Tajiri Tanzanite,
" Arusha imekuawa na historia mbaya ya machafuko ya kisiasa ".
Wewe na serikali yako ya ccm nani mkweli? Maana serikali kila siku inahubiri amani na kutaka watalii wa ndani nje watembelee vivutio vilivyomo ndani ya nchi. Lakini wewe unapingana na serikali yako unapodai kwamba kuna machafuko.
"Tunakumbuka Arusha kwa miaka ya nyumba ilikuwa ni mji ambao serikali ilipendekeza kufanyia mikutano yake ya kimataifa".
Kama kuna kikundi kidogo ambacho kinaweza kuizuia serikali kuendelea na mipango yake kama ilivyo jipangia, je serikali hiyo ina pata uhalali gani wa kuongoza hali yakuwa inashindwa hata kudhibiti kikundi kidogo chenye kuleta machafuko (kuvuruga amani) ndani ya nchi?
"Kitendo cha Rais Magufuli kufufua Reli na kufikisha Arusha".
Kufufua reli maana yake ni kwamba alikuwa imekufa. Swali la msingi, je ni nani aliua usafiri wa treni kuja Arusha? Kivyovyote vile jibu litakuwa ni serikali ya ccm. Je ccm inapataje uhalali wa kubaki madarakani kwa kuua mradi huu kwa miaka karibia 26?
"Hawa wapinzani hawajawahi kuleta maendeleo yeyote hapa Arusha".
Linapokuja suala la maendeleo ndani ya nchi huwa ni jukumu la serikali kutekeleza hayo. Mbunge ni muwakilishi kati ya serikali na wananchi walio mtuma kuwawakilisha bungeni. Na kwa kupitia bunge, mbunge anawasilisha kero za wananchi kwa serikali ili izifanyie kazi. Je serikali yako ya ccm inazifanyia kazi kero za wananchi zinazowasilishwa na mbunge wa upinzani? Je serikali yako ya ccm inashirikiana vipi na mbunge wa upinzani ambae ndiye muwakilishi wa wananchi kuleta maendeleo katika kila jimbo husika?
"Hizo barabara zilizojengwa ndani ya mji wa Arusha ambayo chadema inatumia kama ngao,ya kuwadanganyia hao wafuasi wake ni project ya World Bank iliyoanza kipindi cha Kikwete."
Hivi kuna mradi wowote ndani ya nchi hii unafanyika/uliofanyika bila msukumo wa wahisani kutoka nje? Unajua hata elimu yetu kuna mkono wa wahisani ndani yake? Unajua hata afya zetu kutengemaa kuna mkono wa wahisani ndani yake? Nk? Miaka zaidi ya 50 kuwa huru bado tumekuwa omba omba. Licha ya misaada bado kuna mikopo. Unajua serikali ya ccm mpaka sasa imekopa kiasi gani? Wewe kama mwananchi unajua unadaiwa kiasi katika deni lililo sababishwa na serikali yako ya ccm?
Yaani maswali ni mengi mno, acha tu niishie hapo.