Wanajeshi 11 wa Marekani walijeruhiwa katika shambulio la Iran dhidi ya kambi ya Jeshi la wanaanga ya Ain al-Assad

pembe la ng'ombe halifichiki
 
Kwa anayejua historia ya mabeberu hii haitashangaza hata kidogo..
Hata kipindi kile Iran ilipotungua lile drone marekani alianza kukataa .. lakini baada ya muda akaufyata ikabidi akubali kua alipata kichapo heavy..

Hata hili jambo sasa hivi ataanza kukaza. Maana mwanzo alisema hakuna hata aliyeumia ni infrastructure chache tu ndio zimeharibika.. lakini ghafra leo anasema watu 11 wameumia kidogo. Hivi kuumia kidogo ndio wapelekwe Germany kutibiwa..

Baada ya muda utasikia walikufa 20 mara 80 hadi ukweli utajulikana..

Wale wamarekani weusi kutoka buza wataanza kuweweseka
 
Mimi pia nilikuwa na mashaka na taarifa ya Trump. Nilisema hata wangevurumishiwa maji lazima wangelowa, sembuse mizinga!
 
Hivi ulishajiuliza kwanini hao Wamerekani hawakujibu mapigo wakati wanashambuliwa? Hivi hujawahi kusikia Iran imeshusha drones kadhaa za Marekani kwenye anga lake? Je, kwa umri wako ulishawahi kusikia kambi yoyote ya Marekani imeshambuliwa na kusababisha "concussion symptoms" kwa askari?

Mimi natambua uwezo wa Marekani kivita lakini sipuuzi uwezo wa Iran kuisababishia Marekani au "Mayahudi" ukilema; na bila shaka wako tayari kwa hatua yoyote ya Marekani dhidi yao.

Lakini kwa jinsi tunavyotambua uwezo wa Marekani katika mambo ya vita walishindwaje "ku-intercept" au "ku-diverge" balistic missiles waliovurumishiwa hata yakawasababishia "concussion symptoms" ?
 
Mimi natambua uwezo wa Marekani kivita lakini sipuuzi uwezo wa Iran kuisababishia Marekani au "Mayahudi" ukilema; na bila shaka wako tayari kwa hatua yoyote ya Marekani dhidi yao.
Points ya Maana Sana Hii Ambayo Wengi Wanajifanya Hawataki Kuiongelea.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama wagojwa wanaotembea ukuwaona sembuse maiti ambayo hata kwenye box unaweza kuiweka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nani amekwambia kuwa yameisha?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…