Wanaume waililia Serikali ya Kijiji kisa kunyimwa Unyumba na Wake zao

Wanaume waililia Serikali ya Kijiji kisa kunyimwa Unyumba na Wake zao

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakuu

Mwenyekiti wa kijiji cha Mloda kata ya Mlowa barabarani, wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Adam Philemon amesema miongoni mwa malalamiko yaliyokithiri katika kijiji hicho ni wanaume kunyimwa unyumba, huku akiwataka wanaume kutoa taarifa za vitendo hivyo kwenye sehemu husika ili kutokomeza janga hilo.
1733484222861.png
Philemon pia alibainisha kuwa wanaume wanaendelea kunyanyaswa na wake zao hasa wenye vipato vikubwa, hasa kipindi cha mwisho wa mwaka wanapovunja vikoba vyao. Aidha, wanawake wa kijiji hicho, wakiongozwa na Mariam Mahajile, wameeleza kuwa changamoto hizi mara nyingi husababishwa na wanaume kushindwa kuwajibika kifamilia au kuwa na uhusiano nje ya ndoa.
"Na kuna kesi moja ya mwanamke alikuwa hampi mume wake unyumba na haki hiyo anampatia mtu mwingine ambaye sio mume wake yaani ni kama anaishi na mume lakini unyumba anapewa mtu mwingine."
"Mwezi huu wa Desemba wakati akina mama wanavunja vikoba vyao tumekuwa tukipokea malalamiko mengi ya wanaume kunyanyaswa na wake zao sisi kama serikali tunayapata sana malalamiko haya kutoka kwa wanaume wengi," amesema Philemon.

Nuru Mpanda kutoka Jukwaa la Wakulima Wanawake amewashauri wanawake kuwaheshimu waume zao hata wanapokuwa na vipato vikubwa, huku Mratibu wa Mradi wa TIF, Happy Itros, akielezea juhudi za mradi huo katika kusaidia wakulima wadogo hasa wanawake katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kupitia kilimo endelevu.
1733484303241.png
 
Wakuu

Mwenyekiti wa kijiji cha Mloda kata ya Mlowa barabarani, wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Adam Philemon amesema miongoni mwa malalamiko yaliyokithiri katika kijiji hicho ni wanaume kunyimwa unyumba, huku akiwataka wanaume kutoa taarifa za vitendo hivyo kwenye sehemu husika ili kutokomeza janga hilo.
Philemon pia alibainisha kuwa wanaume wanaendelea kunyanyaswa na wake zao hasa wenye vipato vikubwa, hasa kipindi cha mwisho wa mwaka wanapovunja vikoba vyao. Aidha, wanawake wa kijiji hicho, wakiongozwa na Mariam Mahajile, wameeleza kuwa changamoto hizi mara nyingi husababishwa na wanaume kushindwa kuwajibika kifamilia au kuwa na uhusiano nje ya ndoa.
"Na kuna kesi moja ya mwanamke alikuwa hampi mume wake unyumba na haki hiyo anampatia mtu mwingine ambaye sio mume wake yaani ni kama anaishi na mume lakini unyumba anapewa mtu mwingine."
"Mwezi huu wa Desemba wakati akina mama wanavunja vikoba vyao tumekuwa tukipokea malalamiko mengi ya wanaume kunyanyaswa na wake zao sisi kama serikali tunayapata sana malalamiko haya kutoka kwa wanaume wengi," amesema Philemon.

Nuru Mpanda kutoka Jukwaa la Wakulima Wanawake amewashauri wanawake kuwaheshimu waume zao hata wanapokuwa na vipato vikubwa, huku Mratibu wa Mradi wa TIF, Happy Itros, akielezea juhudi za mradi huo katika kusaidia wakulima wadogo hasa wanawake katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kupitia kilimo endelevu.
Wanawake wana roho mbaya na ubinafsi vitu vyao kuvitoa Kwa waume zao wanaona ni hasara ila mwanaume kutoa Kwa ajili ya familia hapo ni sawa mbaya zaidi hata unyumba wanatunyima, wanawake badilikeni
 
🖐️ Mwenyezi Mungu nijalie mume mwema..naapa akiniheshimu nitamuheshimu,akinipenda nami nitampenda zaidi na kumtunza.
Katika shida na raha ntashikamana nae.akimess up things naachana nae

Hawa wanaume wanaolalamika ni wale waungwana,wale wengine tayari wasahatengeza nyumba ndogo na kukimbilia makahaba sababu ya kunyimwa unyumba.
 
🖐️ Mwenyezi Mungu nijalie mume mwema..naapa akiniheshimu nitamuheshimu,akinipenda nami nitampenda zaidi na kumtunza.
Katika shida na raha ntashikamana nae.akimess up things naachana nae

Hawa wanaume wanaolalamika ni wale waungwana,wale wengine tayari wasahatengeza nyumba ndogo na kukimbilia makahaba sababu ya kunyimwa unyumba.
Nafikiri wanawake kuwanyima unyumba waume zao Inasababishwa na vitu viwili:

1) Wanaume kuwa pasua kichwa, mwanaume unakuta hahudumii pesa ya chakula nyumbani, mume ana michepuko, mume mnyanyasaji ana gubu etc

2) Wanawake kuolewa sababu ya mali za mwanaume, maisha yanakua magumu mdada anaona bora aolewe ili apate unafuu wa kiuchumi (kwa mgongo wa kuhudumiwa), au unakuta mdada anaolewa sababu muda wa kuolewa umefika 30 years plus ila tangu mwanzo anakuwa hampendi mumewe Sister Abigail
 
🖐️ Mwenyezi Mungu nijalie mume mwema..naapa akiniheshimu nitamuheshimu,akinipenda nami nitampenda zaidi na kumtunza.
Katika shida na raha ntashikamana nae.akimess up things naachana nae

Hawa wanaume wanaolalamika ni wale waungwana,wale wengine tayari wasahatengeza nyumba ndogo na kukimbilia makahaba sababu ya kunyimwa unyumba.
Nao waliapa hivyohivyo cute
 
Back
Top Bottom