Uchaguzi 2020 Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania

Uchaguzi 2020 Waraka wa Uchaguzi wa Shura ya Maimamu Tanzania

Status
Not open for further replies.
Walioleta mifarakano ni hao watawala waliopanga mipango mibovu ya ugawanyaji wa madaraka. Kama wao walikuwa wanalifikiria hilo wangekuwa tayari kutafuta suluhu.

Wewe na hao watawala mpo chungu kimoja. Msipoyaona haya mtaiingiza nchi matatani.
Wacha umbea we Mwanamke, wakati hayo yanatokea Waislam mlikuwa wapi?

Tutajie teule za J.M Kikwete hapa.
 
Kalamu...
Ulichosema ni kweli kabisa.

Lakini teuzi lazima zichukuliwe kwa tahadhari hasa katika maeneo ya dini na kabila...
Yaani unataka hata uzushi uonekane ni tatizo?

Weka hapa teuzi zote za J.M. Kikwete akiwa bado ni Rais
 
Nikwambie kitu kimoja ambacho unatakiwa kukifahamu - (Tena umegusa kwenye shina; Elimu) suala la kuiandaa jamii ya kesho ni ya serikali. Hii ikiwa pamoja na elimu ambayo ndio dira ya kupata ajira. Ni ujinga baada ya miaka 60 ya uhuru tukaendelea kulia na makosa aliyoyafanya mkoloni, huku ni kukosa akili. Sasa tulidai uhuru ili iweje? Au unafikiri ili tuendeleze utaratibu ule ule wa mkoloni, tukibadili rangi tu ya mtawala.

Tena umetaja Mmakabila kama wachaga - Huwezi amini kuwa mkoa wa Kilimanjaro unashule nyingi za sekondari kuliko Dar es salaam ambapo uwiano wa wakazi wa mikoa hiyo hata haikaribiani. Tena shule nyingi zaidi zimejengwa baada ya uhuru na mkoloni mweusi. Usishangae kwani hii ndio sera ya serikali ikiwalipa walimu na kuendesha shule hizo kwa kodi za wananchi wote.

Kifupi utaratibu wa maandalizi ya mwananchi yamefanywa kimakusudi kabisa huku wakijua kuwa wao watashikilia tu kuwa hawa hawana elimu.

Kwa ufahamu zaidi soma kitabu cha muandishi Sykes, ndio utaona mpango halisi. Ni lazima mwenendo huu ubadilike toka kwenye elimu, hakuna vipofu sasa hivi. Mambo yote yapo hadharani, humfichi mtu kitu.

J. K. Nyerere amewekwa kama candidate na kanisa katoliki ya kupewa U- Saint, si kwa bahati mbaya. Ni kwa vile katekeleza mpango mahsusi wa kuhakikisha kuwa kuna kikundi fulani kinapata upendeleo. Tunachosema ni kuwa yaliyopita ni ndwele tugange ya sas na yajayo.
Wakati Nyerere anafanya hayo, ninyi mnaosema mlimweka Nyerere madarakani mlikuwa wapi???

Mlipata Upofu? Au mlishindwa kumchallenge vile mlikuwa hamjui kusoma na kuandika

Au mlikuwa mnatawadha tu.
 
Teuzi na upandishwaji vyeo lazima vifanyike kwa kuangalia sifa na vigezo vya mtu husika.
Lazima viwe 'based on merits' siyo sifa ya udini au ukabila.
Mkuu vipi kwani kuna teuzi zinazozingatia Ukabila na Udini?
 
Upuuuz mtupu. Kwahiyo mtu akiitwa John anakuwa Mkristo sio. Au muhamed anakuwa muislam.achanen na woga wa maisha nyie. Mnakera kweli aisee.
Kitali,
Ukiwa unajadili jambo na mwenzio inataka uzingatie kuheshimiana.

Jiepushe na maneno kama "upuuzi."

Kwa mtu muungwana ushamtia hofu anaona mjadala umegeuka kuwa wa matusi na matusi hayajibiwi na mtu mstaarabu.

Atabakia kimya.
 
Nimelisoma vizuri sana, kuandikwa na kithibitisha ni vitu viwili tofauti, Mtu anaweza kuandika chochote

Hebu nitajie hao Wakristo waliohusika kuvunja msikiti.
Wakwanza ni makamu mkuu wa chuo, pili walitolewa waislam 11 wakawekwa wakristo 11, humu watu wengi mnasema waislam hawajaenda shule lakini bado mnasema JK alipendelea waislam sasa hao waislam aliopendelea walikuwa hawana shule, mkitoka hapo mnasema waislam wanalalamika ila wakristo walivyokuwa wanamlalamikia Dau wa nssf mnadhani tumesahau?
 
Wakwanza ni makamu mkuu wa chuo, pili walitolewa waislam 11 wakawekwa wakristo 11, humu watu wengi mnasema waislam hawajaenda shule lakini bado mnasema JK alipendelea waislam sasa hao waislam aliopendelea walikuwa hawana shule, mkitoka hapo mnasema waislam wanalalamika ila wakristo walivyokuwa wanamlalamikia Dau wa nssf mnadhani tumesahau?
Unajua kilichosababisha kutokea kwa huo mgogoro UDOM?

Wewe umeona wapi kanisa linajengwa ndani ya chuo cha serikali?

Kuhusu NSSF Waislam walikuwa wanaingia na mikeka kuswalia maofisini kitu ambacho Mkristo hawezi kuleta msalaba na kutengeneza mimbari katika ofisi ya umma na kuabudia hapo, okay tuachane na hilo unajua kuwa Wakristo wote waliokuwa na sifa za kuajiriwa NSSF hawakuzingatiwa? Au unabwatuka tu?
 
Kitali,
Ukiwa unajadili jambo na mwenzio inataka uzingatie kuheshimiana.

Jiepushe na maneno kama "upuuzi."

Kwa mtu muungwana ushamtia hofu anaona mjadala umegeuka kuwa wa matusi na matusi hayajibiwi na mtu mstaarabu.

Atabakia kimya.
Ujinga unatakiwa uitwe ujinga ili mjinga asiurudie. Huwez kutambua dini ya mtu kwa kuangalia majina achen ujinga bana.
 
Mengine yote sawa... Isipokuwa hayo yanayohusu hizi dini zilizofeli kwa kuendekeza fitina, ufisadi, ubaguzi na ulaghai na ujinga!
Imefikia kipindi dini nyingi zinajiendesha vibaya kuliko vyama vilivyopo vya siasa na mifumo ya kidikteta!
 
Unajua kilichosababisha kutokea kwa huo mgogoro UDOM?

Wewe umeona wapi kanisa linajengwa ndani ya chuo cha serikali?

Kuhusu NSSF Waislam walikuwa wanaingia na mikeka kuswalia maofisini kitu ambacho Mkristo hawezi kuleta msalaba na kutengeneza mimbari katika ofisi ya umma na kuabudia hapo, okay tuachane na hilo unajua kuwa Wakristo wote waliokuwa na sifa za kuajiriwa NSSF hawakuzingatiwa? Au unabwatuka tu?
Hahahaa! Kumbe na nyie mnalalamika eeh? Eti wakristo wameachwa nssf, hivi UDSM hakuna kanisa?
 
Unajua kilichosababisha kutokea kwa huo mgogoro UDOM?

Wewe umeona wapi kanisa linajengwa ndani ya chuo cha serikali?

Kuhusu NSSF Waislam walikuwa wanaingia na mikeka kuswalia maofisini kitu ambacho Mkristo hawezi kuleta msalaba na kutengeneza mimbari katika ofisi ya umma na kuabudia hapo, okay tuachane na hilo unajua kuwa Wakristo wote waliokuwa na sifa za kuajiriwa NSSF hawakuzingatiwa? Au unabwatuka tu?
Mnajichanganya wenyewe aisee mmeilalamimia nssf ambayo ilikuwa na wafanyakazi 69% wakristo na waliobaki ni dini nyingine, ok kumbe mnataka 80 to 20 percent
 
Mnajichanganya wenyewe aisee mmeilalamimia NSSF ambayo ilikuwa na wafanyakazi 69% wakristo na waliobaki ni dini nyingine, ok kumbe mnataka 80 to 20 percent
Wewe hujui hata unachokiandika, Mimi sijalalamika nimekuuliza maswali nikakupa facts.

Hakuna Wakristo wenye muda wa kulialia au kuandamana, huwa wanaungana na kutafuta solution ya mambo yao kimantiki.

Hatutegemei kubebwa, sio kimadaraka au kielimu

That's it.
 
Hii ya kuwa majina si utambulisho wa dini ya mtu Mwalimu Nyerere kaitumia katika hotuba yake ya Diamond Jubilee siku anaaga mwaka 1985:

''Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo. Sasa nipo katika hali ya kufarahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho. Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo. Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.''
 
LAKINI WAKITUMBULIWA WASIJE TENA MARA OOOH SABABU YA DINI YETU NDIO MAANA TUNATUMBULIWA.

1. JAMAA HAANGALII HAYO HATA MASWAIBA WAKE MBONA KAWAPIGA CHINI?

2. HALAFU HAO WAHADHIRI SI BADO WANA TAALUMA ZAO? UKIONA HIVYO UJUE KUNA MAHALI MLIKOSEA KUWENI WAZI MAANA INAJULIKANA.
 
Hamnaga maana nyie,kitu kidogo mnakomaaga utadhani umezuiliwa kuishi au kula,udini hua umekukaeni kupita kiasi,jambo hata kama halijawekwa kidini ninyi mnalichambua kidini, hapa husemi hata hao wa dini moja waliotolewa sehemu moja je hawakuwekana wao kwa wao na yamkini kuna kitu walikua wanavuruga? Maana ninyi mnapenda vita na amani
 
Wewe hujui hata unachokiandika, Mimi sijalalamika nimekuuliza maswali nikakupa facts.

Hakuna Wakristo wenye muda wa kulialia au kuandamana, huwa wanaungana na kutafuta solution ya mambo yao kimantiki.

Hatutegemei kubebwa, sio kimadaraka au kielimu

That's it.

Nyie tayari mnabebwa na mfumo hamna haja ya kulialia. Sasa mlielie ya kazi gani?

Kulialia waachie wale ambao kwa makusudi kabisa wananyimwa fursa sababu ya dini yao hata kama wana vigezo

Bongo ukiwa mkiristu ukaomba kazi na muislamu na nyote mna vigezo sawa, probability ya Mkiristu kupata kazi ni kubwa kuliko huyo muislamu kwa sababu mfumo uko biased in favor ya Wakiristo. Huhitaji kuwa na PhD kuliona hili.
 
Imeandikwa kitaalam sana.
Tatizo lipo kwenye udini ambako wameshindwa kuficha maslahi yao...
Aidha waraka wao pia bado ni mwendelezo wa dhana ya kusubiria serikali itende au iamue kwa maslahi ya wananchi (top down). Hii dhana ni potofu sana.. Na hawa jamaa wamejichanganya sana! Badala ya kuhamasisha wananchi waamke waunganishe nguvu na wadai staki na stahiki zao (bottom up) wao bado wanahisi ipo siku serikali itatenda yenye manufaa kwa wananchi! No way! Serikali inaundwa na watu... So ikija na solution itakuja na ile inayolinda maslahi ya mtawala na wafuasi wake walio wengi!

Tukiendelea na dhana ya top-down kwenye mambo ya haki, utawala na ustawi wa jamii ni obvious kuwa wananchi na umma utapokwa fursa ya kushiriki kwenye michakato mingi!

Historia inaonesha kuwa huu ndo mzizi wa tatizo nchini kwetu... Kusubiria serikali itende na iamue kwa ajili yetu. Michakato mingi ya mabadiliko imefeli baada ya kuiacha serikali iamue na itekeleze... Rejea mwenendo wa Katiba, Uchaguzi, Mahakama, Bunge na Utumishi wa umma...!

Kateni mzizi wa tatizo kwa kuwaamsha wananchi wajue umuhimu na wasiogope kujisimamia. Kabla ya hapo... Endeleeni kukusanya adidu za rejea zitakowasaidia kufikisha ujumbe na kueleweka kwa umma
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom