Uchaguzi 2020 Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania

Uchaguzi 2020 Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania

Status
Not open for further replies.
uko mwanzoni wameenda vizuri sana ila waliponza kuongelea mambo ya udini ndo nikajua hawa jamaa ni wapumbavu sana🙁🙁🙁, wanafikiri juu ya uislam na ukristo tu, je vipi wale wasiokua na dini?? je vipi juu wale wasioamini juu ya mungu?? wao hawastahili hayo yote??? Hizi dini zinajaza watu upumbavu mwingi sana kichwani, badala ya kuangalia mambo ya msingi we unaangalia eti waslam/wakristo wangap wameteuliwa..Dini nyingine wasemaje???
Jamaa ni wapuuzi sana natamani walioandika huu upuuzi wawekwe ndani haraka sana maana wanalisha watu upuuzi na madini ya kikoloni
uislam na Ukristo vyote ni upuuzi mtupu vinatugawa tu
 
Azarel,
Umeghadhibika.

Naijua kweli historia ya Tanzania kuliko watu wengi ndiyo hiyo, "so what."

Watafiti kutoka vyuo vingi ndani na nje ya Tanzania hawapungui nyumbani kwangu.
 
"Nimesoma Informatics udom pale namjua vizuri sana Dr. Masoud Masoud alikuwa yupo mbele sana kwautetezi wa waislam popote akiona kuna ukandamizaji wa waislam alikuwa anakuja juu nadhani hiki ndio kimemponza Alikuwa ni head wa Department ya computer Science. Na prof. Leonard Mselle namjua vizuri sana yeye sio mdini nimtu safi sana huyu mzee mara nyingi husimama kwenye ukweli nimlezi mzuri wa wanafunzi." Mhitimu wa UDOM
kwahyo akiona anakandamizwa asiye na dini za kikristo wala kiislam alikuwa anachekelea sio?
 
Azarel,
Umeghadhibika.

Naijua kweli historia ya Tanzania kuliko watu wengi ndiyo hiyo, "so what."

Watafiti kutoka vyuo vingi ndani na nje ya Tanzania hawapungui nyumbani kwangu.
Hahaha, nilijua utaleta hayo majigambo...!

Leta na zile picha zako za nchi za Nje mbali na Tanzania, pia usisahau vitabu vyako vinavyosomwa Duniani kote.

Sasa ukiijua hiyo historia...then what?
 
MUONGOZO WA SHURA YA MAIMAMU TANZANIA UCHAGUZI MKUU WA TAIFA OKTOBA 2020

Shura ya Maimamu wa Tanzania imetoa waraka unaohusu Uchaguzi Mkuu.

Katika waraka huu au muongozo huu kuna mengi ya kufikirisha sana kiasi mtu atajiuliza haya yanawezekana vipi kutendeka katika nchi inayojinadi kuwa inazingatia haki na usawa kwa wananchi wake wote na inapiga vita ubaguzi wa aina yoyote.

Katika mengi niliyosoma hili hapo chini nikilijua siku nyingi na limekuwa likinisikitisha sana.

Kwa kuwa waraka wamelieieza naona itakuwa vyema nikaliweka hapa kwa faida ya wasomaji:

Uadilifu I

''Januari 11, 2019, serikali ilifanya uhamisho mkubwa wa kushitukiza kwa wahadhiri na watumishi wandamizi katika Chuo Kikuu cha Serikali cha Dodoma-UDOM.

Waliohamishwa walikuwa 11, lakini wote walikuwa Waislamu:

Dk. Maryam Khamis (Director of Graduate Studies), Dk. Ibun Kombo (Political Science), Dk. Mwinyikombo Amir (Mwalimu wa Udaktari wa Binadamu), Dk. Yusuf Kambuga (College of Education), Dk. Masoud Masoud (Informatics) , Bw. Subira Sawasawa (Mkurugenzi Mkuu Rasilimali Watu), Bw. Mohamed Mwandege (Bursar/Mhasibu Mkuu), Bi. Aziza Gendo (Seniour Estate Oficer), Bw. Simba Omary (Senior Supplies Oficer), Bw. Wema Mbegu (Legal Oficer), Bw. Khamis Mkanachi (Mwalimu wa Idara ya Historia).

Barua zao za uhamisho hazikuonesha makosa katika utendaji wao wa kazi au uongozi. Pamoja na kutokuwa wakosaji, uhamisho wao uliambatana na udhalilishaji mkubwa, kunyimwa haki stahiki za uhamisho, kuhamishiwa katika nafasi za chini kinyume na hadhi zao.

Baada ya uhamisho huo, Serikali ilifanya uteuzi mwingine katika chuo hicho hicho cha Serikali.

Katika uteuzi huo walioteuliwa walikuwa 11, wote Wakristo: Prof. Leonard James Mselle, Prof. Adam B. Swebe Mwakalobo, Prof. Julius William Nyahongo, Prof. Justin Ntalikwa, Prof. Frowing Paul Nyoni, Prof. Odass Bilame, Prof. Ainory Piter Gasese, Dkt. Victor George Mareale, Dkt. Alex Shayo, Dkt. Calvin Swai, Dkt. Augustine Mwakipesile.

Kuhamisha wahadhiri 11, katika Chuo Kikuu si jambo dogo.

Vilevile kuhamisha Wahadhiri 11, wa dini moja (Waislamu) katika Chuo Kikuu ukaingiza wahadhiri 11 wa dini moja (Wakristo), na hao Waislamu 11, baadhi yao ukawatoa kabisa katika mfumo wa elimu kwa kuwapeleka sekta nyingine na zisizo lingana na hadhi zao si jambo dogo. Wala si hatua ya kitaalamu ya kuboresha mfumo wa Elimu wa Taifa.

Na wala si hatua ya kijinga bali ya werevu uliofurutu ada dhidi ya maslahi ya Taifa.

Hatuwa hiyo ni salamu nzito kwa jamii yao na Taifa kwa ujumla. (Ndio maana katika maoni yetu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tulipendekeza Katiba Mpya imtambuwe Mwenyezi Mungu na Dini liwe suala rasmi na la wazi katika uendeshaji wa nchi).''
Ndugu nami pia nimeusoma sawa wangeweka na teuzi alizofanya rais wa awamu iliyopita jakaya kikwete(mwislamu) ili tulinganishe
 
Nimekuelewa ndugu. Akutukanae hakuchagulii Tusi. Hili ni Tusi tosha kwa waislam pale usemapo: "sidhani kama kua sababu ya kulilia teuzi hata kama watu hawana vigezo vya kiuongozi" Hewala, Tumekusikia. Ila nakuomba ujitafakari, maana kwa maneno yako, wenye uwezo na vigezo vya kiuongozi ni wakristo.

Over!
Hapana,ni tafsiri yako,Tafsiri yangu ni rahisi tu kwamba hakuna teuzi zinazopatikana kwa kuonewa huruma wala kupendelewa bali ni jitihada za mtu kujionesha uwezo wake,kusimamia anachokiamini na kutafuta fursa.Hii keki ya taifa kila mtu anataka kuila na kama Waislamu katika msingi wa kidini mnaona kwamba mnamegewa kipande kidogo ni jukumu lenu kujitazama ni wapi mnakwama kabla ya kuanza kutafuta wa kumsingizia.

Mimi binafsi nimeanya kazi na Waislamu pamoja na Wakristu.Nimeishi na Waislamu pamoja na Wakristu,Nimesoma na Waislamu pamoja na Wakristu.Na kote huko sijaona popote ambapo kigezo cha uislamu wa mtu kinamkosesha mtu fursa.Nimeona watu wakikosa fursa kwa sababu hawana connection,hawana uwezo wa kujiuza,Hawana wa kutetea wanachokiamni,

Hili sio tatizo la Waislamu ni Tatizo la Watanzania wengi.Ndio maana hata ukitazama wanaokula mema ya nchi ni zile jamii ambazo ziliamka mapema na kutafuta kujikomboa bila kusubiri huruma za watawala.

Kama tutaendekeza fikra za namna hii za kuaminisha umma kwamba watu wanafanyiwa figizu kwa sababu ya uislamu wao bila kuweka Facts za pande zote mezani basi itakuwa ni tatizo.

Tusijifanye hatuoni tatizo la Radical Islamism katika jamii,Elimu ya dini imepewa kipaumbele ila sio kwa ajili ya kujenga misingi ya utu na ubinadamu bali zaidi ni katika kuwa brain wash watu.

Wapo vijana wa Kiislam ambao wanafanya vizuri na ambao wamepewa nafasi,wengine mjifunzo humo mjue walifikiaje hatua hio.Hakuna sababu ya kufikiri kwamba mabadiliko yatakuja kwa neema.

Ni dhahiri shahir kwamba hata mkipewa mamlaka na nafasi mtaanza kupendeleana kama kilichotokea UDOM mpaka wakahamishwa hao wote ni kwa sababu ya kuanza kuonesha ubaguzi wa wazi wazi.Penye ukweli tuambiane ukweli.Sisi ni Watanzania kwanza kisha Waislam baadae.Hizi imani zilikuja na Jahazi,wenye nazo wamekaa wanajenga nchi zao sisi tunalumbana kutaka vyeo kwa msingi wa udini?Mmesikia utumishi wa umma ni sawa na Uimamu au kuwa Mwalimu wa dini?Kama mnao uwezo jitokezeni,Gombeeni,Toni sera zenye mashiko zisizokuwa na udini bali maendelea mpewe nchi then mkifanya vyema tutawachagua tena na tena na tena.
 
Hapana,ni tafsiri yako,Tafsiri yangu ni rahisi tu kwamba hakuna teuzi zinazopatikana kwa kuonewa huruma wala kupendelewa bali ni jitihada za mtu kujionesha uwezo wake,kusimamia anachokiamini na kutafuta fursa.Hii keki ya taifa kila mtu anataka kuila na kama Waislamu katika msingi wa kidini mnaona kwamba mnamegewa kipande kidogo ni jukumu lenu kujitazama ni wapi mnakwama kabla ya kuanza kutafuta wa kumsingizia.

Mimi binafsi nimeanya kazi na Waislamu pamoja na Wakristu.Nimeishi na Waislamu pamoja na Wakristu,Nimesoma na Waislamu pamoja na Wakristu.Na kote huko sijaona popote ambapo kigezo cha uislamu wa mtu kinamkosesha mtu fursa.Nimeona watu wakikosa fursa kwa sababu hawana connection,hawana uwezo wa kujiuza,Hawana wa kutetea wanachokiamni...

Hakuna mahali waislamu wanakwama. Haiwezekani teuzi asilimia 80 zilalie kwa Wakristo halafu uwashutumu waislamu
Waislamu wenye vigezo wapo wengi sana lakini teuzi zimelalia kwa watu wa dini moja, na hii inaonyesha ni makusudi kabisa
 
Hatuwezi kutembelea magari ya dini na makabila kama kweli tunajali maslahi ya umma. Kama kuna mtu ambaye dini yake inaona anafaa kuwa kiongozi, apewe wadhifa huo katika dini yake lakini si kulazimisha serikali. Tunaangalia uwezo wa mtu.

Nafasi ya Makamu wa Raisi ni zaidi ya wakuu wa mikoa 130.
Nafasi za mawaziri ni zaidi ya wakuu wa wilaya 500.

Acheni kubumba migogoro isiyokuwepo. Tushikamane tujenge nchi. Dini na makabila kila mtu abaki na ya kwake.
 
Hapana,ni tafsiri yako,Tafsiri yangu ni rahisi tu kwamba hakuna teuzi zinazopatikana kwa kuonewa huruma wala kupendelewa bali ni jitihada za mtu kujionesha uwezo wake,kusimamia anachokiamini na kutafuta fursa.Hii keki ya taifa kila mtu anataka kuila na kama Waislamu katika msingi wa kidini mnaona kwamba mnamegewa kipande kidogo ni jukumu lenu kujitazama ni wapi mnakwama kabla ya kuanza kutafuta wa kumsingizia...

Ngonjera ndeefuuuuu lakini unarudi kwenye point 1 ile ile. Unachotaka kusema ni kwamba ni 20% ya waislam ndio wachapakazi ukilinganisha na 80% ya wakristo. Huu ndio muhtasari na tafsiri ya ngonjera ndefu.

Umebugi ndugu, haya matatizo yapo miaka toka miaka dahli iliyopita. Unaficha unachokijua huku ukionyesha kuwa wewe ni mdini namabari moja. Utamchagua nani mtu mdini kama wewe!

Maeneo mengi watu walifanyiwa hivyo, ila yakiibuka usiyoyatarajia hata wewe utakuwa mhanga Nr1. Kuwa na pevuka huku ukifumbua macho ili uone.
 
Hatuwezi kutembelea magari ya dini na makabila kama kweli tunajali maslahi ya umma. Kama kuna mtu ambaye dini yake inaona anafaa kuwa kiongozi, apewe wadhifa huo katika dini yake lakini si kulazimisha serikali. Tunaangalia uwezo wa mtu.

Nafasi ya Makamu wa Raisi ni zaidi ya wakuu wa mikoa 130.
Nafasi za mawaziri ni zaidi ya wakuu wa wilaya 500.

Acheni kubumba migogoro isiyokuwepo. Tushikamane tujenge nchi. Dini na makabila kila mtu abaki na ya kwake.

Pangekuwepo na haki nchini kauli yako ingemake sense.

Tatizo ni kwamba tunatembelea gari ya udini halafu tunawaambia wale wanaopiga kelele kkukea hayo kuwa tusitembelee gari ya ya udini.

Unafiki mtupu!
 
Hakuna mahali waislamu wanakwama
Haiwezekani teuzi asilimia 80 zilalie kwa Wakristo halafu uwashutumu waislamu
Waislamu wenye vigezo wapo wengi sana lakini teuzi zimelalia kwa watu wa dini moja, na hii inaonyesha ni makusudi kabisa
Unataka wanapotaka kufanya teuzi watangaze msikitini au watangaze wapi?Unataka wawafuata waislamu majumbani kwao wawateue na kuwapa vyeo?Lazima tukubali kwamba Dini is Identity na hakiwezi kutumika kama kigezo cha kumpa mtu nafasi ya uongozi popote pale.Swali ni Je waislamu wana kwama wapi?kwa nini hawaonekani? Tuanzie hapo kwanza kabla ya kutafuta kuonewa huruma au kupeana Lawama.

Ubaguzi huwa unaanza kwa mtu kujibagua mwenyewe kwa sababu tofauti.Sasa ubaguzi wa namna hio huwezi mlaumu .Nasisitiza.Onesheni uwezo,Tangazeni vigezo vyenu,gombeeni nafasi za uongozi. Tukiwaona na kuwaelewa tutawapa madaraka na kwa hakika mkituongoza vyema tutawachagua tena na tena na tena.
 
Hapana,ni tafsiri yako,Tafsiri yangu ni rahisi tu kwamba hakuna teuzi zinazopatikana kwa kuonewa huruma wala kupendelewa bali ni jitihada za mtu kujionesha uwezo wake,kusimamia anachokiamini na kutafuta fursa.Hii keki ya taifa kila mtu anataka kuila na kama Waislamu katika msingi wa kidini mnaona kwamba mnamegewa kipande kidogo ni jukumu lenu kujitazama ni wapi mnakwama kabla ya kuanza kutafuta wa kumsingizia...
Hawaelewagi Hawa Vilaza Mkuu, labda uandike kinyumenyume kwa kiarabu.
 
Pangekuwepo na haki nchini kauli yako ingemaje sense.

Tatizo ni kwamba tunatembelea gari ya udini halafu tunawaambia wale wanaopiga kelele kkukea hayo kuwa tusitembelee gari ya ya udini.

Unafiki mtupu!
Wekeni na teuzi alizofanya Rais Kikwete hapa.
 
Ngonjera ndeefuuuuu lakini unarudi kwenye point 1 ile ile. Unachotaka kusema ni kwamba ni 20% ya waislam ndio wachapakazi ukilinganisha na 80% ya wakristo. Huu ndio muhtasari na tafsiri ya ngonjera ndefu.

Umebugi ndugu, haya matatizo yapo miaka toka miaka dahli iliyopita. Unaficha unachokijua huku ukionyesha kuwa wewe ni mdini namabari moja. Utamchagua nani mtu mdini kama wewe!

Maeneo mengi watu walifanyiwa hivyo, ila yakiibuka usiyoyatarajia hata wewe utakuwa mhanga Nr1. Kuwa na pevuka huku ukifumbua macho ili uone.
Mkuu hakuna udini zaidi ya hisia zako.Waislamu Mnajibagua wenyewe kwa sababu mnayoijua.Mbaya zaidi mnabaguana wenyewe kwa wenyewe tena kwa kiwango kikubwa sana.Inatosha tu kwa mimi kusema kwamba.Dini sio kigezo cha niniyi kupewa madaraka.Uwezo wako kiutendaji pamoja na elimu na uzoefu ndo Kigezo.

Mtazameni Prof Assad Mwislamu Msomi.Alipewa nafasi akafanya kazi yake kwa kadiri ya uwezo wake na alifanya kazi nzuri na tunamheshimu.Mtazame Zitto Kabwe pamoja na mambo yake flani bado amejijengea heshima katika jamii kwa nafasi yake,Mtazame Lipumba,Mtazame,Maalim Seif Sharif Hamad,Watazame waislamu wengi mashuhuru wenye kuheshimika na useme ni wapi wamebaguliwa kwa sababu ya udini wao.

Kama mnataka kubebwa lazima kwanza mjibebe na muoneshe uwezo wenu ili hata anayejaribu kuwa bagua aone aibu.
 
Hawaelewagi Hawa Vilaza Mkuu, labda uandike kinyumenyume kwa kiarabu.
Hawa sio vilaza.Wanahitaji kuambiwa ukweli ambao hata wao wenyewe hawaambiani.Wahamasishane katika mimbari misikitini na madrasa,wachukue fomu wagombee nafasi za uongozi kwa ngazi zote.Walete sera za maendeleo bila udini na ubaguzi.Tuwachugue kwa uwezo wao.Wafanye kazi kwa bidii.

Kama hawawezi kufanya hivyo hizi lawama zao za ubaguzi bila kuchukua hatua stahiki ni upuuzi tu ambao kwa karne hii hauhitajiki hata kidogo.
 
Hawaelewagi Hawa Vilaza Mkuu, labda uandike kinyumenyume kwa kiarabu.
Hawa sio vilaza.Wanahitaji kuambiwa ukweli ambao hata wao wenyewe hawaambiani.Wahamasishane katika mimbari misikitini na madrasa,wachukue fomu wagombee nafasi za uongozi kwa ngazi zote.Walete sera za maendeleo bila udini na ubaguzi.Tuwachugue kwa uwezo wao.Wafanye kazi kwa bidii.

Kama hawawezi kufanya hivyo hizi lawama zao za ubaguzi bila kuchukua hatua stahiki ni upuuzi tu ambao kwa karne hii hauhitajiki hata kidogo.
 
Mkuu hakuna udini zaidi ya hisia zako.Waislamu Mnajibagua wenyewe kwa sababu mnayoijua.Mbaya zaidi mnabaguana wenyewe kwa wenyewe tena kwa kiwango kikubwa sana.Inatosha tu kwa mimi kusema kwamba.Dini sio kigezo cha niniyi kupewa madaraka.Uwezo wako kiutendaji pamoja na elimu na uzoefu ndo Kigezo.

Mtazameni Prof Assad Mwislamu Msomi.Alipewa nafasi akafanya kazi yake kwa kadiri ya uwezo wake na alifanya kazi nzuri na tunamheshimu.Mtazame Zitt Kabwe pamoja na mambo yake flani bado amejijengea heshima katika jamii kwa nafasi yake,Mtazame Lipumba,Mtazame,Maalim Seif Sharif Hamad,Watazame waislamu wengi mashuhuru wenye kuheshimika na useme ni wapi wamebaguliwa kwa sababu ya udini wao.
Kama mnataka kubebwa lazima kwanza mjibebe na muoneshe uwezo wenu ili hata anayejaribu kuwa bagua aone aibu.

Safari hii shura ya maimamu imewaacha bila nguo. Hizi takwimu huwa hampendi kuzitoa hata siku moja, unajua kwanini? Kwasababu yanayofanyika sikwasababu ya uwezo wa mtu bali ni kwa sababu ya dini yake. Na ndio maana hampendi kutoa takwimu hizo.

Hali ni mbaya zaidi huko katika ajira za serikali. Utashangaa ukiambiwa ni ni chini ya hiyo asilimia 20 kwa Tanzania nzima. Furahieni kwa kupiga kelele za vigezo, iko siku hivyo vigezo vitakuja tu na hiyo asilimia itapanda.

Matatizo yaliyopo ni zaidi ya vigezo upende usipende. Haiwezekani toka mwaka 1970 mpaka leo tatizo lishindwe kutatuliwa. Jiulize kwanini?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom