3. Nianze kuzitumbua
4. Nizihamishe fasta kwenye acc nyingine
5. Nizitoe zote nikae nazo home, sababu wanaweza ku-trace kama nikiweka kwenye acc yangu nyingine?

Wazoefu naombeni ushauri wenu - nimedata hata kazi nashindwa kufanya - Jina la Benki naliweka kapuni kwa sasa.
Twende tubamie ughaibuni, tukutane airport faster unasubiri nini
 
Nilitaka nikushauri hata ununue kitu nje ulipe kwa card yako lakini nikaona ni prosesi sana
Hiyo account nilishaiunganisha na visa - Mastercard....huwa natumia kununulia vitu toka nje....wazo lilikuja nihamishe mzigo wote kwenye acc ya nje ya ndugu yangu...roho ikasita
 
Hiyo account nilishaiunganisa na visa - Mastercard....huwa natumia kununulia vitu toka nje....wazo lilikuja nihamishe mzigo wote kwenye acc ya nje ya ndugu yangu...roho ikasita
Tena iyo ndio nzuri
 
Bado atatiwa katka mikono salama, kwa kuwa kama ni mchongo wa staff wa bank husika ni lazima itakuwa wanaifuatilia muda wote, kwa hiyo ukitia tu upawa kuchota tayari wanakudaka.
Nimexheka sana, " ukiiitia upawa kuchota"
 
Huu uzi wa kazi gani kama pesa ni ndogo? Haya warudishie
Kuna mdau aliniambia nihame nchi...niende China nikawambia nina famiia na nimewekeza TZ - hii nalo likawa kikwazo.
Dola laki moja na ushee ni mzigo mkubwa na nilikuwa nautamani mno.
 
Yes, kuna mdau pia kanitonya hivyo kwamba ikifika mwisho wa siku leo wanaweza kuzitoa - ndiyo maana nataka nikazitoe kabla ya siku kuisha... Kuna mdau kasema kwamba nijilipue - kufa ni mbele kwa mbele ila nasita -sita roho inagoma.
Bang mbaya sana
 
Hiyo account nilishaiunganisha na visa - Mastercard....huwa natumia kununulia vitu toka nje....wazo lilikuja nihamishe mzigo wote kwenye acc ya nje ya ndugu yangu...roho ikasita
Kwahiyo hujaamua chakufanya? na bado imo?
 
Kimeumana mafisadi wanaficha fedha kwenye account za wanyonge!
 
Naomba ushauri tu, leo nimekuta Mil 300 zimo kwenye account yangu ya Benki - Sijui zilikotoka sasa naomba ushauri kwenu:

1. Niripoti bank yangu kwamba kuna mzigo sijui ulikotoka
2. Nikae kimya kwanza kusikilizia
3. Nianze kuzitumbua
4. Nizihamishe fasta kwenye acc nyingine
5. Nizitoe zote nikae nazo home, sababu wanaweza ku-trace kama nikiweka kwenye acc yangu nyingine?

Wazoefu naombeni ushauri wenu - nimedata hata kazi nashindwa kufanya - Jina la Benki naliweka kapuni kwa sasa.
Toa taarifa kwa Manaje wa tawi lako kuhusu ingizo kwenye akaunti yako ambalo hakulitarajia, Meneja atakusaidia kujua kama watendaji kwenye Benki hiyo wametega bomu ambalo wewe kwa tamaa zako utaingia kichwa kichwa.

Kukaa kimya haiwezi kukusaidia maana nyayo za mtandaoni huwa hazifutiki, sana utakuwa umeshiriki wizi wa mtandaoni ambao wewe hukupanga. Inawezekana huko Benki wahudumu wasio waaminifu wanaifahamu mienendo ya miamala ya akaunti yako na wameiotea kufanya uhalifu, kubana kama kobe siku wakikomba akiba yako yote kwenye akaunti hiyo,hutakuwa na uhalali wa kulalamika kuwa salio lako limeibiwa.

Kuhamisha pesa kwenda akaunti nyingine kwa pesa isiyokuwa halali kimsingi utakuwa umeshiriki pia kutakatisha pesa haramu, kuziweka nyumbani kwako au kuzitumia bado siku akiingia CAG mpya hata baada ya miaka mingi kupita, aibu itakupata.
 
Bashiru kaweka huko baada ya kuiba 180B na kukosa pakuweka
 
Wewe ungekuwa una milioni Mia tatu kwenye akaunti yako halafu ghafla zikatoweka ungefanyaje?
 
Back
Top Bottom