Wamiliki wa lodge kuweni serious

Wamiliki wa lodge kuweni serious

Siku moja Moshi mjini mitaa ya Majengo nilichukua room kwenye lodge moja, 20k. Nilipoingia tu nikafunga mlango wa room kwa funguo, nikavua nguo direct kuoga bafuni. Huko bafuni nililazimika kurudishia mlango maana bafu ni dogo sana. Ile nafunga mlango nikasikia kitu kinaanguka upande wa pili wa mlango (upande wa chumbani). Sikujali nikaendelea kuoga.

Nimemaliza kuoga nafungua mlango haufunguki. Kumbe handle ya kitasa upande wa nje na kile kijichuma kinaunganisha handles na kitasa ndio vinedondoka.

Niliita wahudumu kwa nguvu sana ila wasisikie mpaka koo likauma na matusi yote hapo nimeshamaliza, na hakuna hata mteja mwingine room jirani anisikie awaambie. Wamekuja baada ya nusu saa hivi ila hawawezi kuingia chumbani kwangu kwani nimefunga. Funguo za akiba hawana anazo boss mwenye guest house. Boss amepigiwa yupo mbali, shambani. Alikuja baada ya kama 3hrs hivi. Muda wote huo nipo chooni tu.

Walipofungua nikatoka. Jicho nililowakata wakaelewa namaanisha nini. Wakanirudishia hela yangu bila kusema chochote nikaondoka kutafuta lodge nyingine.

Ulikua unaoga, unakauka, unarudia tena kuoga hivo hivo zoezi likawa endelevu
 
Kahama, mbinga, kasulu, nyakanazi, kibondo, sumbawanga, babati, singida, iringa, morogoro, mbeya, mbalizi, newala, bariadi, ngara, biharamuro, muleba, karagwe, mutukula, mpanda, kigoma mjini, manyoni, nzega, igunga, gairo, kibaigwa, tandahimba, Arusha, Mwanza, ngudu, sengerema, tukuyu, mlowo, vwawa, chimala, songea, uvinza, na maeneo mengine mengi ya mikoani chumba cha tsh.25000 hadi 30000 kwa dar unakipata kwa 60000 hadi 100000 na kinakua na hadhi ileile tena muda mwingine kinakua bora zaidi, kwa uzoefu wangu eneo lolote nikifika natafuta lodge au hotel mpya mpya ndio nafikia hapo maana zile zenye majina na za muda mrefu unakuta zimechoka sana hivo sio bora kwa sababu hazina maboresho, kwa mfano hotel au lodge au guest house lazima ifanyiwe ukarabati mdogo kila mara inapotokea kuanzia mfumo wa maji, umeme, na kadhalika lakini lazima kukagua vitanda, kubadili mashuka kila baada ya muda kuangalia vitu kama AC , feni kama zinafanya kazi imara, vitanda walau kukaza kila mara na usafishaji wa chumba inatakiwa ufanyike chumba kizima wengine unakuta chini ya kitanda pachafu au nyuma ya kitanda vumbi, madirisha lazima yafutwe kila mara, ubadilishaji wa mashuka lazima uwe na pea tatu za shuka kwa kila chumba na foronya pea tatu, lakini pia taulo lazima uwe na pea mbili,kila chumba,
 
Halafu kwa wamiliki wa lodges na hotel jitahidi kufunga kamera za usalama kwenye jengo lako hua zinasaidia sana wakati mwingine hasa nje, mapokezi, kwenye korido za kuingia vyumbani, na kila mgeni aandike jina lake halisi either aoneshe kitambulisho au kwa raia wa kigeni lazima akuoneshe hati yake ya kusafiria ili unakili namba zake kwa ufasaha,
 
Kama jengo linaeneo kubwa jitahidi ujenge fence na parking za nje na ndani ziwe bora na sio mbaya ukitenga eneo moja wapo la kupumzikia wateja kijumba cha msonge kidogo, lakini pia jitahidi sana tv za vyumbani uziweke uelekeo sahihi ili mteja asisumbuke kuona screen [emoji342]
 
Room haitakiwi kua na makolokolo mengi yasio na umuhimu, na kwa wamiliki wa hotels na lodges ni muhimu sana kuweka vyoo aina zote japo wateja wengi hupendelea vyoo vya kuchuchumaa vinaweza kua vingi na vya kukaa baadhi na kujitahidi kubadilisha kila vinapochakaa
 
Lakini pia kwenye usafi, mashuka yakifuliwa hapo yakunjwe na kunyooshwa vyema, sabuni za vyooni na air fresh za vyumbani za test tofauti tofauti kama apple, orange, vanila na kadhalika pia usisahau kufanya famigation kila baada ya muda fulani ili kuua wadudu warukao na watambaao, kwenye jengo lako, muhimu sana kutenga chumba kwa ajili ya kunyoshea nguo na ubora wa huduma za ufuaji wa nguo za wateja wetu
 
Wateja wengine hupendelea lodge tulivu, ni vyema usiweke bar, unaweza kuuza hapo vitu kama juice za boksi, soda aina fulani na maji makubwa na madogo ili kwa vitu kama hivo mteja asisumbuke sana bila kusahau condom, walau chumbani kasabuni na kamswaki kadogo viwepo ukiona couple vimiswaki viwili wapatie, na chooni toilet paper zisikose, lakini unaweza kuuza counter ped za dharura wanwake wengine huanza siku zao ghafra hivo huduma iwepo
 
12. Bed sheet jeupee, godoro limechakaa na limevunda
13. Makahaba wanaruhusiwa kiholela kuja kusumbua wateja, Jambo linaloweza kuhatarisha usalama wa mteja na Mali zake.
14. Kibao Cha Lodge kimeandikwa kuna breakfast na TV lakini hakuna kitu.
15. Kiti Ni kibovu, unakikalia unajikuta umeanguka kwa kisogo, unazirai ukija kuzinduka umeibiwa kila kitu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Halafu kwa wamiliki wa lodges na hotel jitahidi kufunga kamera za usalama kwenye jengo lako hua zinasaidia sana wakati mwingine hasa nje, mapokezi, kwenye korido za kuingia vyumbani, na kila mgeni aandike jina lake halisi either aoneshe kitambulisho au kwa raia wa kigeni lazima akuoneshe hati yake ya kusafiria ili unakili namba zake kwa ufasaha,
Ukifanya hivyo wataojielewa tu ndo watakuja, wasiojielewa hutawaona
 
Back
Top Bottom