Wale wa Bwiru Boys: Tukumbushane maisha na mikasa ya Bwiru

Wale wa Bwiru Boys: Tukumbushane maisha na mikasa ya Bwiru

Tuliwahi kugoma tunadai msosi mbaya, kumbe nia ni kuongezewa siku za wali skuli.

Jamaa akatusoma akatuelewa, Siku tumeandamana mpaka ofisini kwake na mabango yetu asubuhi asubuhi anatutimua akasema turudi skuli atakuja huko huko.

Mwisho wa siku akaja akatuchana live kuwa tunagomea jambo la kipuuzi, wanafunzi ni wapuuzi na waalimu wetu nao ni wapuuzi.

Tulichoka.
Teh teh teh teh
Hahahahaha! Nimekumbuka....Mliungana na dada zetu (Advance)...Wameondoka shule asubuhi wamerudi saa 12 jioni wamechooka...Wameshindishwa nje ya ofisi ya Olenjolay...Issue pia ilikuwa kutaka chakula kizuri........Kweli jitihada zao zilisaidia, baada ya hapo tukawa twaletewa samaki mara mbili kwa wiki...siku za ubwabwa + nyama pia zikaongezeka...
 
Hahahahah.....Imagine! Yaani mwenyekiti wa kamati ulinzi na usalama ya mkoa mnamletea uvunjifu wa amani kwa sababu ya kukosa wali maharage?! Bora hata kesi ya kukosa disco na Bwiru girls......mambo ya wanafunzi sometimes very interesting!
He he he he
Ndio hivyo mkuu, na utoto unakuwemo humo humo.

Nyakati hizo siasa hazikuwa zinafahamika sana kama saa hivi.

Kwa hiyo hata chain of command inakuwa hamuwezi kuifuata pindi linapotokea tatizo.
Cha msingi shida yenu itatuliwe hata kama ni Rais wa nchi.
 
Hahahahaha! Nimekumbuka....Mliungana na dada zetu (Advance)...Wameondoka shule asubuhi wamerudi saa 12 jioni wamechooka...Wameshindishwa nje ya ofisi ya Olenjolay...Issue pia ilikuwa kutaka chakula kizuri........Kweli jitihada zao zilisaidia, baada ya hapo tukawa twaletewa samaki mara mbili kwa wiki...siku za ubwabwa + nyama pia zikaongezeka...
Ha ha ha ha
Ina maana ile fuso ya samaki liyokuwa inaleta sangara pale Boys ilikuwa ikitoka Boys inakunja mpaka Gilrs kushusha mzigo??

Mtushukuru sana nyie watoto wa kuwaletea neema kwa "ujinga wetu"
 
Hahahahaha! Nimekumbuka....Mliungana na dada zetu (Advance)...Wameondoka shule asubuhi wamerudi saa 12 jioni wamechooka...Wameshindishwa nje ya ofisi ya Olenjolay...Issue pia ilikuwa kutaka chakula kizuri........Kweli jitihada zao zilisaidia, baada ya hapo tukawa twaletewa samaki mara mbili kwa wiki...siku za ubwabwa + nyama pia zikaongezeka...
Daah, mlikua mnapewa mpaka nyama. Miaka minne ya boys nakumbuka nilikula nyama mara moja na mnofu mmoja tu tena siku ya graduation.
 
Ha ha ha ha
Ina maana ile fuso ya samaki liyokuwa inaleta sangara pale Boys ilikuwa ikitoka Boys inakunja mpaka Gilrs kushusha mzigo??

Mtushukuru sana nyie watoto wa kuwaletea neema kwa "ujinga wetu"
Ndio, ilikuwa ikishusha mzigo kwenu inaingia kwetu...kiroho safi..
Mbarikiwe kwa kujitoa kwakweli.
 
Ndio, ilikuwa ikishusha mzigo kwenu inaingia kwetu...kiroho safi..
Mbarikiwe kwa kujitoa kwakweli.
He he he he
sasa mbona hamkuomba hata siku moja ka disko ka kutupongeza kwa kazi nuri tuliyoifanya??
 
Nakumbuka maisha ya Bwiru Boys miaka hiyo ilikuwa full mikasa.

Kulikuwa na eneo linaloitwa Mombasa, mahali ambapo vijana wa Boys walikuwa wanazama kuwapiga chabo mabinti wa girls pindi wanaoga.
Sehemu hii ilikuwa maarufu sana maana upande wa Ziwa waiokuwa wanautumia wasichana wa Girls maarufu kama "mende" ulikuwa unatenganishwa na upande wa boys kwa kilima fulani hivi kina mawe ya hatari, lakini vijana walikuwa wana risk life kwenda kula chabo.

Nakumbuka ishu ya headmaster wetu kupindi hicho kulikuwa na tetesi kuwa anapita na mistress wa Nganza, sasa kimbembe kilikuwa ole wenu siku ya debate au bugi(disko) mtoe pendekezo la kuwaleta Bwiru Girls, headmaster ataahirisha hata hilo disko, ila mkimletea mabinti wake wa Nganza, hata usafiri atawapa free.

Nakumbuka misemo maarufu kama kuguga likimaanisha kupiga msuli au kusoma, msemo kama kugenya likimaanisha kufariki, msemo kama fororo ukimaanisha uji usio na sukari, msemo kama mnyambo ukimaanisha mtu mwenye tabia za ubaguzi na kujisikia sikia , msemo kama kudabo ukimaanisha kudrudia msosi mara mbili, form one wakiitwa nguruwe na mingineyo mingi.

Nakumbuka pia visa vya mwanafunzi mmoja alikuwa shombe shombe alikuwa bingwa wa kupita na wake za maticha, mpaka akazaa na mke wa ticha mmoja hivi(Jina tunalihifadhi), akazaa kijana shombe shombe na kuleta mtikisiko mkubwa sana kwenye ndoa ya ticha wetu.

Walimu kama Mazebele, Rung'wecha, Begenyeza, Kissuu, Mchizi Mox, Massaba(R.I.P), Ruhiye(R.I.P) na wengineo wengi.

Nasikia pia kuwa hata Founder wa Forum hii muheshimiwa sana Maxence Mello ni product ya Luthuli Domitory pale njia ya kuelekea ukarani na alikuwa ngugi kweli kweli(just kidding).

Tukumbushane life ya Bwiru aisee.

12651326_10201448336607019_3786303634314722495_n.jpg
Bwiru Boys ya wakati huo ilikuwa moto! Headmaster Mkwizu akitokea Mazengo aliipaisha sana shule, combination moja tu PCM Vifaa vya kutosha na Workshops za maana! Ufaulu ukawa juu sana! Madukwa, Makula, Mlanda, Mauma, Maganga, Mwl Mazebele na kigugumizi chake alikuwa poa sana hao ni baadhi ya walimu, wengi wametangulia mbele ya haki wengine wakihama na kustaafu!
Nakumbuka mengi ya shule yangu hii! Max alikuwa mwaka mmoja nyuma yetu!
 
Bila
Bwiru Boys ya wakati huo ilikuwa moto! Headmaster Mkwizu akitokea Mazengo aliipaisha sana shule, combination moja tu PCM Vifaa vya kutosha na Workshops za maana! Ufaulu ukawa juu sana! Madukwa, Makula, Mlanda, Mauma, Maganga, Mwl Mazebele na kigugumizi chake alikuwa poa sana hao ni baadhi ya walimu, wengi wametangulia mbele ya haki wengine wakihama na kustaafu!
Nakumbuka mengi ya shule yangu hii! Max alikuwa mwaka mmoja nyuma yetu![/QUOBila kumsahau Tosili hahahahaa

Bila kumsahau Tosili
 
Ha ha ha ha
yap yule ticha namkumbuka sana, Kanifundisha Brickwork and Masonry yule.
Mpaka nikalamba banda.

Siku hizi yuko Musoma Tech, amechoka sana.
Kawa mlevi wa gongo kupindukia, na anastua kwenye vile vilabu vya uswazi tu.
Nimekutana naye mara kibao.
Mwalimu nani pale Musoma Tech? Maana kuna mwalimu Muganyizi baadae akarudi Boys na kustaafia pale.

Amejenga jirani na shule kuke kijijini!

Pia Chigugu mnamkumbuka? Hahahaaa Bwiru Boys hatari sana!

Nilienda pale miaka ya 2000 katikati nikamkuta mkuu mpya anaitwa Kisuu, Mnyaturu flani, tukabadilishana namba jioni tukakutana SPAROW maeneo ya Ghana kula kilaji!

Aisee anazimeza sana. Ni mtu poa sana!

Dah nimepamisi Mwanza for real!
 
Bwiru Boys ya wakati huo ilikuwa moto! Headmaster Mkwizu akitokea Mazengo aliipaisha sana shule, combination moja tu PCM Vifaa vya kutosha na Workshops za maana! Ufaulu ukawa juu sana! Madukwa, Makula, Mlanda, Mauma, Maganga, Mwl Mazebele na kigugumizi chake alikuwa poa sana hao ni baadhi ya walimu, wengi wametangulia mbele ya haki wengine wakihama na kustaafu!
Nakumbuka mengi ya shule yangu hii! Max alikuwa mwaka mmoja nyuma yetu!
Safi sana mkuu.
Kumbe umesoma enzi za Mkwizu??

Ulikuwa electrical au Mechanical au Civil??
 
Back
Top Bottom