Uchaguzi 2020 Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania

Uchaguzi 2020 Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania

Status
Not open for further replies.
Jibu ni Rahisi,Ni kwa sababu ya watu wenye fikra kama hizi za kusema wanaonewa bila kuchukua hatua kubadili hali halisi.Somesheni watoto wenu,Jitangazeni watu wawajueni kwamba mnaweza,Onyesheni umahiri wenu katika kufanya mambo.Badala ya kutumia muda mwingi kutaka kubebwa wakati hata mkibebwa hambebeki wekezeni katika ilimu ya watoto wenu...
Ndio maana siutaki muungano
 
Walaka nimeusoma upo vzuri....ila naukosoa kwenye swala la udini nchi yetu haina dini ata moja ila watu wake ndio wenye dinii tuishie apo....

Ila vitu vingine vipo sawasawa
 
Mleta WARAKA Umeaibika.....
Mleta WARAKA Umetokota....

Sheikh wenu KUNDECHA amewavua nguo.........

Haya sasa wapi Kalamu na wenzake?!!!!

PINDIPO INAPOWAFIKIA HOJA ICHUNGUZENI KWANZA ILI MSIJE MKADHURU WASIO NA HATIA.
 
UDOM mkaamua mtoe waislam muweke wakristo! Hongereni nchi yenu hii wengine tupo kwa bahati mbaya
Hahaha, hivi are u serious on your comment?

Ukiambiwa uthibitishe hili utaweza? Hebu tuwekee ushahidi kamili hapa.

Daah,
 
Nikwambie kitu kimoja ambacho unatakiwa kukifahamu - (Tena umegusa kwenye shina; Elimu) suala la kuiandaa jamii ya kesho ni ya serikali. Hii ikiwa pamoja na elimu ambayo ndio dira ya kupata ajira. Ni ujinga baada ya miaka 60 ya uhuru tukaendelea kulia na makosa aliyoyafanya mkoloni, huku ni kukosa akili. Sasa tulidai uhuru ili iweje? Au unafikiri ili tuendeleze utaratibu ule ule wa mkoloni, tukibadili rangi tu ya mtawala.

Tena umetaja Mmakabila kama wachaga - Huwezi amini kuwa mkoa wa Kilimanjaro unashule nyingi za sekondari kuliko Dar es salaam ambapo uwiano wa wakazi wa mikoa hiyo hata haikaribiani. Tena shule nyingi zaidi zimejengwa baada ya uhuru na mkoloni mweusi. Usishangae kwani hii ndio sera ya serikali ikiwalipa walimu na kuendesha shule hizo kwa kodi za wananchi wote...
Swala la utakatifu wa Nyerere lisiwatie wehu.Hili tuwaachie watu na Imani yao.Kama alikuwa muumini wao wanayo haki ya kumtangaza mtakatifu kwa mujibu wa desturi zao au na hilo linakuuma?

Serikali ina wajibu kuwaandaa watu ili haiwezi poteza rasilimali kwa watu ambao hawajiongezi.Hao wachaga ukiwajengea shule wanaleta watoto wenyewe mpaka madarasa yanajaa na kufurika.Sehemu zingnie madarasa yanajengwa yanafugia popo.Si bora wawajengee wachaga?Je unafikiri hizo shule za wachaga wanasoma wachaga peke yao?Unaweza kwenda soma hata wewe ili uone duni inakokwenda.Maandalizi ya kuwabana waislamu ni matokeo ya tabia na silka za waislamu wengi.

Waislamu ni wanyonyaji sana.Ukifuatilia matajiri wengi wa kiislamu utagundua kuwa wanalipa wafanyakazi wao ujira mdogo sana kama vile ni watumwa.Ukifuatilia Matajiri wengi waislamu hawawekezi kwenye sekta ya ilimu hata kidgo .Kama serikali imeshindwa kuwapa fursa inuaneni ninyi wenyewe.Mbona kuna shule zinaendeshwa na waislamu ambazo ziko vizuri tu ila tatizo linarudi pale pale kwenye ubagyuz
Nilifikiri utajibu kwanini shule za sekondari Kilimanjaro ni nyingi kuliko Dar es salaam. Kwa vile umeshindwa kujibu hilo, nachukulia kuwa - meseji sent.

Pili. Elimu hii tunayoisoma leo darasani tumeletewa na wakoloni, hata hao unaosema wanapenda kwenda shule leo hawakupenda wakati huo inaletwa. Soma kitabu cha Ngugi wa Thiongo " The river between". Ninachotaka kusema ni kwamba hata hao unaosema hawapendi kwenda shule, ni jukumu la serikali kuwawekea utaratibu na mikakati ya kuijenga jamii hiyo kwa ajili ya kesho yao...
Mkuu,Naona nikujibu hivi,Si kweli kwamba shule ni nyingi kilimanjaro kwa sababu ya serikali au kwa sababu ya mkoloni hapana,shule ni nyingi kule kwa sababu kuna muamko wa elimu na watu ni wachapa kazi. Ukiwajengea shule wanaleta watoto wao kuja kusoma.Huku unakodai wamebaguliwa ni kwamba wengi walikuwa ni wavivu tangu enzi za mkoloni na hivyo wakoloni hawakuona namna ya kuwasaidia.Hata shule chache zilizoko huko kwenu bada hampeleki watoto wenu na zinasommwa na wachaga na hao mnaowachukia.

Kuweni na wivu wa maendeleo.Pelekeni watoto shule na muwasimamie wasome kwa bidii.Tusikike kwamba wanafunzi wamekataliwa shule kwa sababu shule zimejaa sio mlalamike tu kwamba shule zimejaa kule huku hakuna.Shule sio mabanda ya kufugia popo ni sehemu ya watu kupata maarifa,.Sasa kama nyie mnataka kuoaza mabinti zenu wakiwa wadogo na kukaa kwenye vijiwe vya kahawa halafu mnasubiri mpewe nafasi za uongozi mtasubiri sana.Chukueni hatua stahiki acheni kulalamika na kulaumu
 
Ma abdool sijui wakoje.
hivi kwenye sifa za kazi kipengele cha dini huwa kipo?
Ukienda kwneye mkampuni yao hicho ni kigezo.Kuna vijana wengi sana nawafahamu wakristo ambao wanatumia majina ya kiislamu ili tu wapate kazi katika makampuni ya waislamu na ambako bado wananyonywa sana.
 
Titi...
Tutafanyaje inapokuwa waumini wa dini moja tu ndiyo wanakuwa na sifa za elimu, uxoefu, uadilifu, uchapakazi nk. kwa hiyo ndiyo wanaoongoza serikali na wengine wako nje?

Katika hali kama hii tunafanyaje?
Tatizo liko kwenu hapo hapo, hata elimu wengi mmeweka mkazo kwenye elimu ya dini, kwenye elimu nyingine mmo lakini kwa kawaida sana.

Ukweli msioutaka ni mmoja tu, mambo ya siasa yaachwe yashughulikiwe na asasi za kisiasa, hamuelewi kila siku mtabaki kusema wengine wanapendelewa kumbe hakuna lolote.

Hata kama ni asilimia, hao waislamu ni asilimia ngapi kulinganisha na wengine? Sasa unategemea walingane vipi kwenye vitu kama uteuzi na watu wa dini nyingine?
 
Bila shaka yoyote, hivyo ndivyo vigezo halisi kabisa.
Vigezo hivyo pia vinaanzia chini kabisa, kuhakikisha kwamba mTanzania yeyote anapewa fursa sawa ya kuinua maisha yake bila upendeleo unaohusiana na ukabila, udini au uchochote, hii inaanzia katika huduma za elimu katika maeneo yote nchini.
Kalamu...
Ulichosema ni kweli kabisa.

Lakini teuzi lazima zichukuliwe kwa tahadhari hasa katika maeneo ya dini na kabila.

Serikali ikijaza watu dini moja au kabila moja kwa kigezo kuwa hawa wana sifa zinazohitajika basi ijue inajenga matabaka na fitna kubwa na inajipalia makala.

Ikiwa hali ni hii hapa Tanzania au kwengineko basi jua kuna tatizo nchini na hiyo ni saratani mwishowe inaua.

Haiwezekani kuwa sifa ziwe kwa watu wa dini moja au kabila moja tu.

Bahati mbaya ninaposoma michango hapa jamvini hujiuliza kwa nini hawa wachangiaji wanashindwa kufanya uchambuzi na kuona tatizo?

Hili ni tatizo la vyuo vyetu au nini?
 
Nilifikiri utajibu kwanini shule za sekondari Kilimanjaro ni nyingi kuliko Dar es salaam. Kwa vile umeshindwa kujibu hilo, nachukulia kuwa - meseji sent.

Pili. Elimu hii tunayoisoma leo darasani tumeletewa na wakoloni, hata hao unaosema wanapenda kwenda shule leo hawakupenda wakati huo inaletwa. Soma kitabu cha Ngugi wa Thiongo " The river between". Ninachotaka kusema ni kwamba hata hao unaosema hawapendi kwenda shule, ni jukumu la serikali kuwawekea utaratibu na mikakati ya kuijenga jamii hiyo kwa ajili ya kesho yao.

Wakoloni walifanya hivyo kwa wachaga, wanyakyusa, wahaya nk. ni zamu ya serikali kuwa na utaratibu wa kuwainua huko ambako mkoloni hakufika au hakukuwekea utaratibu. Kama serikali iliendelea kule kule ambako mkoloni alikutengeneza, basi huo ni udhaifu mkubwa wa serikali iliyoongoza kwa miaka 60. Na ndio maana ni vigumu kujivunia uhuru wetu. Na ndio maana matabaka bado yanaendelea. Na ndio maana wahanga wataendelea kulalamika.
Usisingizie serikali kuhusu suala la waislamu kutokusoma au kuwa na wasomi wachache. Tangu serikali ya awamu ya kwanza jitihada zilifanyika za kuhakikisha kwamba watoto wengi kama si wote wa Tanzania wanapata elimu ndio maana serikali ilitaifisha shule za dini za kikristo kuwa za serikali ili kuondoa kikwazo cha watoto wa kiislamu na hata wasiokuwa na dini kutopata nafasi ya kusoma maana serikali kwa wakati huo ilikuwa imerithi shule chache tu kutoka serikali ya mkoloni na uwezo wa kujenga shule mpya za kutosha ulikuwa ni mdogo sana.

Serikali iliondoa ada kuanzia elimu ya msingi hadi chuo kikuu kwa lengo la kuhakikisha kwamba watoto wa watanzania wote wanapata nafasi ya kusoma mpaka chuo kikuu au vyuo vingine vya kati.

Pia serikali kuna kipindi ilianzisha utaratibu wa kushusha pass mark (alama za ufaulu) kwa wanafunzi wa shule za msingi hasa maeneo au mikoa ambayo haikuwa na mwamko mkubwa wa elimu (ikiwemo na mikoa ambayo ina idadi kubwa ya waislamu) ili kuchochea wanafunzi wengi kutoka maeneo hayo waeze kujiunga na elimu ya sekondari.

Na mengine kadha wa kadha serikali imefanya kuhakikisha inatoa fursa kwa kila mtanzania bila ubaguzi. Hivi hizi shule za kikristo zilizotaifishwa na serikali kama zingekuwa ni za kiislamu nadhani makelele yangekuwa mengi hadi leo kulalamikia uamuzi huo.
 
Kalamu...
Ulichosema ni kweli kabisa.

Lakini teuzi lazima zichukuliwe kwa tahadhari hasa katika maeneo ya dini na kabila.

Serikali ikijaza watu dini moja au kabila moja kwa kigezo kuwa hawa wana sifa zinazohitajika basi ijue inajenga matabaka na fitna kubwa na inajipalia makala.

Ikiwa hali ni hii hapa Tanzania au kwengineko basi jua kuna tatizo nchini na hiyo ni saratani mwishowe inaua.

Haiwezekani kuwa sifa ziwe kwa watu wa dini moja au kabila moja tu.

Bahati mbaya ninaposoma michango hapa jamvini hujiuliza kwa nini hawa wachangiaji wanashindwa kufanya uchambuzi na kuona tatizo?

Hili ni tatizo la vyuo vyetu au nini?
Uamini wangu katika kuyaandika hayo niliyoandika ni kwamba 'mteuzi' ni mtu mwenye uelewa na busara za kutosha kuweza kuona kwamba nchi yetu si ya kabila/dini moja na sifa nyingi nyingine.

Kwa hiyo ni wajibu wake kufanya uteuzi huo kwa uangalifu mkubwa, ikiwa ni pamoja na kuweka maanani tofauti hizo zilizoko kwenye jamii yetu. Lakini hii ndiyo isiwe msukumo wa juu kabisa anaouangalia katika uteuzi wake.

Kigezo cha uteuzi kikiwa ni kuangalia kabila au dini kwanza mbele ya yote, nina hakika hii itakuwa na tatizo.

Hapa tulipofikia kama taifa, uamini wangu ni kwamba haiwezekani kupatikana watu wenye vigezo mbalimbali vinavyohitajika katika kundi lolote la kabila/dini au tabaka lingine lolote ndani ya jamii zetu.
 
Hata kama shule ni moja tu.Inatosha kuleta mabadiliko kama ikitumika vizuri.Jaribu kufuatilia kwa karibu.Utaona kabisa kuna desturi kwa waislamu wengi kutohimiza ilimu kwa watoto wao,hasa wa kipato cha chini.Ukifuatilia zaidi utaona kuwa waislam wengi hutoa hadi majengo ya nyumba zao kuwa madrasa ya kufundisha elimu ya dini lakini hata kuwafundisha watoto elimu ya kawaida hakuna..

Andoza,
Inaelekea hujui historia ya Waislam na elimu.

Unadhani kuwa Waislam walipuuza elimu ndiyo maana leo wako hivi.

Kitu kimoja ambacho mimi nimekushindeni ni kuwa mimi nimetafiti historia ya Waislam kwa ujumla wake kuanzia kwa nini walikuwa mstari wa mbele kupambana na ukoloni na ilikuwaje baada ya uhuru Waislam wakawa tena katika mapambano na Julius Nyerere mtu waliyempokea na kumfikisha pale alipofika.

Nadhani haya mnasoma kila siku katika makala zangu.

Sababu ya Nyerere kuivunja EAMWS na kuunda BAKWATA ni kuwa EAMWS ilikuwa inajenga Chuo Kikuu na ilikuwa inajenga shule za msingi na sekondari majimboni kote Tanganyika baada ya kupitisha azimio la kushughulika na elimu lililopitishwa na Muslim Congress mwaka wa 1962 baada ya uhuru tu kupatikana.

Waislam hawakutakiwa waelimike walitakiwa wabaki katika hali ile ile waliyokuwanayo katika ukoloni.

Inaaminika pia Kanisa Katoliki lilikuwa nyuma ya njama hizi.

Haya yote nimeyaeleza katika kitabu cha Abdul Sykes na hii pia ndiyo sababu za kufanyika juhudi za kufuta historia ya Waislam katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Mkakati ukawa kuwazuia vijana wa Kiislam kupata elimu na Wizara ya Elimu imehusika sana katika hujuma hii.

Prof. Malima alipokuwa Muislam wa kwanza kuwa waziri katika wizara hii alikutana na mengi na aliitahadharisha serikali kuhusu hatari hii na hiki ndicho kikawa kisa cha Prof. Malima kuchukiwa na kupendwa na Waislam.

Sina haja ya kueleza hujuma za Baraza la Mitihani kwa shule za Kiislam.

Sheikh Ponda aliongoza maandamano yasiyo na kibali licha ya vitisho vilivyotolewa na polisi kufikisha ujumbe serikalini kuwa Waislam wanahujumiwa katika elimu.

Unaweza ukajiuliza tena kwa nini Sheikh Ponda kwa nini si BAKWATA.

Ikiwa unataka kuyajua haya soma kitabu cha Abdul Sykes (1998), kitabu cha Prof. Hamza Njozi, ''Mwembechai Killings....'' (2000), lakini hiki kimepigwa marufuku.

Vinginevyo bila kujua historia ya kweli itakuwa tabu kwako leo kuelewa imekuwaje Shura ya Maimamu wanazungumza jambo zito la dhulma dhidi ya Waislam na BAKWATA iko kimya na kwa nini kwa miaka yote hiyo serikali imekuwa kimya katika tatizo hili la elimu kama Waislam wanavyolalamika.

Nahitimisha kwa kueleza hatari ya jambo hili la Waislam kudhulumiwa katika elimu.

Baada ya yaliyokuwa yanafanyika Baraza la Mitihani kufahamika na serikali ilipopata taarifa kuwa Waislam wataandamana kwa kudhulumiwa katika elimu ikatoa onyo kali.

Ilikuwa siku ya Ijumaa Msikiti wa Kichangani.

Baada ya sala Sheikh Ponda akasimama kuwahutubia Waislam waliojaa msikitini akaeleza kwa kutoa ushahidi kuhusu hii dhulma ya elimu.

Nje ya msikiti yalitanda magari ya polisi na helicopter zikizunguka juu.

Ndani ya msikiti walikuwapo makachero wengi na nje kwa ndani ya uzio wa msikiti.

''Ndugu zangu Waislam kama hatukuandamana kwa hili nini Waislam tufanyiwe ili tuandamane?

Mimi nitaongoza maandamano haya na nitakuwa mstari wa mbele...''

Sheikh Ponda alipomaliza kusema maneno haya aligeuka akawapa mgongo wale aliokuwa akiwahutubia akaelekea kibla akanyanyua mikono yake kuomba dua kumtaka Allah msaada.

Mimi nilikuwa chini nyuma yake na tape recorder yangu na camera nikirekodi na kupiga picha.

Hii picha niliyoweka hapa ni katika picha zangu ninazozipenda sana kupita kiasi.

''Tension,'' niliyoshuhudia ndani ya msikiti ilikuwa ya kutisha na nikasema ndani ya nafsi yangu kuwa ikiwa serikali hii itakuwa na ujinga ikaamuru askari wake wawashambulie Waislam kwa kukataa kudhulumiwa katika elimu basi leo damu itamwagika.

Maandamano yalipofika Jangwani zikaja taarifa kuwa Waislam wanaombwa waandamane kwa amani waelekee Kidongo Chekundu na pale viongozi wao watachukuliwa hadi Wizara ya Mambo ya Nje na waraka wao kwa serikali utapokelewa pale na Waislam wabakie pale hadi viongozi wao watakaporejeshwa Kidongo Chekunde na viongozi wao ndiyo watatoa amri ya Waislam kutawanyika.

Baadhi ya paper kuhusu Waislam na Elimu:

1. Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).

2. The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).

3. Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).

4. Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).
 

Attachments

  • PONDA AKIOMBA DUA MTAMBANI MAANDAMANO YA NDALICHAKO.JPG
    PONDA AKIOMBA DUA MTAMBANI MAANDAMANO YA NDALICHAKO.JPG
    16.1 KB · Views: 1
Andoza,
Inaelekea hujui historia ya Waislam na elimu.
Unadhani kuwa Waislam walipuuza elimu ndiyo maana leo wako hivi...
Kama story ya kijiweni vile. Haingii akilini. Kwa hiyo baada ya hapo waislamu wakasusa kupeleka watoto wao shule za serikali? Au Nyerere aliwakataza pia?
 
Inaelekea hujui historia ya Waislam na elimu.
Unadhani kuwa Waislam walipuuza elimu ndiyo maana leo wako hivi.
Taifa haliwezi kuwa mateka wa historia miaka sitini na kuendelea.

Historia unayoiweka mbele kama kinga, hata kama ingekuwa na ukweli ndani yake, ingekuwa ni kukosa weledi kwa taifa kuendelea kushikilia historia hiyo hiyo miaka yote hii.

Hii historia potofu unayoitumia kujenga ufarakano ndani ya jamii yetu haisaidii kuondoa hayo unayolalamikia; na badala yake unachochea tu mifarakano hiyo na kuzidi kuweka matabaka badala ya kuyaondoa.
 
Hahaha, hivi are u serious on your comment?

Ukiambiwa uthibitishe hili utaweza? Hebu tuwekee ushahidi kamili hapa.

Daah,
Walitolewa waislam 11 na msikiti kuvunjwa, hivi umelisoma bandiko tunalolijadili kweli?
 
Kwani kwa silimia idadi ya qaislam ni ngapu na wakristo ni ngapi kwa Tanzania.
Tua zie hapo
Usaili kuingia shule la kwanza ni ngapi? Sekondari ni ngapi na chuo

Uliyekuwa unaandika ulikuw umevaa Barakoa? Tuishie hapo
 
Umeisoma lakini, au unafikia hitmisho hilo kwa vile imeletwa na watu wa dini?

Mimi nakushauri uisome. Nimeisoma karibu yote. Kuna baadhi nisiyokubaliana nayo, lakini sikuona "udini".

Wewe huo udini umeusoma wapi? Jaribu basi kuweka mfano wa udini uliouona wewe.
Kwahiyo ilikuwa na uongo na ukweli
Sio? Basi ni ya kishetani maana ndiye huchanganya ukweli na uongo
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom