Wananchi wanategemea kuona ukali wa Rais Samia katika kikao cha dharura cha Baraza la Mawaziri leo

Wananchi wanategemea kuona ukali wa Rais Samia katika kikao cha dharura cha Baraza la Mawaziri leo

The Supreme Conqueror

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2017
Posts
458
Reaction score
1,280
Moja kati ya habari inayosubiriwa kwa hamu na umma wa Tanzania ni yatakayojiri leo katika kikao cha dharura cha baraza la mawaziri aliloitisha leo Rais Samia ikiwa na ajenda mficho 4 unaoakisi kutoa majibu sahihi juu ya masuala yafuatayo:

1. Ajali ya ndege ya Precision Air kutokana na kile kinachoaminika kuwa zoezi la uokozi baada ya ajali hiyo ilikua chini ya kiwango

2. Suala la uhaba wa maji hususani jiji la dsm ambapo majibu ya wizara yakiwa tofauti na jitihada au mikakati yakukabiliana na janga hilo ikiwa inaendeshwa kisanii zaidi kuliko uhalisia

3. Ukatikaji wa umeme wa mara kwa mara ambayo inachangia kuongeza umasikini kwa wananchi wengi nchini na imekua ni kero hasa.

4. Mabadiliko ya hali ya hewa na suala la ukame ambalo linaendelea kuathiri sehemu kubwa ya nchi.
Hivyo watu wanamchukulia Rais Samia kama kiongozi mpole ukilinganisha na baadhi ya watangulizi wake hivyo umma wa Tanzania wanategemea kupokea maamuzi magumu kutoka kwa mhe. Rais dhidi ya Wasaidizi wake ambao wamekua siyo waaminifu kwake hasa kutokana na utendaji wao ama kuwa chini ya kiwango au kumsaliti kwa makusudi ili serikali yake ikose mvuto kwa Wananchi.
 
Mhe.Lukuvi na Kabudi warejeshwe kwenye Uwaziri hao ni majembe.
 
Moja kati ya habari inayosubiriwa kwa hamu na umma wa Tanzania ni yatakayojiri leo katika kikao cha dharura cha baraza la mawaziri aliloitisha leo Rais Samia ikiwa na ajenda mficho 4 unaoakisi kutoa majibu sahihi juu ya masuala yafuatayo

1.ajali ya ndege ya Precision Air kutokana na kile kinachoaminika kuwa zoezi la uokozi baada ya ajali hiyo ilikua chini ya kiwango

2.suala la uhaba wa maji hususani jiji la dsm ambapo majibu ya wizara yakiwa tofauti na jitihada au mikakati yakukabiliana na janga hilo ikiwa inaendeshwa kisanii zaidi kuliko uhalisia

3.ukatikaji wa umeme wa mara kwa mara ambayo inachangia kuongeza umasikini kwa wananchi wengi nchini na imekua ni kero hasa.

4.mabadiliko ya hali ya hewa na suala la ukame ambalo linaendelea kuathiri sehemu kubwa ya nchi.
Hivyo watu wanamchukulia Rais Samia kama kiongozi mpole ukilinganisha na baadhi ya watangulizi wake hivyo umma wa Tanzania wanategemea kupokea maamuzi magumu kutoka kwa mhe. Rais dhidi ya Wasaidizi wake ambao wamekua siyo waaminifu kwake hasa kutokana na utendaji wao ama kuwa chini ya kiwango au kumsaliti kwa makusudi ili serikali yake ikose mvuto kwa Wananchi.
Ukali upi huo mkuu?
 
Mama kasemaje? Hukwu kijijini mtandao leo kashida..

Kazi iendeleeeee..
 
Hicho kikao cha kawaida

Kutaka watu waamini unavyojiaminisha ni ujinga na kukosa maarfa
 
Hivyo watu wanamchukulia Rais Samia kama kiongozi mpole ukilinganisha na baadhi ya watangulizi wake
Sio mpole unaposema mpole unamkosea ni Powerless hana Power ndio anavyoonekana huko mtaani yaan yupo km kivuli tu ila nyuma kuna mtu anaendesha Nchi bila kuonekana yeye ndie anaeendesha Nchi sasa hivi, acha ukweli usemwe
 
Back
Top Bottom