Wanywa pombe kali huwa mnajiuliza swali hili mkiwa mnakunywa?

Wanywa pombe kali huwa mnajiuliza swali hili mkiwa mnakunywa?

Aliyekuwmbia situnzi afya yangu kisa pombe ni nani!!?...

Soda sio sumu!?? Vidonge sio sumu!?? ..... Bugia soda acha nibugie gambe .... Afya yangu ni dhamana yangu kama wewe na afya yako ......
Hakuna justification ya kunywa sumu iwe pombe ama soda ama vidonge.
 
Acha kulinganisha gambe na vitu vya kijinga.

Hayo maini hata mbuzi anayo.

Sasa nife nizikwe na maini na figo mpya kwani zinaenda kuliwa na nani huko kaburini?

Hebu waiter leta nyingine kali zaidi. Pesa ni yangu
 
asilima kubwa matajiri huzaliwa hawana pesa wachache huzirithi na hata hao pia hutumia akili kubwa kuzikuza, sasa point ya utafutaji pesa huanzia chini ukianza tuh visungura kwa kigezo hiki ndio kiwango changu wacha nilewe nakuhakikishia hutafika wine,na ukifika kiwango cha mvinyo wa bei ghali hutopata muda wakunywa au pengine ukapata huo muda mara moja kwa mwaka tena kwa kiwango kidogo hivyo hakuna tajiri mlevi kwani huo muda hana wakulewa
Ukweli mchungu mkuu.
 
Walokole/wasabato Wana shida sana ..... Yanajiona tayari yameshafika mbinguni Kwa kutokunywa pombe tu ... Na wazima wa afya Kwa kutokunywa pombe tu ..... Madhambi na masumu ni mengi mno duniani humu ...ila wao kila siku kufungua Uzi pombeee pombeee ....
Hii mada haihusiani na usabato/walokole, mada pia haihusiani na peponi ama mbinguni,
Narudia hakuna justification ya kunywa vilevi ( sumu) pombe kali na nyingine, zaidi unampa utajiri mwenye kampun huku wewe ukiangamia kwa ulevi ..
Sikia nikuambie mzee, nature inasema kuna kuzaliwa kuishi na kufa , sasa ukifa unaenda wapi hio hakuna anaejua mana hakuna aliefika huko akarudi,,,sasa usi justify kunywa sumu sababu unajua kuna kufa, hizo zinazotokea ni uncertainities za kimaisha, you are at wrong place at wrong time, na kuna kufa kwa uzembe wako, kufa kwa kua muda umefika(Gods plan) na kuna kufa kwa uzembe wa mtu/watu wengine ..
 
tajiri halewi napiga mahesabu ya biashara zake anaamka alfajiri mapema sana wakati huo masikini anaamka saa9 kunywa maji kwa kiu ya konyagi
[emoji23] dah. Nacheka kwa masikitiko.
 
Wewe unafikiri wenye viwanda vya Coca-Cola na Pepsi hawana majumba na magari?
Bure kabisa wewe
We kejeli sana mkuu, ila Mada imezungumzia pombe kali, na pombe zingine,
Hata hivyo soda pia ni sumu, mimi kuzungumzia mapombe hayo siyo justification kua niko salama kwa kutumia soda..watoto wetu tunawamaliza wenyewe kwa kuwapa sumu hizo mnazoita soda..ofkoz wenye makokakola na pepsi si unawaona wanautajir wakutisha huko duniani, nyinyi mnaendelea kunywa sumu na kuendelea kuwaongzea utajiri.
 
Usitufokee wewe jitunze uende na maini yako mazuri mbinguni
Utajifariji kwa kejel hizi ila acha pombe sumu acha kuwapa utajir wenye makampun ya pombe huku wewe ukiangamia na kuiweka familia kwenye mateso makubwa.
 
Wasaalam!!!!

Nakaa na kutafakari kwa kina, kwa mnywa pombe haswa vijana na wengineo hata watu wazima, chukulia hizi pombe kali...

Hivi umeshawahi kutafakari kua wewe unaingia kwa bashasha sehem ya burudani ama wapi unaagiza kwa bashasha na umwamba mwingi pombe kali na unachaganya na soda sjui, matokeo ya unywaji huo unaenda kuunguza maini yako na kukusababishia matatizo ya figo, ila kwa tajiri mwenye kiwanda ama hio kampuni anaendelea kua tajiri mkubwa, anajenga majengo ya hatari na magari ya kifahari, pesa ya kutosha iko benki..

Ila wewe huku unaangamia, mbaya zaid unakuta hata hakujui maskin ya Mungu wakat unaanza kwenda hospitali kufanya dialysis , tumbo limevimba, yeye huku anakula maisha, mbaya zaid yeye hatumii, yeye anakunya maji tu na kufanya mazoezi, mwisho wa siku unapata magonjwa kama kansa ya utumbo n.k, wewe ukiwa unakata roho yeye wala anakula.maisha bado. Ukiwaona huko.mitandaoni mixer kutoa shauri nasaha za maisha na jinsi ya kufanikiwa.

Kaa tafakari.

ACHA POMBE..
Waache pombe wanywe mkojo??
Toa tiba mbadala
 
Mkuu

Duniani tunapita tu.. Unataka utunze hizo figo na maini ili uende nayo wapi?
Mwisho wa siku kila mtu atakufa unataka ufe ukiwa na figo nzima ili uende nazo wapi?
Bado haileti tija mkuu kuharibu maini na figo nakupunguza miaka yako ya kuishi sababu kuna kufa na kwamba maini na figo huwez kwenda navyo popote. Hizo fikra kwa sisi waafrika ndizo zilizojaa ila kwa wenzetu , organ hizo kama ni nzima zinaweza kutolewa na kuwekewa mwingine zikamsaidia kama marehemu ataridhia kabla ya kufa kwake kwamba viungo vyake vitumike kwa mwingine mwenye uhitaji
 
Wasaalam!!!!

Nakaa na kutafakari kwa kina, kwa mnywa pombe haswa vijana na wengineo hata watu wazima, chukulia hizi pombe kali...

Hivi umeshawahi kutafakari kua wewe unaingia kwa bashasha sehem ya burudani ama wapi unaagiza kwa bashasha na umwamba mwingi pombe kali na unachaganya na soda sjui, matokeo ya unywaji huo unaenda kuunguza maini yako na kukusababishia matatizo ya figo, ila kwa tajiri mwenye kiwanda ama hio kampuni anaendelea kua tajiri mkubwa, anajenga majengo ya hatari na magari ya kifahari, pesa ya kutosha iko benki..

Ila wewe huku unaangamia, mbaya zaid unakuta hata hakujui maskin ya Mungu wakat unaanza kwenda hospitali kufanya dialysis , tumbo limevimba, yeye huku anakula maisha, mbaya zaid yeye hatumii, yeye anakunya maji tu na kufanya mazoezi, mwisho wa siku unapata magonjwa kama kansa ya utumbo n.k, wewe ukiwa unakata roho yeye wala anakula.maisha bado. Ukiwaona huko.mitandaoni mixer kutoa shauri nasaha za maisha na jinsi ya kufanikiwa.

Kaa tafakari.

ACHA POMBE..
Maisha yampige na pombe asinywe?
 
Wewe ambaye haulewi mbona sio tajiri?
, hio haiwez kua faraja kwa mlevi..utajiri namba moja ni afya, anaweza asiwe kama elon musk lakin akawa ana afya njema na nguvu za kufanya kazi kujipatia rizki.
 
Kama kuna mwanamme hanywi pombe basi namsahuri aanze kunywa pombe ila asiwe mlevi. Asee hamjui tu jinsi ambavyo wanywa pombe hupeana connection za uhakika
 
Acha wivu wa kipumbavu huo.

Yeye ametumia gharama , maarifa na muda kutengeneza kinywaji ili akufurahishe wewe, na wewe unamlipa pesa kwa hiyo furaha unayoipata.
Kuhusu madhara hayo ni juu ya mnywaji na jinsi ya unywaji maana mtengenezaji kwa kushirikiana na serikali wamekushauri kunywa kistaarabu.

Ni sawa tu na wanywa soda, energy drinks, vyakula visivyo na usafi migahawani nk huko kote unaweza hatarisha afya yako usipokua na kiasi na umakini katika uchaguzi wa unachokitumia.

Dogo achana na kuikandia pombe, haijaanza kutumika leo, hata huko tuendako unaambiwa kuna hadi mito sio hizi za 200ml Noo ni mito kabisa itiririshayo mvinyo, acha kabisa mzee.
 
Kuna baadhi hawagusi kabisa kilevi lakini ni mabingwa wa kufukua mitaro
Bado haileti maana wala kujifariji kua sababu wengine wana dhambi kubwa nyingi kwamba wewe uharibu afya yako iwembovu sana sababu kuna wengine wanafanya dhambi kubwa kama hizo ulizosema hapo...yeye atakua na msalaba wake wa kufanya anal sex (ufuska), na wewe unayekunywa sumu( vilevi) pia utakua na msalaba wako
 
Back
Top Bottom