Wanaosema Rais Magufuli hajui Kiingereza leo amewasuta

Wanaosema Rais Magufuli hajui Kiingereza leo amewasuta

Kwa mazungumzo yale inaonekana wazi kabisa kuna kikundi cha watu hawataki au wanapinga kabisa matumizi ya lugha ya kiswahili, lkn huo ni unafiki mkubwa maaana huwezi kuwa mzalendo wa kweli halafu wakati huo huo unadharau lugha ya Taifa lako,
huwezi kujifanya una muenzi baba wa taifa halafu wakati huo huo unadharau lugha ya kiswahili amabayo imeasisiwa na Baba wa Taifa hili na ndiyo kitu pekee kilicho tuunganisha watanzania wote hadi leo hii tuko wamoja.
najivunia kuwa na Rais Jasiri shujaa asiye tetereka maenye kujivunia lugha yake.
Hongera sana JPM

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahah hahaah jiwe na kiingereza wapi na wapi [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hii inaonyesha shuleni watu wanakariri badala ya kuelewa. Kwa vyovyote vile huwezi kujua kuandika kiingereza lakini ukashindwa kuongea.
Mkuu jaribu kufanya uchunguzi hicho ulichokiongea,hilo tatizo la watu kuweza kuandika kiingereza na kushindwa kukiongea lipo duniani kote na ndio maana hata matangazo ya english course utasikia wanasema wanafundisha kiingereza cha kuandika na kuongea.
 
Da!😂😂😂😂😂 Valve eti vali,piston eti biston,bits an'pieces eti vitama,power stroke eti pigo la nguvu taabu kwelikweli clutch eti mfumbato 🙆🙅🙇
 
“Nilipoingia madarakani nikaanza kutoa hotuba kwa Kiswahili, niliambiwa sijui Kiingereza wala sikujali, UDSM nimekaa miaka mitatu nikisoma masomo yangu ya Sayansi, Chemistry na Mathematics zote zinaandikwa kwa Kiingereza, lakini Mtu akasema sijui Kiingereza”-JPM kwenye Siku ya Sheria Dodoma leo.

“Nimefanya PHD bado wanasema sijui Kiingereza, na nikakaa mwaka mzima Uingereza, sijui nilikuwa nazungumza Kisukuma kule!, wakasema sijui Kiingereza, niliamua kuzungumza Kiswahili na kuki-promote kwasababu ni lugha iliyoachwa na Baba wa Taifa”-JPM

View attachment 1691833
Tutaaminije kama kweli anajua kiingereza bila kuongea? Aongee basi tumsikie. Hajui.
 
Basi hayo maelezo yake angeyaongea kwa kiingereza fluently ili tuamini, aseme tu ukweli hajui kiingereza mbona sie wengine tuna ma PhD lakini lugha inatutatiza.
Kweli kabisa mkuu. Kuna Profesa mmoja kule UDSM hawezi kuongea hata sentensi moja ya Kiingereza lakini ni Profesa anafundisha kwa kusoma notes.
 
“Nilipoingia madarakani nikaanza kutoa hotuba kwa Kiswahili, niliambiwa sijui Kiingereza wala sikujali, UDSM nimekaa miaka mitatu nikisoma masomo yangu ya Sayansi, Chemistry na Mathematics zote zinaandikwa kwa Kiingereza, lakini Mtu akasema sijui Kiingereza”-JPM kwenye Siku ya Sheria Dodoma leo.

“Nimefanya PHD bado wanasema sijui Kiingereza, na nikakaa mwaka mzima Uingereza, sijui nilikuwa nazungumza Kisukuma kule!, wakasema sijui Kiingereza, niliamua kuzungumza Kiswahili na kuki-promote kwasababu ni lugha iliyoachwa na Baba wa Taifa”-JPM

View attachment 1691833
Aiseee... Kwani kiingereza kinapimwaje? Kwa makemia, ma PHD, ma doktoreti, kwa kukiongea au kwa namna ipi? Kwa hiyo yule mkinga aliyekuwa na digrii saba (Tuntemeke Sanga), kwa wakati wao, ndo alikuwa anakijuwa kiingereza kuliko wote hapa Tanzania, kwa vile tu alikuwa na manyuzi (degree) mengi?
 
Raisi Magufuli ni sawa na maraisi Putin, Xi Jinping, Angela Markel, Emanuel Macron na wengine ambao hutumia lugha mama.

Hicho kiingereza ni lugha kama lugha zingine za kawaida sana.

Kufahamu kuzungumza kiingereza hakumaanishi wewe umesoma sana na kuelimika.
Ni kweli NA KUNA VICHAA WANAKIMWAGA KIINGLISHI HUKO UINGEREZA BALAA...!! Lakini kama hufahamu, kili tu, na hata usipokili,KIKIVUNJA TUTAKUSIKIA TU KWAMBA UNAKIVUNJA HASWA... !!!
 
Nani kasema Ph.D. holder lazima awe mater of English. Kwani Ph.D. lazima ifanwe kwa Kingereza? Nchi nyingi Ph.D. zinafanywa kwa lugha zao, siyo Kingereza. Muhimu kwenye Ph.D. ni somo. Kama Ph.D. ni kemia lazima uwe matser wa kemia siyo kingereza. Ila tutakushangaa kama una Ph.D. ya Kingereza huku hujui kingereza cha kuandika.
Elimu ya Tz, kuanzia form one mpaka PhD iko kwa kiingeereza. Na PhD za Tz lazima zifanywe kwa Kiingeereza except PhD ya kiswahili.

Hivyo ni kitu abnormal kwa kwa mtu kumaliza PhD hajui Kiingeereza cha kuongea au anaongea hovyo.

Hata kama ni PhD ya kemia, bado hiyo kemia Katika usomaji na kufanya utafiti inakua addressed kwa Kiingeereza.
 
Na hiyo ndio inadhibitisha anajua Kingereza?

Mbona hili suala linamuuma sana?

Akubali hajui Kingereza wala Kiswahili,vyote hajui

Yeye anasema anajua,ila wananchi wake know otherwise!
Ukisema hajui kiingereza sasa hiyo elimu yake ameipata vp kwa lugha ambayo haijui?
 
Raisi Magufuli ni sawa na maraisi Putin, Xi Jinping, Angela Markel, Emanuel Macron na wengine ambao hutumia lugha mama.

Hicho kiingereza ni lugha kama lugha zingine za kawaida sana.

Kufahamu kuzungumza kiingereza hakumaanishi wewe umesoma sana na kuelimika.
Kwani xi jipnping na putin masomo yao wamesoma kwa kiingereza?hoja ni kwanini msomi mwenye level ya PHD asiijue lugha aliyotumia kiasi cha kufikia hiyo ngazi ya ufahamu?
 
Hv haiwezekani mkuu wa nchi kuajiri waalimu wabobezi wa lugha mbalimbali walau kwa mwaka asome lugha mbili? Naona kama suala ambalo liko ndani ya uwezo wake hv.
 
Elimu ya Tz, kuanzia form one mpaka PhD iko kwa kiingeereza. Na PhD za Tz lazima zifanywe kwa Kiingeereza except PhD ya kiswahili.

Hivyo ni kitu abnormal kwa kwa mtu kumaliza PhD hajui Kiingeereza cha kuongea au anaongea hovyo.

Hata kama ni PhD ya kemia, bado hiyo kemia Katika usomaji na kufanya utafiti inakua addressed kwa Kiingeereza.
Kushindwa kuongea kiingereza vizuri ni tofauti na kutokujua kuongea kiingereza kabisa,w atanzania wengi kiingereza cha kuongea kinawashinda hawawezi kuongea vizuri na si kwa sababu ya kiwango cha elimu hadi tufikiri kuwa mwenye PHD ndio ataweza kuongea vizuri.
 
Back
Top Bottom