LGE2024 Wananchi hawajajitokeza kujiandikisha ktk daftari

LGE2024 Wananchi hawajajitokeza kujiandikisha ktk daftari

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
ujinga una mwisho wake, yaani leo mtengeneza jukwaa la kukaa na kupigia kura, wasimamizi na waendesha zoezi zima la kujiandikisha na kupiga kura linasimamiwa na viongozi wa chini wa chama cha mapinduzi, watendaji wa mitaa na kata, waalimu..wamepeana ajira za ulaji.
Pili, kwanini zoezi la kuhakiki lisingeunganishwa na hili la kujiandikisha kupiga kura?, yaani leo uniite mwananchi kujiandikisha alafu kesho uniite tena nije nihakiki taarifa..stupid!!..maisha yalivyo magumu hivi tunapambana tupate chochote tuishi ...nije unipotezee muda wangu wewe...sababu ya ujinga wako. Yaani serikali na tume ya uchaguzi hawana akili kiasi hicho kwamba wananchi hawana uvumilivu kupotezewa muda na mafisadi waliogawa zoezi moja lionekane ni mazoezi mawili tofauti!!?..tusichoshane..kama wanataka waendelee tu kuiba kura kama wanavyoibaga siku zote "Nape". Wasomi wengi hawana ajira na hata wakiomba za muda mfupi hawapati, so hawawezi kubali kupotezewa muda na wahuni
Huu ni ukweli mtupu. Umuhimu wa kujiandikisha unazidi kupungua kwa Kasi sana kwa sababu ya wizi wa kura wenye baraka zote kutoka ccm
 
CCM tunajiandikisha kama kawa, kwa raha zetu,

Wasiyojiandikisha ndiyo atakuja kuwa wa kwanza kulalamika kudhulumiwa kura.

Kondoo wanajulikana.
 
Mkuu siamini kabisa kuwa unaniuliza swali hili na kutaka kweli nilijibu.
Kwani hiyo CCM kama chama sasa hivi ina kitu gani cha ziada zaidi ya hao wengine unaoona wewe hawawezi kuwa mbadala!

Labda nijaribu kukupa jibu kwa swali lako hili kwa njia nyingine inayoweza kuwa rahisi kwako kuelewa.

Sasa hivi, hata kile chama cha "ubwabwa" cha Mzee Rungwe ni bora zaidi kuliko CCM. Hapana, usidharau ninayo kueleza. Ni hivi: chama cha mzee Rungwe kikiingia madarakani sisi wananchi tutaweza kupata fursa ya kukiondoa kama tutaona hakifai. CCM, badala yake, wao ndio wametuweka mateka, na kutufanyia kila aina ya uchafu. Hatuwezi kuwaondoa kwa njia za amani. Kinacho subiriwa tu sasa ni mpaka hapo tutakapo kuwa na ujasiri wa kuwaondoa kwa nguvu, na kumwaga damu za waTanzania.
Sasa nikuulize wewe, huu ndio unafuu wa CCM ambao unaona hakuna chama kingine kinachoweza kuwa mbadala wake?
Ninahisi kuwa umeniuliza hili swali kwa vile wewe ni mnufaika wa CCM kwa njia moja au nyingine. Ninakuomba, unapo nijibu tena, kama utafanya hivyo, jitahidi kuweka mapenzi yako kwa chama chako; jitahidi kuelekeza mapenzi hayo kwa nchi yetu Tanzania.
Mkuu,.let us be honesty on this! Hatuwezi kufanya majaribio ya Uongozi katika Nchi yetu.

Nikiri kuwa mimi sio mtu wa siasa, na pengine baadhi ya michango yangu huwa naonesha kutopendezwa na baadhi ya mambo yanayoendelea.

My concern is,

1. Vyama vijiimarishe kushika dola, na sio hizi drama tunazo ziona kila kukicha!

2. Vyama vitengeneze watu ambao ni wafia chama, sio hawa ambao ni njaa tupu, kila mtu anapigania tumbo lake

3. Vyama bado havina mtaji wa wanachama wa uhakika katika kuimarisha na kukipigania chama kama ilivyo kwa CCM.

4. Vyama havina mbinu mbadala, na hii inasababishwa na kukosa watu mbadala wa kuleta mawazo mapya, wapo na mbinu zile zile za toka mwaka 1992.

Vyama vibadilishe mifumo ya uendeshaji wake ili viweze kushindana na CCM. Ikiwezekana viungane
 
CCM tunajiandikisha kama kawa, kwa raha zetu,

Wasiyojiandikisha ndiyo atakuja kuwa wa kwanza kulalamika kudhulumiwa kura.

Kondoo wanajulikana.
Wapiga kura fake.

Utawala wa Samia watu wameususa kiaina.
 
Swali ni nani afanye huo uhamasishaji?

CHADEMA wanapo itisha maandamano kwa sababu halali kabisa wananchi wanashindwa kujitokeza kwa wingi kuunga mkono maandamano hayo.
Hapa tunaweza tusiwalaumu wananchi, kwa sababu ya vitisho vingi vinavyo fanywa na polisi.

Sasa wakati huu wa kujiandisha kuwa wapiga kura, ingetegemewa kwamba CHADEMA na asasi mbalimbali wangefanya juhudi kubwa kuwa elewesha wananchi kwamba hii ndiyo nafasi yao nzuri ya kutumia haki yao na uhuru wao kwa kupiga kura na kuwapata viongozi wanao taka wawaongoze.
Hata kama CCM wakipanga kufanya mizengwe katika uchaguzi; polisi hawataweza kuwaelekezea wananchi mitutu ya bunduki wakati wakienda kupiga kura kwa wingi wao.

Kwa nini fursa hii wananchi hawaambiwi kuwa ipo na wanaweza kuitumia?
Bila shaka mkuu 'Proved' utakuwa umenielewa ni nani hasa wa kulaumiwa.

Kusema kweli inanishangaza sana kwa nini mambo yana kwenda hivi sasa hivi kama yalivyo. Nilitegemea hivi vyama vya upinzani vingekuwa kwenye kazi kubwa sana wakati huu; lakini ni kinyume kabisa, CCM ndio wanao onekana kufanya wanayo taka yafanyike. Ni ajabu sana.
Unawaonea bure upinzani watumie media ipi ? Ambayo basata hawatailima barua? Maandsmano wanakamatwa kutekwa na kupigwa njia ni moja tu nayo ni.......
 
Wapiga kura fake.

Utawala wa Samia watu wameususa kiaina.
Hizo ni fikra zako, una haki nazo.
Mtafuta basi wako orijino. Maana sisi wote ni feki.

Sisi tumejiandikisha na watu wanaendelea jujiandikisha.

Halazimishwi mtu. Ni hiyari.

Kondoo hawajifichi mvua wala jua.
 
Unawaonea bure upinzani watumie media ipi ? Ambayo basata hawatailima barua? Maandsmano wanakamatwa kutekwa na kupigwa njia ni moja tu nayo ni.......
Kabisa..
 
Watanzania sio wajinga kiasi hicho hata uchaguzi mkuu watu hawatokua wengi, na hii yote ni kuvurugwa kwa chaguzi baadhi wazi wazi , hayo ndio matokeo na hali hiyo haitobadilika karibuni , watu wameona waendelee na shughuli zao kuliko kufanywa wajinga miaka yote, hata Mimi binafsi siwezi kwenda kupoteza muda wangu wakati najua hua Kura zinaibiwa , yaani nilianza kuchagua 85 hadi Leo niendelee kua mjinga haipo hiyo
Aisee..!!
🤔
 
Back
Top Bottom