Wananchi wa Goba wakarabati barabara wenyewe, Serikali za Mtaa washawishi bango litolewe

Wananchi wa Goba wakarabati barabara wenyewe, Serikali za Mtaa washawishi bango litolewe


Hii ni picha ya bango la mradi wa ujenzi na ukarabati wa kilomita mbili (2) Goba kwa Awadhi ambayo imesambaa kwa kwenye mitandao ya kijamii.

Mradi huu ni wa ukarabati na ujenzi wa mitaro ambapo unatokana na nguvu za wakazi wa eneo hilo.


Inaelezwa wakazi hao wamekubaliana kujenga mitaro kwa kutumia zege na makadirio ya bajeti ni Shilingi milioni 40 kutoka kwa wakazi 95 ambao wameahidi kuchangia. Hadi sasa, zaidi ya Shilingi milioni 16 zimekusanywa, na ujenzi umeshaanza.

Sema tofauti na mabango mengine ambayo mara nyingi yamekuwa na ujumbe uliozoeleka kwamba UKIMWI unaua, bango hili limehitimishwa na ujumbe wa “Tuchange wote kujenga barabara yetu”.

Pia inasemekana kuwa mjadala huo umewaibua viongozi wa mtaa ambao waliwashawishi wananchi kuliondoa bango hili bila mafaniko. Wananchi wanasema kuwa endapo watalitoa, basi viongozi waitishe mkutano kuelezea barabara hiyo itatengenezwa lini.

Uamuzi wa wananchi wa Goba wa kujikomboa kwa kujenga barabara yao wenyewe ni ishara ya ujasiri na kujitolea katika kuleta mabadiliko katika jamii yao. Hii ni hatua ya kipekee ambayo inaonyesha nguvu ya umoja na dhamira ya kuboresha maeneo yetu.

Je, mtaani kwenu mnachukua hatua gani kama barabara inazingua?
Miaka 60 wameshindwa, wanataka tufanyeje?
Hao wanawaza matumbo yao na hawara zao, hawawazi barabara wala maendeleo.
Mkitoa bango tu, wanaweka la kwao na maelezo "mama ametuvusha!
 
Ujenzi ukisimamishwa uko chini ya viwango nitacheka

Ila nakubaliana nao, very good
 
Ni upumbavu kuchanga pesa wakati Serikali imekopa pesa kwa ajili hiyo hiyo.

Ujanja ni kusimama kidete na kuhoji pesa zilizotolewa na WB Kwa ajili ya kujenga miundombinu ya nini la Dar?
Kuna njia tofauti tofauti za kufikisha ujumbe. Wao wameamua kutumia hii ya kuchangisha pesa na kujitengenezea wenyewe.

Wewe unadhani ujumbe haujafika kunakotakiwa kuwa kuna uzembe ulifanyika?

Hiyo ya kuwashauri waondoe Bango ni uthibitisho tosha kuwa wahusika wameumbuka...!
 

Attachments

  • IMG-20240321-WA0003.jpg
    IMG-20240321-WA0003.jpg
    107.6 KB · Views: 3
  • IMG-20240321-WA0003.jpg
    IMG-20240321-WA0003.jpg
    107.6 KB · Views: 3
Hawa wakazi wanaakili za Maendeleo muda mwingine ukisubiri mtu akufanyie kitu utarudi mno nyuma.
 
Ni upumbavu kuchanga pesa wakati Serikali imekopa pesa kwa ajili hiyo hiyo.

Ujanja ni kusimama kidete na kuhoji pesa zilizotolewa na WB Kwa ajili ya kujenga miundombinu ya nini la Dar?
Si kila jambo lazima utumie nguvu, apa akili itatoa mwongozo
 
Ni upumbavu kuchanga pesa wakati Serikali imekopa pesa kwa ajili hiyo hiyo.

Ujanja ni kusimama kidete na kuhoji pesa zilizotolewa na WB Kwa ajili ya kujenga miundombinu ya nini la Dar?
Hizo pesa wanazokopa wanatumia kununua mabomu ya machozi na magari ya washawasha ili mkisimama kidete kuhoji wawaoneshe cha mtema kuni.

AU NASEMA UONGO NDUGU ZANGU?!
 

Hii ni picha ya bango la mradi wa ujenzi na ukarabati wa kilomita mbili (2) Goba kwa Awadhi ambayo imesambaa kwa kwenye mitandao ya kijamii.

Mradi huu ni wa ukarabati na ujenzi wa mitaro ambapo unatokana na nguvu za wakazi wa eneo hilo.


Inaelezwa wakazi hao wamekubaliana kujenga mitaro kwa kutumia zege na makadirio ya bajeti ni Shilingi milioni 40 kutoka kwa wakazi 95 ambao wameahidi kuchangia. Hadi sasa, zaidi ya Shilingi milioni 16 zimekusanywa, na ujenzi umeshaanza.

Sema tofauti na mabango mengine ambayo mara nyingi yamekuwa na ujumbe uliozoeleka kwamba UKIMWI unaua, bango hili limehitimishwa na ujumbe wa “Tuchange wote kujenga barabara yetu”.

Pia inasemekana kuwa mjadala huo umewaibua viongozi wa mtaa ambao waliwashawishi wananchi kuliondoa bango hili bila mafaniko. Wananchi wanasema kuwa endapo watalitoa, basi viongozi waitishe mkutano kuelezea barabara hiyo itatengenezwa lini.

Uamuzi wa wananchi wa Goba wa kujikomboa kwa kujenga barabara yao wenyewe ni ishara ya ujasiri na kujitolea katika kuleta mabadiliko katika jamii yao. Hii ni hatua ya kipekee ambayo inaonyesha nguvu ya umoja na dhamira ya kuboresha maeneo yetu.

Je, mtaani kwenu mnachukua hatua gani kama barabara inazingua?
Bango limeondolewa leo baada ya DC kutembelea eneo la mradi wa wananchi.
 
Back
Top Bottom