WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

Mimi mwenyewe nimepinga sana kitendo cha Kanisa Katoliki kurudi nyuma katika kupigania haki za watanzania. Ila ninachofanya ni kuwa realistic. Kuhusu Katiba aliyevuruga ni Jakaya Kikwete baada ya kugeuka nyuma, sijui alionywa na akina Mkapa? Kanisa Katoliki lilifanya kazi kubwa sana, ingawa Kardinali Pengo alivunja nguvu jitihada hizo. lakini mvunjaji hasa ni Kikwete mwenyewe aliyeanzisha huo mchakato toka mwanzo.

Unasema madhehebu mengine yamekuwa yakikemea toka mapema? siyo sahihi! Ni juzi tu wakati wa Krismasi ndio Maaskofu walianza kukemea, nao ni KKKT na Katoliki. kabla ya hapo ilikuwa kimya kabisa. Lakini hata hivyo tofautisha kemea ya Askofu mmoja mmoja, na kauli ya Kanisa zima ambayo ni rasmi. hakuna dhehebu la kikristo wala waislamu ambao wametoa kwa kiwango hicho.

Unauliza Waraka unasaidia nini, kwa kweli hakuna chochote kinachoweza kumzuia JPM kufanya chochote anachotaka hivi sasa. isipokuwa, unapokuwa na Maaskofu wametoa tamko kama hilo, unaondoa ule uhuru wa serikali kuongea kwa kujinasibu. it is on the defensive. hiyo inapunguza kasi yake ya kutenda maovu. pia inagalvanise opposition both from outside and inside. pia taarifa kama hizi zinasaidia vyombo vya nje ambavyo vinaweza kufuta baadhi ya mikataba kutokana na kutoridhishwa na hiki au kile. Kumbuka pia kwamba Madikteta wote wanapenda kusikika vizuri. hivyo publicity kama hii inawakera sana, na watajitahidi kuiepuka. hiyo itatusaidia. pia angalau tutashuhudia kupungua kwa "ziara za Rais katika Makanisa na hotuba za kwenye mimbari" huku akiomba "kuombewa". haituongezei ubwabwa lakini angalau inatupunguzia kero.


Kwani JPM siye chaguo la mungu ???
 
Hao maaskofu wa kanisa katoliki Tanzania ni wasemaji maneno matupu bila matendo kama wenzao wa nchi ya DR Congo.

Waraka wa wajumbe TEC ni kelele za debe tupu hayana athari kwa serikali yao kama mnavyoona sasa kinachoendelea nchini.
"Waraka" ambao kiukweli ni "UJUMBE WA KWARESIMA" una sura nne, mbona mnadandia mada? Kwanini msisome na sura nyingine?
 
Wakati wa JK maaskofu wakiongea utaskia , mfumo kristo huo, wakati huu, walivokuwa kimya utaskia hawaongei kwasababu mwenzao, sasa wameongea utaskia walikuwa wapi muda wote, waislam Mungu anawaona mjue.
 
Somehow jamii sasa inatambua kuwa hawa jamaa wako against na yanayofanyika hapa kwetu kwenye kisiwa cha.......
 
Mara nyingi nyaraka za wakatoliki huwa zinatetemesha sana serikali

Hasa zile serikali ambazo Marais wake huwa ni Waislam daima huandamwa na kanisa kwa nyaraka lukuki. Lakini akitawala mkatoliki mwenzao daima kanisa hujifanya halioni kinachoendelea na hata likitoa waraka huwa unakuwa na lugha ya kubembeleza hivi. Hili ndilo kanisa katoliki mara zote liko kimaslahi zaidi.
 
Ni kama unafiki;
Watu pekee wanaoweza kusikilizwa kirahisi na rais ni viongozi Wa dini;
Maaskofu kila siku wapo na rais huko makanisani wanashindwaje kumkanya? Mtu ambaye kila jumapili mpo naye kanisani sioni haja ya kupoteza sadaka za waumini kukaa kikao ili kuandaa waraka Kwa ajili ya kufikisha ujumbe.
Pamoja na nia ya kuwasemea wananchi, maaskofu wanao uwezo Mkubwa Wa kuomba appointment ya kumuona rais na kumwambia!.

Nashauri rais asipoteze mda kuwajibu maana wameonyesha unafiki;
Haiwezekani mtu unakaa naye meza moja ukamwandikia barua kupitia njia ya Posta!

VIONGOZI WA DINI NDIO ZAO LA KUPATA VIONGOZI HAWA TULIONAO
 
Kwani wewe ndiwe Rais? Au wewe ndiye mwandaaji wa ratiba zote za Rais? Una uhakika gani maaskofu hawakutani naye? Una uhakika gani hawamwelezi hayo? Lakini ule waraka ulijaa mambo mengi ya msingi sio kwa Rais tu; na wala haukumlenga Rais bali ulilenga wote "wenye mapenzi mema".

Kama una mapenzi mema ule waraka hauwezi kukureka kamwe! Na sidhani hata Mh. Rais mwenyewe kama unamkera zaidi ya kukera vibaraka kama ninyi ambao mnadhani mna uzalendo kuliko watanzania wote wakiwamo Wahashamu Maaskofu. Swali muhimu katika waraka ule "Mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?"; tafakari!
 
Katika ujumbe wako huu kuna sehemu umepatia na kuna sehemu umeboronga, ujue nafatilia sana topic zako na huwa nazipenda ila kwa hapa km nilivyokuambia. Ila tusiulizane
 
Kwani kwenye waraka wao umeona kuna sehemu maaskofu wameomba wajibiwe na Rais au ndo kuwashwa kwenyewe!!!!?
 
Kwanza hakuna waraka uliyoandikwa kwa rais isipokuwa kuna waraka unaozungumzia hali ya siasa inayoashiria ukosefu wa haki na hatimaye amani

Wanaoona ujumbe ulioko kwenye waraka unafaa kwa mustakabali wa amani ya watanzania na wanajukumu la kusimamia haki basi ni muda muafaka kujitafakari

Waraka unawakumbusha hasa waumini wakatoliki hasa wajibu wao kama wakristo

Waraka una kurasa ishirini na wamezungumzia siasa kurasa mbili tu lakini unaochoma sana kwa wale wanasiasa wasiopenda haki japo haki hiyo ni kwa mujibu wa katiba ya nchi yetu

Kwa hiyo nia ya waraka kwa ujumla siyo siasa bali imekuwepo kama agenda mojawapo kwa hali inavyoenda ndani ya nchi

Kumbuka wanasiasa ni wengi ndani ya nchi kwa hiyo ujumbe si kwa rais pekee kama unavyotaka kutuaminisha

Pia hakuna dhehebu au dini liko karibu na rais kuliko nyingine kama unavyofikiria kuwa maaskofu wako karibu na rais kuliko mashekhe. Rais ni wa watanzania, Maaskofu ni kwa ajili ya wakristo na Mashekhe ni kwa ajili ya waislamu
 
Umesoma sura zote nne za "UJUMBE WA KWARESIMA"? Usiandike ili kupata likes za JF bali kuelimisha. soma Sura ya kwanza "BASI ENENDENI", Sura ya pili "SASA NI ZAMU YETU" Sura ya tatu "MIMI NI MLINZI WA NDUGU YANGU?" Sura ya nne "NIMRUDISHIE BWANA NINI?" hapo utapata ujumbe kamili waliotaka jamii iupate na kuufanyia kazi.
 
Maamuzi halali ya taasisi yoyote yamewekewa utaratibu, bila kufuata utaratibu maamuzi huwa batili, nafikiri ni vizuri kuheshimu utaratibu wa kanisa, kama una hoha za msingi sema
 
Ukweli unauma waliyoyasema ndo kilio cha walio wengi wanaopinga ni wanufaika tu
 
Tatizo ni kwamba hii siyo nchi ya mtu mmoja. MUACHENI AFANYE KAZI! Hakuna anayetaka wala hakuna anayeweza kumzuia Rais kufanya kazi, ila yeye ndiyo hataki wengine wafanye kazi. Hataki vyama vya siasa vifanye kazi wala hataki mihimili ifanye kazi yake kwa mujibu wa katiba.

Yaani unawezaje kumzuia Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kufanya kazi? wewe ni nani? Inavyoonekana Amiri jeshi huyu wa sasa wa Tanzania ana hofu kiasi kwamba hata chama cha siasa kisichokuwa na jeshi wala silaha, anakiogopa. Hii nchi ina Taasisi na mifumo mbalimbali ambayo yote inatakiwa kufanya kazi. Kuna taratibu za kikatiba za watu kukosoa na kupongeza, na kwa ujumla kutoa mawazo yao. Kuna mihimili ya Bunge, Mahakama, na Serikali, ambayo kila moja ina kazi yake na majukumu yake.

Amiri Jeshi wetu ni mwoga sana kiasi hataki mihimili mingine ifanye kazi yake kwa kujitegemea na uhuru kwa mujibu wa Katiba. anataka awe yeye tu. Na hata alivyosema hakuna siasa mpaa 2020, mwenyewe ameendekeza siasa tena za kijinga, kwa kukwapua wabunge waliochaguliwa na wananchi, na kuwalazimisha warudi tena kwenye uchaguzi! Ndiyo kuchapa kazi huko? kutuingiza hasara za kijinga?

Na bado ana mashitaka mengi tu. hiki kitendo cha kuruhusu ubaguzi wa kiitikadi, kiasi kwamba viongozi wanadiriki kutamka hadharani kwamba ukichagua mtu wa CCM ndio mtapata maendeleo, wakati fedha ni zetu sisi wote, Serikali ni mgawaji tu, huo ni UHAINI. Na ni DHAMBI KUBWA SANA. MAGUFULI ANATAKIWA KUTUBU.

Mwisho, kauli ya Maaskofu siyo ya kubeza. wameitoa iikiwa miaka miwili imepita ya serikali hii. hawakuwa na haraka, wengi wamewalaumu kwa kukaa kimya muda mrefu. wamejitafakari kabla ya kuitoa. Magufuli ajipange, ajipime. Kuwabeza viongozi wa dini pale wanaposimama kwenye UKWELI, NI JAMBO LA HATARI SANA.
Toa povu liishe kabisa. I can guess wewe ni mmoja wa waliotumbuliwa. MUACHE RAIS APIGE KAZI. Period!
 
Back
Top Bottom