Walioshauri viongozi wetu kununua umeme Ethiopia km maelfu badala ya Nyerere wakamatwe wahojiwe km wahujumu uchumi ,Victoria inakuwaje chanzo mbadala

Angalau umejaribu kumuelezea japo sio kwa kisayansi sana. Analaumu kumbe tatizo ni la kwake la kuwa na uelewa mdogo kwenye masuala ya nishati.
Kama umemuelewa MTU ambaye hata muandiko wake hauleweki Basi wote mnafanana akili

Na hizi akili za namna hii ndo zinazofanya viongozi waseme lolote bila kufikiria
 
Kama maarifa ni kununua umeme unaotoka km maelfu kwa fedha za kigeni na kuucha umeme unaozalisha nyumbani
Kisa tu unacopy na kupaste mataifa makubwa yenye viwanda ambavyo return hayo sio maarifa ni ujinga
 
Hahahah. Unaambiwa kununua mchele ni ghali kuliko kununua wali.
 
Viongozi wamejua kuwa wanatuongoza sisi WAFU, hivyo wanajifanyia wanavyopenda.. Wakijua sisi ni kelele za chura
kuna siku watatuweka bondi kwa matajiri wakijua ni wafanyakazi wafarao
 
Tuna Rahisi wa ajabu kweli, anadanganywa na wasaidizi wake kama mtoto mdg...mi5 tena my foot!
 
Wanadai eti kuutoa umeme pale bwawa la nyerere (stigglers gorge) hadi kaskazini zaidi ya km 600~ 700. Umeme mwingi utapotea njiani...!

Sasa cha ajabu wanataka kununua umeme kutoka Ethiopia zaidi ya maelfu ya kilometre! Unajiuliza kama umeme wa kutoka Rufiji utapotea njiani na kupata hasara kwahiyo umeme wa kutoka Ethiopia maelfu ya km haupotei njiani... Na wao kupata hasara???

Inashangaza sana! Na kama wao umeme wao unaotoka mbali zaidi ya wetu haupotei njiani, wao wanafanyaje? Na sisi tujifunze kwao?
Na wakati huo huo tunajenga njia kubwa ya umeme kutoka Rufiji kuelekea Zambia, ili kuwauzia umeme huko umeme hautapotea?!

Wengine usema eti ni kwaajili ya usalama wa taifa kwa ujumla? Hivi kutegemea chakula chako nyumbani na kununua chakula kwa jirani kipi ni salama zaidi kwako? Siku ukigombana na jirani akakuzimia umeme au akakunyima chakula chake utafanyaje?

Felschian Mramba aliwahi kusema eti "hasara ya Ethiopia haituhusu!" haya majibu ni ya kipumbavu sana! Hasa kwa kiongozi kama yeye!

Adios Amigo!
 
Lakini kinacho shangaza zaidi ni kwa huyo anaye shauriwa ujinga na yeye asihoji kitu juu ya ushauri huo!
 
Matapeli wa nchi hii ndio hawa, hata chembe ya aibu hawana usoni mwao! Akina Hamza Johari ndio walanguzi wakuu wa mali za nchi hii, halafu mnageuka na kutudhihaki kama unavyo fanya hapa! Tena kwenye jambo la kipuuzi kama hili!
 
Uvumilivu wetu Kama wazalendo una mwisho pia
Kama hawatahojiwa Kuna siku tutachukua nchi yetu wazalendo tutawahoji

Sio tumalize uchaguzi tusikie skendo ya umeme wa Ethiopia haitusaidii
Hofu yangu kubwa ni kwa hawa viongozi kuendelea kuwepo baada ya huo unaoitwa uchaguzi.
Kama wamekuwa na ujasiri wa kufanya uchafu kiasi hiki katika ngwe ambayo hawakuwa na ridhaa yoyote ya kufanya waliyo fanya, tena kwa siri siri kubwa; kwa mfano: Bandari, mapori ya Carbon credit, gesi ya Ntorya huko Mtwara; wananchi wa Ngorongoro kuhamishwa na waliokataa kutishiwa kunyimwa huduma; itakuwaje hapo watakapokuwa na ngwe yao ya kulazimisha kuwepo kwenye madaraka?
 
Mkuu 'utala utala TU', mimi napenda kuchangia katika swali lako ifuatavyo, na kwa namna hiyo nitakuwa nimejibu sehemu ya swali lako.

Ni hivi mkuu: Pamekuwepo na mpango wa siku nyingi wa kuunganisha gridi ya nchi za Kusini mwa Afrika, na ile ya nchi za kaskazini mwa Afrika kupitia nchi za Zambia, Tanzania na Kenya.
Umeme unaozalishwa kusini mwa nchi za Afrika, ukijulikana kuwa" Southern African Power pool" usafirishwe kwenye waya hizo, kuja Tanzania na kuendelea kuusafirisha kuelekea Kaskazini kupitia Kenya; na wakati panapokuwepo na upungufu kusini mwa Afrika, umeme huo usafirishwe toka Kaskazini.
Mpango huu umekuwepo kwa muda kitambo, na tumechukuwa hadi mikopo ya Benki ya Dunia kuutekeleza. Ni hivi majuzi tumekamilisha eneo la kuunganisha na Kenya.
Inavyo onekana sasa ni wazi kwamba palikuwepo na msukumo toka kwa kundi fulani kuukamilisha haraka mpango huu. Lakini katika mpango wote huu, uwepo wa Bwawa na Mwalimu Nyerere haukuwepo. Ina maana kwamba, uwepo wa Bwawa hilo kume athiri kiasi fulani mipango ya hao walio buni hiyo gridi ya Southern Power Pool na ile ya huku Kaskazini. Kwa bahati mbaya, sasa wapigaji hao wanaona wafanye kila liwezekanalo mpango wao wa mwanzo uendelee bila kujali uwepo wa umeme wa ziada hapa kwetu.
Hawa watu hata hawaoni aibu kufanya utapeli wa namna hii.

Kwa hiyo swala la "kutokuwepo nyaya zinazounganisha mikoa ya Kaskazini, hilo halipo kabisa. Kwani hata kabla ya hiyo gridi niliyo zungumzia hapo juu, mikoa hiyo ilikuwa ikihudumiwa na gridi yetu ya taifa iliyopo sasa.
 
Kama umemuelewa MTU ambaye hata muandiko wake hauleweki Basi wote mnafanana akili

Na hizi akili za namna hii ndo zinazofanya viongozi waseme lolote bila kufikiria
Huyo uliye mjibu hapa ni sehemu ya wakala muhimu wanao inadisha Tanzania sasa hivi.
 
Una point. Ila uelewe kuwa Nile uliopo Ethiopia ni tofauti na unaoanzia Victoria. Pia Ethiopia wana mito mingi ya kuzalisha umeme. Mmoja wapo ni mto Omo unaomwaga maji ziwa Turkana. Kwenye mto huu wanazalisha zaidi ya MW 2500
 
Nakuelewa sana mkuu,shukrani
 
Mimi sio mwanauchumi ila hapo ninapinga kwa nguvu zote. Labda tumuulize professor Lumumba kuhusu viongozi wa Afrika.
 
Maneno mengi umeandika gazeti zima lakini utumbo mtupu. Umeshawahi kumtafuta huyo Mramba akuelezee kitaalam kwanini umeme unanunuliwa huko Ethiopia?

Megawatt 100 zinapotea huko kaskazini, ni masuala ya elimu ya nishati ambayo kwa maandishi yako wewe huna kabisa. Hata huo umeme unaonunuliwa kutoka Ethiopia sio biashara ya kubeba magunia ya mahindi kutoka nayo Msamvu na kuyapeleka Bukoba mjini, ni biashara inayofanyika katika mazingira mengine tofauti na tunavyodhania.
 
Kama umemuelewa MTU ambaye hata muandiko wake hauleweki Basi wote mnafanana akili

Na hizi akili za namna hii ndo zinazofanya viongozi waseme lolote bila kufikiria
Tafuta uelewa mpana wa mada mbalimbali, usipende kuongea maneno mengi wakati elimu ni ya kuokoteza huko google.
 
Matapeli wa nchi hii ndio hawa, hata chembe ya aibu hawana usoni mwao! Akina Hamza Johari ndio walanguzi wakuu wa mali za nchi hii, halafu mnageuka na kutudhihaki kama unavyo fanya hapa! Tena kwenye jambo la kipuuzi kama hili!
Ungejua wanavyofanya kazi usiku na mchana usingekuja na hizi lawama za kudhani kila mtu mwenye cheo anao mpango wa kuiba mali ya umma. Punguza mazingira na sababu za kujirundikia dhambi.
 
Kama maarifa ni kununua umeme unaotoka km maelfu kwa fedha za kigeni na kuucha umeme unaozalisha nyumbani
Kisa tu unacopy na kupaste mataifa makubwa yenye viwanda ambavyo return hayo sio maarifa ni ujinga
Umeme haununuliwi kama machungwa yanavyonunuliwa pale sokoni Tandale. Ethiopia wanauleta mpaka hapo Kenya na Kenya anatuuzia sisi, tukishawalipa Kenya huyo Muethiopia anamalizana na Mkenya.

Sio biashara ngeni duniani, tatizo letu ni ushamba mwingi na kwa bahati mbaya hatujui kwamba hatujui ingawa tunadhani tunajua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…