Uchaguzi 2020 Wana JF, nipeni Pole. Msinicheke wala msinibeze; nimegombea ubunge Kawe kupitia CCM nimeambulia kura 1. Ama kweli CCM ina wenyewe!

Pole brooo! Lkn pia hongera. Binafsi niliishia kusalimia tu Viongozi wa Wilaya nikasave fedha yangu.
Tunaomba memba wengine waliopigwa wajitokeze tuwajue tuwafariji
 
Yaani Mbele za Macho ya CCM Pascal Mayalla hana tofauti na Mwijaku,na Pia Mpoki ni Zaidi ya Paskali
 
USITUFOKEE
 
Bwashee pascal bado nafasi mbalimbali zinaweza kupatikana na huu Ndio mwanzo wa Safari ya siasa kama alivyosema mwenyekiti wako wa wilaya kwahiyo kuteleza sio kuanguka
 
Ukisema kuwa "CCM ina wenyewe" ni kuashiria kutokubali matokeo kama vile yamepangwa kwa kiupendeleo ili kuanufanisha "wenye CCM". Uchaguzi wa Kawe ulikuwa na wagombea wengi sana na pia kuna wengi waliopata kura moja au sifuri. Kubaliana na matokeo hayo usahau yaliyopita ugange na yajayo tu.
 
Pole Pascal lkn usijipendekeze tena[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Afu Kawe mgempa tabu sana mkuu wa Sukuma mlikuwa wengi wengi na wengine powerful kama Gwaji boy afadhali tu mmepata za uso japokuwa aliepita nae nasikia ni wa karibu zaidi na Meza kuu haha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…