Wanawake, mnaponyaje maumivu ya kusalitiwa na wenza wenu?

Wazee wazamani waliwezeje Mambo haya Mana anasafiri harafu anaaga mwezake mwagito ndavikisaga munyamuganga mwezako nasafiri ,hapo Mana anamkabidhi kwahyo hata Kama wanaenda kunywa pombe kilabuni Cha Kijiji wala haina shida ,jamaa akichelewa Bibi pakiuma anasema jamaa anakanyaga Siri kimyakimya
 
Wawapi
Kama nihawa tunaowanunua nakwenda kuwafuga Kama broila hawana ujanja wameshajiweka ok saikolojikali
 
Samahani dada yangu, kwa miaka kumi na tano ya ndoa inafaa nikuite dada. Nimekuomba Samahani kwa sababu we ushauri wa tatizo lako umeomba kwa wanawake na mimi ni mwanaume ila nakuomba usinipuuze nisikilize kama hutojali. Kama umeamua kuiponya ndoa yako naomba fanya haya. Anza kufanya wewe yale ambayo unataka mume wako akufanyie ila ktk hili usitake na yeye akufanyie siku hiyo hiyo jipe muda labda mwezi au wiki tatu. Kwakuwa unamjua vizuri we usiku mwambie kwa kutaja jina lake, Juma au Oswald nimeamua niwe mke mpya hivyo nataka kubadilika. Vyovyote akavyokujibu mazungumzo yasiwe marefu mwambie nimeamua niwe tu hivyo nimeona nikwambie tu. Ukiamka asubuhi mwambie nataka nikupikie chai fulani. Najua unamjua ila kakutoka rohoni ndio maana humpikii anachokipenda. Angalia atakacho jibu. Usivunjike moyo akavyokataa fanya kama ulikuwa unamkejeli ila akikubali pika vizuri anywe ukiwa pembeni naye ila usianzishe mazungumzo. Fanya hivyo wiki kwa vitu tofauti tofauti yaani unaweza mwambie leo nataka unit..mbe. Kama ataonesha kubadilika halafu muombe kitu kimoja . Usimwambie weekend tushinde pamoja ila mwambie juma pili ukitoka kanisani au Ijumaa ukitoka msikiti. Au ukifunga duka nataka tukae sehemu japo lisaa limoja nina stori nataka nikusimulie. Akikubali kwenye hiyo story muulize nilikuambia nataka kuwa mke mpya je nimekua maana nikiwa mke mpya nakuwa mpya kwako vipi unaona nimekuwa mpya. Atakwambia ndio au hata kabla ya hiki Kakao yeye atakwambia umekuwa mpya wiki hii. Maanaumesema nanajirudi, japo kimsingi yeye ndiye atakuwa mume mpya . Nb kwa kipimo mnacho wapimia wenzenu nanyi mtapimiwa hicho hicho. Mpimie kipimo kizuri. Mimi siyo msomi wa ushauri wa ndoa ila huwa nashauri masuala ya ndoa kwa njia ya Jadi kama babu yangu alivyokuwa anafanya. Naomba Kama utafuata njia hii nipe mrejesho hapa hapa hata kama haiwi kama unavyotaka. Kuna mama alikuwa na tatizo kama hili tukilitatua
 
Pole,maana maisha ya ndoa huyawezi kabisa.
 
Utawasikia ooh sisi hata tukichepuka, bado tunawapenda wake zetu na hatutelekezi familia. Pambafffff mtu anabadilika hadi watoto wake mwenyewe wanamuogopa mxieeew

 
Utawasikia ooh sisi hata tukichepuka, bado tunawapenda wake zetu na hatutelekezi familia. Pambafffff mtu anabadilika hadi watoto wake mwenyewe wanamuogopa mxieeew
Hehe siku hizi kuna wanawake nao ni mapro! Wana uwezo wa kuchepuka na heshima kwa mume iko pale pale na wakati kuna wanaume wakichepuka wanaanza dharau na kusahau kabisa familia!

Yaani siku hizi dunia iko vice versa kwenye mambo mengi sana hasa haya ya jinsia nashangaa tu kwanini kaka zetu hawataki kukubali hili! Zamani ilizoeleka wanaume wote ni wagumu na wanawake wote ni walaini ila siku hizi kuna wanaume walaini na wanawake wagumu vile vile na maisha yanaenda poa tu kikubwa uhai!
 
umeongea Theories tupu...doesnt work that way..
 
Utawasikia ooh sisi hata tukichepuka, bado tunawapenda wake zetu na hatutelekezi familia. Pambafffff mtu anabadilika hadi watoto wake mwenyewe wanamuogopa mxieeew
Acha kabisa

Tena hawachelewi kulaimu mwanamke utafikiri huyo mwanamke kajioa mwenyewe


Maisha mafupi sana aisee


Na tunaishi mara moja tu


Heri kutafuta amani ya moyo na furaha ya roho
 
najitahidi.

natumaini kupata uzoefu kwa waliopitia waliwezaje kusamehe na kuvuka hilo!!
 
kuna kipindi nilijaribu kumuomba tutoke...
aliniangalia tu kama nyanya mbichi...

labda kwa kuwa siku hizi kawa mpole nijaribu, ingawa ilishanitumbukia nyongo.

matokeo yake natoka mwenyewe au weekend na watoto!!!
 
dah

inasikitisha. haswa linapokuja swala la watoto!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…