Wangapi zamani waliamini Majaji ni watu wenye uwezo mkubwa lakini Sasa wanaanza kuamini kila mtu anaweza kuwa Jaji?

Wangapi zamani waliamini Majaji ni watu wenye uwezo mkubwa lakini Sasa wanaanza kuamini kila mtu anaweza kuwa Jaji?

Hivi kwenye kesi ya Mbowe kwa mfano, kulikuwa na sababu gani ya kuita mashahidi?
Kama Jaji wa mchongo alishindwa kuangalia maelezo yao yalivyo tofautiana na kuamua kimchongo kumtia Mbowe na wenzake hatiani. Hwlafu tuseme juyu nae ni Jaji?
Kuna mahakimu wa mahakama ya mwanzp wengi ambao wange weza kuamua hii kesi vizuri kuliko huyu jaji wa mchongo.
Tulimshauri Mnyika wamkatae mapema waka fikiri tuna mchukia bila sababu.
Mmeanza tena propaganda mkiaminisha kuwa mweneykiti wenu ni malaika asiyetenda kosa.Siku ya hukumu mtageuka kivingine kama kawaida yenu. Leo mmeanza na Mnyika duuuuu, hiii yote ni wapi pa kutokea
 
JAJI NI JAJI Ukianza tu KUMJAJI JAJI kwa mirengo ya kisiasa huwezi tambua maana ya JAJI,Nimefatillia sana kesi ya Mheshimiwa MBOWE toka inaanza ila honestly speaking from the beggining watoa taarifa hawakuwa objective
Hawawezi kukuelewa mkuu.
Unakuta mtu kama huyu anatoa hoja kama hii ila hakuna anachokijua uhusu Sheria.
Na huwezi kuta mwanasheria naleta hoja kama hii hata siku moja.
Mfano unaweza kuta hata rulling ya jana huyu mtu hajaisoma lakini analeta ujuaji hapa!
 
Jaji alikuwa Samatta na Warioba siyo huyu mchumia tumbo Tigana.
Eti Jaji Warioba. Hebu tafuta Judgment yoyote iliyowahi kuandikwa na Warioba iweke hapa Jamvini ili tulinganishe na hitimisho lako hilo.
Watu mmekuwa makasuku mnandandia vitu hata hamvijui ati
 
Naona watu wengi mitandaoni wanajadili namna majaji wanavyopatikana. Watu wanahoji
1. Jaji anapatikana Kwa kupanda vyeo serikalini?
2. Wanapatikana Kwa UMAHIRI?
3. Wanatokana na perminmance nzuri kwenye private sector?
4. Wanatoakana na ukubwa wa GPA?
5. Wanatokana na mahusiano Yao na wanasiasa au wanapatikana Kwa vigezo vipi?

Wengine wanasema walivyoona akina Samata na Wariaoba waliamini Majaji wote wanazaliwa kuwa majajaji lakini lakini wakiangalia majaji wa tume ya uchaguzi na wengine wa kariba hiyo wanaamini Jaji siyo upeo ni cheo kama vyeo vingine.

Thought ya tatu inajikita kwenye siasa, je majaji wanapatikana Kwa fadhili kutoka kwa anayetawala au mbinu Gani utumika. Thought hii inawaangalia akini Biswalo Mganga na kubaini kumbe Ukiaaribu somewhere unaweza kupelekwa Judicial akasugue bench!

Wewe unaamini Jaji kwa Tanzania ni mwenye qualities zipi na anapatikanaje?
Nebda basi kawe na wewe Jaji. Ili wawe na uwezo mkubwa wanatakiwa waweje na waamue kesi vipi? Wakisema Mbowe kashinda hapo wana uwezo mkubwa, wakisema ana kesi ya kujibu hawana uwezo mkubwa! Duh!
 
Nilitegemea, baada ya kupitia Maelezo ya Mashahidi 13, hakuna Ushahidi wa Moja kwa Moja pasipo shaka, kuwa Watuhumiwa walitenda Kosa. Shahidi A kasema hivi......hapo tungeona panapovuja. Mimi nashauri Washtakiwa wakodi Jaji toka Nchi Jirani. Otherwise Utetezi wa Mashahidi wao utatupiliwa mbali kama Kesi Ndogo zilizopita. Mwisho watafungwa. Inaumiza Judgement za Aina hii Bado zinaExist na Watu wananyamaza😭😭
Brother Kuna tofauti ya Hukumu na uamuzi mdogo wa kuona kama Kuna kesi ya kujibu au laa. Hayo ya jana ni maamuzi madogo, principle ni ushahidi unachukuliwa kwa ujumla wake and not on details!
 
Watu muwe mnaelewa,haiwezekani rais akaombwa na viongozi wa upinzani mbowe aachiwe huru alafu kabla ya rais kutoa maamuzi ety judge akaamua kumuachia huru huyo huyo mbowe ,kwaiyo ni razima mbowe akutwe na hatia afungwe dheni rais aje amtoe kwa msamaha hivyo ndivyo itakavyo kuwa
 
Brother Kuna tofauti ya Hukumu na uamuzi mdogo wa kuona kama Kuna kesi ya kujibu au laa. Hayo ya jana ni maamuzi madogo, principle ni ushahidi unachukuliwa kwa ujumla wake and not on details!
Watu wengi hawatakuelewa. Mimi binafsi nikiwa kama mtu neutral, naamini kabisa, uamuzi mdogo wa jana hauna shida yoyote. Watu wasubiri Mbowe na wenzake wajitetee then hukumu ikitolewa ndio walalamike. Tatizo kuna baadhi ya watu wanaamini haki kutendeka ni lazima wao washinde.
 
Tunachotakiwa kufahamu, ni kwamba jaji hupatikana kutoka jamii yetu. Rais anapatikana kutoka jamii yetu.

Jamii ikiwa na watu wengi wanafiki, waongo, wala rushwa, waoga, basi uwezekano mkubwa:

1) Rais atakuwa na sifa hizo hizo
2) Mawaziri watakiwa wa namna hiyo hiyo
3) Majaji watakuwa wa namna wa namna hiyo hiyo
4) Polisi watakuwa wa namna hiyo hiyo

Inakuwa ni kwa bahati sana, kumpata mtu tofauti na walio wengi katika jamii. Watu hao waliowahi kuwa tofauti na walio wengi, ndiyo kama Mwalimu Nyerere, Warioba, Jaji Lugakingira, Jaji Samata, Jaji Augutino Ramadhani, Jaji Nyalali. Sasa kwa vile walio tofauti ni wachache, ni lazima kuwe na mfumo unaolazimisha kwenye nafasi kama za Urais, jaji, wapatikane watu kama hao. Bahati mbaya mfumo huo hatuna.

Bahati mbaya zaidi, uchaguzi wa mwaka 2015, ulimwingiza Rais asiye na vigezo kabisa, aliyeamini kuongoza kwa kutumia nguvu, udikteta na hila. Ili atawale kwa namna anayoitaka bila bugudha, aliua Bunge, aliua mahakama. Mahakamani akawajaza maofisa wa TISS. Hawa wote waliohusika na kesi ya Mbowe, siyo majaji, ni maofisa wa TISS ambao marehemu aliwajaza mahakamani ili kuua mhimili wa mahakama.

Siku tukibahatika kumpata kiongozi jasiri, mwenye hekima, upeo mkubwa na weledi, hawa maaifa wa TISS, wote wanatakiwa kuondolewa mahakamani. Lakini cha muhimu zaidi ni katiba mpya ambayo italazimisha upatikanaji wa majaji kwa vigezo vya sifa na uwezo.

Bahati mbaya jamii yetu pia imejengwa na watu waoga, na wanafiki kupindukia. Huu ujinga mwingi unaofanywa na watawala, mahakama na bunge, ni matokeo ya unafiki na uoga wa sisi wananchi.

Angalia hata hapa jukwaani, watazame watu kama Jingalao, Cremia, Chinembe, Stroke, qnd the like, ukitazama michango yao unaweza kudhani ni brainless, lakini yawezekana wana akili timamu lakini akili yote imemezwa na unafiki. Wao hata kitu ambacho ni dhahiri kabisa kuwa ni cha hovyo, alimradi kimefanywa na mtu wa CCM, au kiongozi ndani ya Serikali, hata kiwe takataka kwa kiwango gani, watasifia. Hata huko mitaani, watu wa namna hiyo ni wengi. Kuwategemea watu wa namna hiyo kuleta mabadiliko nchini mwetu, ni ndoto. Wao kila kitu hakuna cha muhimu, kikubwa ni matumbo yao. Wengi wanawaza fedha na vyeo.

Kwa ujumla, kwa sasa, majaji wengi hawa waliochongwa na mwendazake ni wala rushwa wakubwa, weledi ni zero, kujipendekeza 100%. Baadhi ya ninaowafahamu, pamoja na hawa walioendesha kesi ya Mbowe na wenzake, ni hovyo kabisa, hata kama wangeondolewa huko TISS, wakabakizwa mahakamani, uwezo wao ni mdogo kuliko hata mahakimu wa Wilaya, wale wenye uwezo.
 
Maswali yote haya ni kwa sababu tu 'mtakatifu' Mbowe amekutwa ana kesi ya kujibu? Duh!
Pamoja na simu namba zamchongo ambazo mbowe hajawahi miliki na hazijaonesha makato bado jaji ameona kupitia laini zile mbowe anakesi yakujibu
 
Watu wengi hawatakuelewa. Mimi binafsi nikiwa kama mtu neutral, naamini kabisa, uamuzi mdogo wa jana hauna shida yoyote. Watu wasubiri Mbowe na wenzake wajitetee then hukumu ikitolewa ndio walalamike. Tatizo kuna baadhi ya watu wanaamini haki kutendeka ni lazima wao washinde.
Kabisa kabisa. Una kuta mtu hajawahi kusoma Hukumu hata moja, au hata huo uamuzi wa jana hajausoma halafu ana kuja na hitimisho hadi unashangaa.
 
Nadhan kinacholeta viulizo na sintofahamu Ni mfumo wa upatikanaji wa majaji hao!

Bahati mbaya sana,, katiba imempa mandatory Rais ya kuwa juu ya kila mtu na juu ya sheria regardless kwamba kiuhalisia wananchi Ni maboss wa Rais, na Rais yupo kuwatumikia wananchi!

Katiba hii ambayo wengi wa wana CCM wanaitukuza sana wakisema hamna haja ya kuirekebisha, ndiyo inampa mandatory Rais kuwateua majaji ambapo anaweza kuwatengua muda wowote!

Mashaka yanakuja kwenye swali kuwa , Ni nini dhamira ya ndani ya Rais kumteua Jaji ( Mathalani Jaji siyani alivyopandishwa cheo katikati ya kesi)?

Maoni yangu!

Majaji wangependekezwa na kuchaguliwa na wanasheria wenyewe kwenye chama Chao ,,, hii ingeondoa mashaka

NB: Jaji Ni Jaji tu , Ingawa jaji wa kuteuliwa anakengeuka sana na kufanya matakwa ya aliyemteua but still anasomeka na kutambuliwa Kama Jaji
 
JAJI NI JAJI Ukianza tu KUMJAJI JAJI kwa mirengo ya kisiasa huwezi tambua maana ya JAJI,Nimefatillia sana kesi ya Mheshimiwa MBOWE toka inaanza ila honestly speaking from the beggining watoa taarifa hawakuwa objective
Kusaja, kuwa objective na wewe. Unaweza kulinganisha hawa majaji wa UPE na akina Rugakingira, Katiti, Kalegeya, Mlay , Rutakangwa, and to crown it all Judge Mwalusanya. Juzi Magufuli kamfanya Jaji mmoja kuwa Justice of Appeal kwa vile ameandika Hukumu kwa Kiswahili. Is that promotion on merit? Huyo Judge anajua Sheria? Anakwenda kufanya Nini CA? Huwezi kumpandisha Medical assistant kuwa daktari bingwa kwa vile ana Moyo wa huruma na wagonjwa. Huyo ataua watu maana hana utaalamu wa ubingwa wa hiyo field of concern.
Hizi zote ni takataka hasa za Magufuli, aliiharibu na kuinajisi Judiciary!
Kesi ya Mbowe mashahidi wote Wànasema hawana ushahidi wowote wa Hawa watuhumiwa kufanya ugaidi, halafu the so called judge anasema they have a case to answer!
Rubbish!
 
Kuna tofauti kubwa kati ya akili, uwezo na uteule.
Jaji ni mteuliwa, hivyo Rais anauwezo wa kumteua yeyoye aliekidhi vigezo hata kama hana uwezo/akili/hekma/busara.
Ama kwa lugha nyepesi ni kwamba kuna tofauti kubwa kati ya kusoma na kuelimika.
Rubbish, Rudia! Rais anateua bila vigezo vilivyowekwa? Soma namna majaji wanavyopatikana
 
Majaji gani hapa Bongo wanaoambiwa "Sikiliza Shauri kisha kwenye maamuzi SOMA hukumu hii"?? Yaani Jaji analetewa Hukumu Mezani Mwake kazi yake yeye ni kusoma tu.

Serikali/Jamhuri inaamua Nani ashitakiwe na Kwa kosa gani na mashahidi ni kina Nani na Jaji/Hakimu awe Nani na Hukumu iwe ipi. Mambo ya ajabu Sana. Kibaya zaidi Yule aliyeaminiwa na raia kuwa mlinzi na mtetezi wao ndiye anaeratibu upuuzi wote huo.

Watz tuamkeni kuidai Katiba Mpya. Kama sio Katiba hii kuwa na mapungufu, isingewezekana kumpata Mkuu wa Mhimili bila kupitia mchakato wa kupigiwa Kura. Kwa Katiba hii Mbovu akipatikana Makamu mwenye Tamaa ni rahisi kufanya lolote ili dodo limdondokee.

KATIBA MPYA KATIBA MPYA KATIBA MPYA ndiyo suluhisho.
 
Tambua kwamba,Jaji, Spika na Rais wanatoka miongoni mwetu ktk jamii hii hii iliyojaa watu wa hovyo na wasiofikiria sawa sawa
 
Tambua kwamba,Jaji, Spika na Rais wanatoka miongoni mwetu ktk jamii hii hii iliyojaa watu wa hovyo na wasiofikiria sawa sawa
Lakini pamoja na uhovyo wao hawa majaji hutakiwa kuhukumu kwa kucite sheria na kama kuna kesi kama hiyo imewahi kutokea.

Akihukumu kwa interests zake means ataenda kinyume na sheria na atakua ameweka reference mbovu ambayo inaweza kutumiwa baadaye na jaji mwingine.
 
Back
Top Bottom