Wale ambao wana stress ya umri kwenda huku hawana chochote, tukutane hapa

Wale ambao wana stress ya umri kwenda huku hawana chochote, tukutane hapa

Kikubwa na cha kushukuru hapo ni hao watoto wanne aliowapata mapema,gari ni nini??? Si combo cha usafiri tu hajasema ni gari gani kuna gari nyingi tu zinauzwa milio 10,au nane hata tano...
Imeandikwa tuzaliane tuujaze ulimwengu,,,bado anatakiwa kushukuru kwa kumiliki vitu visivyomilikiwa na wengi...coz watoto wanazaliwa bro.
 
Wewe kugombea ubunge misungwi si unaogopa wachawi,
Kugombea ubunge sitatoboa mjukuu wangu. Wataniua asubuhi na mapema labda kama uliko unafahamu madawa makali ya Msumbiji na Malawi huko nikomae nayo...

Na unahitaji angalau bilioni tatu hivi kwa ajili ya kuhonga wapiga kura kama ni ubunge. Sasa shida yote ya nini hii mjukuu?
 
Epuka hiyo roho ya kujilinganisha na wengine kwa sababu kila mtu ana safari yake.

Mimi nina ma classmates wana majumba mpaka Dubai na Amerika lakini nami niko kivyangu napambana. Wengine ni vigogo huko serikalini wanajichotea tu mahela wamejenga mahekalu kila kona hapa mjini na wanasukuma ma Vogue. Na mimi hata Corolla ya mchongo sina. Na umri umeenda sana!

Ukijilinganisha na watu utapata msongo wa mawazo kwa maana lazima kutakuwa na watu wanaokuzidi tena mbali mno.

Na ajabu tukijilinganisha na wengine kamwe huwa hatujilinganishi na wengi tuliowazidi (ukiachilia mbali wenzetu wengi waliotangulia mbele ya haki). Huwa naona ni kama vile huwa tunamkosea Mungu kwa kukosa shukrani kwa kutufikisha hata hii hatua tuliyofikia...

Kama ni lazima kujilinganisha basi kufanyike kwa lengo la kujipatia motisha tu wa kupambana na si vinginevyo.

Una afya nzuri. Una gari. Unajenga...Una kazi...Bado uko kwenye 40s.

God has been good to you and you are blessed. Just keep hustling [emoji1545]
[emoji120] Simba ..... Be blessed mkuu

Hili Jambo la kijinga sna mm Kuna jmaaa tumesoma nao Basi kila wakt wannitafuta kujua maendeleo yangu Niko Wapi nafanya nn yaani huwa sipendi jmaaa linakupigia tu na kukuambia fln Yuko HV Mara yule jamaa mwingine Ni head master Mara jamaa fln amenunua gar Sasa huyu jamaa najiuliza HV anadhani mm nitamuambia niniacho hiki au kile bas namuacha tu atiririke

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Sasa kumbe watu mna magari na mapagale mnataka mpewe nini gunia la chawa? ndio mshukuru?

Shukuruni kwa mlivyonavyo na mna michongo

Kuna watu hapa 35 zinagonga hakuna ramani Wala mchongo wowote.

Asubuhi anatoka home hajui anaenda wapi.

Ukiona wewe umetoka home unajua unakoenda shukuru Sana.
Kuna jamaa nampta alikuna kupata kazi akiwa na around 39 HV ndio anaingia mzigoni na hapo alikuwa hajaoa mungu Ni mwema san

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Bro wewe ndo nikushangae kama uko timamu!!!.. kwahiyo ukiwa na pumzi hutakiwi kufanya mambo mengine na kujisahihisha ulipokosea?
Kitendo tu cha kuwa hai na unavuta pumzi hadi dakika hiyo ni mafanikio tosha. Kama unahisi mafanikio ni suala la kiuchumi, niambie leo Mansq Musa na utajiri wake yuko wapi, Nabii Suleiman yuko wapi ?

Jifunze kumshukuru Mungu kwa kila khali unayopitia. Sawa ?
 
Epuka hiyo roho ya kujilinganisha na wengine kwa sababu kila mtu ana safari yake.

Mimi nina ma classmates wana majumba mpaka Dubai na Amerika lakini nami niko kivyangu napambana. Wengine ni vigogo huko serikalini wanajichotea tu mahela wamejenga mahekalu kila kona hapa mjini na wanasukuma ma Vogue. Na mimi hata Corolla ya mchongo sina. Na umri umeenda sana!

Ukijilinganisha na watu utapata msongo wa mawazo kwa maana lazima kutakuwa na watu wanaokuzidi tena mbali mno.

Na ajabu tukijilinganisha na wengine kamwe huwa hatujilinganishi na wengi tuliowazidi (ukiachilia mbali wenzetu wengi waliotangulia mbele ya haki). Huwa naona ni kama vile huwa tunamkosea Mungu kwa kukosa shukrani kwa kutufikisha hata hii hatua tuliyofikia...

Kama ni lazima kujilinganisha basi kufanyike kwa lengo la kujipatia motisha tu wa kupambana na si vinginevyo.

Una afya nzuri. Una gari. Unajenga...Una kazi...Bado uko kwenye 40s.

God has been good to you and you are blessed. Just keep hustling [emoji1545]
Kweli kabisa mkwe wanasema ukitaka kujua neema zako na kabla hujajilinganisha na mtu bas muangalie Alie chini Yako ndo utajua kuwa nawe umebarikiwa
 
Daa mada tamu Sana we unasema umiliki gari wakati wengine tuliwaza kumiliki anga we acha tu pesa Haina umri Bali pale inapokukuta unafanya wonders

Cha msingi KUEPUKA stress don't compare yourself with others, each and every one has different question paper, wengine wameandaliwa maisha kwa kurithi Mali, wengine wameweka mizizi mikali.
 
f78c5832-d169-4795-a153-91925e4762ce.jpg
 
Kugombea ubunge sitatoboa mjukuu wangu. Wataniua asubuhi na mapema labda kama uliko unafahamu madawa makali ya Msumbiji na Malawi huko nikomae nayo...

Na unahitaji angalau bilioni tatu hivi kwa ajili ya kuhonga wapiga kura kama ni ubunge. Sasa shida yote ya nini hii mjukuu?
Bora hiyo bilion tatu tukalime nyanya tu,. Wajumbe si watu wazuri

Waganga ni waongo
 
Aisee pole sana na hiyo ndio dunia.
Sema nimekuja kugundua kwamba malengo watu tunatofautiana sana pia mitazamo jinsi tunavyoya pima maisha ndio maana wengine wanapokuona umepiga hatua wewe unajiona bado sanaaaaaa.

Binafs stress za umri pia zinanitafuna sana na kama isingekua huyu Mungu inawezekana ningetafuta ushirikina.
Kwangu kuwa na nyumba wala gari sioni kama ni hatua kivile.Nina nyumba ya kisasa tu na kagari pia nina watoto wa4 wanasoma wa kwanza anaingia form 1 mwakani na yoote haya yote nikiwa ndio nafunga 33 years.

Ila kwangu ndoto kubwa inayonifanya nijione kama nimechelewa sana ni ku establish buznes empire..hilo tu na kwa umri huu wa 33 najina kama nishazeeka tayat japo najitia moyo kwamba Mungu atanisaidia tuu...Kikubwa ni kuomba baraka na mkono wa Mungu utusaidie tusikate tamaa na kujikinai
huwa nakuona upo blessed mbaya haswa kwa familia brother 😁😁

Mengine Mungu atanyoosha 🙏🏽🙏🏽
 
Epuka hiyo roho ya kujilinganisha na wengine kwa sababu kila mtu ana safari yake.

Mimi nina ma classmates wana majumba mpaka Dubai na Amerika lakini nami niko kivyangu napambana. Wengine ni vigogo huko serikalini wanajichotea tu mahela wamejenga mahekalu kila kona hapa mjini na wanasukuma ma Vogue. Na mimi hata Corolla ya mchongo sina. Na umri umeenda sana!

Ukijilinganisha na watu utapata msongo wa mawazo kwa maana lazima kutakuwa na watu wanaokuzidi tena mbali mno.

Na ajabu tukijilinganisha na wengine kamwe huwa hatujilinganishi na wengi tuliowazidi (ukiachilia mbali wenzetu wengi waliotangulia mbele ya haki). Huwa naona ni kama vile huwa tunamkosea Mungu kwa kukosa shukrani kwa kutufikisha hata hii hatua tuliyofikia...

Kama ni lazima kujilinganisha basi kufanyike kwa lengo la kujipatia motisha tu wa kupambana na si vinginevyo.

Una afya nzuri. Una gari. Unajenga...Una kazi...Bado uko kwenye 40s.

God has been good to you and you are blessed. Just keep hustling [emoji1545]
Maneno ya hekima kabisa. Asante Docta.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
huwa nakuona upo blessed mbaya haswa kwa familia brother 😁😁

Mengine Mungu atanyoosha 🙏🏽🙏🏽
Kuhusu family honestly sina cha kusema brother..ila hayo mengine sasa...nimekaa juz namwambia shemej ako kwamba after 6 tutakua tunapaswa ku inject almost 10M kwa mwaka kwa ajili ya malipo ya ada tu kwa watoto hapo mengine weka kando..na hapo unasomesha vishule vya kawaida tu hiv... sasa imagine ndio na umri ushasogea na ishu hazielewi hapo liku ag 50..si unaweza ukajitundika?
 
Back
Top Bottom