Wanaume tuelimishane ulinzi, ni silaha gani nje ya bunduki ni nzuri kuimiliki sehemu unayoishi?

Wanaume tuelimishane ulinzi, ni silaha gani nje ya bunduki ni nzuri kuimiliki sehemu unayoishi?

Chukua mfano wamefanikiwa kuingia mipaka ya eneo lako, wewe ndio mwanaume upo chumbani ama upo na wanafamilia chumbani, kwenye situation kama hiyo ni silaha ipi nzuri kukabiliana na wavamiaji?

Binafsi nina firimbi zile za walinzi na sungusungu, zinasaidia kumpa wenge mvamiaji kudhani kwamba pana ulinzi shirikishi, filimbi hizi hazizidi elf 2 kwa machinga.

Kwa mashambulizi ya mbali nina manati na golori za chuma, sio ya kuyachukulia poa hata kidogo, nikivuta hadi mwisho nikiachia, lazima ukae ama ubebwe.

nina rungu kama la komredi kipepe kwa mashambulizi ya ana kwa ana man to man, lakini ningependa tuelimishane zaidi.

Kupitia uzi huu tuelimishane silaha za kuwa nazo, kuzificha, matumizi sahihi, n.k.
Silaha nzuri kuliko yote ni kuishi na majirani vizuri, hasa wale third class.

Hautakaa uvamiwe.
 
Mimi nimenunua tundikali nimeiweka kwenye syringe na iko peaceful packed kwenye drawer ya MEZA ya kitanda.... yaani ukijichanganya naispray usoni chap
Hivi tindikali huwa inauzwa kwenye maduka ya kemikali au hata pharmacy?
 
Usikose panga
Nyundo
Rungu
Msumeno
Tochi


Kuna taa za nje zimeona wengi wanazitumia
Zinasense,mtu akipita tu nje ya fance Yako taa inawaka sana.
Hiyo kidogo itamshtua mwizi.
 
Unaweza ukawa na vyote na wakakutight kama kawaida tu.

Mwizi aliyeamua kuvunja akaingia ndani anajua ni either afe yeye au wewe, do he's prepared.

Tuliowahi kutaitiwa tunaelewa, wabebe kila kitu waniache na familia.

Though sikosi sime, manati, koroba, tochi ya mwanga mkali.
 
Silaha nyingine ni kujichanganya simetimes na vijana kijiweni,Mimi huwa napata time ya kukaa na vijana wahuni,nanunua mizinga ya k vant pack za sigara tunakaa,unakuta wanajimaliza wenyewe .utasikia sema nin mshua hata nisikie jambo gani baya kwako ntakustua tuu huna bayaa.kuna siku niliibiwa nondo nje walirudisha
Kuchangamana na wahuni inategemea sana personality na mwonekano wako, sie wengine tuna sura za kiaskari afu ni introverts tukifika tu maeneo walokaa wahuni wanahis tumeenda kuwapeleleza.
 
Mamati,Kaka manati usikose home.Rungu mpaka mkalibiane lakini manati kwa mbali tuu,Kama una wife hakikisha anayo manati ba umfundishe.Alikuja mwizi home nikastuka nikasogeza kioo nikamuweka usawa wa upenyo wa grili nikampa golori ya kichwa.Akaanguka majirani wanasema nina bastora.
Utawapiga wangapi na hiyo manati, yanakuja yamevaa makoti mazito na mizura hiyo manati ni kama unawakuna tu na wakijua uelekeo ilipotoea kwisha habari yako.

Machete ndio dawa yao, ukishamshusha mmoja wao bega wakiona damu imemwagika hawakai hiyo sehemu hata sekunde wanajua wamevamia nyumba ya jambazi mwenzao.
 
Silaha yangu kubwa ni kutokuishi Keko, Temeke, Vinguguti, Tandale, Mbagala na maeneo yote yasio na watu waliostaarabika. Hio ndio silaha ya kwanza.

Ya pili sipendagi vurugu vurugu kwahio sijiweki katika mazingira ya kutibuana na watu. Nahakikisha marafiki na jamaa ni wengi kuliko maadui.
Basi utakuwa unaishi peponi wewe.
 
Silaha nzuri ili usalimike na wale majamaa ni kuwa na HELA.
Wakikuvamia ujue wana clue kwamba una mzigo ndani na pengine hadi amount kamili.
Sasa ili kunusulu uhai wako na familia kwaujumla yapasa uyasikilize yale majamaa hayana maskhara.
Huku kumiliki bunduki sijui manati na podo ni kubahatisha na timing tu!
Kumbuka jambazi mpaka anaingia ndani ujue kauza roho.

Mbinu nzuri ya kujizatiti na majambazi ni kuishi na majirani zako vizuri pasipo kujenga mazoea yanayopita kiwango cha ustaarab.
Pindi majambazi wakikuvamia, chap una escalate incidency kwa majirani. Kelele au kuvizia kwa kutokea nje ni rahisi sana kutibua mipango na kuzua taharuki kwa majambazi waliojipanga kwa uvamizi.
Najengaje mazoea na jrani wakati nyumba yangu ina fence, yake ina fence, yaan hakuna tunachoshare, wala kuingiliana!! Natoka sa moja narudi saa 1 usku, huyo jran tutazoeana sa ngap?
 
Tafuta mkia wa Taa samaki au kausha Mwanzi unaoweza kuushika mkononi vizuri na hakikisha angalau umekuzidi kidogo urefu. Utaja shukuru siku nyingine
 
Najengaje mazoea na jrani wakati nyumba yangu ina fence, yake ina fence, yaan hakuna tunachoshare, wala kuingiliana!! Natoka sa moja narudi saa 1 usku, huyo jran tutazoeana sa ngap?
Mkuu hapo ndo unapokosea sasa kujifanya upo busy na matawi ya juu. Matukio ya ujambazi husukwa nje huko kazini, kwenye biashara zako, marafiki ama hata ndugu lakini lazima ili yatekelezwe kiufasaha kuna mtu watamplant hapo nyumbani hasa mara nyingi ma house gal hutumiwa sana kujua chumba unacholala na uwezekano wa wapi unahifadhi pesa na lini uliingia na zigo la pesa.

Sasa ikiwa kama una mahusiano mazuri na jirani zako japo wawili mkapeana mikakati ya kujihami na matukio ya ujambazi, ni rahisi sana kuharibu mipango ya uvamizi kuliko kujihami pekeyako wakati tayari umevamiwa.

Huwezi kuwa busy siku zote kiasi cha kukosa upenyo wa kuonana na majirani zako. Kuna matukio mhimu lazima yawakutanishe i.e msiba na mikutano ya mtaa siku za wkend n.k
Jitahidi ubadili mindset mkuu...!
 
Well umeongelea manati ni sawa yanaweza kukusaidia kwa mbali,lakini chukua mfano wameishafanikiwa kuingiza sebuleni wewe uko chumbani, kwenye situation kama hiyo bastola ni muafaka haswa kama umejificha kwenye Kona fulani unawadondosha mmoja mmoja, lakini swali je ni Kila mmoja wetu ana sifa ya kumiliki bastola jibu ni hapana,

trick inayoweza kukusaidia ni kuwa na switch inayoweza kuzima umeme nyumba nzima, halafu unavaa miwani Yako ya night vision, huku umeshika chupa ya plastic ya nusu Lita, zile za maji ya kunywa, ikiwa imejaa maji yaliyochaganywa na pilipili ya unga Kali kabisa kifuniko kikiwa kimetobolewa tundu dogo unene wa njiti mbili za kiberiti, kwa sababu hawakuoni wewe unawaona unawaminyia maji ya pilipili kwenye macho, wakati wanafikicha macho unamaliza game na silaha za jadi halafu unawasachi mifukoni kama walitembea na hela'then unaripoti tukio kwa vyombo vya usalama.
Kwani wao hawatembei na torch?
 
Back
Top Bottom