Wanawake mnaojenga nyumba kwa siri bila mwenza kujua huwa mnamaanisha nini?

Wanawake mnaojenga nyumba kwa siri bila mwenza kujua huwa mnamaanisha nini?

Hivi ni kweli hamna uelewa wa haya mambo ya migogoro ya kifamilia na kadhia za talaka au kutengana.

Wanaume wangapi wanaendelea kuhudumia watoto ipasavyo baada ya ndoa kuvunjika na bila kushurutishwa na ustawi wa jamii au mahakama? Wapo ila ni wachache, wengi wanaamini mkiachana jukumu la watoto ni la mama.

Ndoa ikivunjika, taratibu za kutafuta mpaka kupata talaka inaweza kuchukua miaka. Hicho kipindi chote hao watoto uliomwachia mkeo wanaishije? Kama mke hajasimama kiuchumi ni either watoto watateseka au atarudi kwao kusaidiwa kulea na ndugu zake.
Naona kama majadiliano mengine tunalazimisha tutoke nje ya maisha yetu ya kiuhalisia kwenye jamii.

Kuna shida kubwa sana ya malezi ya watoto na mwanamke kwa kiwango kikibwa ndiye anayeathirika ndoa ikivunjika. Sheria za mgawanyo zimewekwa ili kulinda maslahi wa wanandoa wote na watoto. Kisheria, ni kosa kuidanganya mahakama na kuficha mali iwe amefanya mwanamke au mwanaume.
Tena wanaume wengi akijitahidi sanaa kuhudumia mtoto basi atamlipia ada tu, kuhusu kula, mavazi, afya jukumu anaachiwa mwanamke.
 
Wana akili! Kwa ndoa za nyakati hizi wanajua wataachika
muda wo wote.
Sasa akiachika afikie wapi?
 
Unafikiri wanaume wote wapo kama mzee wako?.

Kiasili mwanamke ni MBINAFSI,hela yake ni chungu haijawahi kuwa tamu.Hela yake inamatusi na masimango.Yaani nyinyi sio watoaji hata mkiwa nazo na mkitoa hata senti moja kuna siku utaitumia kumkejeli au kumsimanga mmeo kupitia hiyo senti moja.

Halafu unakuta nyie mnajenga kwa siri na tena inawezekana akawa ana mali nyingi, ila siku ya kuachana zinagawanywa za wanaume.
Yani umekataa generalization ya wanaume wote (hawako kama baba yake) ila wanawake wote wana asili moja 😂.
  • Wanaume wote siyo wabaya wala wabinafsi.
  • Wanawake wote siyo wabaya wala wabinafsi.
Kuwa fair kwao wote, tabia zinatengenezwa na utashi wa mtu na mazingira.
 
Mimi mama yangu kajenga mikoa tofauti na hadi mshua anaenda kaburini hajui lolote. Wakati wa uhai wake kampiga sana matukio hataki afanye kazi na hataki awe na maendeleo yoyote eti mke wa mtu na alimkuta kasoma na ana kazi tayari. Mtu hawazi ya mbele na ukoo wake ni ule wanaamini cha ndugu yoyote ni cha ukoo mzima. Akaona isiwe kesi katafuta mahala pengine kimya kimya. Na mzee alipofariki tu fujo zikaanza haya niambie kama hakua kajiongeza mapema hali ingekuaje.
Kabisa, baadhi ya wanawake wanasukumwa kufanya hivi kwa sababu ya mazingira magumu ndani ya familia.
 
Karibu chamani usifikilie mara kumi kumi karibu tunafuunga dirisha dogo
 

Attachments

  • SGN_02_10_2025_1739195321930.png
    SGN_02_10_2025_1739195321930.png
    1.9 MB · Views: 2
Nataka kujua ndio ujanja,umaarufu,ukisasa, usomi,kiburi,majigambo,majivuno,dharau,umwamba au!!?

Na tena wakati unafanya hivyo upo kwako na mlishajenga pa kuishi,na mwenza anakushirikisha Kila jambo la kifamilia analofanya!

MSAADA TAFADHALI,sio kwamba natumika baadae nitangulizwe baada ya mpangokazi wake wa ukwasi kukamilika!

Maoni yenu nitayazingatia!

Kataa ndoa mje pole pole!!

Na wale waume wenza mliopo humu mje pole pole nawajua!
Hiyo inaitwa PREPAREDNESS FOR UNKNOWN FUTURE IN MARRIAGE na wako sahihi, uzuri ni kwamba watoto pia watakuwa ni sehemu ya hizo mali za kificho:2bSway:
 
Kabisa masimango ni mengi mimi mpaka nimepunguza upendo kwake
pole sana mkuu, wanawake nature yao ni ubinafsi, ndio maana hata wao kwa wao hawapendani, kuna Singo maza mmoja alipata mwanaume wa kumuoa kabisa na huyo mwanaume alikuwa serious, kikwazo kikawa kwa mama wa mwanaume, akamwambia mwanangu kama mimi ni mama yako hutamuoa huyo mwanamke ambaye amezaa
 
Kuna sehemu nimeandika wanaume wote wapo kama mzee wangu???? Huo ni mfano tu wenye uhalisia ila wanaume wa aina hiyo wapo tena wengi. Mwanamke mpaka anaamua kufanya mambo yake lazima kuna sababu. Kuna wengine kweli ni ubinafsi lkn kuna wengine matendo ya waume zao ndio sababu hufikia maamuzi ya kufanya mambo yao kimya kimya bila kushirikisha waume zao.

Nakupa mfano mwengine najua umetanguliza hisia tu, kuliko uhalisia.Ukipata muda kama unarafiki HR muulize hivi wanaume wamewaandika wakina nani kama wafuatiliaji wa mirathi yao makazini na wanawake wamewaandika wakina nani?Utarudi palepale,NYIE NI WABINAFSI KIASILI NA NI WACHOYO ipo hivyo.

Sawa mnafanya mambo yenu kimya kimya bila kuwashirikisha waume zenu,sasa why ndoa ikivunjika mnataka mgawane vya wanaume wenu ila vyenu hamtaki viguswe?Kama umechoka si uondoke na unaweza uakauta hata hizo mali mnazojenga kimya kimya zina mchango wa mwanaume.
 
Nakupa mfano mwengine najua umetanguliza hisia tu, kuliko uhalisia.Ukipata muda kama unarafiki HR muulize hivi wanaume wamewaandika wakina nani kama wafuatiliaji wa mirathi yao makazini na wanawake wamewaandika wakina nani?Utarudi palepale,NYIE NI WABINAFSI KIASILI NA NI WACHOYO ipo hivyo.

Sawa mnafanya mambo yenu kimya kimya bila kuwashirikisha waume zenu,sasa why ndoa ikivunjika mnataka mgawane vya wanaume wenu ila vyenu hamtaki viguswe?Kama umechoka si uondoke na unaweza uakauta hata hizo mali mnazojenga kimya kimya zina mchango wa mwanaume.
Baba yangu sijui kamuandika nani🤔
 
Hao watoto aliwazaa peke yake!?mume wake hawamhusu!!?
Ina maana huyo mwanamke alijilala mwenyewe ndio akazaa au watoto sio was huyo mume!!?

Funguka zaid wenye akili timamu tuelewe!!
Hii dhana ya wanawake kujimilikisha watoto huwa inanitoa sana mchezoni. Na wangekuwa wanajipa mimba wenyewe sijui ingekuwaje...
 
Nakupa mfano mwengine najua umetanguliza hisia tu, kuliko uhalisia.Ukipata muda kama unarafiki HR muulize hivi wanaume wamewaandika wakina nani kama wafuatiliaji wa mirathi yao makazini na wanawake wamewaandika wakina nani?Utarudi palepale,NYIE NI WABINAFSI KIASILI NA NI WACHOYO ipo hivyo.

Sawa mnafanya mambo yenu kimya kimya bila kuwashirikisha waume zenu,sasa why ndoa ikivunjika mnataka mgawane vya wanaume wenu ila vyenu hamtaki viguswe?Kama umechoka si uondoke na unaweza uakauta hata hizo mali mnazojenga kimya kimya zina mchango wa mwanaume.
😀kumbuka hata mama zetu walifanya hivyo kwa ajili ya security yetu watoto, ila huwezi jua kabisa, so wako right kufanya hivyo
 
Kwanini, mkitaka kuachana mkadai na talaka mnakimbilia kutaka kugawana mali, halafu za kwenu mlizozipata ndani ya ndoa hiyo hiyo hamtaki ziguswe?
Sina jibu la moja kwa moja ya swali hili.
Kwa upande wangu siwezi kumfanyia hivi mtu niliyenaye kwasababu hela zake nazitumia nitakavyo halafu sio mchoyo.
Hela zangu tutazitumia wote hata nikipata kazi akitaka na mshahara wangu nitampa kila mwezi.
 
Hivi ni kweli hamna uelewa wa haya mambo ya migogoro ya kifamilia na kadhia za talaka au kutengana.

Wanaume wangapi wanaendelea kuhudumia watoto ipasavyo baada ya ndoa kuvunjika na bila kushurutishwa na ustawi wa jamii au mahakama? Wapo ila ni wachache, wengi wanaamini mkiachana jukumu la watoto ni la mama.

Ndoa ikivunjika, taratibu za kutafuta mpaka kupata talaka inaweza kuchukua miaka. Hicho kipindi chote hao watoto uliomwachia mkeo wanaishije? Kama mke hajasimama kiuchumi ni either watoto watateseka au atarudi kwao kusaidiwa kulea na ndugu zake.
Naona kama majadiliano mengine tunalazimisha tutoke nje ya maisha yetu ya kiuhalisia kwenye jamii.

Kuna shida kubwa sana ya malezi ya watoto na mwanamke kwa kiwango kikibwa ndiye anayeathirika ndoa ikivunjika. Sheria za mgawanyo zimewekwa ili kulinda maslahi wa wanandoa wote na watoto. Kisheria, ni kosa kuidanganya mahakama na kuficha mali iwe amefanya mwanamke au mwanaume.
Duniani sheria za mgawanyo wa mali hazijawahi kuwa rafiki kwa wanaume ndio maana hata US wameanza kufuatili hili na moja ya jimbo waliolipitisha hili ni Miami mgawanyo na Allomony wanangalia umeishi na mwanaume kwa kipindi gani na mchamgo wako kwake. Huko US talaka zinaongoza kuwaumiza na kuwafilisi wanaume na kuwachia Mental Health kwani, kwani kwenye mgawanyo wa mali alizo tafuta kwa jasho lake wanapunjwa,Allomony wanalipa wao na bado wananyimwa nafasi ya kuwaona watoto. (Si zungumzii hisia bali na zungumza uhalisia).

Halafu unaposema jukumu la watoto ni la mama,wakati kuna wazee kibao wanakimbizana kulipa ada na mahitaji mengine ya msingi ya mtoto hawa wazee jukumu lao ni lipi ambalo ww unataka walifanye? By nature wanaume sio waongeaji na hawanaga kelele,wanaume wengi wanatelekeza mahitaji ya msingi, hata kama wengi wenu hamuadmit, ila wengi wenu mnataka mfaidike kupitia hela ile ile anayopewa mtoto.


Nimekuulizwa swali umeriruka mnajenga na kuwekeza kimya kimya why sasa ndoa ikivunjika unataka mgawanyo kwenye mali za mwanaume ila zako hutaki?Najua huwezi jibu sababu si kosa lako bali by nature mwanamke ni mbinafsi.
 
Yani umekataa generalization ya wanaume wote (hawako kama baba yake) ila wanawake wote wana asili moja 😂.
  • Wanaume wote siyo wabaya wala wabinafsi.
  • Wanawake wote siyo wabaya wala wabinafsi.
Kuwa fair kwao wote, tabia zinatengenezwa na utashi wa mtu na mazingira.
Hamna sehemu niliyo sema ke ni wabaya,ila by nature mwanamke ni mbinafsi ukubali ukatae ipo hivyo.
 
Hivi ni kweli hamna uelewa wa haya mambo ya migogoro ya kifamilia na kadhia za talaka au kutengana.

Wanaume wangapi wanaendelea kuhudumia watoto ipasavyo baada ya ndoa kuvunjika na bila kushurutishwa na ustawi wa jamii au mahakama? Wapo ila ni wachache, wengi wanaamini mkiachana jukumu la watoto ni la mama.

Ndoa ikivunjika, taratibu za kutafuta mpaka kupata talaka inaweza kuchukua miaka. Hicho kipindi chote hao watoto uliomwachia mkeo wanaishije? Kama mke hajasimama kiuchumi ni either watoto watateseka au atarudi kwao kusaidiwa kulea na ndugu zake.
Naona kama majadiliano mengine tunalazimisha tutoke nje ya maisha yetu ya kiuhalisia kwenye jamii.

Kuna shida kubwa sana ya malezi ya watoto na mwanamke kwa kiwango kikibwa ndiye anayeathirika ndoa ikivunjika. Sheria za mgawanyo zimewekwa ili kulinda maslahi wa wanandoa wote na watoto. Kisheria, ni kosa kuidanganya mahakama na kuficha mali iwe amefanya mwanamke au mwanaume.
Alafu acha kutoa mawazo ya kiuwanaharakati,toa mawazo kama mwanafamilia anaependa familia iwe pamoja siku zote, wwe akili zako zote umeziweka kwenye mgawanyo wa Mali!!
 
Back
Top Bottom