Waraka wa wataalam wa maabara Tanzania kuhusu ajira za TAMISEMI na Wizara ya Afya

Waraka wa wataalam wa maabara Tanzania kuhusu ajira za TAMISEMI na Wizara ya Afya

Wana hoja za msingi sana unaenda hospitali anayekupima ndiye anakupa dawa sababu y upungufu wa wataakamu hii si sawa.
Ila hapo kujiunga shahada bila GPA y diploma kufika
inayohitajika hapako sawa na hii ni condition karibu kwenye taaluma zote.
 
Wana hoja za msingi sana unaenda hospitali anayekupima ndiye anakupa dawa sababu y upungufu wa wataakamu hii si sawa.
Ila hapo kujiunga shahada bila GPA y diploma kufika
inayohitajika hapako sawa na hii ni condition karibu kwenye taaluma zote.
Upo sahihi
 
Tuwe wapole kiongozi
Ni kweli kuwa wapole ni jambo la muhimu pia, lkn hamkupata hata wasaa wa kukaa mkapitia neno moja baada ya jingine kisha mkawasilisha kwa umma kitu kilicho sahihi?.
 
Ni kweli kuwa wapole ni jambo la muhimu pia, lkn hamkupata hata wasaa wa kukaa mkapitia neno moja baada ya jingine kisha mkawasilisha kwa umma kitu kilicho sahihi?.
sijaona ulipokosea lengo la kuleta huu uzi ni maoni tu.., na wewe umeona waraka na kutoa maoni kwahyo sioni tatizo
 
N
Ninawafahamu A to Z halafu asilimia 90 elimu zao ni za kuungaunga
Ndo maana hawawpendi degree holders fresh from school. Kumbe hawana maajabu. Kama jamaa anavyosema unawezadhan watu makn Sana kumbe hakuna kitu. Inakuwaje unabagua wengine?
 
https://twitter.com/tmla_tanzania Login • Instagram


Mhe waziri mwenye dhamana ya afya ummymwalimu
pengine hata wewe unajiuliza kwa nini wataalamu wa maabara wanalalamika.

Kifupi, hakuna aliyeonekana kuyasemea haya, hata tuliowaita viongozi wa taaluma walikaa pembeni wakishuhudia chombo hiki kinazama.

Mheshimiwa Waziri, haya ni malalamiko kwa uchache.

1. HAKUNA USAWA KATIKA MGAWANYO WA AJIRA ZA AFYA NCHINI

Tangu mwaka 2021 mpaka mwka 2023, ajira kwa upande wa Kitengo cha

maabara zimekuwa zikitolewa kwa kiwango kidogo mno, shughuli za vipimo vya maabara zinafanywa na

kada nyingine ambazo hazina utaalamu wa kutosha hivyo kupelekea

wateja wengi kupewa majibu yasiyo sahihi.

AJIRA ZA OR- TAMISEMI MWAKA 2021

Astashahada walipewa nafasi 142 sawa na
Wenye Stashahada walipewa nafasi 10 (0.3%
Shahada hawakupewa nafasi hata moja Sawa na 0%

Jumla ajira zilikua 2726.

MWAKA 2022

Astashahada nafasi 152 sawa na 2.2%

Stashahada nafasi 197 sawa na 2.8%
Shahada walichaguliwa 35 tu Sawa na 0.5%

Jumla ajira zilikua 6873

MWAKA 2023

Astashahada nafasi 56 sawa na 1.05%

Stashahada nafasi 18 sawa na 0.33%

Shahada nafasi 13 sawa na 0.24%

Jumla ajira zilikua 5319

Mheshimiwa, asiseme mtu hitaji halipo, tumefanya tafiti na tumegundua vituo hivi havina wataalamu wa maabara hata mmoja, je nani anafanya vipimo?

Vituo hivi havina wataalamu wa maabara.

Bulela dispensary - GEITA

Didia Dispensary - SHINYANGA

Mavota dispensary - KAGERA
Mselekea dispensary - MOSHI

Ibologero dispensary - TABORA

Bukondo dispensary - MWANZA

Kemgesi dispensary - MARA

Kisa dispensary - RUKWA

Mawe dispensary - ARUSHA

Tewe dispensary - TANGA

Ligumbiro dispensary - NJOMBE

Chajo dispensary - KILIMANJARO

Kilimani dispensary - MANYARA

Chumo Dispensary - LINDI

Na hivi ni vichache tu, Sasa je, Hawa wananchi huduma wanapewa na nani?

2. MAFUNZO YA UPIMAJI KWA WATU WASIO WATAALAMU WA

MAABARA NCHINI (NON LABORATORY

TESTERS) YAFUTWE.

Sheria hii iliwekwa mwaka 2007 kwa sababu kulikua na upungufu, huu upungufu haupo tena, wataalamu wa kufanya kazi zao wapo, huu utaratibu UFUTWE.

3. USAWA WA UONGOZI KATIKA KADA YA AFYA.

Mheshimiwa, kuna nafasi mpaka zimekaririwa anatakiwa kukaa daktari au muuguzi, kwa nini?

Nafasi ambayo sio ya kutumia taaluma bali uwezo wa uongozi, kwa nini tunakua kama tunaamini waliosoma maabara hawawezi kuwa viongozi?

Nafasi ya facility incharge, nafasi ya DMO kwani hizi nafasi zinawataka madaktari watibu?

Tunaomba ziwe nafasi za wazi, ziruhusu mtaaluma yeyote wa kada ya afya aongoze.

Kada hii pia mheshimiwa watu wamesoma management na leadership na hizi nafasi zinahitaji uongozi ila sio nafasi za kutumia ujuzi wa taaluma zao.

4. IDARA ZILIZOPO NDANI YA MAABARA ZISIMAMIWE NA WATAALAMU WA MAABARA.

Mheshimiwa, nenda Muhimbili pale kitengo cha maabara madaktari ndio wasimamizi wa vitengo vya maabara, kwa nini?

Tunatambua utaratibu huu unatokana na hoja kwamba kipindi cha nyuma tulikua hatuna wasomi wengi wa kada hii, leo tunao mheshimiwa, tuna wasomi wa PHD maabara, acha wakae vitengo vyao.

Ni sawa na kusema leo mtaalamu wa maabara asimamie kitengo cha mama na mtoto kisa alijifunza kuhusu hedhi.

Haiwezekani. Tunaomba vitengo vyetu tuvihudumie wenyewe.

Hata uwepo wa ulazima wa mkurugenzi wa diagnosis wizarani kuwa daktari haitakiwi mheshimiwa, tupo, mtutumie.

5. SIFA ZA KUJIENDELEZA NA KOZI MBALIMBALI ZIRUDIWE UPYA.

Mpaka leo kuna kozi huwezi soma kama sio daktari licha ya kuwa ni kozi zinazomuhusu mtaalamu wa maabara moja kwa moja.

Mfano Histopathology na Cytopathology.

6. VIONGOZI WA TAALUMA HAWAENDANI NA KASI.

Mheshimiwa, kwanza haya yote yangefaa kusemwa na wao.

Leseni zinachelewa, utaratibu wa mitihani unachelewa, sasa kuna maswala ya CPD utaona nako hakutiliwi mkazo, kuna swala la gharama za matumizi ya vyeti vya wanataaluma katika kufungua vituo vya huduma za afya bado hazijakaa sawa

Mheshimiwa binafsi namjua mtu alifanya mitihani ya shule akafaulu, ikabidi alipie kufanya mtihani wa provisional licence ambayo anakaa nayo kwa mwaka mmoja kisha analipia kufanya mtihani mwingine wa full registration.

Sasa Mheshimiwa, hii ni sawa? Mfululizo wa mitihani yote hii ni kupima nini? Kama hatuviamini vyuo tuvifunge, chuo kimempika mtaalamu akaiva, kafanya mtihani wa chuo kafaulu, kafanya mtihani kwa leseni wa kwanza kafaulu, kwa nini baada ya provisional asipewe full registration bila mtihani?

Utaona kuna mengi sana ya kuyasemea ila viongozi wanajua na hawaoni kama wana nafasi ya kufanya hivyo.

Mhe ummymwalimu
tuna imani kubwa na wewe, tunaomba utusikilize, tunaomba uyapokee haya, hakuna huduma bora bila mihimili iliyosimama.

Tunahitaji muhimili wa maabara usimame, ukusaidie kuboresha huduma za afya nchi wananchi wapate huduma inayostahili.

IMG_16868196697698504.jpg
 
Hizi ni baadhi ya sababu zao za wataalam wa maabara, kufikia hatua ya kua na kurugezi yao.



Huu ni mlolongo wa usimamizi kutoka wizara ya Afya pamoja na kurugezi zake ambao uliidhinishwa na Rais tarehe 7 Julai, 2018,



MUUNDO WA KAZI NA SHIRIKA ULIOIDHINISHWA WA WIZARA YA AFYA,

MAENDELEO YA JAMII, WAZEE, JINSIA NA WATOTO

(Iliyoidhinishwa na Rais tarehe 7 Julai, 2018)



Kama ifuatavyo :-

1. WIZARA YA AFYA



2. KATIBU MKUU



3. MGANGA MKUU



3. WAGANGA WA MIKOA



4. KITENGO CHA HUDUMA ZA KINGAM KINA KURUGENZI



5. KITENGO CHA HUDUMA ZA TIBA KINA MKURUGENZI



6. KITENGO CHA UUGUZI NA UKUNGA KINA MKURUGENZI



7. KITENGO CHA MADAWA KINA MKURUGENZI



8. KITENGO CHA MATAYARISHO YA AFYA NA MITIKIO KINA MKURUGENZI



9. MGAO WA MAENDELEO YA RASILIMALI WATUKKINA MKURUGENZI


10. KITENGO CHA UHAKIKI WA UBORA WA AFYAK KINA MKURUGENZI



11. MGAWANYIKO WA SERA NA MIPANGO KINA MKURUGENZI



12. KITENGO CHA UTAWALA NA USIMAMIZI WA RASILIMALI WATU KINA MKURUGENZI



13. KITENGO CHA FEDHA NA HESABU KINA MHASIBU MKUU



14. KITENGO CHA HUDUMA ZA KISHERIA KINA MKURUGENZI



15. KITENGO CHA UKAGUZI WA NDANI KINA MKAGUZI MKUU WA NDANI



16. KITENGO CHA USIMAMIZI WA MANUNUZI MKURUGENZI



17. KITENGO CHA TEHAMA KINA

(a) MTAWALA MKUU

(b) MKURUGENZI


WATAALAM WA MAABARA TUNA KURUGENZI IPI??? 🤔🤔😐😐 NA KWA NINI HAINA MKURUGENZI
 
Mtaalam wa maabara ni ' Paramedical'. Unaweza ukawa na hoja kutaka muwe na kurugenzi yenu ila kuwa Facility Incharge ama DMO ni ngumu.
 
Mtaalam wa maabara ni ' Paramedical'. Unaweza ukawa na hoja kutaka muwe na kurugenzi yenu ila kuwa Facility Incharge ama DMO ni ngumu.
Lengo kuu ni kuwa na Kurugenzi.. Maana kero wanashindwa wazipeleke wapi.... DAKTARI hawezi kutatua kero za maabara
 
Back
Top Bottom