Uchaguzi 2020 Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania

Uchaguzi 2020 Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania

Status
Not open for further replies.
Mnabebwa na mfumo hamna haja ya kulialia.

Kulialia waachie wale ambao kwa makusudi kabisa wananyimwa fursa sababu ya dini yao hata kama wana vigezo

Bongo ukiwa mkiristu ukaomba kazi na muislamu na nyote mna vigezo sawa, probability ya Mkiristu kupata kazi ni kubwa kuliko huyo muislamu kwa sababu mfumo uko biased in favor ya Wakiristo. Huhitaji kuwa na PhD kuliona hili.
Hahaha, hatapata kazi kwasababu ya Ukristo wake ila atapata kwasababu ya sifa zake.

Kuna mahali penye ubaguzi kama kwenye makampuni ya AZAM? kuanzia kule factories

Halafu bado nakusubiri unithibitishie lile ulilosema pale juu sheikh.
 
Wewe hujui hata unachokiandika, Mimi sijalalamika nimekuuliza maswali nikakupa facts.

Hakuna Wakristo wenye muda wa kulialia au kuandamana, huwa wanaungana na kutafuta solution ya mambo yao kimantiki.

Hatutegemei kubebwa, sio kimadaraka au kielimu

That's it.
Thubutu eti wakristo hawabebwi nchi hii, facts eti nssf iligeuzwa msikiti una uthibitisho wa hilo au hearsay tu? Nimekwambie kitu kule kwenye elimu mlifungua kigango kabisa na prof kighoma malima akaanza kuwaumbua, yule mama tulimueleza ukweli akawa anabisha ila alivyokuja kukamatwa live akasingizia ni kompyuta sio yeye
 
Tatizo lipo kwenye udini ambako wameshindwa kuficha maslahi yao...
Aidha waraka wao pia bado ni mwendelezo wa dhana ya kusubiria serikali itende au iamue kwa maslahi ya wananchi (top down). Hii dhana ni potofu sana...
Wewe umeona kwa jicho hilo ila mimi nimeona kwa jicho tofauti hasa kwenye aina ya uongozi ninaopaswa kuupigania
 
Thubutu eti wakristo hawabebwi nchi hii, facts eti nssf iligeuzwa msikiti una uthibitisho wa hilo au hearsay tu? Nimekwambie kitu kule kwenye elimu mlifungua kigango kabisa na prof kighoma malima akaanza kuwaumbua, yule mama tulimueleza ukweli akawa anabisha ila alivyokuja kukamatwa live akasingizia ni kompyuta sio yeye
Huko kulialia hamkuanza Leo

Halafu hata katika waraka huu bado mnalia na kutaka kusaidiwa wala sio kuonesha lengo la ninyi kama Waislam kufanya jambo flani

Hata huu muda wa kulia humu ni bora mngeenda kujadili namna ya kuinua shule zenu na ufaulu sheikh,
 
Thubutu eti wakristo hawabebwi nchi hii, facts eti nssf iligeuzwa msikiti una uthibitisho wa hilo au hearsay tu? Nimekwambie kitu kule kwenye elimu mlifungua kigango kabisa na prof kighoma malima akaanza kuwaumbua, yule mama tulimueleza ukweli akawa anabisha ila alivyokuja kukamatwa live akasingizia ni kompyuta sio yeye
Mnataka mtafuniwe na kumezeshwa kabisa yakhee?
 
Hao hawatusemei waislamu wote.....hao Wala hawatambuliki KISHERIA kutusemea....

Muislam Mimi SIYATAKI HAYO WAYASEMAYO.....
Muislam mimi na wenzangu tulio wengi tunataka kuiona tume HIIHII iendelee kwani iko KISHERIA na haina dosari zozote.......

Waislam tunasemewa na BARAZA letu kuu BAKWATA......

WENGINE WANAKUWAGA WALE WACHOCHEZI WACHACHE.
Jumbe Brown,

Inaelekea hujui historia ya Waislam na elimu.

Unadhani kuwa Waislam walipuuza elimu ndiyo maana leo wako hivi.

Kitu kimoja ambacho mimi nimekushindeni ni kuwa mimi nimetafiti historia ya Waislam kwa ujumla wake kuanzia kwa nini walikuwa mstari wa mbele kupambana na ukoloni na ilikuwaje baada ya uhuru Waislam wakawa tena katika mapambano na Julius Nyerere mtu waliyempokea na kumfikisha pale alipofika.

Nadhani haya mnasoma kila siku katika makala zangu.

Sababu ya Nyerere kuivunja EAMWS na kuunda BAKWATA ni kuwa EAMWS ilikuwa inajenga Chuo Kikuu na ilikuwa inajenga shule za msingi na sekondari majimboni kote Tanganyika baada ya kupitisha azimio la kushughulika na elimu lililopitishwa na Muslim Congress mwaka wa 1962 baada ya uhuru tu kupatikana.
Kinara wa haya yote alikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na taasisi yake Daawat Islamiyya fi Tanganyika (Wito kwa Waislam wa Tanganyika).

Waislam hawakutakiwa waelimike walitakiwa wabaki katika hali ile ile waliyokuwanayo katika ukoloni.

Inaaminika pia Kanisa Katoliki lilikuwa nyuma ya njama hizi.

Haya yote nimeyaeleza katika kitabu cha Abdul Sykes na hii pia ndiyo sababu za kufanyika juhudi za kufuta historia ya Waislam katika TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Mkakati ukawa kuwazuia vijana wa Kiislam kupata elimu na Wizara ya Elimu imehusika sana katika hujuma hii.

Prof. Malima alipokuwa Muislam wa kwanza kuwa waziri katika wizara hii alikutana na mengi na aliitahadharisha serikali kuhusu hatari hii na hiki ndicho kikawa kisa cha Prof. Malima kuchukiwa na kupendwa na Waislam.

Sina haja ya kueleza hujuma za Baraza la Mitihani kwa shule za Kiislam.

Sheikh Ponda aliongoza maandamano yasiyo na kibali licha ya vitisho vilivyotolewa na polisi kufikisha ujumbe serikalini kuwa Waislam wanahujumiwa katika elimu.

Unaweza ukajiuliza tena kwa nini Sheikh Ponda kwa nini si BAKWATA.

Ikiwa unataka kuyajua haya soma kitabu cha Abdul Sykes (1998), kitabu cha Prof. Hamza Njozi, ''Mwembechai Killings....'' (2000), lakini hiki kimepigwa marufuku.

Vinginevyo bila kujua historia ya kweli itakuwa tabu kwako leo kuelewa imekuwaje Shura ya Maimamu wanazungumza jambo zito la dhulma dhidi ya Waislam na BAKWATA iko kimya na kwa nini kwa miaka yote hiyo serikali imekuwa kimya katika tatizo hili la elimu kama Waislam wanavyolalamika.

Nahitimisha kwa kueleza hatari ya jambo hili la Waislam kudhulumiwa katika elimu.

Baada ya yaliyokuwa yanafanyika Baraza la Mitihani kufahamika na serikali ilipopata taarifa kuwa Waislam wataandamana kwa kudhulumiwa katika elimu ikatoa onyo kali.

Ilikuwa siku ya Ijumaa Msikiti wa Kichangani.

Baada ya sala Sheikh Ponda akasimama kuwahutubia Waislam waliojaa msikitini akaeleza kwa kutoa ushahidi kuhusu hii dhulma ya elimu.

Nje ya msikiti yalitanda magari ya polisi na helicopter zikizunguka juu.

Ndani ya msikiti walikuwapo makachero wengi na nje kwa ndani ya uzio wa msikiti.

''Ndugu zangu Waislam kama hatukuandamana kwa hili nini Waislam tufanyiwe ili tuandamane?

Mimi nitaongoza maandamano haya na nitakuwa mstari wa mbele...''

Sheikh Ponda alipomaliza kusema maneno haya aligeuka akawapa mgongo wale aliokuwa akiwahutubia akaelekea kibla akanyanyua mikono yake kuomba dua kumtaka Allah msaada.

Mimi nilikuwa chini nyuma yake na tape recorder yangu na camera nikirekodi na kupiga picha.

Hii picha niliyoweka hapa ni katika picha zangu ninazozipenda sana kupita kiasi.

''Tension,'' niliyoshuhudia ndani ya msikiti ilikuwa ya kutisha na nikasema ndani ya nafsi yangu kuwa ikiwa serikali hii itakuwa na ujinga ikaamuru askari wake wawashambulie Waislam kwa kukataa kudhulumiwa katika elimu basi leo damu itamwagika.

Maandamano yalipofika Jangwani zikaja taarifa kuwa Waislam wanaombwa waandamane kwa amani waelekee Kidongo Chekundu na pale viongozi wao watachukuliwa hadi Wizara ya Mambo ya Nje na waraka wao kwa serikali utapokelewa pale na Waislam wabakie pale hadi viongozi wao watakaporejeshwa Kidongo Chekunde na viongozi wao ndiyo watatoa amri ya Waislam kutawanyika.
Ukiingia kujadili mambo ya Waislam nawe huna elimu ya historia yao utatabika sana.

Hapo chini ni ''paper'' zangu katika somo hili:

1. Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).

2. The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).

3. Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).

4. Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
 

Attachments

  • PONDA AKIOMBA DUA MTAMBANI MAANDAMANO YA NDALICHAKO.JPG
    PONDA AKIOMBA DUA MTAMBANI MAANDAMANO YA NDALICHAKO.JPG
    16.1 KB · Views: 2
Imeandikwa kitaalam sana.

Bila chenga

1. Tume huru ya uchaguzi

2. Katiba mpya bora

3. Uwiano wa kimadaraka

4. Haki na kuthamini utu wa mtanzania

5. Uadilifu sio maamuzi ya upande mmoja tu

6. Ukandamizaji uhuru, haki na utu wa mtanzania

Nknknk

Mashekh wametisha

Tunasubiri la kanali pengo
 
Kuna mengi nakubaliana na waraka huu ila hili la kuangalia na kumlazimisha kuwa mtanzania huyu ni wa dini hii au ile hilo lina utata.

Kugawana keki ya taifa n.k kungetumia kikokotoo cha kanda maana kutumia imani bado imani fulani itazidiwa wingi na kuleta mgawanyiko ktk taifa, jamii na familia ila kuangazia kanda inafuta mgawanyiko kwa kufuata imani.

Lakini sio kwa 80% vs 20%

Endapo wanasema ukweli that's 8acceptable
 
Mleta mada kwa upande mmoja upo sahihi sana ila kuna jambo linasahaulika hapa tukirudi nyuma ku examine teuzi zao kuwa katika hizo idara hapo awali kulikuwa na sintofahamu nyingi ila jambo hilo halikupewa tija sana kwa kipindi kile mi nadhani kuwe na miongozo thabiti ya namna hawa wabobezi wa elimu wanavyoteuliwa iliyowekwa rasmi na sheria husika za mahala husika lakini ili la mimi ni fulani basi na wateuwa wakina fulani kuwa sehemu fulani halitofika kikomo nadhani hapo ndipo tukazie
 
Kumbe huwa mnahesabu, ? na kuweka asilimia, wengine hatujawahi kufikiria hayo kabisa.
 
Huko kulialia hamkuanza Leo

Halafu hata katika waraka huu bado mnalia na kutaka kusaidiwa wala sio kuonesha lengo la ninyi kama Waislam kufanya jambo flani

Hata huu muda wa kulia humu ni bora mngeenda kujadili namna ya kuinua shule zenu na ufaulu sheikh,

Hao unaosema wanalialia ndiyo Majority walioanzisha harakati za kumng'oa mkoloni, wakati huo Wakiristu wengi wakiwa ni watoto watiifu wa mkoloni.

Baada ya Uhuru badala ya kuwa treated fairly, bahati mbaya yule mtu waliyemuamini kuwa atakuwa fair kwa wote akasimika mfumo unaofavor watu wa dini yake nchini, mfumo ambao ni pasua kichwa kwelikweli, Vitengo vyote muhimu kajaza watu wa dini yake, Maraisi wauslamu walipojaribu kuwa fair kwa wote wanakutana na barua kali za kichungaji zenye maonyo yaliyofichika ya kutishia kuvuruga amani ya nchi iwapo zitafanyika reforms za haki nchini.

Ndiyo maana hata mkuu wa mkoa wa Dar es salaam anasema nchi hii iko chini ya Kanisa. Yuko sahihi, anazungumza ukweli mchungu.

Kwa hiyo waache waislamu waendelee kulialia kwa sababu wanabaguliwa katika ajira, na teuzi za kuitumikia nchi.

Wewe huwezi kuelewa feelings za waislamu kwa sababu ni mnufaika wa mfumo, hapa unachokifanya unatetea maslahi yako na watoto na wajukuu zako.

But Fahamu kwamba, Wanaosimamia mfumo wa ajira na utumishi na teuzi za kiserikali nchini ni dhahiri wako too biased against Muslims.

Unaweza kuwabeza waislamu, lakini hawako radhi na jinsi mambo yanavyofanywa.

Unaweza wewe kama wewe ukapuuza madai haya lakini waislamu in majority wanayaunga mkono na hawapendezwi na hali hii. Sasa chagueni tu muendelee na business as usual au muaddress madai haya ya waislamu, Msipoyaddress basi hili ni bomu linalosubiri kupasuka, It is a matter of time
 
Kumbe huwa mnahesabu, ? na kuweka asilimia, wengine hatujawahi kufikiria hayo kabisa.

Mamlaka za teuzi it seems zinafikiria hayo.
How come always waislamu ni minority katika hizo teuzi, kama siyo sampuli iliyofanywa makusudically ni nini?
 
Hii ya kuwa majina si utambulisho wa dini ya mtu Mwalimu Nyerere kaitumia katika hotuba yake ya Diamond Jubilee siku anaaga mwaka 1985:

''Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo. Sasa nipo katika hali ya kufarahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho. Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo. Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.''
Mi niliwah kuwa na kesi mahakama ya ardhi pale mwananyamala. Hakim alikuwa anaitwa Mohamed.nilikuja kugundua Alikuwa mlokole wa kufa mtu. So jina lisikuhakikishie din ya mtu
 
Sasa hao walioahimishwa ni madr? Mana hao uliosema wameamia hao karibu wengi ni madr.waliohamishwa bw.bw....waongeze kisomo cha dunia ili warudi hapo Dodoma.mambo yasiwe mengi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom