Wanajeshi wa Urusi waingia ndani zaidi ya mji wa Mariupol

Wanajeshi wa Urusi waingia ndani zaidi ya mji wa Mariupol

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Wanajeshi wa Urusi wamesonga ndani zaidi katika mji wa Mariupol ulioathirika zaidi na vita vinavyoendelea nchini Ukraine ambapo inaarifiwa kuwa mapigano makali yamepelekea kufungwa kwa kampuni moja kuu ya chuma cha pua huku serikali ya eneo hilo ikitoa wito wa msaada zaidi kutoka mataifa ya Magharibi.

Mkanda wa vidio uliokuwa na ujumbe kwa viongozi wa nchi za Magharibi uliothibitishwa na shirika la habari la Associated Press, umemuonyesha wa afisa mmoja wa polisi wa Mariupol akisema kwamba watoto na wazee wanafariki kutokana na mashambulizi ya Urusi katika mji huo.

Kutekwa kwa mji wa Mariupol itakuwa ni hatua kubwa ambayo imepigwa na wanajeshi wa Urusi katika vita hivyo, ukizingatia kwamba wamekuwa na wakati mgumu kupenya katika miji mikuu, wiki tatu baada ya kuanza uvamizi huo.

Gazeti la New York Times limemnukuu mwanajeshi mmoja wa Ukraine akisema shambulizi la roketi limesababisha vifo vya hadi wanamaji 40 katika mji wa kusini wa Mykolaiv hapo jana.
 
Katika makosa ya watu wa Ukraine ni kuchagua msanii, kwenye maisha ya watu unachagua kupambana na taifa kama Urusi? Haiwezekani ukisema tunapambana ukachagua wananchi wapigane na taifa kama Urusi, ukasema kila mwanaume 18 to 60 years abaikie ndani,huo ni uhalifu wa kivita, mtu hana utalaam, hujawahi kushika silaha, wengine hawajawahi kusikia mabomo, raisi wa Ukraine nimemchukia kisa kuzuwia watu wasikimbie.
 
Katika makosa ya watu wa Ukraine ni kuchagua msanii, kwenye maisha ya watu unachagua kupambana na taifa kama urusi?haiwezekani ukisema tunapambana ukachagua wananchi wapigane na taifa kama urusi,ukasema kila mwanaume 18 to 60 years abaikie ndani,huo ni uhalifu wa kivita,mtu Hana utalaam,hujawahi kushika silaha,wengine hawajawahi kusikia mabomo,raisi wa Ukraine nimemchukia kisa kuzuwia watu wasikimbie
Hivi ukivamiwa nyumban kwako na jiran yako mwenye nguvu unasarenda kiboya tu na kumpa watoto na mke kisa ana nguvu bila kuonesha reaction yoyote. Yaan wanaumme wa dar ni shida tupu
 
Back
Top Bottom