Walimu jiongezeni maarifa mitandaoni kabla ya kuingia Darasani maana wanafunzi wenu wanawaona vilaza mkijongea hapo ubaoni na kushika chaki

Walimu jiongezeni maarifa mitandaoni kabla ya kuingia Darasani maana wanafunzi wenu wanawaona vilaza mkijongea hapo ubaoni na kushika chaki

Kwani wewe unafikiri unaakili zaidi ya waalimu wote mkuu?mimi ni mwalimu lakini huwezi kuingia hata robo kwenye uelewa wangu mkuu.hata hicho unachokizungumza haulijua kiundani kivile.
Uelewa gani? Mngekuwa mnatapeliwa na vishoka pensheni zenu uzeeni?
 
Huyu dogo akiwezeshwa akapata hata scholarship anaweza kufuata ndoto yake na kuwa astronaut, kwanini afanye biashara ya mihogo wakati ana ndoto ya kuishi Mars
Sikua na maana afanye biashara ya mihogo,ajue namna gani biashara huendeshwa,
Kama ni ndoto yake wazazi wake wahakikishe mtoto anapata kilicho bora
 
Sasa wewe unapeleka watoto English Medium, wanajifunza kwa kukariri tu, wakati msingi wa elimu bora huanzia nyumbani. Unajiitaje mzazi wa mtoto msomi ilhali huna hata shelf moja ya vitabu nyumbani? Ni wakati wa kubadilika – si kwa walimu tu bali pia kwa wazazi! Tukumbuke, elimu bora huanzia katika mazingira tunayowapa watoto wetu. Tubadilike!
Mkuu una maanisha ma profesa wote Duniani wamezaliwa na wazazi wasomi? wazazi wa profesa lipumba walikuwa na degree ngapi?

Mbona kuna wazaz hawajui kusoma wala kuandika lakini watoto wao ni wasomi hatari na ni mifano mingi tu?
 
Mkuu una maanisha ma profesa wote Duniani wamezaliwa na wazazi wasomi? wazazi wa profesa lipumba walikuwa na degree ngapi?

Mbona kuna wazaz hawajui kusoma wala kuandika lakini watoto wao ni wasomi hatari na ni mifano mingi tu?
Kina Lipumba wachache sana tena unakuta walipitia mazingira ambayo kwa bahati yakawafikisha mbali, mimi nataka ikija kwenye suala la kupalilia vichwa konki isiwe tu bahati bali mazingira wezeshi ya kufanikisha hilo
 
Aisee hakuna kada ina dharaulika kama ya ualimu nchini Tanzania. Najiulizaga hii inasababishwa na nn hasa?
 
Sasa kwa mtazamo wako elimu inaendeshwa kiholela tu..
Kuna vitabu vya kiada na ziada..hivi vya ziada ni special kwa kuongeza maarifa..
Sasa nikuulize vitabu vya kiada vinasema kuna sayari tisa kuu mtoto yeye akajaza elfu moja kwa mujibu wa google je atakua amepata hilo swali?
 
Elimu bora ina athiriwa na ushindani wa mitihani. Wanafunzi wanataka wafaulu ilibwa songe mbele, Mwalimu anataka aonekane amefaulisha, anapaswa kumaliza mada zote kwa wakati. Shule zinataka jina kwa kukuza ufaulu na mnyororo unaendelea.

Ni mkanganyiko wa kufamtu: sera ya elimu itungwe na wizara husika, mtaala wa kufundishia utungwe na TIE, kitabu cha kufundishia kitoke TIE , anae taini na kutunga mitihani NECTA: wanatoa format, watunga mitihani na wanasaisha mitihani, na mwalimu kazi yake: kufundisha TIE wanavyoelekeza, kufanyisha mazoezi kutosha ili wafaulu kama NECTA wanavyotaka.

Maabara zipo lakini hazitumiki kufundishia, walimu hawana muda huo; zinatumika tu kwa ajili ya madarasa ya mitihani. Miongozo na maelekezo kibao inayoua ubunifu wa mwalimu darasani, watoto wanapewa elimu kavu; unafundishwa kitakachotoka kwenye ntihani wako wa mwisho.

Katika elimu hii inayopimwa kwa makaratasi inaleta ugumu wa mwalimu katika kuonesha ubunifu unaoacha elimu kwa mwanafunzi. Elimu hii imekuwa kama mechi za mtoano, matokeo yanazingatiwa zaidi kuliko michakato
 
Sasa kwa mtazamo wako elimu inaendeshwa kiholela tu..
Kuna vitabu vya kiada na ziada..hivi vya ziada ni special kwa kuongeza maarifa..
Sasa nikuulize vitabu vya kiada vinasema kuna sayari tisa kuu mtoto yeye akajaza elfu moja kwa mujibu wa google je atakua amepata hilo swali?
Mitaala inabidi iwe inanyumbuka kutokana na taarifa mpya, utakaririshaje watoto taarifa zilizopitwa na wakati ?
 
Back
Top Bottom