Wanawake wengi wanaofanikiwa Kupata ndoa ni wale Wanaokabia Juu

Wanawake wengi wanaofanikiwa Kupata ndoa ni wale Wanaokabia Juu

Hii mbinu, mi mwenyewe naigwaya kabisa kwani sina ujasiri kabisa wa kufukuza mwanamke....hii mbinu kataa NDOA tusipoangalia, itambeba mpaka mwenyekiti wetu.....bila shaka hii mbinu imetoka kwa shetani moja kwa moja....

😂😂😂

Kwenye Biblia Mbinu hii ilitumiwa na Ruthi kwa Boazi.
Boazi hakuwa na chakufanya zaidi ya kuchekacheka tuu
 
Mimi nawajua vijana wengi wabishi ambao walikuwa Kataa ndoa Pro lakini shambulizi Hilo liliwamaliza Kabisa.

Binti kakukabia juu.
Anatekeleza majukumu yake kama Mke
Hana ubishani na wewe
Ni mpole na mstaarabu.
Anakusikiliza,
Unamfokea anaomba Msamaha hata kama KOSA ni Lako 😂😂

Mwisho unajishtukia kuona unamkosea HAKI na hastahili ubaya unaomfanyia.

Unasema Acha nimpe Nafasi nimtazame kwa miezi kadhaa huku ukijaribu kumtafutia makosa ili umfukuze, lakini huyapati.
Mwisho unakuwa umekwisha.

Unajiuliza, kwa Zama hizi kama nikimfukuza huyu ni mwanamke hani mwingine atakuwa Bora na mvumilivu kumshinda huyo. Mwisho unakata shauri na kujikuta unaanza kumpenda.

Kwisha

Yes nimependa Sana zuchu akili yake
 
Hii mbinu, mi mwenyewe naigwaya kabisa kwani sina ujasiri kabisa wa kufukuza mwanamke....hii mbinu kataa NDOA tusipoangalia, itambeba mpaka mwenyekiti wetu.....bila shaka hii mbinu imetoka kwa shetani moja kwa moja....
Ha ha ha..😂
 
Mimi nawasapoti timu kataa ndoa kimyakimya

Nawashauri wapaki basi kupooza mashumbulizi!
 
Sio Kila Mtu Ana Faa Kuwa Na Familia.
Wewe nani mpk useme hivyo.. kama Mungu aliuweka huo mfumo maana yake kila mwanadamu anapaswa kuwepo humo
Hakuna asiyestahili ndoa.. kila mtu ni sawa mbele za Mungu… ni suala la muda tu na wakati sahihi

Mungu ndio hujua hatima ya mwanadamu
 
Uwape na hasara ya hii mbinu mkuu
Hii mbinu ilikuwa nzuri kwa miaka ya zamani kuliko miaka hii.. maana zamani ukikaa na mtu moja kwa moja wanakuhesabia ni mke ila now days unaulizwa tu una cheti cha ndoa?? Kama huna wewe huna cha kumkabia huyo mwanaume na atawaambia wanawake zake wote yupo single hajaoa wala hajawai oa

Maana wanaume wote hamfanani.. ukikutana na limwanaume lenye Roho mbaya anakuacha ndani.. anaenda kuoa mwanamke alietulia kwao akasubiri mwanaume amtake yeye kumuoa
Sogea tuishi sio ndoa mkuu lolote linaweza kutokea and what if mwanamke kapoteza 5 or 4 years with man then mwanaume anaenda oa mwanamke mwingine

Mimi siwezi shauri binti yangu afuate hii njia maana hasara ni nyingi kuliko faidaa na hasara kubwa sana ni kufanywa singomaza na kuumizwa moyo

Mabinti tulieni wanaume wenye nia watawaoa tu wakati wa Mungu ukifika sogea tuishi ilikuwa zamani sio kwa wakati huu
 
Hawa wanawake wa hapa kwetu sio kama unamuoa yeye, unaoa matatizo yake na ya ndugu zake yote. Sorry, mimi sio bwege kiasi hicho
 
WANAWAKE WENGI WANAOFANIKIWA KUPATA NDOA NI WALE WANAOKABIA JUU

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Kuna Mbinu mbili za kupambana. Kuna wale wanaotumia Mbinu ya KUPAKI BASI na MBINU YA KUKABIA JUU

1. MBINU YA KUPAKI BASI
Hawa ni wale kwenye mahusiano ambao wanasubiri Mpaka mwanaume afuate taratibu zote. Aende nyumbani kwa Wazazi ajitambulishe, atoe sijui Mahari na taratibu zingine za kiutamaduni.
Mbinu hii ilikuwa mbinu yenye Tija kwa nyakati za zamani Kipindi ambacho Mila za kijadi na wazazi walikuwa na nguvu dhidi ya watoto wao.
Ninaposema nguvu ninamaanisha Wazazi walikuwa full responsible na majukumu ya kimalezi. Ikiwa ni pamoja na kuacha urithi kwa watoto.
Kwa zamani pia jukumu la Mahari lilikuwa jukumu la familia ya Mwanaume hasa Baba.
Hivyo kijana wa kiume jukumu lake ni kutoa taarifa kwa Wazazi kuwa amepata Mchumba sehemu Fulani au wazazi wanasema wamemtafutia kijana wao Mchumba.
Na shughuli za Posa na Mahari zinaratibiwa na Wazazi wa kijana.
Wajibu huu wa Wazazi ndio uliwapa nguvu Wazazi kuingilia mahusiano ya vijana wao na wakiamua waliweza kuyavunja Kabisa.
Pia wajibu huu ndio uliifanya desturi ya kuchaguliwa Mke kuwa Jambo la kawaida na kijana asingeweza kufurukuta kukaidi.
Kifupi Mwanamke aliolewa na Ukoo Mzima WA mwanaume kwa Sababu ukoo au familia husika ilihusika kutoa Mahari.

Lakini Mbinu hii imejikufa Kifo cha ASILI baada ya wazazi kushindwa vibaya kutimiza jukumu Hilo.
Zama hizi kijana ndiye mwenye jukumu la kuhangaika mwenyewe Kutafuta mwenza wake na kujitafutia Mahari.
Mila ya kujitafutia Mahari kwa kijana mwenyewe imekuja na faida na hasara Zake.

Hasara Mojawapo ni vijana kuchelewa Kuoa.
Wazazi kutokuwa na nguvu na Mamlaka kwenye mahusiano ya vijana wao.
Mabinti waliolewa kutoona nguvu ya wazazi wa mwanaume kwa Sababu hawana nguvu yoyote ya kuamua lolote ndani ya Mahusiano Yao.
Ndoa kuachana kwa urahisi.

Mabinti hawakuwa na njia yoyote zaidi ha kutumia Mbinu ya KUPAKI BASI mpaka pale mwanaume atakapokuja nyumbani kumchumbia na kumuoa.

2. MBINU ya KUKABIA JUU
Mbinu hii ni matokeo ya vijana kuachiwa jukumu la kuchagua mwenza na kutafuta Mahari Kwa mwenza wake.
Jambo hili limefanya vijana wengi kuchelewa Kuoa na wengine kufikia Hatua ya kutooa Kabisa.

Wanawake wengi wamejikuta wakibadili Mbinu na kuiacha Ile Mbinu ya KUPAKI BASI.

Kumsubiria mwanaume Mpaka aje nyumbani kwao imekuwa Kusubiri Embe kwenye mti wa Mpapai.

Wanawake wengi wameamua kuishi kinyumba na Wanaume na kuzaa watoto Kabisa. Kisha baada ya Miaka mingi ndio huna kubariki ndoa.

Mbinu ya kumfuata mwanaume ili akuoe ndio huitwa MBINU ya KUKABIA JUU.

Katika Mbinu hii inakanuni zake kama zilivyokanuni za Mbinu ya KUPAKI BASI.

Ni kosa kubwa mwanamke ku-date na mwanaume na kushiriki tendo la ndoa huku kila Mmoja anaishi kivyake. Hilo ni kosa la kiufundi ambalo wanawake wengi wanalifanya.
Huwezi kushriki tendo la ndoa na kijana alafu hajakuoa alafu hamuishi pamoja. Ni kutengeneza mazingira ya kutumika na kuachwa kirahisi Kabisa.

Ni Bora uamue Moja, utumie Mbinu ya Kusubiri Kabisa nyumbani na usifanye ngono na huyo kijana Mpaka Akuoe.
Au uamue kwenda kuishi naye Kabisa moja kwa Moja kiunyumba muanzishe maisha yenu. Kisha baadaye mtafunga Ndoa.
Kisheria, Kukaa na mwanamke au mwanaume kiunyumba, nyumba Moja Kwa zaidi ya miezi sita tayari huyo kisheria hiyo ni Ndoa.

Lakini ku-date na mwanaume hata Miaka Saba au kumi, lakini kila mtu anaishi kivyake hautambuliki kama Mke na Mume hapo hakuna Ndoa.

Utagundua kuwa, Njia Bora ni Bora ukabie JUU, ukaishi na huyo kijana wote sehemu Moja ili ijulikane Moja kama atakufukuza tokea mwanzoni au atakubali ukaze humohumo ndani ya nyumba. Hapa kuna Mbinu nyingine za kimedani.

Binti yangu usiwe Mjinga.

Ndoa ni ya watu wawili tuu. Yaani mwanamke na mwanaume tuu. Wengine ni mashahidi tuu.
Ndoa sio lazima pawepo na wazazi, sio lazima pawepo na Askofu au Sheikhe, ndoa sio lazima iwepo serikali ndio ifungwe. Ndoa ni yenu wawili. Sisi wengine Tu mashahidi tuu.

Usikariri Mbinu. Badilika kulingana na Dunia inavyoenda. Angalia ni Mbinu ipi utaitumia itakupa unafuu na faida.

Usijesema Babaako sikukuambia.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Hii ni kweli 100%✓
 
😂😂😂

Sisi wanaume lazima tujilete kwenu kutokana na Miili yetu kuumbwa na kiu ya mara kwa mara.
Sasa wewe mwanamke Kwa kujua Hilo unatakiwa uandae Mpango Kazi mkakati kuhakikisha atakayejileta amekwisha
Nmeshindwa kuwa king'ang'anizi wallah
Na kukabia juu siwezi labda nipewe clear chance😅
 
Wewe nani mpk useme hivyo.. kama Mungu aliuweka huo mfumo maana yake kila mwanadamu anapaswa kuwepo humo
Hakuna asiyestahili ndoa.. kila mtu ni sawa mbele za Mungu… ni suala la muda tu na wakati sahihi

Mungu ndio hujua hatima ya mwanadamu
Mimi Naongea Kifalsafa Zaidi Kuwa Makini Na Coment Zangu Usiingie Kinguruwe Kunikosoa Utavamia Ukuta.

Kazi Ya Uumbaji Mwanadamu Ilishamalizwa Na Huyo Kiumbe Mwanadamu Akapewa Njia Ya Kuifuata Wapo Ambao Huifwata Njia Ya Mungu Wapo Wengine Hufuata Njia Ya Shetani.
Ndoa Ni Tendo Takatifu Linafaa Lifanyike Na Watu Watakatifu
Matatizo Mengi Ya Kwenye Ndoa Huwa Hiki Kipengele Kinakiukwa
We Unaona Sawa Mwanamke Ana Idadi Ya Wanaume Waliomgonga Kubwa Kuliko Idadi Ya Siku Alizonyonya Ziwa La Mama Ake?

Nadhani Akili Yangu Ni Juu Ya Mbingu Ya Fikra Zako Naomba Niishie Hapo.
 
Back
Top Bottom