kiredio Jr
JF-Expert Member
- Jul 8, 2024
- 989
- 1,843
Habarini ndugu, Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ya Mzee wangu, nimeamua kushare story hii fupi inayohusu jambo ambalo lilimkuta enzi za uhai wake.
Kama ilivyo kawaida katika jamii zetu, mtu akiwa na mafanikio huitwa majina yote mabaya pasipo kujali uhakika wa madai hayo..
Siku moja ya jumapili, mzee alikuwa nyumbani na kama Kawaida yake jioni hupendelea kutoka na kwenda jirani kidogo na nyumbani kwa lengo la kukutana na kubadilishana mawazo na wadau ( kijiweni).
Baada ya kufika kijiweni, kwa bahati mbaya sendo aliyokuwa amevaa ikakatika na ikabidi ampe fundi viatu kwani hakuwa mbali na pale, alibaki na kiatu kimoja na alikataa kuvaa ndala ambazo alipatiwa na fundi.
Mwisho akaona amuachie fundi viatu vyote viwili ili arekebishe vyote, yeye akabaki peku kwa muda wa zaidi ya nusu saa huku akiwa bado anazunguka huku na kule.
Watu walimuona na kuanzia hapo maneno yakaanza, kwamba mzee amepewa masharti atembee peku, wengine wakaanza kusema ni Freemason.
Baada ya wiki kadhaa kupita, taarifa zikamfikia bimkubwa na akamweleza mzee kwamba mtaani watu wanasema hayo maneno, mzee hakupata wasiwasi na alicheka tu.
Ikafika jumapili nyingine, mzee akaona ngoja achochee moto vizuri kwani alikuwa ni mtu ambaye anapenda kucheza na akili za watu hasa wajinga, basi akaondoka nyumbani bila viatu (peku) akaenda kijiweni na akakaa huko kwa muda mrefu.
Watu walimuona na wakazidi kusema na kuzidi kumshutumu na ulozi, mzee hakujali na alifanya hivyo makusudi. Walikuwa na wasiwasi na mambo yake kwasababu hakuna aliyekuwa anajua mzee anafanya mishe au shughuli gani ambazo zinampa kipato.
Kwa sasa mzee wangu ni marehemu, Mungu amfanyie wepesi huko alipo, alikuwa mtu jasiri asiye yumbishwa na maneno ya walimwengu.
FUNZO: Wakiamua kukukanyaga kwa bahati mbaya na wewe walipue kwa makusudi.
Kama ilivyo kawaida katika jamii zetu, mtu akiwa na mafanikio huitwa majina yote mabaya pasipo kujali uhakika wa madai hayo..
Siku moja ya jumapili, mzee alikuwa nyumbani na kama Kawaida yake jioni hupendelea kutoka na kwenda jirani kidogo na nyumbani kwa lengo la kukutana na kubadilishana mawazo na wadau ( kijiweni).
Baada ya kufika kijiweni, kwa bahati mbaya sendo aliyokuwa amevaa ikakatika na ikabidi ampe fundi viatu kwani hakuwa mbali na pale, alibaki na kiatu kimoja na alikataa kuvaa ndala ambazo alipatiwa na fundi.
Mwisho akaona amuachie fundi viatu vyote viwili ili arekebishe vyote, yeye akabaki peku kwa muda wa zaidi ya nusu saa huku akiwa bado anazunguka huku na kule.
Watu walimuona na kuanzia hapo maneno yakaanza, kwamba mzee amepewa masharti atembee peku, wengine wakaanza kusema ni Freemason.
Baada ya wiki kadhaa kupita, taarifa zikamfikia bimkubwa na akamweleza mzee kwamba mtaani watu wanasema hayo maneno, mzee hakupata wasiwasi na alicheka tu.
Ikafika jumapili nyingine, mzee akaona ngoja achochee moto vizuri kwani alikuwa ni mtu ambaye anapenda kucheza na akili za watu hasa wajinga, basi akaondoka nyumbani bila viatu (peku) akaenda kijiweni na akakaa huko kwa muda mrefu.
Watu walimuona na wakazidi kusema na kuzidi kumshutumu na ulozi, mzee hakujali na alifanya hivyo makusudi. Walikuwa na wasiwasi na mambo yake kwasababu hakuna aliyekuwa anajua mzee anafanya mishe au shughuli gani ambazo zinampa kipato.
Kwa sasa mzee wangu ni marehemu, Mungu amfanyie wepesi huko alipo, alikuwa mtu jasiri asiye yumbishwa na maneno ya walimwengu.
FUNZO: Wakiamua kukukanyaga kwa bahati mbaya na wewe walipue kwa makusudi.