Waraka kwa Rais Samia kuhusu vilio vyetu sisi Wahandisi tulioajiriwa kama Walimu

Waraka kwa Rais Samia kuhusu vilio vyetu sisi Wahandisi tulioajiriwa kama Walimu

hadi tukasomee post graduate
Hii ndio point. Sheria ipo hivyo, mnajisumbua tu., soneni miezi 9 PGD, Mbona mna akili.
Kuna watu wamesoma BSC phy maths,bio,bila ualimu wanaozea mtaani, shukuruni nyie mmepata ajira.
Kwa andiko lako hili bado kuna mambo/sheria za kiutumishi inabidi uzisome.
Kumbuka utumishi kazi yao kukuita na kukuajiri baada ya hapo TSC ndio anakuwa bosi wako mpya. Imetokea mara nyingi sana utumishi /tamisemi wanamuajiri mwalimu halafu TSC wanamkataa kata kata.
Ndugu kuna mkanganyiko mkubwa sana ktk sekta ya utumishi ya TZ wizara ya elimu vs tamisemi, hawana maelewano kabisa hawa watu, hata utekelezaji wa sera wanakanganyana tu.
 
Ila mlikimbia ualimu mkaona haulipi sasa mmerudi kwa mlango wa nyuma.
Mlisoma kwa mihemko bila kuwa na vision. Kitendo cha engineer kurudi kwenye chaki maana yake mmefeli dream zenu.
Sasa nyie mainjinia mmeshindwa kujiajiri na digrii zenu, je hao watoto wa veta watajiajiri kweli?
Acheni kulia lia, anzisheni side husle, warabu,wachaga hawana hiso dugrii zenu ila wana workshop kubwa, nyie mnaujuzi mnalialia.
Nchi hii mtalalamika sana, hata wakiwaongezea hayo madaraja maisha bado ni magumu. Bungueni bongo.
 
Mkuu shukrani sna Kwa mawazo yako yakinifu, na tumeyapokea, binafsi nimekuelewa sna

Kuhusu iyo point no: 6, tulimuandikia barua katibu Mkuu utumishi wa umma kuhusu hili swala na majibu yake ni kuwa hili swala lenu lipo chini ya Mkurugenzi, Yeye ndiye anayehusika na kuthibitishwa kwenu.

Point no: 08, Yes Kwa baadhi ya barua tumezipeleka Kwa dispatch, mfano iliyoenda Kwa Katibu Mkuu Tamisemi na nakala kupekwa Kwa RAS na DED.

Masuala ya Utumishi hayaendi kwa utashi wa mtu, kuwa na akili na kama hujui kitu tulia, tumia muda wako kusoma comments za wanaoelewa nawe ujifunze.
Mleta Post nakushauri masuala yafuatayo:
1. Angalia Cheo chako cha muundo ulichoajiriwa, kisha tafuta muundo wa Kada yako uone utaratibu uliowekwa wa kupanda madaraja kutoka ngazi moja na nyingine.
2. Kuthibitishwa kazini ( kwa mujibu wa Sheria) ni kuanzia miezi 8 hadi mwaka baada ya kuajiriwa, na pale unapoona hujapewa barua baada ya muda huo kuisha Sheria inaelekeza kwamba wewe tayari unethibitishwa by pressumption.
3. Mwajiri wako alipaswa kukupa barua ya sababu ya kutokukuthibitisha kazini baada ya mwaka kuisha, kama hajafanya hivyo ni kwamba alishakuthibitisha isipokuwa hajakupa barua.
4. Kwenda kusoma postgraduate diploma ya ualimu maana yake unataka uhame kutoka kada ya uhandisi na kuingia kada ya ualimu, ukirejea uajiriwe na uanze upya( kataeni upuuzi huo) na anayewashauri hivi ni Afisa Utumishi asiye na akili au Afisa Elimu wa magumashi.
5. Kwakuwa mna miaka 3 kazini, bado mwaka mmoja tu msitahili kupanda daraja hivyo msipofuatilia haraka mnaweza kupoteza haki zenu kwani hamtakuwa kwenye eligible list kwa ajili ya promo kwenye mfumo wa HCMIS.
6. Mwenye Mamlaka ya Miundo ya Utumishi wa Umma Nchini ni Katibu Mkuu_ Utumishi na ndiye aliyetoa kibali muajiriwe kwa Kada hiyo na kupelekwa Shuleni, ni katika sura hiyo kuwa malalamiko yenu lazima yaelekezwe kwake yakiwa na barua zenu za ajira.
7. OR TAMISEMI ni wizara tumizi, inawatumia Watumishi huku wakiwa si wasimamizi wa Miundo na Mishahara, kwahyo malalamiko yenu mliwasilisha kwa watu wasiojua kitu mathalan ukute ziliangukia idara ya Elimu iliyojaa walimu wenzenu kama mlio nao huko.
8. Poleni, zingatieni taratibu hizo. Barua zote mlizowahi kuandika kwenye mamlaka mlizotaja mzitunze kwa matumizi ya baadaye maana kwenye Utumishi jambo likikaa vibaya kila mtu huruka, ni vyema zaidi kama zilipokelewa kwa Dispatch.
Ahsanteni na karibuni shambani tulime
Mizega.
 
Shukrani Mkuu tunaufanyia kazi
Kila la kheri Mkuu, Halmashauri nyingi hazina Wahandisi hasa baada ya wengi kuhamia Tarura na Ruwasa baada ya Kuanzishwa kwake hizo taasisi, kwahiyo recategolization ingefanyika nyie wote mngehamia Idara za Ujenzi za Halmashauri iwapo mna Bachelor degree za Civil Engineering
 
Mkuu unamawazo bora sna na chanya Mungu akubariki sna

Tunaomba sna hii serikalini itusikie na kutusaidia,

Kwa asilimia kubwa Sisi wahandisi tulioajiriwa kama walimu, ndilo tunalotamani serikali yetu itufanyie

Natumai tutasikiwa na kutatuliwa hii changamoto yetu
Swala la kwenda kusomea PGD lisiwe swala la ulazima liwe option maana katika walioajiriwa kuna wengine walisomea ELImu ya ufundi(vocational teachers)

Pia swala hili katibu mkuu analijua maana alishawahi fikishiwa na Abdul nondo na akasema atalifanyia kazi lkn kimya mpk leo hawa vijana hawajui hatma yao katika hio ajira wakurugenzi na maafisa utumishi wao wanawaambia wanasubiri maelekezo toka juu huu mwaka wa 3 sasa unaenda kuisha. Na Huku tume ya waalimu haiwatambui pia.
Ikiwa hawa wahandisi wazalendo wanajitoa katika kuelimisha wadogo zao

Kikubwa serikali iwathibitishe hao wahandisi kwa fani zao lakini viendelee kuwa hapo mashuleni hii itasaidia baadae mtu atapanda daraja na cheo kutokana na taaluma yake. Na hata akitaka kuhama hawezi anza upya katika idara atakayohamia na pia itawasaidia serikali pale watakapoitaji wataalam.

Pia serikali iajiri walimu wa ufundi maana kuna kozi imeanzishwa pale MUST na vijana wanamaliza mwaka huu.

Pia hawana 1)barua ya ajira 2) mkataba wa kazi 3) barua ya kituo cha kazi 4) barua ya uthibitisho kazini. Kitu ambacho kinapingana na standing orders ya utumishi wa umma.

Katibu mkuu tamisemi tatua hili tatizo watu wajue wanaitumikia vp nchi yao.
 
Mkuu asante Kwa ushauri wako

Embu fikiria baadhi ya watu wameajiriwa na Diploma za Engineering lakini analipwa mshara wa TGTS C3,

Ana deni la bodi ya mikopo Kwa maana wakati anaajiriwa alikua final year ya Bachelor Degree in Engineering

Amejaribu kupeleka cheti cha Bachelor Degree in Engineering, Maafisa utumishi wanasema system haikubali hadi apeleke cheti cha ualimu Kwa maana bachelor degree in education (yaani akasome tena 3 years Kwa gharama zake)[emoji24]

ana familia, amepanga nje Kwa mshahara wa around 400K

Mkuu acha tu,

Mbona yuko sahihi

1. Diploma ya engineering ndio unaanza na TGS C
2. Kama umepeleka bachelor ya engineering then DHRO anasema "Ulete education" means kwasasa han uhitaji wa engeers.

Nakushuri hama halmashauri uende kwenye halmashauri zenye uhitaji halafu huko ndio ufanyiwe recategorization.

#YNWA
 
Tulipata bahati iyo ya kuajiriwa Mkuu wakati anamalizia kipindi cha kwanza na kwenda kipindi chake cha pili
Nyie hiyo 2020 mliajiriwaje ilhali tunaambiwa serikali haikuwahi kuajiri kipindi cha miaka sita toka 2016?
 
Mkuu point yako no:1, viwango vya walimu vya mshahara Kwa maana ya scale ni tofauti na scale ya wahandisi,

Mfano mwalimu wa science anaanza na scale TGTS D na mhandisi anaanza na TGS E,

Kwaiyo scale ya mwalimu wa Diploma sio sawa na Scale ya mhandisi mwenye Diploma,

Hivyo mwandisi (Mwenye Diploma) analipwa scale ya mwalimu wa Diploma ya science, hiki kitu sio sawa pia sio haki

Point ya 2: kama DHRO alikubali Diploma ya Engineering, Akafundishe shule ya ufundi anashindwa nini kumu upgrade mtu Kwa cheti chake cha Bachelor Degree in Engineering, ingawa anaendelea kufundisha shule? Na analipwa mshahara sawa mwalimu wa science?

Point 3: Watu tunatamani sna kuhama Ila changamoto Wakurugenzi wamekuwa hawapitishi barua za kuhama kwenda halmashauri zingine zenye uhitaji wa wahandisi
Mbona yuko sahihi

1. Diploma ya engineering ndio unaanza na TGS C
2. Kama umepeleka bachelor ya engineering then DHRO anasema "Ulete education" means kwasasa han uhitaji wa engeers.

Nakushuri hama halmashauri uende kwenye halmashauri zenye uhitaji halafu huko ndio ufanyiwe recategorization.

#YNWA
 
Mkuu asante Kwa ushauri wako

Embu fikiria baadhi ya watu wameajiriwa na Diploma za Engineering lakini analipwa mshara wa TGTS C3,

Ana deni la bodi ya mikopo Kwa maana wakati anaajiriwa alikua final year ya Bachelor Degree in Engineering

Amejaribu kupeleka cheti cha Bachelor Degree in Engineering, Maafisa utumishi wanasema system haikubali hadi apeleke cheti cha ualimu Kwa maana bachelor degree in education (yaani akasome tena 3 years Kwa gharama zake)[emoji24]

ana familia, amepanga nje Kwa mshahara wa around 400K

Mkuu acha tu,
Mwenye TGTS C3 atapanda daraja baada ya miaka mingapi ili awe tgts DI na mwenye TGTS C1 atapanda daraja baada ya miaka mingapi awe tgts D I Naomba maelekezo, pole Kwa changamoto nitaifanyia kazi
 
Shukrani Mkuu

TGTS (C1,C2 na C3) ni daraja moja
Kwa scale za kiualimu

The same kama D, kuna D1, D2 na D3.

Utofauti mfano mwalimu wa Diploma ya masomo ya arts ataanza na C1, na Mwalimu wa Diploma ya masomo ya sayansi ataanza na C3.

Ila kuna utofauti mdogo wa mshahara kati ya C1 na C3.

Mfano mwingine mwalimu wa Degree ya arts kabla ya nyongeza ya Mama alikua anapata D1 =716K na wa science alikua anapata D3 = 750K .


Kwenye inshu ya kupanda madaraja wote watapanda baada ya miaka 4 kwenda wa 5, (daraja Lao la Kwanza kupanda)

Natumai utalifanyia kazi kama ulivo ahidi

Uwe na wakati mwema Mkuu
Mwenye TGTS C3 atapanda daraja baada ya miaka mingapi ili awe tgts DI na mwenye TGTS C1 atapanda daraja baada ya miaka mingapi awe tgts D I Naomba maelekezo, pole Kwa changamoto nitaifanyia kazi
 
Sawa Mkuu nimekuelewa, inaweza kuonekana rahisi kwenda kusoma, Ila Mkuu ajira yetu ina complications nyingi ambazo tunaamini katibu Mkuu alikuwa anaweza kuziondoa

(Tunasubiri Tamko lake mwaka wa 2 huu)

Lakini imeshindikana tunaomba Burasa na hekima za Mkuu wa nchi mama yetu Dr. Samia Suluhu Hassan.
Lakini soma tu hio postgraduate mambo yakuendee ukikaza fuvu/kukaidi maboss utapata shida sana

Kubali tu usome yaishe mkuu
 
Mkuu asante Kwa ushauri wako

Embu fikiria baadhi ya watu wameajiriwa na Diploma za Engineering lakini analipwa mshara wa TGTS C3,

Ana deni la bodi ya mikopo Kwa maana wakati anaajiriwa alikua final year ya Bachelor Degree in Engineering

Amejaribu kupeleka cheti cha Bachelor Degree in Engineering, Maafisa utumishi wanasema system haikubali hadi apeleke cheti cha ualimu Kwa maana bachelor degree in education (yaani akasome tena 3 years Kwa gharama zake)[emoji24]

ana familia, amepanga nje Kwa mshahara wa around 400K

Mkuu acha tu,
Duuuh bora kuacha hiyo kazi,.

Mfano mie miaka hii 4, afu baadae niende Education miaka 3.

Sasa si bora ningeenda zangu BSc ED 3yrs. Lol.
 
Back
Top Bottom