Waraka uliowaondoa Zitto Kabwe na Kitila Mkumbo CHADEMA huu hapa

Kama unadhani anatumika, basi ujue hata huko nako watamtosa, maana amadhara ya kutumia huwezi kuaminika tena mbele ya jamii zote

 
Naamini huu ni uamuzi mbovu na unaokiangamiza chama, waraka uko clear na kwa busara za kawaida si jambo baya watu kuhitaji uongozi. kwani kiongozi aliyepo si aliwakuta wengine, kwahiyo alikuwa msaliti kipindi alipotaka kuingia kwenye uongozi. Naipenda chadema ila roho inaniuma kinapoangamizwa na watu then tunawashangilia. Mungu ibariki Tanzania mungu inusuru chadema
 

Kweli Wajinga ndio waliwao,naona Ben Saanane hajasahau kujifagilia hapo kwenye hiyo riwaya yao walioitengeneza.

Hapa ni either Mbowe na Dr Slaa ni wajinga sana mpaka wanadanganyika kirahisi hivi au wanamuogopa sana Zitto mpaka kupelekea wao wenyewe ku-engineer huu mchezo wa kitoto wa kujitekenya kisha kucheka wenyewe.

Zitto,tunakuamini!!propaganda za kitoto kama hizi haziwezi kufanikiwa na hazitafanikiwa.Chukua muda huu kutafakari kwa makini na fahamu kuwa tunausubiri mwongozo wako na tutakuunga mkono.
 
Aisee kweli cdm hakuna demokrasia,leo zitto na wengne,kesho lissu, chama cha wachaga hicho,tena wa familia moja. baba mkwe,mke na mbowe . duuh 2tafika kweli.

USISEME ZITTO. SEMA MSALITI au AGENT WA CCM NDANI YA CHADEMA, WE ROFA NINI?
HII IMEKULA KWENU CCM, NAILAUMU CHADEMA KUCHUKUA MDA MREFU KUFANYA UAMUZ HUU AMBAO NI MWIBA KWA CCM.

LKN WANA KIGOMA MJITAFAKALI PIA KWANI MMEKUWA CHEAP SANA KWA CCM ????????????????
KWA USANII HUU WA AWA VIONGOZI WAHUNI MKIANDAMANA KUMUUNGA MKONO ZITO MTADHIHIRISHA UKOLA WENU,
Hebu angalia hapa;
[*]Nsanzugwako alikuwa NCCR baadae akarudi magambani akapewa uwaziri

[*]Kaburu alikuwa cdm akarudi magambani akapewa u-rc

[*]Kafulila alikuwa cdm akatimuliwa na kwenda nccr nako nusura atimuliwe

[*]ZZK alikuwa mwanachadema kwa masaa ya mchana na usiku akitumika ccm
 
Chama cha mwiz hakimtak askari ila kinaweza kuish na mgambo.
Kuna makosa gan?swala ni kila kukubal kukosolewa,politics good game politician dirty players,VIVA VIVA anð SOLOLABYee.
 
Ni sawa kuhitaji uongozi ni jambo zuri lakini USIRI uliogubikwa na huo mkakati na usaliti ni dhambi kubwa zaidi let the traitors GOOOOOOOOOO!! it is better to remain with five pure wolves than 1million wolves in sheep skin!!
 
Chadema imeshakufa, thats all. Kwenye uchaguzi kunakuwa na kambi, kwann chadema ni dhambi kuwa na kambi na ni dhambi kutofautiana kimawazo na mtizamo?

Elewa kuwa huu waraka sio wa mabadiriko bali ni waraka wa MAPINDUZI hivyo walichokifanya hawa jamaa walikuwa wanaandaa MAPINDUZI pasipo umwagaji wa damu na sitawaweka mbali sana na akina RUGANGIRA, TAMIM MACGEE na wengineo ambao walitaka kumpindua Marehemu Baba wa Taifa kipindi kile. na elewa hawa jamaa kwa kuwa walikuwa wakiratibiwa na CCM walikuwa wapo tayari hata kutoa uhai iwapo mbinu hii ingeshindwa na kwa tafakuri ya kina kumbuka tukio la bomu la Soweto Arusha kwani mmojawapo kati ya hawa M1,MM,M2 na M3 alihusika kupanga mkakati ule.
 
Chama cha mwiz hakimtak askari ila kinaweza kuish na mgambo.
Kuna makosa gan?swala ni kila kukubal kukosolewa,politics good game politician dirty players,VIVA VIVA anð SOLOLABYee.

Naomba unijibu maswali yafuatayo
1. Kwa nini Horace Kolimba aliuliwa na CCM na aliuliwa baada ya kutamka nini?
2. Juzi CCM imemfukuza na kumvua uanachama yule mzanzibari ni nini hasa alichokifanya hadi CCM kufikia uamuzi ule?
3. Hiki walichokifanya hawa wasaliti ndani ya CDM kina tofauti na walichokifanya hao waliwajibishwa ndani ya CCM?
 
Hapa Zito anataka kutuambia kuwa yeye ni maarufu sana, anajua kujenga hoja! Ni mtu makini! anakubalika! anajua kushawishi! Hivyo yeye ndie anafaa kuwa "mkuu wa CDM'

Mpuuzi kweli huyu mtu! Hayo yote ni UBINAFSI, kutumiwa, UKUWADI na uroho wa madaraka! Kaazishe chako basi tuone kama una nguvu ya kuwa na watu wengi kama unavyojuvuna! Huna lolote, mbona hata UDSM hukuwa na lolote darasani ulikuwa wa kawaida tu Zito? Jeuri ya fedha ndio inakupa KIBRI tu.:frusty:
 
umeandika vizuri. Kinachonipa taabu ni kama matatizo yaliyopo cdm leo ni ya aslili au ni ya kupandikiza kama inavyodaiwa na baadhi ya watu. Kama ni matatizo halisi basi huu ni 'mwanzo wa mwisho' wa cdm lakini kama ni ya kupandikiza tutarajie matokeo makubwa na mazuri kuliko wakati wowote.
Kwenye red hapo kama mwananchi wa kawaida nasikitika sana kuona ccm ikiwa na uwezekano wa kubakia madarakani si kwa sababu ya uimara na utendaji wake bali kwa sababu ya 'kufa' kwa upinzani ambao miaka ya karibuni umekuwa ukifanya vizuri na kutupa matumaini.

 
Kama umeusoma waraka huu hadi mwisho, nona ni ampeni za kawaida ndani ya vyama kila uchaguzi mkuu unapokaribia wala sioni usaliti wowote. Kuna haja ya viongozi wa cdm kujitazama na kuvumiliana na wenzao wenye mtazamo tofauti na ndio demokrasia yenyewe.
Kama kweli uongozi uko imara, wasiwasi wa nini juu ya hizi hekaya ambazo wala hazijaanza? Badala ya kufukuzana, viongozi makini wangetumia nafasi huu kuwadhibiti wahusika na huenda hta kwenye uchaguzi wasingefika kokote, badala yake jazba imeachwa kuamua na matokeo wanawanufaisha ccm ambao huenda wanashangilia huko waliko.
 

Mkuu hayo mengine siwezi sana kutolea majibu kwani waraka wenyewe ukiuanzia juu hado chini utaona vijana na wazee walitaka kutengeneza movie ya 007 kwa fikra za bongo movies.

Well, labda tuu nikuambie kwa jinsi ulivyojitambulisha kuwa Kitila mkumbo ndie aliyekuvutia ,na hivyo sasa unapata blow sana.Huo ndio ukweli ila umekosea kitu kimoja..hapa ulipaswa umia sana kwa Mtu uliyemtazama anapofanya kitu irresponsibly hivyo.NIlitegemea kwa umri wako ungekuwa umeona jinsi Zitto alivyo irresponsible na mwenye jazba na papara km Waraka unavyosema.Tena kw akiasi ambacho waandaji wameona kuwa ndio tishio lake kuu.Hayo ndiyo tumekuwa tukiyasema sana humu.Na ujumla wake ni kukosa BUSARA km waraka ungeandikwa na mwingine neno Busara lingetumika ktk hii CV ya Zitto au mkakati.

Mkandara kuna watu wengi tuu huvinjwa mionyo yao na Viongozi wa dini waliowamini na kuja kuta wakiwabaka(si madrassa, sunday schools, shule za kidini etc), wapo watu walihisi salama mikoni mwa wazee wao na kujibuka wakiwabaka na kuwaua, wapo walioamini waume na wake zao ni rijali kumbe ni mashoga, wapo walioamini walimu wao wa uchumi ni wachumi kweli,kumbe personala finance ni issue hadi wanajiua.Ndio maana tunakatazwa kumtegemea mwanadamu hata ktk mema.

Dr.Kitila isku zote sijawahi weza pata namna ya kumwondoa ktk uchafuwa UDSM Political Science nanimekuwa nikisema haya sana .Wapenda propaganda na wneye uwezo mdogo wamekuwa wakidhani nashambulia kwa ukanda, sijui ukabila.Nae kwa akili yake akabweteka akidhani Ni msomi wa daraja lake, bila kuw ana clue kuwa shida ni shule aliyosoma na waliomfundisha,ndio wamemwaribu sana pamoja na kwamba propaganda za mlima zinafanya watu waone kuwa ni chuo bora sana.
 

Mkuu huu waraka ulikuwa wa siri, haukuwa wazi, lengo lake kuu ilikuwa kuweka kundi flan madarakani iwe kwa lengo baya au zuri hiyo ni siri yao....unadhani kama hawa watu wanataka madaraka wangetoa sifa yoyote kwa wapinzani wao?
 
Kinachotokea Chadema ni Ushamba wa demokrasia. Huu waraka haujamtukana mtu yeyote ni moja ya mbinu hasa katika siasa za ushindani. Hata nyinyi Chadema mnamikakati yenu ya kuchukua Dola 2015 na kuiondoa CCM madarakani je na ninyi mchukuliwe hatua???Acheni ushamba wa demokrasia bhana.Mkiwafukuza uanachama ati kwa kivuli cha waraka huu basi na nyie mtafutiwa usajili wa saccos yenu kwa ku'mastermind matukio mbalimbali ya mauaji kama mbinu mojawapo ya kuingia madarakani.
 
Zitto na wenzake watavuna walichokipanda.. Kama analalamika chama kuyumba wakati yeye ni Naibu katibu Mkuu, je mchango wake yeye umeonekana wapi katika kukijenga chama?
Na kwa nini aandae vikao vya siri kama hivi badala ya kutumia vikao halali vya chama kama anaona kuna issues hazitulia?
Hawa ni masalia tu watapotezwa kama akina Juliana Shonza, na Mwampamba... Shame on Zitto and his friends.
 
Maneno haya hayamsafishi ZZK wako na kashfa ya kelele nyingi kutafuta hongo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…