Nimeshuhudia mara 2, ya kwanza ana miaka 40 kaolewa tena ndoa ya kanisani Kwa mara ya kwanza, Hana mtoto ata 1.
Mara ya 2 ndoa ni mwaka huu mwez wa 10, mwanamke ana miaka 33 Ila ana mtoto mmoja. Haya mambo hayatabiriki bhn lkn kutwa kukaa na kuwasema wanawake kuwa walipoteza bahati
Je wale ambao wanavumiliwa Toka hawana kitu, mpaka anakuja kuwa na kitu, alafu akishainuka anakuja kuolewa mtu mwengine, yule aliyevumilia tabu na shida anaonekana mchafu ananuka, Hana thamani tena. Lkn hili wanaume hawaliongelei kbs. Unamsubiri Mtu 5 to 6 yrs unavumilia shda zote lkn siku akipata mafanikio unastukia anaolewa mwenzio, tumeshuhudia sn tu izi mambo lkn si wanaume wote Wana hizi tabia.
Wanawake wengine mnawasingizia tu kuwa eti alikuacha kisa huna kitu, je? Hao wote mlikuwa na Nia ya kuwaoa jamani?, Sio mwsho wa siku umepata mafanikio unamuona hajui kutumia unamtft yule mtu ambaye hajui ata izo pesa umetumia nguvu gani kuzitafuta.
Na elewa kuwa usitake Kila mwanamke akakuelewa maana Kila mtu ana aina ya mtu anayemtaka, maana ata wanaume Wana watu wanaowataka, mala namtaka mwenye kiuno mbinuko, mala namtaka mwenye wowowo, mala namtaka mwembamba na apo Kuna wengine mnawachezea tu. Anafikisha mpk 28 yrs anakusubr ww but end of the day unamkacha unaenda oa mwengine.
Hao wengine mnaumia kwasbb mliwapenda, laiti ungekuwa humpendi bs ata usingekuwa na muda wa kumkumbuka usingekuwa nao. Ni kweli Kuna wadada Wana majibu machafu ambayo si vzr kumjibu mtu km humpendi na Kuna wengine huwa wanapoteza bahati wenyewe Kwa kuwakataa hao wanaume wenye malengo nao kiukweli. Uwe unacho, uwe huna km amekukataa bs jua hakupendi na hukupangwa kuwa nae usifosi, lakini km umempata wa kupendana nae Dunia hii ni jambo la kushukuru Mungu, dumisheni penzi lenu tu lkn mambo ya kuzogoana kuhusu umri si vyema. Kila mtu ana wkt wake wa kuanzisha familia yake.