Wanaofanya mazoezi ya mbio (jogging) hayana faida kiafya, ni matokeo ya matangazo ya biashara ya Nike

Wanaofanya mazoezi ya mbio (jogging) hayana faida kiafya, ni matokeo ya matangazo ya biashara ya Nike

janabi muongo kuliko waongo, mimi maisha yangu nakula mlo mmoja tu saa kumi na moja jioni basi lakini bado nina kitambi na nina presha
Tatizo siyo kula mlo mmoja, tatizo ni unakula nini katika huo mlo wako mmoja? Unatumia Sukari, Ngano iliyokobolewa na ya Kisasa? Mafuta ya kupikia ya aina gani unayotumia? Unafanya mazoezi na mazoezi ya aina gani? Je unakunywa Pombe? Unakula sana Cabs? Sasa kabla hujamlaumu Janabi jiangalie wewe kwanza.
 
Kwa hiyo akili zako zinakubaliana na huyo mzungu

Wazungu wanavyosapoti ushoga, wewe unakubaliana nao??

Yaani mtu apate madhara kisa anafanya jogging??


Ficha ujinga wako
Huyo jamaa ameandika facts ila itakuwa ngumu kumuelewa sababu tulisha Kengeja kwenye akili zetu kwamba jogging inaleta afya,kwa uzoefu wangu wa mambo ya mazoezi nikiwa kama binadamu aliyeshiriki michezo kwa kipindi kirefu,karate,football na basketball,naweza kueleza kuwa mazoezi yoyote kama yatafanywa bila kipimo maalumu yatamuumiza anayeyafanya,mfano wataalamu wengi wanashauri ufanye mazoezi kwa nusu saa kila siku ili mwili wako na mifumo yake iwe fit,sasa hebu fikiria mtu anayekimbia jogging kuanzia saa kumi na mbili asubuhi mpaka saa tatu asubuhi anakuwa ametumia masaa mangapi?na je huo mda mwingi wa mazoezi alioutumia umemletea afya au ameuchosha na kuuzeesha mwili wake.
Watu wanatakiwa wajue kutofautisha kati ya mazoezi ya kuupa afya mwili na mazoezi ya mtu anayetafuta fitness kwa ajili ya mashindano au mechi fulani.
 
Duniani hapa hapajawahi kuwepo kitu kisicho na madhara. Chochote unachofanya lazima kiwe na kiasi.
Iwe kula
Kulala
Kunywa maji
Kujambba
Kufanya mapenzi
Kufanya kazi
Kuongea
Kukaa kimya
Kusali
Kutambika
Na kadhalika.
Mazoezi nayo yawe ya kukimbia, kunyanyua vitu vizito au kuogelea lazima ufanye kwa kiasi kutokana na mwili wako. Unapozidisha lazima utaharibu.

Binafsi nafanya mazoezi nakimbia na ya viungo. Pale napozidisha km huwa napata maumivu. Ila yamenisaidia kwa kiasi kikubwa mno.
1. Kupunguza uzito kutoka 98kg mpaka 78kg. Kwa urefu wa cm 180 ni inatosha.
2. Mwili kutochoka choka.
3. Nikiingia msimu wa mazoezi naacha na pombe.
4. Kuongeza ufanisi wa kazi.
5. Kupata usingizi mwanana hata kama nina stress
6. N. K n. K

Nakushauri fanya kwa kiasi usizidishe uta enjoy.
Hapa nasubiri kukuche nichape km 8 siku ianze vyema.
 
Nashangaa watu kuleta mashambulizi kwa mleta mada,mimi kila siku napanda ghorofa hadi ya sita,kwa miguu tena zaidi hata ya mara kumi,na huwa natoka jasho,uniambie nikafanye jogging ili nitafute nini?
Wewe ambaye kupata kwako riziki ni kwa kukaa muda mwingi ndiye unatakiwa ufanye hayo majogging napo ufanye kwa kiasi,ukixidisha ndiyo ile unakomaa unakua kama Kipchoge ambaye anaitwa kijana,ilhali ukimuona ni kama mbabu kabisa.
Mnamponda mleta mada kisa tena kamtaja mzungu,ilhali hata hizo jogging wamezileta haohao,madaktari wakitaka kujifunza sijui mambo ya upasuaji kwa njia ya kompyuta,wanaenda Ulaya kwa haohao wazungu kujifunza,then wanakuja huku kututibu,saa hizi mnamponda mtu kisa kataja mzungu.
Fanyeni jogging nyie mnaokaa tu,mimi siwezi na sina kitambi wala presha,maisha yangu ni zaidi ya jogging,mambo ya kukimbia bila kupima afya,matokeo yake ni kupanua mioyo yenu,mnaishia kulundikana cardiolgy mnasema mmerogwa,kumbe ni maxoezi bila mpangilio.
 
Jogging kuuza sura tu, wakalime mashamba wazalishe waache ubishoo wa mijini. Jogging jumamosi na jumapili, wakitoka hapo wanaenda kula kiti moto na mi beer ya kutosha. Jumatatu hadi ijumaa hakuna moderation, wana kula na kunywa hovyo, sasa hiyo afya itatokea wapi?
 
Tupostie picha yako hapa tukuone muonekano wako wa mwili kama uridhisha tutaacha, maana inavyosemekana mtu akitafuta excuse ya kutokufanya jambo basi hatoikosa.
Picha iko profile hapo.
Mimi natembea tu kwa miguu muda mwingi. Nikiamua kukimbia ni kidogo tu umbali mfupi tu.

Unene hauna uhusiano na mazoezi. Unauhusiano na elimu ya lishe. Huitaji kufanya mazoezi ili usinenepe. Unahitaji kula vizuri ili uwe na mwili wa kawaida wenye afya.

The safiest exercise in the world is Walking.
 
Nashangaa watu kuleta mashambulizi kwa mleta mada,mimi kila siku napanda ghorofa hadi ya sita,kwa miguu tena zaidi hata ya mara kumi,na huwa natoka jasho,uniambie nikafanye jogging ili nitafute nini?
Wewe ambaye kupata kwako riziki ni kwa kukaa muda mwingi ndiye unatakiwa ufanye hayo majogging napo ufanye kwa kiasi,ukixidisha ndiyo ile unakomaa unakua kama Kipchoge ambaye anaitwa kijana,ilhali ukimuona ni kama mbabu kabisa.
Mnamponda mleta mada kisa tena kamtaja mzungu,ilhali hata hizo jogging wamezileta haohao,madaktari wakitaka kujifunza sijui mambo ya upasuaji kwa njia ya kompyuta,wanaenda Ulaya kwa haohao wazungu kujifunza,then wanakuja huku kututibu,saa hizi mnamponda mtu kisa kataja mzungu.
Fanyeni jogging nyie mnaokaa tu,mimi siwezi na sina kitambi wala presha,maisha yangu ni zaidi ya jogging,mambo ya kukimbia bila kupima afya,matokeo yake ni kupanua mioyo yenu,mnaishia kulundikana cardiolgy mnasema mmerogwa,kumbe ni maxoezi bila mpangilio.
Sasa eti mtu anakimbia kilometer hadi sita au kumi na hana vision ya kuwa mwanariadha kisa anataka atume takwimu za App ya adidas mitandaoni aonekane anakimbia.

Huu ni ujinga na kupoteza muda wa uzalishaji.
 
Mazoezi ya jogging ni mazuri kwa afya na uimara wa mwili hasa kwa nyakati hizi za vyakula vya viwandani .. Huyo mzungu ana lake jambo

Sent using Jamii Forums mobile app
Huwezi kula vyakula vya kiwandani ili uje ufanye mazoezi.
Tembea kwa miguu tu mkuu katika shughuli za kila siku inatosha.

Vyakula vya kiwandani vipo tangu industrial revolution miaka ya 1800 lakini hadi kesho hata Bill gate huwezi kumkuta anafakamia kila kitu ili aje afanye mazoezi.
 
Siku hizi limeibuka vuguvugu la watu kukimbiakimbia mbio mabarabarani. Unaweza kukuta mmoja mmoja au kikundi.

Miaka ya zamani hii kitu ilikuwa haipo maana maisha ya mtanzania wa kawaida ni jogging na nyongeza.

Leo katika pitapita zangu online nimekutana na mzungu anaponda hiyo kitu. Anasema ni Nike ambao walipromote hizo jogging ili wauze viatu huko US. Hii ilikuwa mwaka 1965.

Haina maana kukimbia klm hadi 10 eti kiafya wakati ungetembea kwa miguu klm hata moja na unakuwa fiti kabisa.

Wengi wa joggeres waliokubuhu wanasura za Kichovu, kizee na zisizo na nuru. Wale chronic joggers, Pia hapo baadae watakuwa wanaugua magonjwa ya misuri na kutetemea.

Haijengi afya, inaua afya.

Ni hayo tu.
Ushauri:
The safiest exercise in the world is Walking.
Chakula kina play part kubwa sana kwenye swala la afya kuliko jim na Joging
 
Waache wafanye jogging, jioni nakaa zangu pale kwa Sunda barabara ya kuelekea Ngaramtoni ya juu kuna wadada na mijimama inafanya mazoezi ya kuonesha chupppi zao na kutingisha mitako yao ,tunasuuza macho
 
Huyo jamaa ameandika facts ila itakuwa ngumu kumuelewa sababu tulisha Kengeja kwenye akili zetu kwamba jogging inaleta afya,kwa uzoefu wangu wa mambo ya mazoezi nikiwa kama binadamu aliyeshiriki michezo kwa kipindi kirefu,karate,football na basketball,naweza kueleza kuwa mazoezi yoyote kama yatafanywa bila kipimo maalumu yatamuumiza anayeyafanya,mfano wataalamu wengi wanashauri ufanye mazoezi kwa nusu saa kila siku ili mwili wako na mifumo yake iwe fit,sasa hebu fikiria mtu anayekimbia jogging kuanzia saa kumi na mbili asubuhi mpaka saa tatu asubuhi anakuwa ametumia masaa mangapi?na je huo mda mwingi wa mazoezi alioutumia umemletea afya au ameuchosha na kuuzeesha mwili wake.
Watu wanatakiwa wajue kutofautisha kati ya mazoezi ya kuupa afya mwili na mazoezi ya mtu anayetafuta fitness kwa ajili ya mashindano au mechi fulani.
Seems like unafosi kuandika vitu out of hoja

JOGGING maanayake ni kukimbia taratibu nukta. Hio ndio maana yake mtu kukimbia masaa 10 Ni yeye mwenyewe na ukiweka hoja hio hakuna zoezi ambalo watu hawafanyi kwa zaidi ya masaa mawili kunyanyua chuma, Boxing, Cross-Cutting, Yoga, Cardio nk hayo mazoezi yote Kuna watu wanafanya zaidi ya lisaa je hayana faida just kwasababu Kuna watu wanna Overdo.... Strictly kwenye definition ya zaoezi sio umemuona Juma kanyanyua chuma kutwa mzima unakuja hitimisha chuma hakina faida WHAT THINKING IS THIS.
 
Back
Top Bottom