Wanajeshi wastaafu wanaruhusiwa kujiunga na vyama vya Upinzani?

Wanajeshi wastaafu wanaruhusiwa kujiunga na vyama vya Upinzani?

Nawasalimu kwa jina la JMT.

Hivi wanajeshi wastaafu wanaruhusiwa kujiunga na vyama vya upinzani katika majukumu yoyote yale?

Watu wa itifaki majawabu Tafadhali!
Hapana, wanaruhusiwa kujiunga CCM tu.
 
Mbona hujajibu swali?
Swali lake limekuja baada ya yeye kusikia kwenye kesi ya Mbowe kuwa kuna makomandoo wa jeshi walikuwa wanaenda kupewa ajira ya kumlinda Mbowe.

Ndipo mimi nikashangaa na swali lake hilo na ndipo nikataka nipate ufafanuzi zaidi wa swali lake kwanza ili niweze kulijibu vizuri kwa kumuuliza kuwa je kumlinda kiongozi wa chama cha upinzani ni kujiunga na chama hicho?

Kuna ubaya wa kuomba ufafanuzi wa swali kabla ya kujibu swali?
Jibu gumu kwa swali jepesi
Jibu gumu kwa swali jepesi na jibu jepesi kwa swali jepesi yote ni majibu.
 
Mkuu hata kama ingekuwa kujiunga - haki hiyo raia wa Tanzania anapewa na katiba. Ulinzi ni kazi halali. Nadhani tunakosea kujadili mada hii - maswali ya nani hii ndio chanzo cha imani kuwa ukiwa serikalini basi uko katika kutenda mambo yanayotakiwa na serikali iliyo madarakani hata kama mambo hayo ni kukiuka haki!!
Hoja yake ina makosa mawili:
1.Kwanza kufikiri kuwa kuomba ajira ya kumlinda kiongozi wa chama cha upinzani ni kujiunga na chama hicho.
2.Kufikiri kuwa ukishafanya kazi serikalini huna haki ya kikatiba kuwa mwanachama wa chama cha upinzani kama ulivyofafanua vizuri hapo juu.

Mimi nilikuwa interested katika kujibu na kumpa changamoto katika hoja namba moja.
 
Mtoa mada utakuwa na akili finyu, uelewa Mdogo wa mambo au umejitoa ufahamu umeamua uwe unapostiposti utumbo utumbo huku jf, utakuwa mpumbavu Sana wewe jamaa

 
Back
Top Bottom