Uchaguzi 2020 Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania

Uchaguzi 2020 Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania

Status
Not open for further replies.
Kama story ya kijiweni vile. Haingii akilini.
Kwa hiyo baada ya hapo waislamu wakasusa kupeleka watoto wao shule za serikali? Au Nyerere aliwakataza pia?

Inaelekea mwenzetu bado mchanga sana wa historia ya Tanzania kwa waislam na elimu, BAKWATA na EAMWS. Sijui kama hata unaelewa kirefu cha EAMWS.

Ila ninachokushari usiwe mvivu wa kusoma vitabu, kakisome kwanza kitabu cha Abdul Sykes (1998). Hiki kitabu kitakupa picha nzuri sana na kuelewa kwanini Nyerere alifanyiwa mpango wa kuwa Saint na kanisa katoliki.
 
Taifa haliwezi kuwa mateka wa historia miaka sitini na kuendelea.

Historia unayoiweka mbele kama kinga, hata kama ingekuwa na ukweli ndani yake, ingekuwa ni kukosa weledi kwa taifa kuendelea kushikilia historia hiyo hiyo miaka yote hii.

Hii historia potofu unayoitumia kujenga ufarakano ndani ya jamii yetu haisaidii kuondoa hayo unayolalamikia; na badala yake unachochea tu mifarakano hiyo na kuzidi kuweka matabaka badala ya kuyaondoa.

Walioleta mifarakano ni hao watawala waliopanga mipango mibovu ya ugawanyaji wa madaraka. Kama wao walikuwa wanalifikiria hilo wangekuwa tayari kutafuta suluhu.

Wewe na hao watawala mpo chungu kimoja. Msipoyaona haya mtaiingiza nchi matatani.
 
Walioleta mifarakano ni hao watawala waliopanga mipango mibovu ya ugawanyaji wa madaraka. Kama wao walikuwa wanalifikiria hilo wangekuwa tayari kutafuta suluhu.

Wewe na hao watawala mpo chungu kimoja. Msipoyaona haya mtaiingiza nchi matatani.
Hebu nieleze ni watawala gani unaowazungumzia hapa, maanake sikuelewi.

Katika haya uliyoandika hapa, nakuona wewe huna ufahamu wowote mbali ya kuimba tu unayolishwa.
 
Andoza,
Inaelekea hujui historia ya Waislam na elimu.

Unadhani kuwa Waislam walipuuza elimu ndiyo maana leo wako hivi.

Kitu kimoja ambacho mimi nimekushindeni ni kuwa mimi nimetafiti historia ya Waislam kwa ujumla wake kuanzia kwa nini walikuwa mstari wa mbele kupambana na ukoloni na ilikuwaje baada ya uhuru Waislam wakawa tena katika mapambano na Julius Nyerere mtu waliyempokea na kumfikisha pale alipofika.

Nadhani haya mnasoma kila siku katika makala zangu.

Sababu ya Nyerere kuivunja EAMWS na kuunda BAKWATA ni kuwa EAMWS ilikuwa inajenga Chuo Kikuu na ilikuwa inajenga shule za msingi na sekondari majimboni kote Tanganyika baada ya kupitisha azimio la kushughulika na elimu lililopitishwa na Muslim Congress mwaka wa 1962 baada ya uhuru tu kupatikana.

Waislam hawakutakiwa waelimike walitakiwa wabaki katika hali ile ile waliyokuwanayo katika ukoloni.

Inaaminika pia Kanisa Katoliki lilikuwa nyuma ya njama hizi.

Haya yote nimeyaeleza katika kitabu cha Abdul Sykes na hii pia ndiyo sababu za kufanyika juhudi za kufuta historia ya Waislam katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Mkakati ukawa kuwazuia vijana wa Kiislam kupata elimu na Wizara ya Elimu imehusika sana katika hujuma hii.

Prof. Malima alipokuwa Muislam wa kwanza kuwa waziri katika wizara hii alikutana na mengi na aliitahadharisha serikali kuhusu hatari hii na hiki ndicho kikawa kisa cha Prof. Malima kuchukiwa na kupendwa na Waislam.

Sina haja ya kueleza hujuma za Baraza la Mitihani kwa shule za Kiislam.

Sheikh Ponda aliongoza maandamano yasiyo na kibali licha ya vitisho vilivyotolewa na polisi kufikisha ujumbe serikalini kuwa Waislam wanahujumiwa katika elimu.

Unaweza ukajiuliza tena kwa nini Sheikh Ponda kwa nini si BAKWATA.

Ikiwa unataka kuyajua haya soma kitabu cha Abdul Sykes (1998), kitabu cha Prof. Hamza Njozi, ''Mwembechai Killings....'' (2000), lakini hiki kimepigwa marufuku.

Vinginevyo bila kujua historia ya kweli itakuwa tabu kwako leo kuelewa imekuwaje Shura ya Maimamu wanazungumza jambo zito la dhulma dhidi ya Waislam na BAKWATA iko kimya na kwa nini kwa miaka yote hiyo serikali imekuwa kimya katika tatizo hili la elimu kama Waislam wanavyolalamika.

Nahitimisha kwa kueleza hatari ya jambo hili la Waislam kudhulumiwa katika elimu.

Baada ya yaliyokuwa yanafanyika Baraza la Mitihani kufahamika na serikali ilipopata taarifa kuwa Waislam wataandamana kwa kudhulumiwa katika elimu ikatoa onyo kali.

Ilikuwa siku ya Ijumaa Msikiti wa Kichangani.

Baada ya sala Sheikh Ponda akasimama kuwahutubia Waislam waliojaa msikitini akaeleza kwa kutoa ushahidi kuhusu hii dhulma ya elimu.

Nje ya msikiti yalitanda magari ya polisi na helicopter zikizunguka juu.

Ndani ya msikiti walikuwapo makachero wengi na nje kwa ndani ya uzio wa msikiti.

''Ndugu zangu Waislam kama hatukuandamana kwa hili nini Waislam tufanyiwe ili tuandamane?

Mimi nitaongoza maandamano haya na nitakuwa mstari wa mbele...''

Sheikh Ponda alipomaliza kusema maneno haya aligeuka akawapa mgongo wale aliokuwa akiwahutubia akaelekea kibla akanyanyua mikono yake kuomba dua kumtaka Allah msaada.

Mimi nilikuwa chini nyuma yake na tape recorder yangu na camera nikirekodi na kupiga picha.

Hii picha niliyoweka hapa ni katika picha zangu ninazozipenda sana kupita kiasi.

''Tension,'' niliyoshuhudia ndani ya msikiti ilikuwa ya kutisha na nikasema ndani ya nafsi yangu kuwa ikiwa serikali hii itakuwa na ujinga ikaamuru askari wake wawashambulie Waislam kwa kukataa kudhulumiwa katika elimu basi leo damu itamwagika.

Maandamano yalipofika Jangwani zikaja taarifa kuwa Waislam wanaombwa waandamane kwa amani waelekee Kidongo Chekundu na pale viongozi wao watachukuliwa hadi Wizara ya Mambo ya Nje na waraka wao kwa serikali utapokelewa pale na Waislam wabakie pale hadi viongozi wao watakaporejeshwa Kidongo Chekunde na viongozi wao ndiyo watatoa amri ya Waislam kutawanyika.
Mzee wangu Mohamed Said,Nakubaliana na wewe kwamba mimi sio msomi wa Historia ya Waislam na huwa naheshimu sana jitihada zako za kutaka kuweka sawa historia ya nchi yetu mintarafu nafasi ya "Uislam" Sitaki kusema kwamba kuna ukweli au hamna ukweli katika maelezo yako na ya wengine ila nataka mimi na wewe tukubaliane kwamba Islamic radicalization ni tatizo hata ndani ya uislamu wenyewe.

Na hili ndilo tatizo kubwa linalokabili jamii nyingi duniani za kiislam yaani Religious extremism.

Pili mimi na wewetukubaliane kwamba wasomi wengi wa kiislamu hawautendei haki uislamu hasa katika eneo la kuhamasisha dhidi radical sentiments ndani ya uislam.Adui mkubwa wa uislamu na waislamu wenyewe kwa kushindwa kutenganisha harakati za kidini,harakati za kisiasa na harakati za kimaisha.Lazima tukubali kwamba zama zimebadilika na utamaduni wetu lazima ubadilika.

Hebu tutafakari kwa pamoja ni kwa nini nyerere alikosana na wale waislam waliompokea Dar es Salama?Je aliuchukia uislamu au kulianza kuibuka kwa radical sentiments na Nyerere hakuwa Tayari kuruhusu hilo litokee kwamaslahi makubwa ya taifa?Najua unaweza usikubali lakini maandiko yako yanaonesha kabisa kwamba hicho ndio chanzo."Nyerere alihofia radical sentiments ndani ya uislamu na akachukua hatua kudhibiti"Binafsi nafikiri ulikuwa uamuzi sahihi kwa kuzingatia mazingira.

Mzee wangu wewe umebahatika kupata ilimu kidogo ya kutosha,nafikiri kwa kiwango chako cha elimu tunaweza kusema ulikutana na mengi katika safari yako ili sidhani katika yote uliwahi kunyimwa elimu kwa sababu ya dini yako.Naamini kabisa ungebaguliwa wakati ukitauta elimu yako usingekuwa hapa ulipo.Nina hakika uliweka jitihada ndio maana uko hapa leo.Na hata maanikio yako uliyo nayo katika taaluma yako ni matokeo ya jitihada zako na bahati kidogo.

Jaribu kufikiri wakristu uliosoma nao tangu msingi na waislamu uliosoma nao halafu uangalie kwa kina kabisa kama kuna sehemu wakristo walibebwa zaidi ya waislamu(Achilia mbali zile personal connection ambazo ni kawaida katika maisha)Nazungumzia nyakati ambazo yupo muislam na mkristu wenye vigezo vyote sawa na mwislamu akaachwa mkristu akachukuliwa.Kama hayo matukio yapo ni machache sana kuweza kuwa kielelezo cha ubaguzi.

Ambianeni ukweli kwamba lazima muweke jitihada ya kupatia wanenu hamasa pamoja na elimu ya kutosha.Haitoshi tu kuwa mazamifu katika elimu akhera,elimu dunia pia ina nafasi yake.

Religious extremism ni tatizo sio tu kwa waislam bali kwa dini zote.Yote kwa yote Tanzania hatuna kiwango cha ubaguzi wa dini kama mnavyotaka kutuaminisha ingawa kuna weza kuwa na changamoto hapa na pale lakini haziwezi kufika kiwango cha kuitwa ubaguzi wa kidini tena "Systemic"
 
Mzee wangu Mohamed Said,Nakubaliana na wewe kwamba mimi sio msomi wa Historia ya Waislam na huwa naheshimu sana jitihada zako za kutaka kuweka sawa historia ya nchi yetu mintarafu nafasi ya "Uislam" Sitaki kusema kwamba kuna ukweli au hamna ukweli katika maelezo yako na ya wengine ila nataka mimi na wewe tukubaliane kwamba Islamic radicalization ni tatizo hata ndani ya uislamu wenyewe...
Ondoza,
Wanaotakiwa kujibu haya ni serikali si wewe kwani uhusiki.

Mimi si mtu wa kubishana huingia pale ninapoona kuna watu hawaujui ukweli.

Shura ya Maimamu imetoa waraka tuwe na subira.
 
Hunijui...
Subira waliokusudiwa watakuja na majibu.

Ama kuhusu wasio na dini utapata shida kuwafananisha na Waislam.

Soma historia jinsi Waislam walivyopigania uhuru wa Tanganyika kuondoa ukoloni ili pawe na haki na usawa kisha watafute hao wasiokuwa na dini uangalie walikuwa wapi.

Tanganyika haikuwa na kundi hilo si katika Vita Vya Maji Maji wala katika TAA/TANU.

Hivyo hivyo hii leo kundi hilo halipo.
mbona kwenye quran haijaandikwa kwamba waislam ndo walipigania uhuru wa tz?? quran yenyewe inakukana, hizi dini ni chanzo cha watu wengi kwenda motoni
 
MUONGOZO WA SHURA YA MAIMAMU TANZANIA UCHAGUZI MKUU WA TAIFA OKTOBA 2020

Shura ya Maimamu wa Tanzania imetoa waraka unaohusu Uchaguzi Mkuu.

Katika waraka huu au muongozo huu kuna mengi ya kufikirisha sana kiasi mtu atajiuliza haya yanawezekana vipi kutendeka katika nchi inayojinadi kuwa inazingatia haki na usawa kwa wananchi wake wote na inapiga vita ubaguzi wa aina yoyote..
Duh!!Hatari sana hii!!
 
Ondoza,
Wanaotakiwa kujibu haya ni serikali si wewe kwani uhusiki.

Mimi si mtu wa kubishana huingia pale ninapoona kuna watu hawaujui ukweli.

Shura ya Maimamu imetoa waraka tuwe na subira.
Hapana, sio kubishana,Waraka umeshawekwa mbele ya umma,nimependa maudhui yote ya waraka huu isipokuwa msingi wake tu wa kwamba hao walotendewa au yanayotendwa ni ya kuwalenga waislamu kwa sababu ya uislamu wao.Hapana sidhani ni sahihi kuliweka swala hili kwa namna hio.

Kama utaratibu ulikiukwa basi tudai haki kwa msingi wa haki bila kujificha nyuma ya mwamvuli wa dini kukataa kukubali kwamba hata sisi tuna makosa fulani au mapungufu.

Hakuna mja asiye na mapungufu.Serikali itajibu kwa namna yake ya kawaida ila halitamaliza mjadala kuhusu tabia hii isiyo njema ya kujificha nyuma ya mwamvuli wa udini pale tunapokiuka taratibu za nchi katika utendaji au tunaposhindwa kutimiza wajibu wetu wa kiraia
 
Soma kwanza kwa furaha wacha jaziba
Gavana eee shaykh Kundecha kawaumbua na UONGO WENU...
Waongo Kama TUMBA MBICHI....

Haya Sasa Mambo ngw'enyuu halitaki HATA tochi....

WARAKA ule feki......
WARAKA ule Koko....
WARAKA ule haujapitia kwa masheikh wenu aaaagh "innal baatwila kana Zahuka"

Kul ul Haq Lau Kanna mura,rudini kumheshimu na kumtii kiongozi wetu wa kiroho na kiimani Tanzania kwa BARAZA letu mtambuka BAKWATA, Ashaykh ul Muadhama Mufti Zubeir Bin Ally.

Ametusisitizia Mara elfu KIDOGO;


1.TUJITAMBUE
2.TUBADILIKE
3.TUACHE MAZOEA
 
Walitolewa waislam 11 na msikiti kuvunjwa, hivi umelisoma bandiko tunalolijadili kweli?
Nimelisoma vizuri sana, kuandikwa na kithibitisha ni vitu viwili tofauti, Mtu anaweza kuandika chochote

Hebu nitajie hao Wakristo waliohusika kuvunja msikiti.
 
Inaelekea mwenzetu bado mchanga sana wa historia ya Tanzania kwa waislam na elimu, BAKWATA na EAMWS. Sijui kama hata unaelewa kirefu cha EAMWS.

Ila ninachokushari usiwe mvivu wa kusoma vitabu, kakisome kwanza kitabu cha Abdul Sykes (1998). Hiki kitabu kitakupa picha nzuri sana na kuelewa kwanini Nyerere alifanyiwa mpango wa kuwa Saint na kanisa katoliki.
Wewe .hivyo vitabu tulishavosoma tangu 2010 kariakoo. Kumbe vitabu vya MS ndio unavyovijua tu vinavyoongelea Uhuru wa Tanganyika? Poor you

East African Muslim Welfare Society ya kuanzia 1945 kiuhalisia haikuuliwa na Nyerere na wala Vatican haikuweka mkono, tatizo ilikuwa Management. Mbona hata baada ya kucolapse 1968 kule Uganda ikasurvive?

Mbona Uislam ukaspread zaidi Rwanda?

Mbona ni Mombasa tu na Bongo ndio tatizo likaendelea? Nyerere alikuwa na influence gani Mombasa?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom