Wanafunzi wa Shule ya Wasichana Bwiru watakiwa kwenda na Malimao na Tangawizi shuleni

Wanafunzi wa Shule ya Wasichana Bwiru watakiwa kwenda na Malimao na Tangawizi shuleni

Sasa kama unajua maji na sabuni lazima viwepo kwa nini unataka wajaze hayo maneno kwenye karatasi?
Rudia kusoma ujumbe wangu wa kwanza kabisa niliongea nini kuhusu sabuni.

Sijui huko shuleni mnafundishaje kwenye lugha sehemu ya ufahamu (kiswahili) au comprehension(English)!
 
Sasa kama unajua maji na sabuni lazima viwepo kwa nini unataka wajaze hayo maneno kwenye karatasi?
Kwa hivyo kuandika limao ya unga, tangawizi ya unga hakujazi makaratasi kama ukiandika sabuni?
 
Uongozi wa shule hii wana shida kubwa sana mahali.

Wanasema wanafunzi hawatatoka wala kutembelewa na wazazi.
Je, waalimu nao hawata onana na watu wengine au na familia zao pia zifugiwe au wafungiwe waalimu tu?

Sanitizer nusu lita kwa mtu mmoja ni nyingi sana kwa muda mfupi wanaokaa shuleni sabuni za maji ndiyo muhimu sana kuliko sanitizer.

Kutembea na barakoa wakati wote siyo vizuri kiafya watawaumiza watoto wa watu wapate shida za mfumo wa upumuaji.

Limao ya unga sidhani kama ina virutubisho au kemikali muhimu zinazosaidia kuongeza Vitam C na wala kuondoa ute kwenye koo, shule iwaagize waje na pesa ya kununua malimao mabichi ambayo pesa wanapewa shule na kuwagawia wanafunzi limao bichi moja kila siku.

Tangawizi mbichi ndiyo bora zaidi hivyo shule ifanye kama hapo nilivyo shauri kwenye limao halisi siyo ya unga.

Mwisho waalimu wapunguze uoga, kama wanaogopa waache kazi wabakizwe waalimu vijana wenye afya wawafundishe wadogo zao badala ya kuwanyanyapaa na kuwatesa na makemili na mabarakoa kila saa.

Serikali itoe muongozo maana maagizo kama haya ni vurugu tupu, kuna wanafunzi wenye shida za ulcers na nyinginezo za tumbo au kuna wale wenye allergy na sanitizer flai wasije kulazimishwa haya makemikali ya sanitizer na malimao feki, watoto wasije wakarudi nyumbani matumbo yashatoboka na madonda ya tumbo.
Vitu hivi vya nini wakati corona imeisha bad enough ni ugonjwa mdogo
 
Uongozi wa shule hauna shida, shida kubwa iko kwako. Ni upumbavu kutoa ushauri huku ukiamini ushauri wako ndio sahihi zaidi.
Hoja zako ni dhaifu sana kupelekea kusema uongozi wa shule unashida.

1. Hili tangazo limetolewa kwa ajili ya wanafunzi na si kwaajili ya walimu. Walimu pia huwa wanapewa muongozo wao.

2. Sanitizer ni rahisi na haraka zaidi kutumia kuliko maji. Maji hayapatikani kila sehem, huwezi weka maji darasani wala bwenini ila sanitizer inaweza kutumika sehem yeyote.

3. Yani unajiona unaakili kabisa kupinga matumizi ya barakoa? Njia zote zikifeli barakoa ndio defence ya mwisho na ndio ina %kubwa ya kukinga maambukizi.

4. Tofauti kati ya limao fresh na unga ni water content tu basi. Kama unabisha lete uthibitisho. Vivyo hivyo kwa tangawizi.

5. Hizo ni zana ambazo mwanafunzi anatakiwa awe nazo na hakuna atakae lazimishwa na hakuna namna ya kuwalizimisha wanafunzi kutumia limao, wala kutumia tangawizi, wala kunawa na sanitizer. Sidhani kama kuna mwanafunzi wenye allergy na vitu vyote hivyo kwa pamoja.

- Barakoa ndio inatakiwa waweke ulazima zaidi. Na ndicho kimeandikwa kwenye tangazo.
mazojms njoo umsome mtu mwenye akili timamu Profesa Ndalichako.
Hapa ndiyo utafunguka akili kujuwa nilikuwa sahihi na hao uliowatetea na wewe mwenyewe hamkuwa sahihi.
Kwenye post yangu niliomba wizara husika itoe muongozo na hatimae imejibu ombi langu na la wengine wengi.

Shukran zikufikie mkuu wangu dubu kwa nukuuu safi kabisa ya kusafisha vichwa vya watu wagumu kufikiri.
Shukrani @JamiiTalk kwa muongozo mzuri.
Nmependa Dada Ndalichako alivyo kazia hapa.

‘Marufuku wanafunzi kwenda na limao, tangawizi vyuoni, shuleni’

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema ni marufuku kwa wanafunzi kwenda shule na malimao, tangawizi na spiriti pamoja na shule kutoza wanafunzi malipo ya ziada.

Aidha, amesema yeyote ambaye atabainika kukiuka maelekezo ya serikali, kwa kutoza wanafunzi malipo ya ziada, atachukuliwa hatua ikiwamo kufutiwa usajili. Serikali kupitia Rais John Magufuli ilitangaza wiki iliyopita kwamba vyuo vyote nchini pamoja na wanafunzi wa kidato cha sita watarejea masomoni kuanzia Juni Mosi, mwaka huu, baada ya nchi kuwa na unafuu mkubwa wa maambukizi ya virusi vya corona vinayosababisha ugonjwa wa homa kali ya mapafu (Covid-19).

Profesa Ndalichako alitoa kauli hiyo jana kutokana na tatizo lililoibuka hivi karibuni kwa baadhi ya shule, kutoa mwongozo wa vitu ambavyo wanafunzi wanatakiwa kwenda navyo na kutakiwa kulipa ada.

Alisema ni marufuku kwa wanafunzi kwenda na spiriti shuleni, kwani inaweza kuchoma shule na mabweni na pia inaweza kutumika kama kilevi.

“Watu waache kutumia tatizo la corona kama kitegauchumi, watu wanaanza kuagiza hela za ziada za kazi gani, wanafunzi walikuwa wamekwishalipa ada kabla ya kufunga shule na walienda nyumbani kwa sababu kulikuwa na changamoto ya mlipuko wa ugonjwa corona,” Profesa Ndalichako aliwaambia waandishi wa habari jana.

“Serikali imefanya juhudi na maambikizi yamepungua na ndio maana imeamua kufungua shule na vyuo, wanafunzi wanaenda kuendeleza pale pale walipoachia kwa fedha zao zile zile, hakuna malipo ya ziada.

“Nitumie nafasi hii kukemea shule ambazo zinataka kutumia corona kama kitegauchumi, hapa hakuna kitegauchumi, tulikuwa na tatizo kama taifa, tumeungana pamoja, tumeweka na maombi na Mungu wetu ametusikia, sasa tusianze kuumizana kwa sababu ambazo hazina msingi wowote,” aliongeza.

Aidha, alisema wizara itafuatilia shule zitakazotumia janga la corona kama kitegauchumi na kuwa yeyote atakayebainika kufanya hivyo, atachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufutiwa usajili.

“Wizara itafuatilia, shule ambazo zinataka kutumia janga la corona kama kitega uchumi kuweka michango michango ambayo haina uhalali wowote…wizara itachukua hatua ikiwa ni pamoja na kuzifutia shule usajili, kwa sababu tumekuwa tukiwaambia kila mara watu wanaoendesha shule wanatoa huduma kwa Watanzania wasiwe na roho ya kukomoana, imekuja changamoto ya corona watu wameona ni fursa, hili jambo halikubaliki,” alisema.

Aidha, alisema kwa wanafunzi ambao mpaka shule zinafungwa walikuwa hawajakamilisha ada, kufanya hivyo ili fedha hizo zitumiwe na shule kujiendesha.

“Wanafunzi ambao hawakuwa wamekamilisha kulipa ada, walipe ili shule ziweze kujiendesha vizuri, lakini wale ambao mpaka shule zinafungwa walikuwa wamelipa warejee shuleni kuendelea na masomo kama kawaida,” alisema.

Alisisitiza kuwa hata pale wanafunzi wengine watakapofungua shule, utaratibu utakuwa huo huo wa kutokuwa na malipo ya zaida.

“Ni lazima tuwaondolee hofu wananchi, unaposema mwanafunzi aje na limao ya unga, sijui hata inauzwa maduka gani, sasa tunapotoa taratibu ambazo hata utekelezaji wake unakuwa mgumu unazidisha hofu kwa jamii.

“Au unapomwambia mwanafunzi aje na kilo mbili za tangawizi mwanafunzi anayekwenda kukaa shuleni mwezi mmoja na wiki mbili, hilo koo lake litakuwa salama? Tuangalie pia na afya za watoto kwa kuzingatia kuwapa watoto vyakula vyenye vitamin C kwa wingi,” alieleza Waziri wa Elimu.

Alisisitiza kuwa ni vyema vyuo na shule, kuzingatia mwongozo uliotolewa na Wizara ya Afya ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa corona pindi watakapofungua shule. Alisema matumizi ya vitakasa mikono ni kitu cha zaida, na si lazima mwanafunzi kuwa navyo.

Credit: Habari leo
 
Serikali itoe muongozo maana maagizo kama haya ni vurugu tupu,
mazojms soma hapo juu niliandika nini kwenye kipande tu cha yale niliyoa andika na kisha soma hiyo post ya juu niliyo kunukuu uone ,muongozo wa @JamiiTalk na muongozo wa serilikali kupitia tamko la Prof. Ndalichako Waziri wa Elimu.
 
Back
Top Bottom