Mimi najuta sababu nimeharibiwa future yangu na huu upuuzi .
Nimekulia dasalam sehemu ya ushuani hasa zama hizo za baba wa taifa , nikasoma nje baada ya mzee kupelekwa huko nje .
Nikala kitabu mpaka nikapata proffession yangu huku mzee akiwa bado yuko ofisini .
Tukazaliwa wawili mimi na sister yangu sikujua kupika wala kufua sio mimi tu hata dada yangu .
Nikalelewa kizungu ujinga ukanijaa nikahitimu masomo nikala kazi mapema sana hapa bongo , ushenzi ukaanza pale kazini nilipokutana na majungu nikawa mtu wa kufyumu na kupotezea namaanisha nimeacha kazi mara sita ya saba haitotokea maana mzee ashatangulia mbele za haki nikijiroga yatanikuta [emoji3]
Nilianza kunywa pombe nikiwa na miaka kumi na nne , leo hii pombe imenighalimu sana yaani kwasasa nimepelekwa vijijini sana kisa pombe kuzidi kazini mpaka nhamishiwa vijijini kama adhabu .
Mzee hakunijenga kama mwanaume ili niweze kuendeleza mali zake , kadanja kamuacha bi mkubwa naye bi mkubwa baadae kadanja hivi navyoongea sina mali ya mzee niliyorithi zaidi ya elimu tu na gari lake la kitambo na nyumba hiyo ya ushuani (nayo sister naona kama vile ataiuza alafu mimi aniteme maana naye mtata tu )
Ukiniuliza hata sielewi maana mama alisema sijui ni nini basi nimeishia tu kuwaona ujombani wakiwa na maisha bora baada ya mama kufa hivyo najua walichukua kila kitu .
Sina maisha ya kuungaunga ila sasa nawaza ningeandaliwa misingi ya kuwa mwanaume kweli basi hata leo ningekuwa na mali nyingi ila ndiyo hivyo nimebaki kupaangalia nyumbani tu kama mgeni maana hata kwa kwenda sijui ni wapi ujombani au kwa akina baba maana mimi siwaelewi na wao hawanielewi sababu wazazi hawakuwa na ukaribu na ndugu zao kabla ya kifo yaani ule ukaribu wa sisi labda kamsalimie bibi mara uncle hayo hayakuwepo
Sijui kufua wala kupika na umri huu wa sitini kasoro .
Ngono nimeanza kufanya na miaka kumi na mshua alikuwa anajua ila anaishia kusema be care .
Oyaa ngoma nimepona tu kwa vile wazungu wengi ngoma hawana sio kama hapa kwetu .
Nilileta ukishua vijijini kwa watu nikaozeshwa ndoa ya mkeka [emoji3] na sasa niko na mwanamke ila ukiniuliza niliwahi kuwaza kuoa sijui hata kama hilo wazo liliwahi nijia .
Naishi kwa akili za mwanamke maana yeye ameyajua madhaifu yangu hivyo kadi ya benki na mahitaji ya kiume yote utoa yeye baada ya kuninyang'anya kadi ya benki baada ya kunishtaki kwa wakubwa .
Kutokuwekewa misingi ya maisha halisi yalivyo kumenifanya baada ya mzee kufariki nijichanganye sana na jamii ya watoto wa uswazi yaani Keko , Tandika , Temeke , Mwananyamala , Mburahati huniambii chochote na hunidanganyi chochote .
Sijaambulia maarifa ya maisha zaidi walinifunza kuvuta bangi na mwisho wakawa machawa wangu ila sasa nilishawatema .
Nakunywa pombe mpaka sijielewi na kuacha nawaza japo sio leo [emoji848]
Ni nyumba tu iliyoko huko ushuani ndiyo natamba nayo kuwa hapa ndiyo kwetu ila ushua wa kwetu changanya na uzungu basi nilikuwa kama mbwa wa kisasa aliyekosa matunzo baada ya wazee kutangulia .
Nachofurahia kazi ninayoifanya naipenda japo kabla sijalewa nikilewa wewe pita kule .
Nipende kuwaasa wazazi na walezi , uwe na hela usiwe na hela pambana sana umlee mtoto katika mazingira ambayo yanaendana na jamii itakayomzunguka wewe ukiwepo na usipokuwepo .
Uzungu ukizidi mtoto unamuharibu leo ukiwepo na kesho usipokuwepo .
Nawasalimu wanangu wa nguvu advocate
Pascal Mayalla , kaka mkubwa
GENTAMYCINE , mkubwa
mdukuzi bila kumsahau mwamba
Abiola