Wananchi wawashambulia wabunge kufuatia adhabu kwa Askofu Gwajima na Silaa

Wewe ni mpumbavu tu,hata huko Ulaya kuna akina Joyce meyer,na wanakusanya watu kuliko akina Gwajima
 
Kwani Magufuri ndiye aliyesema uchumi umekua au,ni mabwana wenu WB na IFM,kawalaumu hao maana nyinyi anachosema mzungu mnaona sawa,labda la kusema Tanzania imeingia uchumi wa kati ndio mnaona uongo,ila chanjo ni salama kwasababu mzungu kasema 😃😄😄
 
Acha uwongo.

Nchi gani iliyo na idadi kubwa ya waliochanjwa, halafu idadi ya vifo haijapungua? Maambukizi yapo lakini vifo vimepungua sana.

Msiwe mnamezeshwa ujinga, halafu nanyi mnaubeba kama ulivyo.
Hata hapa kwetu vifo vimepungu sana ingawa waliochanja ni laki tatu katika watu milioni 60,sasa kama corona ingelikuwa inaua kama wanavyo shadadia akuna Mtanzania hata mmoja angelibaki, Maana mashariti akuna ayeyafuata,na chanjo watu wamezikataa
 
Hiyo adhabu waliyochangia kuwaadhibu wabunge wenzao itawagharimu na hawataamini ambapo mpaka iviongozi wa juu wataathirika kwa uamuzi waliofanya watunga sheria wasiojielewa
 
Kwani chanjo ni lazima? Au kwasababu ni ukoo wapanya hakuna kuumizana, hata kwenye familia hamwezi kukubaliana vyote!
 
Swala la chanjo Gwajima kapata uungaji mkono kwa wananchi wengi kwasababu kuu moja ni Legacy ya upumbavu wa Mwendazake kuwaongopea wananchi na kuwashawishi wananchi kuwa chanjo ni feki na kutumia kivuli Cha dini
Ww umedanganywa na mzungu.....
kila siku watu wanajazana mwendo kasi lakini hatuoni hiyo mass killing
 
Gwajima sauti ya mtanzania gani? Labda mtanzania mjinga mjinga! Mbona kipindi Cha raisi aliyepita alikuwa athubutu kuzungumza? Gwajima ni mpiga dili tu! Samia ni number one
Leo Rais yupo na Gwajiboy ziarani Kawe hapo vp!
 
Kwahiyo gwajima kutoa shutuma ambazo ameshindwa kuzithibitisha bado wananchi wengi wanashambulia wabunge? Ndio maana hata chizi anaweza kuongoza hii nchi kwa aina hiyo ya wananchi

mkuu
hii nchi wananchi walishaichoka ccm ndiyo sababu hata umshutumu rais kwa uongo, na wanajua ni uongo bado watakusupport. Watu hawawezi kuisupport serikali ya ccm tena. people are fed up.

ccm ilishakuwa kama kula ugali na maharage kila siku. tena ugali uwe wa dona, maharage chukuchuku na vyote vimepoa
 
Umesema ya kitalaamu ni sawa Ila Kuna ulimwengu mwingine nadhani haujui. Ambao wanaamua ulipwe Bei gani na uishi vipi.
Ugonjwa mpya umetoka wapi ama ulikuwa bado haujazaliwa,wazazi wa huo ugonjwa walikuwa hajawaoana na kumzaaa huyo gonjwa.
Unapolishwa na hao jamaa walioamua kuwa unatakiwa usome miaka mingapi ili uitwe mtalaamu wa kada fulani.
Nina Imani unamuona Elon Musk ameanza kupinga mtaala uliopo ameanzisha shule yake. Wanawe wanasoma huko wote.ana watt wasiozidi 20.

Tuje huku kwako Sasa.

Unajua kuwa ugonjwa umetengenezwa kwa maslahi ya wakubwa wa dunia.

Unakumbuka yule mmama aliyetutisha kuwa maiti zitagaa mitaani huku Afrika Mana tuna umasikini mkubwa wa kuto combat abrupt calamities.

So wakati unakula chakula Cha hao jamaa wanaokulisha please and please leave a room of pessimistism don't swallowed by them.
 

Gwajima ana hoja...kama wale waliochanja wanavyosema wana hoja. Na Slaa amekosea nini? Bunge nalo mtihani sana
 
Binafsi yangu nakataa hatuna wananchi wakuibana na kuikosoa Serekali iliyopo madarakani wala kuigusa Serekali labda TZ ingine ila sio hii kamwe. Walisha tujulia na wanatupindua watakavyo nyuma ya key board hahha tutasema sana njoo kiuhalisia hakuna atakaye jitokeza kamwe.
 
Mama yuko vizuri sana! Kama unafuatilia vizuri takwimu cha uchumi sasa najua unaelewa kuwa mshamba wenu alikuwa anatuchelewesha sana kimaendeleo
 
🤣🤣
Hayaa mkuu.....huo ulimwengu utakuwa unaujua wewe pekee nami siujui mkuu wangu......

Yasiyoonekana unayayakinishiaje?!!!

Inawezekana huo ulimwengu ndio uliotutengenezea magari tunayoendesha mimi na wewe....hapo ulimwengu huo ni mzuri....🤣

Ok Mzee wa "conspiracy theories"...

#Yetzer-Ha-Tov
 
Kuna kirusi kipya mzao wa corona

Gwajima yupo sahihi
 
Kwahiyo gwajima kutoa shutuma ambazo ameshindwa kuzithibitisha bado wananchi wengi wanashambulia wabunge? Ndio maana hata chizi anaweza kuongoza hii nchi kwa aina hiyo ya wananchi
Ushahidi aliotoa katika kamati umewekwa hadhalani au na wewe unaweweseka tu?
Kamatai imepewa ushahidi kisha ukaufunikwa na kuja na adhabu bila sisi wananchi kuambiwa askofu alikwa wapi,

Sasa wewe uliyekuwa kwenye kamati twambie alukwama wapi kwenye ushahidi?
 
Nyinyi wenye akili hebu tujibuni ukichanjwa chanjo huumwi corona na je nchi zinazo chanja mbona vifo bado viko vingi n wamechanjwa sasa kuna maana gani ya kuchanjwa kama bado nikich kwaanjwa lazima nijikinge.
Na je, chanjo wanazojichanja wao ni sawa na wanazotuletea? Kama ni sawa kwa nini wanataka kujiangamiza pamoja nasi? Kama si sawa wataalamu wetu wabobezi waliobobea kwa kutumia kodi zetu wako wapi? Mbona wamekaa kimya kama vile hawahusiki! Wametuachia vipofu tuongozane kuelekea kusikojulikana!! Wanafanya hivyo kwa maslahi gani? Tunadanganywa na kudanganyana wao wanatu enjoy tu. Sitaki kuamini kwamba hawapo labda kama wameenda majuu kula bata..
 
Wewe kuandika tu kiswahili ni majanga, unadhani unaweza kujua na kuchambua vizuri hoja za Askofu Gwajima kama “sauti ya nyikani” na kinachoendelea nchini!
Hivi hoja za Gwajima ni zipi kwa maslahi ya hoja yako uliyowasilisha hapa. Achana na maoni ya mitandaoni kwanza!
 
Gwajima kawasilisha ushahidi gani mkuu kwa maslahi ya hoja ya MsemaUkweli na afya ya mjadala huu?
 
Swala la chanjo Gwajima kapata uungaji mkono kwa wananchi wengi kwasababu kuu moja ni Legacy ya upumbavu wa Mwendazake kuwaongopea wananchi na kuwashawishi wananchi kuwa chanjo ni feki na kutumia kivuli Cha dini
vizuri sana na wale 50% mpk 80% ya wamarekani ambao wamekataa kuchanjwa na sasa wanapewa mrungura ili wachanjwe
itakuwa walisikiliza legacy ya kipumbavu ya mwendazake hasa baada video yake ya papai kukutwa na Corona kusambaa sana duniani
nimekupata sana bwana mkubwa
wamarekani wanamsikiza sana magufuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…