Wanawake wote ndivyo mlivyo hata mkikataa. Wanaume kuweni makini katika maamuzi yenu

Wanawake wote ndivyo mlivyo hata mkikataa. Wanaume kuweni makini katika maamuzi yenu

Leo hii Mr aniletee mtoto kazaa huko nje nimlee, kiukweli atakua ananitafutia dhambi za bure.

Yaani nitakua kila nikimuona naona ni matokeo ya kuchepuka kwa Mr, hapana sitoweza vumilia kwa kweli siwezi.

Kila mtu apambane na uzao wa tumbo lake.

Mtoto wa ndugu nitalea bila shida yoyote hata wawe wangapi ila sio mtoto wa mume.
uko sahihi nawaelewa wanawake ni ngumu sana kwenu ni ngumu kweli wala sikupingi.
 
Hakuna mtu atayempenda mtoto ambae sio wake kwa asilimia 100. Haina jinsia hiyo. Na hata Kama hatamchukia utaona kasoro tu siku zote
Ni kweli nakubaliana na wewe ila kuna kuchukia kimoyo moyo na kuchukia wazi wazi

kwanini sasa mshindwe kubaki na chuki moyoni mpka mnafikia hatua ya kuzionyesha nnje?

yani mtu anajua kabisa mama flani hampendi yule mtoto,kwann hii chuki isibaki siri yako ndani ya moyo?
 
ila BABA ukirudi nyumbani mtoto huyo huyo aliekua akifinywa mashavu ukiwa haupo

utamuona mama (mkeo) akimuita na kujifanya anampakata na kujitia anamdekeza (basi hapo mwanaume unaona yeees)

Kumbe zote zuga tu, ukiondoka kazini mambo ni yale yale.

Ni basi tu watoto hawawezi kusema kwa kuogopa vitisho alivyopewa (ole wako baba ako akija nikuone fyoko fyoko fyoko)
Noma sana!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usaidizi wenyewe ndio huo sasa alishe watoto,ila asimlishe BABA,watoto ni TUNU jamani hawatakiwi kuteswa kwa namna yeyote,hawatakiwi hata kujua kuwa wewe si mama ake,mpende jitoe,tembea hata peku kwa ajili ya mtoto.

ila usijitese kwa ajili ya mumeo ambae ni mzigo,huyo mwanamume mkimaliza kula osheni vyombo akirud akute hotput nyeupe,yani ukatli wote mfanyie huyo mwanamume ila si watoto wake.

Kutesa watoto kunaonyesha ni jinsi gani hauja qualify kuwa MAMA neno MAMA ni pana sana ukiona MAMA ujue n mzazi aasie tayari hata kuona mtoto waa jirani analia,achilia mbali kula.

MAMA wa kweli akiskia tu hata sauti ya mtoto nyumba ya jirani analia kila siku MAMA ataenda kuuliza whats wrong,ila huyo ni MAMA na s mwanamke.

wanawake wengi wa sasa si kina MAMA ila wamebaki na sifa ya kuwa MWANAMKE,sikubaliani na huyo mama kuumia kisa eti watoto wa mume wake wanakula anachotafuta,Huyo sio mama huyo ni Mwanamke.

Achana na mtoto wa mume wake,huyo mwanamke anaweza toa pesa yake akamnunulia chakula au nguo mtoto wa jirani wa mwanamke mwenzie baki? HAWEZI nakuhakikishia.
It's hard CONTROLA ni ngumu mno, haya mambo tuombe Mungu tu atupe hekima hakika
 
It's hard CONTROLA ni ngumu mno, haya mambo tuombe Mungu tu atupe hekima hakika
Upendo ni AMRI tuliyoachiwa sio OMBI hatukupewa kama OPTION na hapo zaidi ni kwa mtoto huo upendo lazima uwe wa vipimo visivyopimika.
 
Kabisa. Au ndo wewe unakutana na single mom afu anakwambia "my kid comes first"; hivi kuna haja ya kulisema hilo?
Yani hapo itaharibu kila kitu maana nitaona kwaio mimi niliekubali kua na wewe ndo 2nd option hakuna mtu anapenda jambo la hivyo
 
Hii ilinitokea mimi kipindi niko mdogo sanaaaa! mwaka 2000. Namkumbuka sana yule mama wa kambo,namkumbuka sana sana yule Mrangi alitaka kunitupa katika kisima cha Maji pale Dodoma.

Bila jitihada za majirani nadhani story yangu ingeishia pale Dodoma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoto wangu halelewi na mwanaume mwingine nikiwa Hai. Kuna wanaume hawana akili kabisa ya kulea. Namleta hapo kwa mama wa kambo na Ole wake nisikie mtoto akilalama.

Kuna njia nyingi sana za kujua kama Mwanao ana furaha ama la, na hapo nyumbani cctv lazima ziwe 24/7.

Wazee wenzangu mlio na watoto nje ya ndoa' chukua mtoto wako ishi nae hapo afahamiane na ndugu zake' kuwa nao karibu na mkeo afahamu kabisa hatari ya kumnyanyasa huyo wa kambo.
 
Hii ilinitokea mimi kipindi niko mdogo sanaaaa! mwaka 2000. Namkumbuka sana yule mama wa kambo,namkumbuka sana sana yule Mrangi alitaka kunitupa katika kisima cha Maji pale Dodoma.

Bila jitihada za majirani nadhani story yangu ingeishia pale Dodoma.

Sent using Jamii Forums mobile app
Khaaaa; ilikuwaje? Pole na hongera kwa kunusurika
 
Akili zao zinasikitisha...!
the best way is to solve your issues swala la kujali mtoto wa mtu mwingine ni moyo wa mtu tu na lipo very natural hata ukitizama kwa wanyama,
hivyo usijiaminishe men are better kila mmoja anatizama maslahi yake..
 
hao nao tabu tupu unaweza kumjali akaja kufanya tukio ukabaki unashangaaa
wapelekwe boarding school
likizo wapokezane kuwalea
Mimi mtazamo wangu ni kukaa na mwanagu ili nimuonye pindi akitaka kuharibika.

Kuhusu mama yake wa kambo ni kujitahidi kuwa karibu wa wanao, kila kitu kitakuwa okey.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
the best way is to solve your issues swala la kujali mtoto wa mtu mwingine ni moyo wa mtu tu na lipo very natural hata ukitizama kwa wanyama,
hivyo usijiaminishe men are better kila mmoja anatizama maslahi yake..

Uko sahihi kimtazamo ila niruhusu nikulishe neno kidogo kwenye hoja yako, point mezani sio kuwa ‘men are better’ bali ni kwamba men hawana cha kumfanya mtoto anayeishi na mama yake mzazi (mkewe).... sana sana itamlazimu kuonesha upendo zaidi ili kumfurahisha mkewe.

Mama ndiye mlezi, mama ndiye mlishi na mvishi na mambo yote... ni rahisi kwa mama kumlinda mwanaye dhidi ya ‘baba mbaya’ kuliko kinyume chake.
 
100% mwanaume mwingine ana uwezo wa kumpenda mwanao kama vile ni wake

ila hamna mwanamke wa kumpenda mtoto wa mwanamke mwingine (tena aliezalishwa na mume wake)

kama wake aliyemzaa.

Uwezo huo wanao wanaume TU.
Si kweli hakuna kiumbe anayependa mtoto wa mwingine ni wachache sana angalia hata wanyama asogee mtoto sio wake uone atakavyompiga mateke. Kina mama wanaonekana wana roho mbaya kwa sababu muda mwingi wanakaa na watoto ila kina baba wa kambo wenye roho mbaya wapo sana nimeona baba wa kambo akibaka wengine hata kuua watoto wa mke wake ambao si wake. Na nimeona mama wa kambo wakiishi na watoto kama wamezaa sema wengi wa hawa inategemea na tabia ya mme pia.
 
Back
Top Bottom