Walimu jiongezeni maarifa mitandaoni kabla ya kuingia Darasani maana wanafunzi wenu wanawaona vilaza mkijongea hapo ubaoni na kushika chaki

Walimu jiongezeni maarifa mitandaoni kabla ya kuingia Darasani maana wanafunzi wenu wanawaona vilaza mkijongea hapo ubaoni na kushika chaki

Rorscharch

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2013
Posts
878
Reaction score
2,014
Kwa kizazi hiki cha kidigitali, kama mwalimu unaendelea kufikiri kwa mtazamo wa kianalogia, ni wazi kwamba wanafunzi wako watakudharau sana. Fikiria, unawafundisha kuwa kuna sayari tisa, lakini wao wakigoogle wenyewe wanagundua kuwa zipo zaidi ya 1,000. Unategemea watachukulia masomo yako kwa uzito gani? Kwanini usijitahidi kuendana na wakati na kuepuka kuonekana kilaza?

Hivi unajua kwamba baadhi ya wanafunzi wako tayari wanaitumia ChatGPT na teknolojia nyingine za kisasa? Lakini wewe bado unashindwa kujiimarisha na kujifunza mbinu mpya za kufundisha? Kwanini wasikuone kama mfano wa kale kila unapojongea ubaoni? Siku hizi, watoto hawakusikilizi kwasababu tu ya mamlaka yako au ukali, wanakusikiliza kwa sababu kile unachowafundisha kinagusa akili na maslahi yao.

Ninakumbuka mfano mmoja wa mtoto wa mjomba wangu, ambaye amekuwa akilelewa na baba yake msomi mwenye upendo mkubwa wa vitabu. Mtoto huyu, sasa yupo darasa la saba, lakini ana shauku kubwa ya kusoma vitabu vya astronomia. Nilimfanyia majaribio madogo kuhusu mada tofauti za anga za juu – ambayo nilikuwa nimegugulisha – na kwa mshangao wangu, kila kitu alikuwa anakielewa kwa undani. Mtoto huyu, aliyekuzwa katika mazingira ya elimu ya nyumbani, anaonekana kuwa mbele zaidi kuliko walimu wengi wanaomfundisha shule.

Sasa wewe unapeleka watoto English Medium, wanajifunza kwa kukariri tu, wakati msingi wa elimu bora huanzia nyumbani. Unajiitaje mzazi wa mtoto msomi ilhali huna hata shelf moja ya vitabu nyumbani? Ni wakati wa kubadilika – si kwa walimu tu bali pia kwa wazazi! Tukumbuke, elimu bora huanzia katika mazingira tunayowapa watoto wetu. Tubadilike!
 
Kwa kizazi hiki cha kidigitali, kama mwalimu unaendelea kufikiri kwa mtazamo wa kianalogia, ni wazi kwamba wanafunzi wako watakudharau sana. Fikiria, unawafundisha kuwa kuna sayari tisa, lakini wao wakigoogle wenyewe wanagundua kuwa zipo zaidi ya 1,000. Unategemea watachukulia masomo yako kwa uzito gani? Kwanini usijitahidi kuendana na wakati na kuepuka kuonekana kilaza?

Hivi unajua kwamba baadhi ya wanafunzi wako tayari wanaitumia ChatGPT na teknolojia nyingine za kisasa? Lakini wewe bado unashindwa kujiimarisha na kujifunza mbinu mpya za kufundisha? Kwanini wasikuone kama mfano wa kale kila unapojongea ubaoni? Siku hizi, watoto hawakusikilizi kwasababu tu ya mamlaka yako au ukali, wanakusikiliza kwa sababu kile unachowafundisha kinagusa akili na maslahi yao.

Ninakumbuka mfano mmoja wa mtoto wa mjomba wangu, ambaye amekuwa akilelewa na baba yake msomi mwenye upendo mkubwa wa vitabu. Mtoto huyu, sasa yupo darasa la saba, lakini ana shauku kubwa ya kusoma vitabu vya astronomia. Nilimfanyia majaribio madogo kuhusu mada tofauti za anga za juu – ambayo nilikuwa nimegugulisha – na kwa mshangao wangu, kila kitu alikuwa anakielewa kwa undani. Mtoto huyu, aliyekuzwa katika mazingira ya elimu ya nyumbani, anaonekana kuwa mbele zaidi kuliko walimu wengi wanaomfundisha shule.

Sasa wewe unapeleka watoto English Medium, wanajifunza kwa kukariri tu, wakati msingi wa elimu bora huanzia nyumbani. Unajiitaje mzazi wa mtoto msomi ilhali huna hata shelf moja ya vitabu nyumbani? Ni wakati wa kubadilika – si kwa walimu tu bali pia kwa wazazi! Tukumbuke, elimu bora huanzia katika mazingira tunayowapa watoto wetu. Tubadilike!
Sayari kwenye mfumo wetu wa solar zipo 9 ndio, labda kama unaonhelea za nje wa mfuno wa Solar, ambapo idadi yake ni infinite, yaa trillions to the power of trillions bado ni ndogo..
 
Nafundisha kulingana na muongozo wa ufundishaji sio kulingana na google
We nyumbani kwako mwambie ajaze sayari 10000 mi nitamwambia kulingana na kitabu
Fundisha kutokana na muongozo lakini pia jua zaidi ya huo muongozo unasema nini maana ili yakiibuka ya kuibuka usikimbilie kuchapa watoto za watu eti kisa tu wanajua zaidi yako wewe unaona wanakuletea dharau
Utaheshimikaje kwa kumwambia mtoto kuna "four states of matter" wakati yeye kaangalia ukurutu wa taarifa kutoka wanasayansi mashuhuri wakitaja "states" zaidi ya hapo?
 
Sayari kwenye mfumo wetu wa solar zipo 9 ndio, labda kama unaonhelea za nje wa mfuno wa Solar, ambapo idadi yake ni infinite, yaa trillions to the power of trillions bado ni ndogo..
Correction: zipo 8, ya 9 ambayo ni Pluto imeshushwa hadhi na sio sayari tena tangu 2006
 
Unaamini kuna mwanafunzi wa huku Sanu Guwang atakua anatumia chat gpt?
 
Fundisha kutokana na muongozo lakini pia jua zaidi ya huo muongozo unasema nini maana ili yakiibuka ya kuibuka usikimbilie kuchapa watoto za watu eti kisa tu wanajua zaidi yako wewe unaona wanakuletea dharau
Utaheshimikaje kwa kumwambia mtoto kuna "four states of matter" wakati yeye kaangalia ukurutu wa taarifa kutoka wanasayansi mashuhuri wakitaja "states" zaidi ya hapo?
Hii ni dhana umeijenga akilini mwako
Kifupi huwa natambulisha mada kwa kuwauliza wanafunzi kile wanajua kabla sijasema kile muongozo wa elimu na sera ya elimu vinataka wajue kwa hiyo nikikuta anajua zaidi nafurahi na kumjenga zaidi mtoto na nikikuta hawajui hata kidogo Wala hainifurahishi
 
Hata akijua sayari ziko milioni,hazimsaidii lolote,akishazijua anafanya nazo nini,
Mfundisheni basi ata kusimamia biashara ya mihogo/duka/kampuni inafanyaje kazi na inasimamiwa vipi na biashara kwa ujumla inataka nini,
Ama mpeni elimu ya vitendo lakini mambo ya kusoma kila kitu cha theory alafu iwe kitu gani
 
Hata akijua sayari ziko milioni,hazimsaidii lolote,akishazijua anafanya nazo nini,
Mfundisheni basi ata kusimamia biashara ya mihogo/duka/kampuni inafanyaje kazi na inasimamiwa vipi na biashara kwa ujumla inataka nini,
Ama mpeni elimu ya vitendo lakini mambo ya kusoma kila kitu cha theory alafu iwe kitu gani
Huyu dogo akiwezeshwa akapata hata scholarship anaweza kufuata ndoto yake na kuwa astronaut, kwanini afanye biashara ya mihogo wakati ana ndoto ya kuishi Mars
 
Kwa kizazi hiki cha kidigitali, kama mwalimu unaendelea kufikiri kwa mtazamo wa kianalogia, ni wazi kwamba wanafunzi wako watakudharau sana. Fikiria, unawafundisha kuwa kuna sayari tisa, lakini wao wakigoogle wenyewe wanagundua kuwa zipo zaidi ya 1,000. Unategemea watachukulia masomo yako kwa uzito gani? Kwanini usijitahidi kuendana na wakati na kuepuka kuonekana kilaza?

Hivi unajua kwamba baadhi ya wanafunzi wako tayari wanaitumia ChatGPT na teknolojia nyingine za kisasa? Lakini wewe bado unashindwa kujiimarisha na kujifunza mbinu mpya za kufundisha? Kwanini wasikuone kama mfano wa kale kila unapojongea ubaoni? Siku hizi, watoto hawakusikilizi kwasababu tu ya mamlaka yako au ukali, wanakusikiliza kwa sababu kile unachowafundisha kinagusa akili na maslahi yao.

Ninakumbuka mfano mmoja wa mtoto wa mjomba wangu, ambaye amekuwa akilelewa na baba yake msomi mwenye upendo mkubwa wa vitabu. Mtoto huyu, sasa yupo darasa la saba, lakini ana shauku kubwa ya kusoma vitabu vya astronomia. Nilimfanyia majaribio madogo kuhusu mada tofauti za anga za juu – ambayo nilikuwa nimegugulisha – na kwa mshangao wangu, kila kitu alikuwa anakielewa kwa undani. Mtoto huyu, aliyekuzwa katika mazingira ya elimu ya nyumbani, anaonekana kuwa mbele zaidi kuliko walimu wengi wanaomfundisha shule.

Sasa wewe unapeleka watoto English Medium, wanajifunza kwa kukariri tu, wakati msingi wa elimu bora huanzia nyumbani. Unajiitaje mzazi wa mtoto msomi ilhali huna hata shelf moja ya vitabu nyumbani? Ni wakati wa kubadilika – si kwa walimu tu bali pia kwa wazazi! Tukumbuke, elimu bora huanzia katika mazingira tunayowapa watoto wetu. Tubadilike!
Hivi unawaonaje walimu, ???? Katika mfumo WA elimu kuna kitu kinaitwa syllabus na vitabu vya kiada ,mwalimu anajiongeza kulingana na syllabuses na vitabu vya kiada na sio Google ndugu yangu,, ualimu Ni professional kijana, na walimu wengi saiz wanatumia laptops maofisini

Naona unaongozwa na dharau na kada ya ualimu
 
Kwani wewe unafikiri unaakili zaidi ya waalimu wote mkuu?mimi ni mwalimu lakini huwezi kuingia hata robo kwenye uelewa wangu mkuu.hata hicho unachokizungumza haulijua kiundani kivile.
 
Kwa kizazi hiki cha kidigitali, kama mwalimu unaendelea kufikiri kwa mtazamo wa kianalogia, ni wazi kwamba wanafunzi wako watakudharau sana. Fikiria, unawafundisha kuwa kuna sayari tisa, lakini wao wakigoogle wenyewe wanagundua kuwa zipo zaidi ya 1,000. Unategemea watachukulia masomo yako kwa uzito gani? Kwanini usijitahidi kuendana na wakati na kuepuka kuonekana kilaza?

Hivi unajua kwamba baadhi ya wanafunzi wako tayari wanaitumia ChatGPT na teknolojia nyingine za kisasa? Lakini wewe bado unashindwa kujiimarisha na kujifunza mbinu mpya za kufundisha? Kwanini wasikuone kama mfano wa kale kila unapojongea ubaoni? Siku hizi, watoto hawakusikilizi kwasababu tu ya mamlaka yako au ukali, wanakusikiliza kwa sababu kile unachowafundisha kinagusa akili na maslahi yao.

Ninakumbuka mfano mmoja wa mtoto wa mjomba wangu, ambaye amekuwa akilelewa na baba yake msomi mwenye upendo mkubwa wa vitabu. Mtoto huyu, sasa yupo darasa la saba, lakini ana shauku kubwa ya kusoma vitabu vya astronomia. Nilimfanyia majaribio madogo kuhusu mada tofauti za anga za juu – ambayo nilikuwa nimegugulisha – na kwa mshangao wangu, kila kitu alikuwa anakielewa kwa undani. Mtoto huyu, aliyekuzwa katika mazingira ya elimu ya nyumbani, anaonekana kuwa mbele zaidi kuliko walimu wengi wanaomfundisha shule.

Sasa wewe unapeleka watoto English Medium, wanajifunza kwa kukariri tu, wakati msingi wa elimu bora huanzia nyumbani. Unajiitaje mzazi wa mtoto msomi ilhali huna hata shelf moja ya vitabu nyumbani? Ni wakati wa kubadilika – si kwa walimu tu bali pia kwa wazazi! Tukumbuke, elimu bora huanzia katika mazingira tunayowapa watoto wetu. Tubadilike!
Kwa hiyo umewashambulia walimu ukaona haitoshi! Mwisho umeamua utamwagie povu na sisi wazazi wenye watoto wanaosoma English medium!!
 
Umasikini ndugu yangu unasababisha hata muda wakuandaa vipindi na kuongeza maarifa haupo.
 
Hivi unawaonaje walimu, ???? Katika mfumo WA elimu kuna kitu kinaitwa syllabus na vitabu vya kiada ,mwalimu anajiongeza kulingana na syllabuses na vitabu vya kiada na sio Google ndugu yangu,, ualimu Ni professional kijana, na walimu wengi saiz wanatumia laptops maofisini

Naona unaongozwa na dharau na kada ya ualimu
Hiyo kada ingekuwa ina heshima yoyote mngekuwa hamtotoi watoto kwa kukaririsha mpaka leo; joblessness tunayoiona mtaani lawama zinaanza kwenu
 
Kwa hiyo umewashambulia walimu ukaona haitoshi! Mwisho umeamua utamwagie povu na sisi wazazi wenye watoto wanaosoma English medium!!
Mimi mwenyewe nimesoma English Medium, pesa iliyochomwa hapo bora hata wazazi wangemwaga tuition ya English
 
Back
Top Bottom