Wamarekani wanawezaje kufanya uchaguzi bila purukushani za polisi?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Inawezekanaje kwa miaka zaidi ya 200 Marekani kubwa hivyo yenye wapiga kura takribani milioni 150 na maelfu ya wagombea uchaguzi unafanyika bila wagombea kukamatwa na polisi au mikutano ya siasa kuzuiwa kama ambavyo huwa inatokea katika nchi ndogo za Africa?

Japo kipindi hiki Trump anaweza kuzua balaa akishindwa na kuharibu historia hiyo. Awamu hii tujiandae kuwapatanisha Wamarekani.

Pia soma:
LIVE - Yanayojiri kuelekea Uchaguzi Mkuu Marekani 2024: Nani kuibuka kidedea?
 
Marekani hakuna chama chenye mihemko na ghadhabu, wala hakuna chama chenye kutegemea huruma za wananchi kwa kuibua hisia za kuibiwa kura hali ya kua chama hicho huenda hakina sera, hakiaminiki wala kukubalika kwa wananchi, na matokeo yake huibua fujo na vurugu ambazo zitawalazimu polisi kuingilia kati kujaribu kudhibiti makaidi hayo ya vyama vyao siasa ili amani ya uchaguzi itawale miongoni mwa wananchi wanaoshiriki uchaguzi huo Africa.

Ni hivyo tu.
Kinyume na hapo Chaguzi hususan Tanzania zinaweza kua za Amani zaid kuliko maeneo mengine yote duniani.

Na kuna viongozi wa vyama mbalimbali hususan Tanzania hawajajiandikisha, halafu eti kwenye uchaguzi wao ndio watakaleta fujo, kwahiyo ni lazima polisi kuwadhibiti vilivyo πŸ’
 
Hiyo ni demokrasia iliyokomaa ...
 
Shangaa hapo sasa, sisi ka uchaguzi tu haka ka serikali za mitaa yetu kanatutoa jasho kama si kamasi, mara wapokea form wamekimbia ofisi, mara tumeandikisha wasio wakazi wa mitaa, mara tumeaddika watoto under 18, mara yameingizwa majina hewa etc

Yaani kuufikia ustaarabu wa wamarekani tutahitaji miaka 1000 mingine toka leo. Mwaka 3024 yawezekana kwa watakaokuwepo.
 
Zanzibar Wapiga Kura Laki 5, uchaguzi siku mbili, vurugu mwezi mzima.

πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…
 
Afrika is the symbol of failure in the world
 
Afrika is the symbol of failure in the world
 
Mpumbavu anapojimwambafai
 
US is not a shithole country.

Marekani kuna mifumo ya uongozi wa nchi, nchi inaongozwa kwa mifumo shirikishi ambayo ipo wazi katika utendaji wake wa kazi, hakuna magenge ya watu ambayo yamehodhi madaraka yote katika kuitawala nchi.
Nchi hiyo inaongozwa kwa mujibu wa Katiba ya nchi, Sheria, Kanuni na taratibu zao ambazo wamejiwekea wao wenyewe kwa umoja wao. Wakati katika nchi nyingi Sana za kiafrika, nchi hizi zinatawaliwa kwa mtindo wa magenge ya watu.
Watawala wa nchi wamekuwa wakiunda magenge yao ya Utawala ili kuweza kuwatawala Wananchi na nchi husika kwa ujumla.

NB: Elewa tofauti iliyopo kati ya neno 'Uongozi' na 'Utawala.' Nchi nyingi za Afrika kuna Watawala, Hakuna Viongozi.
 
Uchaguzi Africa hadi vifaru vya kijeshi vinaingia mtaani!🀣
Afrika is the symbol of failure in the world
Zanzibar Wapiga Kura Laki 5, uchaguzi siku mbili, vurugu mwezi mzima.

πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…

"Black people are not complete human beings because they don't have a good brain to govern the society as White people. They are still under the process of becoming the complete human beings."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era.
 
miaka yote hio ya nini... ustaarabu unaweza kuanza hata kesho endapo CCM itajirekebisha
 
Mkuu tanaweza kujitawala, mbona Botswana mambo yameenda vizuri tu?
South Africa na Zambia mambo huwa yanaenda vyema tu.
 
Mkuu tanaweza kujitawala, mbona Botswana mambo yameenda vizuri tu?
South Africa na Zambia mambo huwa yanaenda vyema tu.
Nchi zote hizo ulizotaja Siasa zao za nchi zimeegemea katika mrengo wa Siasa za Itikadi ya Ubepari (imperialism), hizo ni Sera, itikadi na siasa za nchi za Magharibi. Kwenye hizo nchi hakuna siasa zenye Itikadi za Ukomunisti/Ujamaa.
Wakati kwenye nchi nyingi Sana za kiAfrika (ikiwamo na ya kwetu) kuna Siasa za Itikadi ya Ukomunisti/Ujamaa, ndio maana unaona kwamba kwenye hizi nchi zetu nyingi kuna migogoro isiyokwisha daima milele, kuna Watawala madikteta wengi Sana.

NB: Rejea Visa na sababu zilizopelekea kuibuka kwa janga la 'Vita Baridi' (Cold War) hapa duniani pamoja na madhara yake kwa dunia.
 
huku Tanzania kwa mfano. poisi wenye vyeo vikubwa, hupigania chama kilicho madarakani mfano CCm kulinda ufisadi wao, ufisadi wa wakubwa zao (Viongoxi wa CCM) na future za watoto wao na viongozi wao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…