Rabonn
JF-Expert Member
- Nov 7, 2018
- 5,789
- 11,106
Ndio chief....alizaliwa nikiwa mwaka wa pili chuo..nilikua at 22 yrs plus nilimuanzisha shule mapema sanaaaMiaka 33 una mtoto anaingia sekondari?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ndio chief....alizaliwa nikiwa mwaka wa pili chuo..nilikua at 22 yrs plus nilimuanzisha shule mapema sanaaaMiaka 33 una mtoto anaingia sekondari?
Kawaida si anaingia mwakani,yaani mwaka huu yupo darasa la Saba,Miaka 33 una mtoto anaingia sekondari?
Wewe kugombea ubunge misungwi si unaogopa wachawi,Epuka hiyo roho ya kujilinganisha na wengine kwa sababu kila mtu ana safari yake.
Mimi nina ma classmates wana majumba mpaka Dubai na Amerika lakini nami niko kivyangu napambana. Wengine ni vigogo huko serikalini wanajichotea tu mahela wamejenga mahekalu kila kona hapa mjini na wanasukuma ma Vogue. Na mimi hata Corolla ya mchongo sina. Na umri umeenda sana!
Ukijilinganisha na watu utapata msongo wa mawazo kwa maana lazima kutakuwa na watu wanaokuzidi tena mbali mno.
Na ajabu tukijilinganisha na wengine kamwe huwa hatujilinganishi na wengi tuliowazidi (ukiachilia mbali wenzetu wengi waliotangulia mbele ya haki). Huwa naona ni kama vile huwa tunamkosea Mungu kwa kukosa shukrani kwa kutufikisha hata hii hatua tuliyofikia...
Kama ni lazima kujilinganisha basi kufanyike kwa lengo la kujipatia motisha tu wa kupambana na si vinginevyo.
Una afya nzuri. Una gari. Unajenga...Una kazi...Bado uko kwenye 40s.
God has been good to you and you are blessed. Just keep hustling [emoji1545]
😂😂 niombee ninayemdate ndo aje kuwa faza mjengoUmri wako?? Tukuombee Nini?,,,,,Trako?,kazi?,mume?mtoto?
Siyo tunakuombea kumbe hats 20yrs bado haujafika
Mie nina 35yrs hapa nikifikia 45+ndiyo nikimiliki kitanda na godoro vyatosha yaani maisha nitakuwa nishayapatia.
Kyai Kya motoMiaka 33 una mtoto anaingia sekondari?
Mtu upo hai halafu unasema huna chochote, wewe ni timamu kweli ?Nakumbuka nilihitimu chuo nikiwa umri mdogo tu wa miaka 24 kasoro miezi kadhaa. Kwa enzi zile za JK sikuwa na shida sana ya kupata ajira kwahiyo nilianza ajira kwenye sekta binafsi siku chache tu baada ya mtihani wa mwisho chuo ilikuwa Julai.
Pia tangu nikiwa chuo nilikuwa nikijishughulisha sana na madili ya town kwahiyo kiukweli haikuwa shida kupata sehemu ya kujishikiza. Ile ajira niliifanya nikiwa na malengo ya kuja kujiajiri muda sio mrefu.
Wakati naanza kazi nikasema ndani ya miaka mitano lazima niwe na masters, nyumba nzuri, gari na ule mwaka wa sita naoa. Kwa hesabu za haraka ilikuwa nikiwa na miaka 29 niwe nimefikia hizo ndoto.
Kiukweli kwenye ile miaka mitano nilikutana na dhoruba nyingi sana ikiwemo kufeli karibu kila kitu nilichojaribu kwenye biashara kwasababu ajira niliacha ndani ya mwaka mmoja na nusu.
Nakumbuka kwenye hiyo miaka mitano nilipata admission ya kusoma Masters UDSM ila changamoto ikawa ada. Kuhusu nyumba na gari nilikubaliana na ukweli kwamba haiwezekani. Nikaona nitazame suala la mke. Huko pia nilifeli.
Wakati naelekea kutimiza miaka 30 ndo angalau ramani zikaanza kunyooka. Gari nikanunua nikiwa na 33yrs. Nyumba bado haijaisha.
Kimsingi nakaribia 40 ila hakuna uhalisia wa zile ndoto zangu za wakati ninatoka chuo. Kwa wananchi wengi wanaona niko poa ila binafsi naona muda unazidi kuchanja mbuga na ndoto za kushika kibunda zikiwa bado kutekelezeka.
Ninawashauri wote wenye changamoto ya umri kwenda huku hawajafikia malengo wazidi kupambana. Mbona Babu wa Loliondo alitoboa akiwa kikongwe?
Bro wewe ndo nikushangae kama uko timamu!!!.. kwahiyo ukiwa na pumzi hutakiwi kufanya mambo mengine na kujisahihisha ulipokosea?Mtu upo hai halafu unasema huna chochote, wewe ni timamu kweli ?
Unafikiri hiyo pumzi ya uhai ni jambo dogo
Relax... huu uzi ni wa kutiana hasira pia. 😄😄Uzi huu kila mtu atakuwa na nyumba nzuri na gari na familia ila ndoto yake itakuwa kitu kingine ili kujikweza tu.
Mijitu mingi miongo miongo 😂🤣
Miaka 33 una mtoto anaingia sekondari?
Afu kuna mimi sasa nna 36yrs sina chochote hapa napambana nikifika kwenye 45yrs niwe nakula goodtime tuBora ww ata una pagale na gari unayo,kuna wengine km walivyomaliza chuo ndio wako hvyo hvyo na ngoma ishagonga 40....
Haina shida, nakuelewa sana na kiufupi ni wakati sahihi wa kuwa hivyo na hata zaidi. Ni vile tu wengine 40+ hata nusu ya hapo bado.Pole sana halikua lengo mkuu ila kiukwel wengi sana tuna stress za maisha...unaweza usinielewe ila tuko njia moja
Jf bana[emoji1787]Aisee pole sana na hiyo ndio dunia.
Sema nimekuja kugundua kwamba malengo watu tunatofautiana sana pia mitazamo jinsi tunavyoya pima maisha ndio maana wengine wanapokuona umepiga hatua wewe unajiona bado sanaaaaaa.
Binafs stress za umri pia zinanitafuna sana na kama isingekua huyu Mungu inawezekana ningetafuta ushirikina.
Kwangu kuwa na nyumba wala gari sioni kama ni hatua kivile.Nina nyumba ya kisasa tu na kagari pia nina watoto wa4 wanasoma wa kwanza anaingia form 1 mwakani na yoote haya yote nikiwa ndio nafunga 33 years.
Ila kwangu ndoto kubwa inayonifanya nijione kama nimechelewa sana ni ku establish buznes empire..hilo tu na kwa umri huu wa 33 najina kama nishazeeka tayat japo najitia moyo kwamba Mungu atanisaidia tuu...Kikubwa ni kuomba baraka na mkono wa Mungu utusaidie tusikate tamaa na kujikinai
Ujue kinachonitafuna sana mimi ni ile hali ambayo tumekua tukiishi nayo wengi kwamba mtu anakua na pesa kwa vipindi flan tuuu..mfano kwa mfanya kazi ni kile kipindi. Ha mishahara...katika harakat zangu za ujasiriamali kuna kipindi mtu unafulia balaa buzness zinakua sio za uhakika kila kitu kinasuasua mpaka inafika hatua elfu 20 inakua adimu 😂😂😂sasa maisha haya ndio naonava ufala kwann mtu usifike hatua unakua na pesa anytime uko full.??Haina shida, nakuelewa sana na kiufupi ni wakati sahihi wa kuwa hivyo na hata zaidi. Ni vile tu wengine 40+ hata nusu ya hapo bado.
Naaam kamandaJf bana[emoji1787]
Kikubwa na cha kushukuru hapo ni hao watoto wanne aliowapata mapema,gari ni nini??? Si combo cha usafiri tu hajasema ni gari gani kuna gari nyingi tu zinauzwa milio 10,au nane hata tano...Unamiliki gari na nyumba bado una-complain,,,we jamaa hemu piga goti chini daily mshukuru Mungu.
Hii ni katika kujipa courage tu mzee ila life is serious sio masihara..so wewe usipokua serious kuumia nje njeLife is temporary,dont take it much serious