Wanaume wengi tulioko JF hasa MMU ni reject

Wanaume wengi tulioko JF hasa MMU ni reject

Habari.

Wakuu sina lengo la kukashifu watu ila naomba niweke wazi mtazamo wangu kuhusu wanaume wenzangu tulioko MMU.

Kwa muda ambao nimekua mwanachama humu,nimegundua kua wanaume wengi wa humu ni reject mtaani.

Idadi kubwa ya wanaume humu huwa ni kulalamika tu hawakubaliki,wameachwa,hawapati wachumba nk japokua idadi ya wanawake ni kubwa kuliko wanaume,huwa najiuliza hao wanawake wasiopatikana ni wapi? Nimekuja kugundua kwamba vidume wenzangu humu wengi ni reject,hawana sifa wanawake wanazozitaka.

Nenda love connect,mwanamke ataandika anataka mwanaume,akaambatanisha vigezo vichache,tena vya kawaida sana lakini ataishia kukatishwa tamaa na wanaume kua vigezo hivyo ajiumbie mwanaume wake maana hawezi kumpata.

Utakuta mwanamke kaandika anataka mwanaume mrefu,mwenye elimu kuanzia diploma,miaka 30,awe na ajira au kazi binafsi,masharti ya kawaida kabisa,ataishia kuambiwa ajiumbie,najiuliza kweli watu wenye sifa hizo au zaidi hawapo MMU?

Maana yake ni kwamba wanaume wengi wa humu ni wafupi,wasio na kazi,walioishia sekondari.

Sasa nimekubali kwamba wengi wetu humu ni reject.

Cha msingi nionacho hapa ni kwamba ume-FAKE ID na kujifanya mwanaume!! Inauma sana kuwa Ke, umri unaenda alafu unakuwa reject kila kona, sasa umekuja na ujio mpya wa jinsia!
Wewe kama ungekuwa Mwanaume unaletaje hoja ya mwanaume kuwa reject kwa wanawake????
Labda sijui maana ya reject! Ila Ngoja nikwambie kuhusu sisi wanaume, ukitongoza wanawake sita, sio wote watakubali, kwa hiyo, we were made to be rejects at some point inapokuja suala la mahusiano!! Ndo maana tukikataliwa, hatuachi mpaka kieleweke! Sasa kama wewe 'mwanaume' unatongoza mwanamke mmoja, ukikataliwa unakuja kulalamika huku, wewe ni mwanaume suruali!
Vinginevyo wewe ni SUPU YA MAWE weird tafiti zako!
 
Last edited by a moderator:
hahahaaa!! leo ni leo, mmekamatika!!!
 
Wajua sijaelewa, sisi ni reject kivipi??? Huko mtaani wanawake wametureject au humu jamvini??

hahahaaa!! hujaelewa eti!!! haya endelea kusoma labda utaelewa!
 
Kwanza salaam kwako“
Pili naona wewe sio mwanamme wewe ni mwanamke“kama ungekua mwanamme kweli usingeandika hayo ulioandika”kama kukataliwa kuwa reject ni wewe na kwenu huko`
Tatu kinachoonekana wewe ni bwana mdogo sana hata definition ya what is life hujui`fahamu wanaopitia mitandao wapo watu wa aina mbalimbali na kazi mbalimbali wengine wapo na familia zao wengine wafanyabiashara”wengine kwenye taasisi mbalimbali” wengine wehu kama wewe”
Kwa hiyo usirealize kuwa watu wako kama ulivyoandika”
Inavyoonyesha wewe unatafuta wanawake humu thus why umeandika hivyo”
Jitahidi kama mwanamme uwe kamili ila kama ke sawa tu ndiyo zenu”
Mwisho kumbuka jinsia moja hua hazipondani wewe nahisi ni jinsia ke•

Teh teh teh
 
.......Daah! simo katik hao uliowafanyia huo utafiti wako. Vigezo vya hao reject vyote vimenipitia pembeni. Vile vile utafiti wako wa kikuda subiri wenye sifa hizo ulizozitaja waje kukurushia mawe.
 
Habari.

Wakuu sina lengo la kukashifu watu ila naomba niweke wazi mtazamo wangu kuhusu wanaume wenzangu tulioko MMU.

Kwa muda ambao nimekua mwanachama humu,nimegundua kua wanaume wengi wa humu ni reject mtaani.

Idadi kubwa ya wanaume humu huwa ni kulalamika tu hawakubaliki,wameachwa,hawapati wachumba nk japokua idadi ya wanawake ni kubwa kuliko wanaume,huwa najiuliza hao wanawake wasiopatikana ni wapi? Nimekuja kugundua kwamba vidume wenzangu humu wengi ni reject,hawana sifa wanawake wanazozitaka.

Nenda love connect,mwanamke ataandika anataka mwanaume,akaambatanisha vigezo vichache,tena vya kawaida sana lakini ataishia kukatishwa tamaa na wanaume kua vigezo hivyo ajiumbie mwanaume wake maana hawezi kumpata.

Utakuta mwanamke kaandika anataka mwanaume mrefu,mwenye elimu kuanzia diploma,miaka 30,awe na ajira au kazi binafsi,masharti ya kawaida kabisa,ataishia kuambiwa ajiumbie,najiuliza kweli watu wenye sifa hizo au zaidi hawapo MMU?

Maana yake ni kwamba wanaume wengi wa humu ni wafupi,wasio na kazi,walioishia sekondari.

Sasa nimekubali kwamba wengi wetu humu ni reject.

Leo umekumbuka kuvaa pampers.
 
Aisee,wewe ni me?hebo ngoja ninywe maji nije.

Umesema wewe ni me,unataka tuonane nione kama una sifa au ni mzuri,real?unataka nikuone kisha nije kukusifia humu?

Tafadhali,nina mpenzi wangu na ana wivu sana. Ushauri,nenda mombasa mkuu ndio wanawatafta watu kama wewe.

Dogo haujui unachoandika, shule zimefungulia siku nyingi nashangaa wewe hadi leo bado haujarudi shule...kasome dogo sisi kaka zako!!!!
 
Ukinidelete wenzako wananidownload tena na antivirus protection juu.

Mwanaume kama uko vizuri unapaswa kumiliki wanawake wanne kwa uchache ili kuondoa uhaba wa wanaume unaoikabili dunia.

Watu wa mashambani thread zao utawagunduwa tu hapa watu wanaconect the world na kumeet new friend and new challenge.

Hawa ndio aina ya watu Facebook marafiki zake ni walewale wa mtaani badala ya kuconnect na watu wapya.

Huu ni ukenge pasee.
 
Mtoa mada unahitaji maombi hakika.Awali ya yote ukitaka kudig in mwanamke yyote anaetafuta mwanamume kwa JF ndio rejected kitaa au mahali alipo inapelekea kuanza kutafuta wanaume mtanadaoni.inshort hanamaadili kabsa ya Kiungu au kiafrika.Pili sisi wanaume ndio tunapropose kwa wanawake sasa wanawake kututokea sisi hatujazoea hizo culture mwambie aende Ulaya huyo mwanamke.Tatu hakuna mwanaume ambae hanaweza kukosa mwanamke katika sehemu alipo labda awe ana mapepo.
Next time leta mada poa hacha ujinga.
 
Back
Top Bottom