Wapenda haki hatutompa Kura Diamond Platnum kama tulivyokubaliana

Wapenda haki hatutompa Kura Diamond Platnum kama tulivyokubaliana

Msilipize baya kwa baya,mpeni za kumwaga na atakuwa amejifunza katika hilo unapokuwa msanii nyimbo zako ni za watu wa vyama vyote na mbaya zaidi fans wake ni vijana ambao wengi wapo upinzani.
 
WAPENDA HAKI HATUTAMCHAGUA DIAMOND PLATNUM


Na, Robert Heriel


Katika Tuzo za BET Diamond ni moja ya Wasanii wanaowania Tuzo hizo.


Wapenda haki, wanaharakati na Wana mtandao wote kuanzia Facebook, Instagram, JamiiForums, na Twitter Kama tulivyokubaliana hatutampa Kura Diamond Platnum na hatashinda tuzo hizo Kwa sababu ameshindwa kutumia nafasi yake vizuri kuilinda, kuijenga na kuitetea jamii yake.


Diamond hajawahi kutetea jamii ya Watanzania.


Utekaji na mauaji yalivyopamba Moto Diamond alikuwa wakwanza kutoa kibao chenye ujumbe usemao " Acha Nikae kimya" maudhui ya wimbo ule yalilenga kuhafifisha na kutia uoga jamii isipige kelele kuhusiana na vitendo hivyo vya udhalimu.


Diamond ni tofauti kabisa na Wasanii wa Nigeria Kama kina P Square, Burns boy, Davido n.k ambao mara kadhaa walijitokeza kuungana na jamii kuipinga serikali pale inapokosea mpaka kuandamana kabisa.


Diamond hawezi chaguliwa na watu wote walioenda shule, waliostaarabika, wapenda haki na wanaharakati.


Kwa hapa Nchini waliojaribu na wanaojitahidi kutetea haki na kutetea jamii ni kina Ney wamitego, Roma mkatoliki, Profesa Jay miongoni mwa wengine.


Diamond ni Aina ya wanamuziki wanaoiona jamii Kama jamii ya vibushuti sio ajabu ndio maana nyimbo zake nyingi hasa za siku hizi niza vibushuti, zinalenga watu wenye Low IQ.


Diamond Kama angenoga Kama angeimba nyimbo Kama za kipindi kile mathalani "nimpende Nani" ukimuona" Nitampata wapi" lakini sio hizi za Jeje na mfano wa zile za nyoka pangoni.


Kama tulivyokubaliana Kura asipate.


Ili iwe funzo Kwa Wasanii wa kizazi kinachokuja.


Msanii ambaye ni kioo cha jamii badala aungane na jamii yeye anaungana na serikali. Ajabu hii.
Hii ipo katika nchi yetu pekee.


Hata Marekani wenye muziki wao Wasanii wao huwa upande wa wananchi.


Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Tutapimaje kama nyie ni watenda haki?
 
Msilipize baya kwa baya,mpeni za kumwaga na atakuwa amejifunza katika hilo unapokuwa msanii nyimbo zako ni za watu wa vyama vyote na mbaya zaidi fans wake ni vijana ambao wengi wapo upinzani.

Hakunaga kanuni ya hivyo Duniani na mbinguni.

Ubaya hulipwa Kwa ubaya
Wema Kwa wema. Tit for tat
 
Nyie nanyi mna chuki zenu za ajabu ajabu khaa!!!

sababu ya kawaida kabisa inayofanya baadhi ya watu wasimpigie kura ni uswahili ,akipata hio tuzo itakua kama fimbo ya kuwachapia wengine.

Lakini hizi chuki zenu za kisiasa aisee inabidi zioungue hazina mantiki yoyote.
 
Kwakuwa Diamond anapambanishwa na wasanii wa mataifa mengine, kwa maana hio ni msanii pekee kutoka Tanzania na pekee kutoka ktk ukanda huu wa Afrika Mashariki kupeperusha bendera basi kwa kauli moja TUTAMPA KURA KIJANA WETU DIAMOND PLATNUM

Mambo ya siasa na uanaharakati uwepo wa akina Zitto, Mbowe, Lissu unatosha sana ktk uwakilishi

Kwenye soka tunawakilishwa na Samatta, kwenye Music Diamond ndie nembo ya nchi kimataifa

Go go Diamond Platnum,,, You are the true icon of Tanzania Music
 
Nyie nanyi mna chuki zenu za ajabu ajabu khaa!!!

sababu ya kawaida kabisa inayofanya baadhi ya watu wasimpigie kura ni uswahili ,akipata hio tuzo itakua kama fimbo ya kuwachapia wengine.

Lakini hizi chuki zenu za kisiasa aisee inabidi zioungue hazina mantiki yoyote.

Kalia chuki hapo.

Ujumbe huu haukuhusu.

Chuki Kwa kipi hasa?

Au umasikini unakusumbua?
 
WAPENDA HAKI HATUTAMCHAGUA DIAMOND PLATNUM


Na, Robert Heriel


Katika Tuzo za BET Diamond ni moja ya Wasanii wanaowania Tuzo hizo.


Wapenda haki, wanaharakati na Wana mtandao wote kuanzia Facebook, Instagram, JamiiForums, na Twitter Kama tulivyokubaliana hatutampa Kura Diamond Platnum na hatashinda tuzo hizo Kwa sababu ameshindwa kutumia nafasi yake vizuri kuilinda, kuijenga na kuitetea jamii yake.


Diamond hajawahi kutetea jamii ya Watanzania.


Utekaji na mauaji yalivyopamba Moto Diamond alikuwa wakwanza kutoa kibao chenye ujumbe usemao " Acha Nikae kimya" maudhui ya wimbo ule yalilenga kuhafifisha na kutia uoga jamii isipige kelele kuhusiana na vitendo hivyo vya udhalimu.


Diamond ni tofauti kabisa na Wasanii wa Nigeria Kama kina P Square, Burns boy, Davido n.k ambao mara kadhaa walijitokeza kuungana na jamii kuipinga serikali pale inapokosea mpaka kuandamana kabisa.


Diamond hawezi chaguliwa na watu wote walioenda shule, waliostaarabika, wapenda haki na wanaharakati.


Kwa hapa Nchini waliojaribu na wanaojitahidi kutetea haki na kutetea jamii ni kina Ney wamitego, Roma mkatoliki, Profesa Jay miongoni mwa wengine.


Diamond ni Aina ya wanamuziki wanaoiona jamii Kama jamii ya vibushuti sio ajabu ndio maana nyimbo zake nyingi hasa za siku hizi niza vibushuti, zinalenga watu wenye Low IQ.


Diamond Kama angenoga Kama angeimba nyimbo Kama za kipindi kile mathalani "nimpende Nani" ukimuona" Nitampata wapi" lakini sio hizi za Jeje na mfano wa zile za nyoka pangoni.


Kama tulivyokubaliana Kura asipate.


Ili iwe funzo Kwa Wasanii wa kizazi kinachokuja.


Msanii ambaye ni kioo cha jamii badala aungane na jamii yeye anaungana na serikali. Ajabu hii.
Hii ipo katika nchi yetu pekee.


Hata Marekani wenye muziki wao Wasanii wao huwa upande wa wananchi.


Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Maskini hajawahi kumpenda mwenye uwezo
 
Kwakuwa Diamond anapambanishwa na wasanii wa mataifa mengine, kwa maana hio ni msanii pekee kutoka Tanzania na pekee kutoka ktk ukanda huu wa Afrika Mashariki kupeperusha bendera basi kwa kauli moja TUTAMPA KURA KIJANA WETU DIAMOND PLATNUM

Mambo ya siasa na uanaharakati uwepo wa akina Zitto, Mbowe, Lissu unatosha sana ktk uwakilishi

Go go Diamond Platnum,,, You are the true icon of Tanzania Music

Ujumbe umefika, ni kutekeleza tuu Mkuu.
Muda utajibu
 
Kila mtu ana haki ya kupanga ,kuchagua na kufanya kile anachoona kwake Ni sahihi Kwan uyo Diamond Ni nani Hadi Kila mtu amfanyie kinachomfaa.kura n haki ya mtu na Ni Siri .mashabiki zake watampa kura na wengine wampgie kura wanaeona Ni sahihi.
 
Natumaini watakua katika categories tofauti hivyo nawapigia wote.

Ni Haki yako

Ila uzi huu unahusu wanaharakati, wapenda haki, wanamtandao wenye kusomwa na watu wengi. Hatutompa Kura mond ndivyo tulivyokubaliana na ndivyo itakavyokuwa.

So wewe kampe Kura Diamond ni haki yako ili kumfanya apate walau Kura ya kumezea mate
 
Back
Top Bottom